Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MUNGU ANAONA VITA NAMNA GANI?

Namna Mungu Aliona Vita Wakati wa Zamani

Namna Mungu Aliona Vita Wakati wa Zamani

Watu walikuwa wanaonewa. Walisali tena na tena kwa Mungu ili awasaidie, lakini hawakupata musaada palepale. Watu hao walikuwa Waisraeli, watu wa Mungu wa zamani. Taifa lenye nguvu la Misri ndilo lilikuwa linawaonea. (Kutoka 1:13, 14) Walingojea Mungu kwa miaka mingi ili awatoshe katika mateso ya Wamisri wenye walikuwa wanawaonea. Mwishowe, wakati wenye kufaa wa Mungu ili kutenda ulifika. (Kutoka 3:7-10) Biblia inasema kama Mungu mwenyewe alipigana vita na Wamisri. Alileta mapigo hatari sana yenye kufuatana juu ya inchi ya Misri, na kisha akaua mufalme wa Misri na jeshi lake katika Bahari Nyekundu. (Zaburi 136:15) Yehova Mungu alijionyesha kuwa ‘mutu wa vita’ kwa ajili ya watu wake.—Kutoka 15:3, 4.

Kwa sababu Mungu alipigana vita na Wamisri, jambo hilo linaonyesha kama hachukie vita zote. Wakati mwengine, aliruhusu watu wake Israeli wapigane vita. Kwa mufano, aliwaomba wapigane vita na Wakanaani wenye walikuwa wabaya sana. (Kumbukumbu la Torati 9:5; 20:17, 18) Alimuongoza Mufalme Daudi wa Israeli kupigana vita na Wafilisti wenye walikuwa wanawaonea. Na hata alimuambia Daudi njia ya kupigana vita yenye ilifanya apate ushindi.—2 Samweli 5:17-25.

Habari hizo za Biblia zinaonyesha kama wakati Waisraeli waliteseka kwa sababu ya ubaya wa aina fulani na kwa sababu ya kuonewa, Mungu aliruhusu vita ili kulinda watu wake na ibada ya kweli. Lakini, ona mambo tatu ya maana yenye kufuata juu ya vita hizo zenye Mungu aliomba zipiganwe.

  1. MUNGU MWENYEWE ALIAMUA NI NANI ALIPASWA KUPIGANA VITA. Wakati moja, Mungu aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Hamutahitaji kupigana katika kisa hiki.’ Sababu gani? Mungu mwenyewe angepigana vita. (2 Mambo ya Nyakati 20:17; 32:7, 8) Alifanya hivyo mara nyingi, kama vile inaonyeshwa mwanzoni mwa habari hii. Wakati mwengine, Mungu aliwaomba watu wake wa Israeli la zamani kupigana vita zenye alikubali, ni kusema, vita zenye zilipiganwa ili kulinda na kupigania Inchi yao ya Ahadi.—Kumbukumbu la Torati 7:1, 2; Yoshua 10:40.

  2. MUNGU MWENYEWE ALIAMUA NI WAKATI GANI VITA KAMA HIZO ZILIPASWA KUPIGANWA. Watumishi wa Mungu walipaswa kungojea kwa uvumilivu mupaka wakati wenye Mungu aliweka ili kupiganisha watu wenye waliwazunguka, ambao walikuwa wanawaonea na kufanya mabaya. Mbele wakati huo ufike, wao wenyewe hawangepaswa kuamua kupigana vita. Wakati walifanya hivyo, hawakukubaliwa tena na Mungu. Kwa kweli, Biblia inaonyesha kama wakati Waisraeli waliamua wao wenyewe kupigana vita yenye Mungu hakuruhusu, mara nyingi walipata matokeo mabaya sana. *

  3. Hata kama Mungu alipigana vita na Wakanaani, hakuua watu fulani kama vile Rahabu na jamaa yake

    MUNGU HAFURAHIE KIFO CHA WATU, HATA KIFO CHA WATU WABAYA. Yehova Mungu ndiye alianzisha uzima na ndiye Muumbaji wa watu. (Zaburi 36:9) Kwa hiyo, anachukia kuona watu wanakufa. Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba kuko watu wenye wanapanga kwa ujanja kuonea wengine ao hata kuwaua. (Zaburi 37:12, 14) Ili kumaliza matendo hayo mabaya, wakati fulani Mungu aliruhusu Waisraeli wapigane vita na watu wabaya. Lakini, kwa miaka mingi yenye aliomba Waisraeli wapigane vita, Mungu alikuwa “mwenye rehema” na hakukuwa “mwepesi wa hasira” kuelekea wale wenye walionea Waisraeli. (Zaburi 86:15) Kwa mufano, alitoa sheria yenye kusema kama mbele Waisraeli wapigane vita na muji fulani, walipaswa ‘kuutangazia pia masharti ya amani,’ ili kuwapatia wakaaji nafasi ya kubadilisha njia zao na kuepuka vita. (Kumbukumbu la Torati 20:10-13) Katika njia hiyo, Mungu alionyesha kama ‘hapendezwe na kifo cha muovu [mutu mubaya], bali [lakini] kwamba mutu muovu ageuke na kuiacha njia yake na kwa kweli aendelee kuishi.’—Ezekieli 33:11, 14-16. *

Mambo hayo yenye tunatokea kuzungumuzia yanaonyesha kama, Mungu aliona vita kuwa njia ya haki ya kumaliza aina mbalimbali ya matendo ya kuonea wengine na ya ubaya. Lakini ni Mungu ndiye alikuwa na haki ya kuamua ni wakati gani vita kama hizo zilipaswa kupiganwa na ni nani alipaswa kupigana; mwanadamu hakukuwa na haki ya kufanya hivyo. Lakini, Mungu alipigana vita kwa njia yenye kuonyesha kama alikuwa na hamu ya kumwanga damu? Hapana kabisa. Kwa kweli, anachukia jeuri. (Zaburi 11:5) Mawazo ya Mungu juu ya vita yalibadilika wakati Yesu, Mwana wake, alianza kazi yake ya kuhubiri wakati wa mitume?

^ fu. 7 Kwa mufano, wakati fulani Waisraeli walishindwa katika vita yenye walipigana na Waamaleki na Wakanaani kwa sababu Mungu alikuwa amewakataza kufanya hivyo. (Hesabu 14:41-45) Miaka mingi kisha hapo, Mufalme muaminifu Yosia alipigana vita bila Mungu kumuruhusu, na alikufa kwa sababu ya kutenda hivyo bila kufikiri.—2 Mambo ya Nyakati 35:20-24.

^ fu. 8 Waisraeli hawakutangaza masharti ya amani mbele ya kupigana vita na Wakanaani. Sababu gani? Kwa sababu Wakanaani walikuwa wamepewa miaka 400 ili wabadilishe matendo yao mabaya. Wakati Waisraeli walikuja kuwapiganisha vita, Wakanaani, kwa ujumla, walikuwa watu wabaya sana wasiotaka kubadilika. (Mwanzo 15:13-16) Kwa hiyo, walipaswa kuuawa kabisa. Hata hivyo, kila Mukanaani mwenye alibadilisha matendo yake, hakuuawa.—Yoshua 6:25; 9:3-27.