Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Baba ya Yosefu alikuwa nani?

Yosefu, seremala (mwenye kufanya kazi ya mbao) wa Nazarethi, alikuwa baba mwenye alikomalisha Yesu. Baba ya Yosefu alikuwa nani? Kizazi cha Yesu chenye kuwa katika Injili ya Mathayo kinataja mwanaume mumoja mwenye kuitwa Yakobo, lakini kizazi chenye kuwa katika Injili ya Luka kinasema kama Yosefu alikuwa “mwana wa Heli.” Sababu gani inaonekana kuwa zinapingana?—Luka 3:23; Mathayo 1:16.

Habari ya Mathayo inasema hivi: ‘Yakobo akamuzaa Yosefu.’ Inatumia neno la Kigiriki lenye kuonyesha waziwazi kama Yakobo alikuwa baba muzazi wa Yosefu. Kwa hiyo, Mathayo alionyesha kizazi cha Yosefu, ni kusema, utawala wa kifalme, wenye ungemupitishia Yesu, mwana mwenye Yosefu alikomalisha, haki ya kisheria ya kukaa kwenye kiti cha Ufalme.

Lakini, Injili ya Luka inasema hivi: “Yosefu, mwana wa Heli.” Maneno hayo, “mwana wa,” yanaweza kueleweka ‘mwana-mukwe wa.’ Maneno kama hayo yanapatikana katika andiko la Luka 3:27, kwenye Shealtieli, mwenye baba yake muzazi alikuwa Yekonia, anatajwa kuwa “mwana wa Neri.” (1 Mambo ya Nyakati 3:17; Mathayo 1:12) Inawezekana Shealtieli alioa mutoto wa Neri mwenye hatajwe jina, katika njia hiyo akakuwa mwana-mukwe wake. Ndiyo maana Yosefu anatajwa kuwa “mwana” wa Heli, kwa sababu alioa Maria, mutoto wa Heli. Kwa hiyo, Luka anataja kizazi cha Yesu “kulingana na mwili,” kupitia Maria, mama yake muzazi. (Waroma 1:3) Ndiyo sababu Biblia inatupatia vizazi viwili vya maana vya Yesu vyenye kuwa tofauti.

Wakati wa zamani kulikuwa nguo na rangi za namna gani?

Nguo ya sufu yenye kutiwa rangi, ya tangu mwaka wa 135 kisha kuzaliwa kwa yesu, ilipatikana katika mwamba karibu na Bahari ya Chumvi.

Manyoya ya kondoo, ya mbuzi, na ya ngamia yalitumiwa sana ili kutengeneza nguo katika Mashariki ya kati ya zamani. Nguo nyingi zilitengenezwa na manyoya ya kondoo, na mara nyingi Biblia inazungumuzia kondoo, kukata manyoya ya kondoo, na nguo za manyoya ya kondoo. (1 Samweli 25:2; 2 Wafalme 3:4; Ayubu 31:20) Mumea wa kitani wenye ulitumiwa ili kutokeza kitani ulipandwa katika Misri na Israeli. (Mwanzo 41:42; Yoshua 2:6) Inawezekana Waisraeli wa zamani hawakulima pamba, lakini Maandiko yanazungumuzia kutumikishwa kwa pamba katika Persia. (Esta 1:6) Hariri ilikuwa bei sana, pengine ililetwa tu na wafanyabiashara wenye walifanya safari kutokea Asia Mashariki.—Ufunuo 18:11, 12.

Kitabu kimoja kinasema hivi: “Manyoya ya kondoo yalikuwa na rangi mbalimbali za kiasili, kuanzia rangi nyeupe kidogo kufikia rangi ya kahawia ya giza-giza (café sombre) yenye kuwa na rangi nyingi.” (Jesus and His World) Tena, mara nyingi sufu ilikuwa inatiwa rangi. Rangi ya zambarau ya bei ilitokea kwenye wanyama fulani kama vile konokono na mimea mbalimbali, mizizi, majani, na vidudu vilitumikishwa ili kutokeza rangi kama vile ya mwekundu, ya kimanjano, ya bleu, na nyeusi.