Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Jina la Mungu (linaonyeshwa wazi) kama vile liko katika maandishi fulani ya zamani ya Biblia

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Mungu ana jina?

WATU FULANI WANASEMA kama hakuwake na jina, wengine wanasema kama jina lake ni Mungu ao Bwana, na wengine wanasema kama ana majina mengi sana. Wewe unawaza namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Hata kama Mungu ana majina mengi ya cheo, amejipatia jina moja tu.—Kutoka 3:15.

  • Mungu haiko fumbo; anataka tumujue. —Matendo 17:27.

  • Kujua jina la Mungu linaweza kuwa jambo la kwanza la kufanya ili kuwa rafiki yake.—Yakobo 4:8.

Ni mubaya kutaja jina la Mungu?

UNAWEZA KUJIBU NINI?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Inalingana na hali

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa [ya mubaya].” (Kutoka 20:7) Ni mubaya kutumia jina la Mungu ikiwa tu ni kwa njia ya kukosa heshima.—Yeremia 29:9.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?