Biblia Inasema Nini?
Ibilisi ni nani au nini?
JE, UNGESEMA Ibilisi ni . . .
Kiumbe wa roho?
Uovu ulio ndani ya mtu?
Jambo lililobuniwa na mwanadamu?
BIBLIA INASEMA HIVI
Ibilisi aliongea na ‘alimjaribu’ Yesu. (Mathayo 4:1-4) Hivyo, Ibilisi si kiumbe wa kubuniwa tu au alama ya uovu. Ni kiumbe wa kiroho aliye mwovu.
NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?
Mwanzoni, Ibilisi alikuwa malaika mtakatifu, hata hivyo “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Akawa mwongo na kisha akamwasi Mungu.
Malaika wengi waliunga mkono uasi wa Shetani.—Ufunuo 12:9.
Ibilisi amepotosha watu wengi kwa kuwafanya waamini kwamba hayuko.—2 Wakorintho 4:4.
Je, Ibilisi anaweza kuongoza watu?
BAADHI YA WATU WANASEMA si kweli kwamba Ibilisi anaongoza watu, na wengine wanaogopa sana roho waovu. Una maoni gani?
BIBLIA INASEMA HIVI:
“Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) Ingawa Ibilisi amefanikiwa kushawishi idadi kubwa ya wanadamu, haongozi kila mwanadamu.
NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?
Ibilisi anatumia uwongo ili kushawishi watu wengi zaidi.—2 Wakorintho 11:14.
Katika visa fulani roho waovu huongoza watu.—Mathayo 12:22.
Mungu anaweza kukusaidia ufanikiwe ‘kumpinga Ibilisi.’—Yakobo 4:7.