Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Ibilisi ni nani au nini?

JE, UNGESEMA Ibilisi ni . . .

  • Kiumbe wa roho?

  • Uovu ulio ndani ya mtu?

  • Jambo lililobuniwa na mwanadamu?

BIBLIA INASEMA HIVI

Ibilisi aliongea na ‘alimjaribu’ Yesu. (Mathayo 4:1-4) Hivyo, Ibilisi si kiumbe wa kubuniwa tu au alama ya uovu. Ni kiumbe wa kiroho aliye mwovu.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?

  • Mwanzoni, Ibilisi alikuwa malaika mtakatifu, hata hivyo “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Akawa mwongo na kisha akamwasi Mungu.

  • Malaika wengi waliunga mkono uasi wa Shetani.—Ufunuo 12:9.

  • Ibilisi amepotosha watu wengi kwa kuwafanya waamini kwamba hayuko.—2 Wakorintho 4:4.

Je, Ibilisi anaweza kuongoza watu?

BAADHI YA WATU WANASEMA si kweli kwamba Ibilisi anaongoza watu, na wengine wanaogopa sana roho waovu. Una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) Ingawa Ibilisi amefanikiwa kushawishi idadi kubwa ya wanadamu, haongozi kila mwanadamu.

NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?

  • Ibilisi anatumia uwongo ili kushawishi watu wengi zaidi.—2 Wakorintho 11:14.

  • Katika visa fulani roho waovu huongoza watu.—Mathayo 12:22.

  • Mungu anaweza kukusaidia ufanikiwe ‘kumpinga Ibilisi.’—Yakobo 4:7.