Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Shetani ni nani ao ni nini?

UNAWEZA KUJIBU kama Shetani ni . . .

  •  Kiumbe wa roho?

  •  Alama ya ubaya wenye kuwa ndani ya mutu?

  •  Matokeo ya mawazo ya mutu?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Shetani alizungumuza na Yesu na ‘alimujaribu.’ (Mathayo 4: 1-4) Kwa hiyo, Shetani haiko mutu wa kuwazia tu, na haiko tu alama ya ubaya. Ni kiumbe mubaya wa roho.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Mwanzoni, Shetani alikuwa malaika mutakatifu, lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alifikia kuwa muongo na akamuasi Mungu.

  • Malaika wengine walijiunga naye katika uasi. —Ufunuo 12:9.

  • Shetani anafunga watu wengi macho ili wasijue kama anaishi kabisa.—2 Wakorintho 4:4.

Shetani anaweza kuongoza watu?

WATU FULANI WANASEMA kama kuongozwa na Shetani ni uongo, lakini wengine wanaogopa sana kuingiwa na roho waovu. Wewe unawaza namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

‘Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’ (1 Yohana 5:19) Shetani anaongoza watu wengi, lakini haongoze kila mutu.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Shetani anatumia uongo ili kuongoza watu wengi.—2 Wakorintho 11:14.

  • Katika hali fulani, watu wanaweza kuingiwa na roho waovu.—Mathayo 12:22.

  • Kupitia musaada wa Mungu, unaweza ‘kumupinga Ibilisi [Shetani].’—Yakobo 4:7.