Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Ni jambo gani lenye haliko la kawaida Yesu alifanyia watu wenye ukoma?

Wayahudi wa zamani waliogopa aina fulani ya ukoma wenye ulienea sana wakati wa zamani. Ugonjwa huo mubaya sana ungeweza kuharibu sehemu ya mwisho ya mishipa ya mugonjwa na kufanya umbo ao sura ya mutu huyo iharibike lote. Ugonjwa wa ukoma haukuwa na dawa yenye kujulikana. Lakini, wale wenye walikuwa na ugonjwa huo walitengwa na watu wengine na walilazimishwa kujulisha wengine hali yao.—Mambo ya Walawi 13:45, 46.

Viongozi wa dini ya Kiyahudi walitunga sheria nyingi juu ya ukoma zenye ziliomba kufanya mambo yenye Maandiko hayaseme. Sheria hizo zilifanya maisha ya wenye ukoma yakuwe nguvu bila sababu yoyote. Kwa mufano, sheria za marabi zilikataza mutu yeyote kumukaribia mwenye ukoma kwa urefu wa mikono 4, ni kusema, metre 2 hivi. Lakini, kama kulikuwa upepo, mutu alipaswa kuwa mbali na mwenye ukoma kwa urefu wa mikono 100, ni kusema, metre 45 hivi. Waandikaji fulani wa Talmudi walifasiria kwamba sheria ya Maandiko yenye kuonyesha kwamba watu wenye ukoma waishi ‘inje ya kambi’ inamaanisha kwamba hawapaswe kuishi katika miji yenye kuwa na kuta. Kwa hiyo, wakati rabi mumoja angeona mwenye ukoma ndani ya muji, angemutupia majiwe na kumuambia: “Rudia kwenye nafasi yako ili usichafue watu wengine.”

Lakini, Yesu alitendea wenye ukoma kwa njia tofauti. Kuliko kuwafukuza, alikuwa tayari kuwagusa, na hata kuwaponyesha.—Mathayo 8:3.

Ili viongozi wa dini ya Kiyahudi wakubali mutu avunje ndoa, kulipaswa kuwa sababu gani?

Cheti cha kuvunja ndoa cha tangu mwaka wa 71/72 k.k.y..

Kati ya mwaka wa 1 na 100 kisha kuzaliwa kwa Yesu, viongozi wa dini walibishana juu ya kuvunja ndoa. Kwa mufano, siku moja Mafarisayo fulani walimujaribu Yesu kwa kumuuliza ulizo hili: ‘Je, ni halali mwanaume kumutaliki [ao, kuvunja ndoa] muke wake kwa kila sababu?’—Mathayo 19:3.

Sheria ya Musa ilionyesha kwamba mwanaume angeweza kuvunja ndoa na bibi yake kama ‘alipata kitu fulani kisichofaa katika mwanamuke huyo.’ (Kumbukumbu la Torati 24:1) Katika siku za Yesu, vikundi viwili vya marabi vilikuwa na mawazo tofauti juu ya sheria hiyo. Kikundi kimoja chenye kuitwa Shammai kilifuatilia sheria sana. Kwa hiyo, kilielewa kwamba kulingana na sheria hiyo, sababu moja tu yenye kufaa ili kuvunja ndoa ni “kukosa uaminifu,” ni kusema, uzinifu. Lakini, kikundi cha Hillel, kilionyesha kwamba mwanaume alikuwa na haki ya kuvunja ndoa kwa sababu ya tatizo lolote katika ndoa, hata kama ni tatizo ndogo sana. Kulingana na kikundi cha Hillel, mwanaume angeweza kuvunja ndoa kama bibi yake hakupika chakula muzuri ao kama alipata mwanamuke mwengine mwenye aliona kuwa na sura ya muzuri kuliko ya bibi yake.

Sasa, namna gani Yesu alijibia ulizo la Mafarisayo? Alisema waziwazi hivi: ‘Yeyote anayemutaliki muke wake na kumuoa mwingine, ila kwa sababu ya uasherati, anafanya uzinzi.’—Mathayo 19:6, 9.