Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Jambo la Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini na Biblia

Ni Jambo la Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini na Biblia

WEWE ni Mukristo? Kama jibu ni ndiyo, uko kati ya watu zaidi ya miliare mbili katika dunia, ni kusema, mutu 1 juu ya kila watu 3 mwenye kujiita Mukristo. Leo, kuna maelfu ya vikundi vya dini vyenye kujiita kuwa za Kikristo, lakini mafundisho na mawazo ya vikundi hivyo hayapatane. Kwa hiyo, mambo unaamini yanaweza kuwa tofauti na mambo yenye watu wengine wenye kusema kuwa ni Wakristo wanaamini. Ni jambo la maana kabisa kujua mambo yenye tunaamini? Jibu ni ndiyo kama unataka kufuata Ukristo wenye kufundishwa katika Biblia.

Wanafunzi wa kwanza wa Yesu Kristo walifikia kuitwa “Wakristo.” (Matendo 11:26) Haikuwa lazima wakuwe na majina mengine ya kuwatambulisha, kwa sababu kulikuwa imani moja tu ya Kikristo. Wakristo walifuata kwa umoja mafundisho na mambo yenye Yesu Kristo, mwenye alianzisha Ukristo, aliwaomba wafanye. Kanisa lako linafanya hivyo? Uko hakika kwamba kanisa lako linafundisha mambo Kristo alifundisha na mambo wanafunzi wa kwanza waliamini? Ni jambo gani linaweza kukusaidia ukuwe hakika? Kuna jambo moja tu la kufanya: kutumia Biblia ili kulinganisha mambo yenye unaamini na mambo Biblia inasema.

Fikiria jambo hili: Yesu Kristo aliheshimia sana Maandiko; aliyaona kuwa Neno la Mungu. Yesu hakukubali wale wenye walizarau mafundisho ya Biblia kwa kutia pa nafasi ya kwanza desturi za watu. (Marko 7:9-13) Tunaweza kusema na uhakika wote kwamba mafundisho ya wanafunzi wa kweli wa Yesu yanapaswa kutegemea Biblia. Kwa hiyo, ni muzuri kila Mukristo ajiulize, ‘Mafundisho ya kanisa langu yanapatana na mambo Biblia inasema?’ Ili kujibu ulizo hilo, sababu gani usilinganishe mambo kanisa lako linafundisha na mambo Biblia inasema kabisa?

Yesu alisema kwamba ibada yetu kwa Mungu inapaswa kupatana na kweli, na kweli hiyo inapatikana katika Biblia. (Yohana 4:24; 17:17) Na mutume Paulo alisema kwamba kupata “ujuzi sahihi wa kweli” ni jambo la maana sana ili tupate wokovu. (1 Timotheo 2:4) Kwa hiyo, mambo yenye tunaamini yanapaswa kutegemea kweli sahihi ya Biblia. Ni lazima kufanya hivyo, kwa sababu wokovu wetu uko katika hatari.

NAMNA YA KULINGANISHA MAMBO YENYE TUNAAMINI NA BIBLIA

Tunakualika kusoma maulizo sita yenye kuwa katika habari hii na uone majibu ya Biblia kwa maulizo hayo. Soma maandiko ya Biblia yenye kutajwa, na uwaze sana juu ya majibu ya maulizo hayo. Kisha, ujiulize, ‘Mafundisho ya kanisa langu yanapatana na mambo Biblia inasema?’

Sehemu hii fupi ya maulizo inaweza kukusaidia kufanya jambo la maana sana, ni kusema, kulinganisha mambo unaamini na Biblia. Uko tayari kulinganisha mafundisho mengine ya kanisa lako na mambo Biblia inasema? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia kuchunguza kweli yenye kuwa wazi ya Biblia. Sababu gani usiombe Shahidi mumoja ajifunze na wewe Biblia bila kulipa? Ao unaweza kufungua adresi yetu ya Internete, jw.org.