Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Nilifikia Kuweza Kisha Kushindwa Mara Nyingi

 

Nilifikia kuweza kisha kushindwa mara nyingi

  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1953

  • INCHI: AUSTRALIA

  • ALIKUWA: MUTUMWA WA PORNOGRAFIA

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Katika mwaka wa 1949, baba yangu alitoka katika inchi ya Ujerumani na kuhamia katika inchi ya Australia. Alikuja kutafuta kazi katika kompanyi za umeme na zenye kutafuta majiwe ya bei kali, na aliishi katika muji mudogo wa Victoria. Alioa mama yangu katika muji huo, na nikazaliwa katika mwaka wa 1953.

Kisha miaka kidogo tu, mama yangu alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ndiyo sababu kati ya mambo ya zamani sana yenye nilikumbuka, kulikuwa pia mafundisho ya Biblia. Lakini, baba yangu alichukia dini zote. Alianza kuwa mukali na muchokozi sana, na mama yangu alimuogopa sana. Aliendelea kujifunza Biblia kwa siri na akafikia kupenda mafundisho ya Biblia. Wakati Baba hakuwa pamoja na sisi, mama alizoea kutuambia, mimi na dada yangu, mambo yenye alijifunza katika Biblia. Alituelezea juu ya paradiso duniani ya wakati wenye kuja na furaha yenye tungepata kwa kuishi kulingana na kanuni za Biblia kuhusu mwenendo.—Zaburi 37:10, 29; Isaya 48:17.

Wakati nilikuwa na miaka 18, nililazimika kuondoka nyumbani kwa sababu Baba alikuwa mukali sana. Hata kama niliamini mambo yenye Mama alinifundisha katika Biblia, sikuyaona kuwa ya maana kwangu. Kwa hiyo, nilishindwa kuishi kulingana na mambo yenye nilifundishwa. Nilianza kufanya kazi ya umeme katika mines za makaa ya majiwe (mines de charbon). Nilioa wakati nilikuwa na miaka 20. Kisha miaka tatu, tulizaa mutoto mwanamuke, na nikaanza kufikiria tena mambo ya maana katika maisha yangu. Nilijua kwamba Biblia ingesaidia familia yetu, kwa hiyo nilianza tena kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Lakini, bibi yangu alipinga sana Mashahidi wa Yehova. Wakati nilifika kwenye mukutano wao mumoja, alinipatia angalisho. Alisema nichague kati ya kuacha kujifunza Biblia ao kuacha familia. Kwa sababu nilikosa la kufanya, nilikubali jambo lenye aliniomba na nikavunja urafiki wote na Mashahidi. Lakini, nilifikia kuhuzunika sababu gani nilishindwa kufuata mambo yenye nilijua kwamba ni ya kweli.

Siku moja, mufanyakazi mwenzangu alinionyesha pornografia. Ilikuwa yenye kuvutia na yenye kuchukiza, na ilifanya nijisikie kuwa mwenye makosa sana. Kukumbuka mambo yenye nilijifunza katika Biblia, kulinifanya niamini kabisa kwamba Mungu angenipatia malipizi. Kwa sababu niliendelea kuangalia picha za mubaya sana, nilianza kuona pornografia kuwa ya muzuri. Kisha, nikakuwa mutumwa wa pornografia.

Kwa miaka 20 yenye ilifuata, niliendelea kutenda zaidi na zaidi tofauti na kanuni zenye mama yangu alijaribu kunifundisha. Tabia yangu ilifanana na mambo yenye nilikuwa ninatia katika akili yangu. Nilitumia maneno machafu, na nilifurahia mizaha yenye kuzungumuzia mambo ya uasherati. Nilianza kuwa na mawazo yenye hayafae juu ya kitendo cha ndoa. Hata kama niliendelea kuishi na bibi yangu, nilikuwa ninatoka na wanawake wengine. Siku moja nilijiangalia katika kioo na kujiambia hivi katika akili: ‘Sikupendi.’ Kuliko kujiheshimia, nilianza kujichukia sana.

Ndoa yangu ilifikia kuvunjika, na maisha yangu yakaharibika sana. Kisha nilisali kwa Yehova kwa moyo wangu wote. Nilianza tena kujifunza Biblia, hata kama nilikuwa nimefanya miaka makumi mbili hivi bila kujifunza. Wakati huo, baba yangu alikuwa amekufa, na mama yangu alikuwa amebatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Kulikuwa tofauti kubwa sana kati ya mambo yenye nilifanya na kanuni za juu za Biblia. Lakini, wakati huo, niliamua kufanya nguvu yangu yote ili kupata amani ya akili yenye Biblia inaahidi. Nilianza kutumia maneno yenye kuwa safi na kuzuia hasira yangu. Niliamua pia kuacha mwenendo wangu muchafu, michezo ya feza, kunywa pombe kupita kipimo, na niliacha kumuiba mukubwa wangu wa kazi.

Wafanyakazi wenzangu hawakuelewa sababu gani nilitaka kufanya mabadiliko hayo makubwa. Kwa miaka tatu waliendelea kunijaribu ili nirudilie mwenendo wangu wa zamani. Wakati nilikosea hata kidogo tu, kama vile kuonyesha hasira ao kusema neno la mubaya, walisema kwa sauti kubwa ya ushindi: “Aha! Josef wa zamani amerudia tena.” Maneno hayo yaliniumiza kabisa! Mara nyingi nilijiona wa bure.

Kwenye nilitumikia, watu waliona sana pornografia, ikuwe kwa njia ya kielektroniki ao katika vitabu vyenye kuchapishwa. Wafanyakazi wenzangu walizoea kupatiana picha chafu sana kupitia ordinatere zao, kama vile nilikuwa ninafanya zamani. Nilijikaza kuepuka pornografia, lakini inaonekana walikuwa na kusudi la kunifanya nishindwe. Niliomba mutu mwenye alikuwa ananifundisha Biblia anisaidie na kunitia moyo. Wakati nilikuwa ninamuambia mambo yote yenye kuwa katika moyo wangu, alinisikiliza kwa uvumilivu. Alitumia maandiko fulani ya Biblia ili kunionyesha namna ninaweza kupiganisha mwenendo wangu, na alinitia moyo niendelee kutafuta musaada wa Yehova kupitia sala.—Zaburi 119:37.

Siku moja, niliita wafanyakazi wenzangu. Wakati walifika, niliwaambia wapatie pombe watu wawili kati ya wale wenye walisema waziwazi kama wanakunywa pombe kupita kipimo. Wote walikataa kwa sauti kubwa: “Haiwezekane! Wanaume hawa wanapiganisha hali yao ya kuwa watumwa wa pombe!” Niliwajibia: “Ndiyo, na mimi ni hivyo.” Kuanzia siku hiyo, walielewa kwamba nilikuwa ninapiganisha hali yangu ya kuwa mutumwa wa pornografia, na hawakunikaza tena ili nirudilie mwenendo wangu wa zamani.

Kwa musaada wa Yehova, nilifikia kuweza kuachana na utumwa wa pornografia. Katika mwaka wa 1999, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Nilifanya hivyo ili kuonyesha Yehova shukrani ya kupata tena nafasi ya kuishi maisha yenye heshima na furaha.

Sasa, ninaelewa sababu gani Yehova anachukia mambo yenye nilipenda kwa muda murefu. Kwa sababu yeye ni Baba mwenye upendo, alipenda kunilinda na hatari yenye pornografia inaleta. Maneno ya Methali 3:5, 6 ni ya kweli kabisa! Andiko hilo linasema hivi: ‘Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.’ Kanuni za Biblia hazinilinde tu, lakini pia zinanisaidia ili maisha yangu yakuwe muzuri.—Zaburi 1:1-3.

FAIDA YENYE NIMEPATA:

Zamani, nilijichukia sana, lakini sasa ninajiheshimia na niko na amani ya moyo. Ninaishi maisha safi na ninajisikia kwamba Yehova amenisamehe na kwamba ananitegemeza. Katika mwaka wa 2000, nilioa dada Karolin, Mukristo mwenye sura ya muzuri na mwenye kumupenda Yehova. Katika nyumba yetu kuko amani. Tunaona kwamba ni pendeleo kubwa kuwa katika familia safi ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada wenye upendo.