Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | TUNAWEZA KUPATA KITULIZO WAPI?

Sisi Wote Tuko na Lazima ya Kitulizo

Sisi Wote Tuko na Lazima ya Kitulizo

Unakumbuka namna ulianguka wakati ulikuwa mutoto? Pengine ulijiumiza kwenye mukono ao kujikwaruza kwenye goti. Unakumbuka namna mama yako alikufariji ao kukutuliza? Pengine alisafisha kidonda chako na kukifunga kwa kitambaa. Ulilia, lakini kupitia maneno yake yenye kutuliza na namna alikukumbatia ulijisikia muzuri zaidi. Wakati huo, ulipata kitulizo kabisa.

Lakini, maisha yanakuwa nguvu zaidi wakati tunaendelea kukomaa. Magumu yanakuwa makubwa zaidi, na inakuwa nguvu zaidi kupata kitulizo. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, magumu yenye watu wakubwa wanapata, mara nyingi hayaishe kupitia kukumbatiwa ao kwa kufungwa kitambaa. Tuzungumuzie mifano fulani.

  • Umekwisha kupata huzuni kwa sababu ya kupoteza kazi yako? Julian anasema kwamba wakati alifukuzwa kwenye kazi, jambo hilo lilimuhangaisha sana. Alijiuliza: ‘Namna gani nitatunza familia yangu? Kisha kutumika kwa miaka mingi kwa nguvu yangu yote, sababu gani kompanyi hii inawaza kwamba sina faida?’

  • Pengine unahangaika sana kwa sababu ndoa yako imevunjika. Raquel anasema hivi: “Wakati bwana yangu aliniacha bila kuwazia, kumepita miezi 18, nilijisikia mubaya sana. Ilikuwa kama moyo wangu umevunjika vipande viwili. Niliumia kimwili na nilijisikia mubaya katika moyo. Jambo hilo liliniogopesha sana.”

  • Pengine uko na matatizo makubwa ya afya; na hauone kabisa alama yenye kuonyesha kwamba kutakuwa mabadiliko. Inawezakana wakati fulani unajisikia kama vile Ayubu. Alisema hivi kwa huzuni: “Ninachukia uzima wangu, sitaki kuishi siku zote.” (Ayubu 7:16, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Pengine unajisikia kama vile Luis, mwanaume wa miaka 80 hivi. Alisema hivi: “Wakati fulani, ninajisikia tu kama ninangojea kifo.”

  • Ao pengine kifo cha mutu mwenye unapenda kinakufanya ukuwe na lazima ya kupata kitulizo. Robert anasema hivi: “Wakati mutoto wangu alikufa katika aksidenti ya avion, kwanza sikuamini jambo hilo. Kisha nilisikia maumivu, maumivu yenye Biblia inalinganisha na upanga murefu wenye kupita ndani ya mutu.”—Luka 2:35.

Robert, Luis, Raquel, na Julian walipata kitulizo hata kama walikuwa katika hali hizo zenye kuleta huzuni. Walipata Mutu wa kuwatolea kitulizo hicho chenye walikuwa nacho lazima. Mutu huyo ni Mungu Mweza-Yote. Namna gani Mungu anatolea watu kitulizo? Atakupatia pia kitulizo chenye uko nacho lazima?