Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | TUNAWEZA KUPATA KITULIZO WAPI?

Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo

Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo

Mutume Paulo anasema kwamba Yehova * ni ‘Mungu wa faraja [ao, kitulizo] yote ambaye anatufariji katika ziki yetu yote.’ (2 Wakorintho 1:3, 4) Kwa hiyo, Biblia inatuhakikishia kwamba hakuna mutu mwenye Yehova anaweza kushindwa kusaidia na kwamba hakuna musiba wenye unaweza kufanya Baba yetu wa mbinguni ashindwe kutoa kitulizo.

Lakini, tunapaswa kufanya jambo fulani kama tunapenda Mungu atutolee kitulizo. Namna gani munganga anaweza kutusaidia kama hatukupatana kuonana naye? Nabii Amosi aliuliza hivi: “Je, watu wawili watatembea pamoja isipokuwa wawe wamekutana kwa mapatano?” (Amosi 3:3) Kwa hiyo, Maandiko yanatutia moyo hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.

Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atatukaribia? Kwanza, kwa sababu anatuambia kila mara kwamba anapenda kutusaidia. (Ona  kisanduku chenye kuwa katika habari hii.) Pili, kwa sababu tuko na ushuhuda wenye kusadikisha wa watu wa kweli kabisa wenye Mungu alitolea kitulizo. Kati ya watu hao, kuna watu wa zamani na wa wakati wetu.

Mufalme Daudi alipata magumu mengi kama vile watu wengi wenye kutafuta musaada kutoka kwa Yehova leo. Wakati fulani alimuomba Yehova hivi: “Uisikie sauti ya kusihi kwangu ninapokulilia unisaidie.” Yehova alimusaidia? Ndiyo. Daudi alisema tena hivi: “Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu unashangilia.”—Zaburi 28:2, 7.

DARAKA LA YESU KATIKA KUTOLEA KITULIZO WATU WOTE WENYE KUOMBOLEZA

Mungu alikamata mipango ili Yesu akuwe na daraka kubwa katika kutolea watu kitulizo. Kati ya mambo yenye Mungu alimuomba afanye, Yesu alipaswa “kufunga majeraha [ao, vidonda] ya waliovunjika moyo” na “kuwafariji wote wanaoomboleza.” (Isaya 61:1, 2) Kama vile Maandiko yalionyesha zamani, Yesu alihangaikia sana watu wenye walikuwa ‘wanataabika [ao, kusumbuka] na kulemewa na mizigo.’—Mathayo 11:28-30.

Yesu alitolea watu kitulizo kwa kuwatolea mashauri yenye hekima, kwa kuwatendea kwa wema, na hata, katika hali fulani, kwa kuponyesha magonjwa yao. Siku moja mutu mwenye ukoma alimuomba Yesu hivi: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” Kwa sababu ya kumusikilia huruma, Yesu alimujibu hivi: “Ninataka. Takasika.” (Marko 1:40, 41) Na mutu mwenye ukoma akapona.

Leo, Mwana wa Mungu haiko hapa duniani ili kutolea watu kitulizo moja kwa moja. Lakini Yehova, Baba yake, “Mungu wa faraja yote,” anaendelea kusaidia wote wenye kuwa na lazima ya kitulizo. (2 Wakorintho 1:3) Tuone njia ine kubwa zenye Mungu anatumia ili kutolea watu kitulizo.

  • Biblia. ‘Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tukuwe na tumaini.’—Waroma 15:4.

  • Roho Takatifu ya Mungu. Muda kidogo tu kisha Yesu kufa, kutaniko lote la Kikristo liliingia katika kipindi cha amani. Sababu gani? Kwa sababu ‘lilitembea katika kumuogopa Yehova na katika faraja ya roho takatifu.’ (Matendo 9:31) Roho takatifu, ni kusema, nguvu yenye Mungu anatumia ili kutenda, ni yenye nguvu sana. Mungu anaweza kuitumia ili kumutolea kitulizo mutu yeyote katika hali yoyote.

  • Sala. Biblia inatushauria hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote.’ Kuliko kuhangaika, inasema, ‘maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.’—Wafilipi 4:6, 7.

  • Wakristo Wenzetu wanaweza kuwa marafiki wa kweli wenye tunaweza kutegemea ili kupata kitulizo wakati wa magumu. Mutume Paulo alisema kwamba Wakristo wenzake ni ‘musaada wenye kutia nguvu’ wakati wa ‘uhitaji na ziki.’—Wakolosai 4:11; 1 Wathesalonike 3:7.

Lakini unaweza kujiuliza namna gani mambo hayo yote yanawezekana kabisa. Tuzungumuzie sasa watu wenye walikutana na mambo yenye kuwa katika habari ya kwanza. Kama watu hao, utaona kwamba Mungu anatimiza ahadi yake hii yenye kutia moyo: ‘Kama vile mutu ambaye mama yake mwenyewe anaendelea kumufariji, ndivyo mimi nitakavyoendelea kuwafariji ninyi.’—Isaya 66:13.

^ fu. 3 Biblia inaonyesha kama jina la Mungu ni Yehova.