Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Bonde la Ela

Habari Juu ya Daudi na Goliathi—Ni ya Kweli Kabisa?

Habari Juu ya Daudi na Goliathi—Ni ya Kweli Kabisa?

Watu fulani wanajiuliza kama habari juu ya Daudi na Goliathi ni ya kweli ao ya kuwazia tu. Wewe pia ulikuwa na mashaka wakati ulikuwa unasoma habari yenye kutangulia? Kama ni hivyo, acha tufikirie maulizo tatu yenye kufuata.

1 | Inawezekana kabisa mutu akuwe na urefu wa metre 2,9 hivi?

Biblia inasema kwamba urefu wa Goliathi “ulikuwa mikono sita na shubiri moja.” (1 Samweli 17:4) Urefu wa mukono moja wenye kuzungumuziwa katika andiko hilo ulikuwa santimetre 44,5; urefu wa shubiri moja ulikuwa santimetre 22,2. Yote pamoja inaleta urefu wa karibu metre 2,9. Watu fulani wanasema kwamba Goliathi hakuwa na urefu huo, lakini fikiria jambo hili: Mwanaume murefu zaidi duniani wa wakati wetu alikuwa na urefu zaidi ya metre 2,7. Ni vigumu kabisa kusema kwamba Goliathi alimupita santimetre 15 ao zaidi? Goliathi alikuwa wa kabila la Refaimu, watu wenye walijulikana kuwa na urefu wenye hauko wa kawaida. Maandishi fulani ya Misri ya kipindi kati ya miaka ya 1300 na 1201 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu yanaonyesha kwamba wapiganaji wenye kuogopesha sana katika eneo la Kanaani walikuwa na urefu zaidi ya metre 2,4. Kwa hiyo, hata kama urefu wa Goliathi hauko wa kawaida, inawezekana kabisa alikuwa na urefu huo.

2 | Daudi alikuwa mutu wa kuwazia tu?

Wakati fulani, watu wenye elimu walijaribu kuonyesha kwamba Mufalme Daudi alikuwa mutu wa kuwazia tu, lakini jambo hilo halikuwezekana. Wachunguzi wa vitu vya zamani walipata nafasi kwenye kuandikwa “nyumba ya Daudi.” Zaidi ya hilo, Yesu Kristo alionyesha kwamba Daudi hakuwa mutu wa kuwazia tu. (Mathayo 12:3; 22:43-45) Kujulikana kwa Yesu kuwa Masiya kunaungwa mukono na liste mbili za vizazi zenye kuonyesha wazi kwamba alitoka katika kizazi cha Daudi. (Mathayo 1:6-16; Luka 3:23-31) Ni wazi kwamba Daudi hakuwa mutu wa kuwazia tu.

3 | Mambo yenye kuzungumuziwa katika habari ya Daudi na Goliathi yalifanyika kwenye nafasi ya kweli kabisa?

Biblia inasema kwamba vita hiyo ilifanyika katika Bonde la Ela. Lakini inasema kwa njia yenye kuwa wazi zaidi, kwa kuonyesha kwamba Wafilisti walipiga kambi kwenye kilima fulani katikati ya miji mbili, Soko na Azeka. Waisraeli walikuwa karibu na bonde kwenye kilima kingine. Hizo zilikuwa nafasi za kuwazia tu?

Tuone mambo yenye mutu mumoja mwenye alitembelea eneo hilo hivi karibuni anasema: “Kiongozi wetu, mwenye hakuwa mutu wa dini, alitupeleka katika Bonde la Ela. Tulipita katika njia yenye ilitupeleka juu ya kilima fulani. Wakati tulikuwa tunaangalia katika bonde, alituambia tusome andiko la 1 Samweli 17:1-3. Kisha, alionyesha katika bonde na kusema: ‘Mabomoko ya muji wa Soko yako kule, kwenye mukono wenu wa kushoto.’ Wakati aligeuka, alisema, ‘Mabomoko ya muji wa Azeka yako kule, kwenye mukono wenu wa kuume. Wafilisti walipiga kambi katikati ya miji hiyo mbili, nafasi fulani kwenye kilima chenye kuwa mbele yenu. Inawezekana tunasimama nafasi kwenye Waisraeli walipiga kambi.’ Nilifikiria namna Sauli na Daudi walikuwa wanasimama nafasi kwenye nilikuwa. Kisha tulishuka katika bonde na kuvuka nafasi kwenye kulikuwa kunapita muto. Nafasi hiyo ilikuwa inakauka sana na ilikuwa inajaa majiwe mengi. Nilifikiria tu namna Daudi alikuwa anainama ili kuokota majiwe tano mazuri. Daudi alitumia moja kati ya majiwe hayo ili kumuua Goliathi.” Kama vile watu wengine wengi, mutu huyo mwenye alitembelea eneo hilo alishangaa sana kuona kwamba habari ya Biblia juu ya Daudi na Goliathi ni ya kweli.

Hakuna sababu yoyote yenye kutufanya tukuwe na mashaka juu ya habari hiyo ya Biblia. Inazungumuzia watu wenye waliishi kabisa, na nafasi za kweli kabisa. Na jambo la maana zaidi, habari hiyo ni sehemu ya Neno la Mungu lenye kuongozwa na roho yake. Kwa hiyo, habari hiyo inatoka kwa Mungu wa kweli, Mungu “asiyeweza kusema uwongo.”—Tito 1:2; 2 Timotheo 3:16.