Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Inasema ni Nini?

Biblia Inasema ni Nini?

Ufalme wa Mungu ni nini?

BAADHI YA WATU HUSEMA kwamba Ufalme wa Mungu upo moyoni; wengine wanafikiri kwamba ni jitihada za wanadamu za kuleta ulimwengu wenye amani na undugu. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. . . . Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [za wanadamu].” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu ni serikali halisi.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Ufalme wa Mungu utakuja lini?

UNGEJIBUJE?

  • Hakuna anayejua

  • Hivi karibuni

  • Hautakuja kamwe

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Baada ya habari njema kuhubiriwa kikamili, Ufalme huo utakuja na kukomesha mfumo huu mwovu.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?

  • Hakuna hata mtu mmoja duniani anayejua kikamili wakati ambao Ufalme wa Mungu utakuja.—Mathayo 24:36.

  • Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba Ufalme huo utakuja hivi karibuni.—Mathayo 24:3, 7, 12.