Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Ufalme wa Mungu ni nini?

WATU FULANI WANAAMINI kama unamaanisha utawala wa Mungu wenye kuwa ndani ya moyo wa mutu; wengine wanawaza kama ni matokeo ya nguvu za wanadamu za kuleta amani na umoja katika dunia. Wewe unawaza namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. . . . Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [za wanadamu].” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli kabisa.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

Ufalme wa Mungu utakuja wakati gani?

UNAWEZA KUJIBU NINI?

  • Hakuna mutu mwenye anajua

  • Hivi karibuni

  • Hautakuja hata siku moja

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Kisha habari njema kuhubiriwa kabisa, Ufalme wa Mungu utakuja kuharibu ulimwengu huu muovu.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Hakuna mutu duniani mwenye anajua kabisa wakati Ufalme wa Mungu utakuja.—Mathayo 24:36.

  • Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba Ufalme utakuja hivi karibuni.—Mathayo 24:3, 7, 12.