Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tai

Mambo Yenye Tunajifunza Kupitia Ndege wa Mbinguni

Mambo Yenye Tunajifunza Kupitia Ndege wa Mbinguni

‘Tafazali uliza, . . . viumbe vya mbinguni vyenye mabawa, navyo vitakuambia. Ni nani kati ya hao wote ambaye hajui vema kwamba ni mukono wa Yehova ambao umefanya haya?’—Ayubu 12:7, 9.

ZAIDI ya miaka 3 000 yenye imepita, Ayubu alifikia kuona kama ndege wa mbinguni wanaweza kutufundisha mambo mengi kuhusu vitu vyenye Mungu aliumba. Lakini pia tabia zao zinafanya watumiwe sana katika mifano na katika kulinganisha mambo. Katika Biblia, mara nyingi ndege wanatumiwa ili kutupatia somo nzuri kuhusu maisha na kuhusu urafiki wetu pamoja na Mungu. Acha tuone mifano fulani.

NAFASI KWENYE MBAYUWAYU WANAJENGA NYUMBA ZAO

Mbayuwayu

Wakaaji wa muji wa Yerusalemu walijua muzuri mbayuwayu, wenye walizoea kujenga nyumba zao chini ya paa za majengo. Mbayuwayu fulani walijenga nyumba zao katika hekalu la Sulemani. Pengine, mbayuwayu wenye walijenga katika hekalu kila mwaka waliona nafasi hiyo kuwa salama, kwenye wangeweza kukomalisha watoto wao bila kusumbuliwa.

Muandikaji wa Zaburi ya 84, ambaye ni mumoja kati ya watoto wa Kora, mwenye alitumikia kwenye hekalu juma moja kila miezi sita, aliona nyumba hizo katika hekalu. Kwa sababu alipenda kuwa kama mbayuwayu hao wenye walikuwa kila mara katika nyumba ya Yehova, alisema hivi: ‘Jinsi ilivyo nzuri maskani yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi! Nafsi yangu imetamani sana na pia imezoofika kwa kutamani nyua za Yehova. Hata ndege amepata nyumba, na mbayuwayu amepata kiota [ao, nyumba] chake, ambapo ameweka vifaranga [ao, vitoto] vyake​—⁠Mazabahu yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi, Mufalme wangu na Mungu wangu!’ (Zaburi 84:1-3) Sisi na watoto wetu, tunaonyesha kama tuko na tamaa hiyo ya kuwa pamoja na kutaniko la watu wa Mungu kwa ukawaida?—Zaburi 26:8,12.

KORONGO ANAJUA WAKATI WAKE

Nabii Yeremia aliandika hivi: “Korongo juu mbinguni anajua vema nyakati zake.” Hakuna shaka kwamba alijua muzuri namna korongo walikuwa wanahama kupitia Inchi ya Ahadi. Wakati wa kuchipuka kwa majani, zaidi ya korongo 300 000 wenye rangi ya mweupe wanahama kutoka Afrika kuenda Ulaya ya Kaskazini kwa kupitia Bonde la Yordani. Saa yao ya asili inawachochea kuwa na tamaa ya kurudi mahali pao pa kuzaana katika kipindi cha joto. Kama ndege wengine wenye kuhama, ‘wanaangalia vema wakati wa kila mumoja wao kuingia.’—Yeremia 8:⁠7.

Kitabu kimoja kinasema hivi: “Jambo lenye kushangaza kuhusu kuhama ni kwamba kunachochewa na hekima ya kisilika.” (Atlas Des Oiseaux Migrateurs) Yehova Mungu alipatia ndege wenye kuhama hekima ya kisilika ya kujua wakati wa kuhama, lakini alipatia wanadamu uwezo wa kutambua wakati na nyakati. (Luka 12:54-56) Tofauti na hekima ya kisilika ya korongo, ujuzi wa Mungu ndilo jambo lenye linaweza kusaidia mutu atambue maana ya mambo yenye kutokea leo. Waisraeli wa wakati wa Yeremia hawakutambua maana ya mambo yenye yalikuwa yanatokea wakati wao. Mungu alionyesha ni nini ilitokeza jambo hilo kwa kusema hivi: “Wamelikataa neno la Yehova, nao wana hekima gani?”—Yeremia 8:9.

Leo, tuko na ushuhuda mwingi wenye kuonyesha kama tunaishi katika wakati wenye Biblia inaita “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5) Utafuata mufano wa korongo na kutambua “nyakati”?

TAI ANATAZAMA MBALI SANA

Tai

Tai anatajwa mara nyingi katika Biblia. Katika eneo lenye Biblia inaita Inchi ya Ahadi, ni kawaida kuona na kutambua ndege hao hata kama wako mbali. Biblia inasema kama akiwa kwenye mwamba juu kabisa, tai ‘anatafuta chakula; macho yake yanaendelea kutazama [ao, kuona] mbali sana.’ (Ayubu 39:27-29) Tai iko na uwezo mukubwa sana wa kuona mbali. Inasemekana kama anaweza kuona sungura mwenye kuwa kwenye kilometre moja.

Kama vile tai anaweza “kutazama mbali sana,” Yehova anaweza kuona mambo yenye yatatokea wakati wenye kuja. Kwa hiyo, Yehova Mungu alisema hivi: “Yeye anayetangaza tangu mwanzo ule mwisho, na kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.” (Isaya 46:10) Kama tunasikiliza mashauri ya Yehova, tunaweza kupata faida kutokana na hekima yake yenye haina mipaka na uwezo wake wa kuona mambo ya wakati wenye kuja.—Isaya 48:7, 18.

Biblia inalinganisha watu wenye kumutumainia Mungu na tai. Inasema hivi: ‘Wale wanaomutumaini Yehova watapata nguvu mupya. Wataruka juu kwa mabawa kama tai.’ (Isaya 40:31) Tai anaruka kwa kutumia hewa yenye joto ambayo inapanda. Wakati tai anatambua kwenye kuwa hewa yenye joto, anatandaza mabawa yake na anazunguka katika hewa hiyo, na inamupandisha juu zaidi. Tai hatumainie nguvu yake ili kuruka mbali sana. Vilevile, wale wenye kumutumainia Yehova wanaweza kumutegemea kwa sababu anaahidi kuwapatia “nguvu zinazopita zile za kawaida.”—2 Wakorintho 4:7,8.

‘KAMA VILE KUKU ANAKUSANYA VIFARANGA VYAKE’

Kuku na vitoto vyake

Muda mufupi mbele ya kifo chake, Yesu alichukua muda fulani ili kuangalia jiji kubwa la Wayahudi. Kwa huzuni alisema hivi: ‘Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na ambaye huwapiga kwa majiwe wale waliotumwa kwake, ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka.’—Mathayo 23:37.

Kati ya uwezo wa kisilika wenye nguvu sana wa ndege, kuko tamaa ya kulinda vitoto vyao. Ndege wenye kutagia mahali fulani kwenye udongo, kama vile kuku, wanapaswa kuwa macho sana ili kuepuka hatari. Kama kuku anaona ndege mwenye kuitwa mwewe (ao, kibeba-kuku) anazunguka-zunguka juu, kuku huyo anatoa mulio fulani wa kuonyesha hatari, na kisha kusikia mulio huo, vitoto vyake vyote vinakimbilia chini ya mabawa yake ili kuwa salama. Tena, chini ya mabawa hayo, vitoto hivyo vinaweza kupata ulinzi wakati wa jua kali ao mvua nyingi. Yesu pia alipenda kutolea wakaaji wa Yerusalemu ulinzi wa kiroho. Leo, Yesu anatualika tukuje kwake ili atutolee ulinzi na musaada wa kupiganisha magumu na mahangaiko yetu ya kila siku.—Mathayo 11:28,29.

Kwa kweli, kuko mambo mengi yenye tunaweza kujifunza kupitia viumbe hivyo vyenye mabawa. Wakati unachunguza tabia zao, jaribu kukumbuka ulinganisho mbalimbali wa Maandiko wenye kuzungumuzia viumbe hivyo. Mbayuwayu akusaidie upendezwe na nyumba ya Yehova ya ibada. Uendelee kumutegemea Mungu ili akupatie tumaini lenye litakusaidia kuruka juu kama tai. Ukuje kwa Yesu ili upate kweli ya kiroho yenye itakulinda kama vile kuku analinda vitoto vyake. Na korongo akusaidie uendelee kubakia macho ili kutambua maana ya mambo yenye kutokea leo.