Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hangaikia Hali Yako ya Kiroho Wakati Unatumikia Katika Kutaniko la Luga ya Kigeni

Hangaikia Hali Yako ya Kiroho Wakati Unatumikia Katika Kutaniko la Luga ya Kigeni

“Moyoni mwangu nimeweka hazina ya [nimechunga kwa uangalifu] maneno yako.”​—ZABURI 119:11.

NYIMBO: 14292

UTAJIBU NAMNA GANI?

Ni nini ilisaidia Danieli na muandikaji wa Zaburi ya 119 waendelee kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova?

Ndugu na dada wenye kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni wanaweza kufanya nini ili waendelee kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova?

Namna gani wazazi wanaweza kuzoeza watoto wao ili wakuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova?

1-3. (a) Ni mambo gani tunapaswa kutia sikuzote pa nafasi ya kwanza katika maisha? (b) Wale wenye kujifunza luga ingine wako na magumu gani ya pekee, na hilo linatokeza maulizo gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

LEO, Mashahidi wengi wa Yehova wanatumika kwa bidii ili kutimiza unabii wa kuhubiri ‘kwa kila taifa na kabila na luga na watu.’ (Ufunuo 14:6) Uko kati ya wale wenye wanajifunza luga ingine? Ndugu na dada fulani ni wamisionere ao wanahubiri mahali kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri katika inchi ingine. Wengine wameanza kuenda kwenye mikutano katika kutaniko fulani la luga ya kigeni lenye kuwa katika inchi yao.

2 Watumishi wote wa Mungu wanapaswa kutia hali yao ya kiroho na ya watu wa familia yao pa nafasi ya kwanza katika maisha. (Mathayo 5:3) Hata hivyo, wakati fulani, inaweza kuwa vigumu kupata wakati wa kufanya muzuri zaidi funzo letu la pekee, kwa sababu tuko na mambo mengi ya kufanya. Lakini wale wenye kuwa katika kutaniko la luga ya kigeni wako na magumu mengine.

3 Wale wenye kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni wanapaswa kujifunza luga ingine, lakini pia wanapaswa kuhakikisha kama wanajifunza kwa ukawaida mambo mazito ya Mungu. (1 Wakorintho 2:10) Namna gani wanaweza kufanya hivyo ikiwa hawaelewe muzuri mambo yenye yanafundishwa katika kutaniko? Na sababu gani wazazi Wakristo wenye kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni wanapaswa kuhakikisha kama kweli inagusa mioyo wa watoto wao?

URAFIKI WETU PAMOJA NA YEHOVA UNAWEZA KUWA KATIKA HATARI

4. Ni nini inaweza kutia urafiki wetu pamoja na Yehova katika hatari? Toa mufano.

4 Ikiwa hatuelewe mafundisho ya Biblia katika luga fulani ya kigeni, hilo linaweza kutia kabisa urafiki wetu pamoja na Yehova katika hatari. Wakati Nehemia alirudia Yerusalemu, alitambua kama watoto fulani hawakuweza kusema luga la Kiebrania. (Soma Nehemia 13:23, 24.) Kwa sababu watoto hao hawakuweza kuelewa Neno la Mungu, urafiki wao pamoja na Yehova ulikuwa zaifu.​—Nehemia 8:2, 8.

5, 6. Wazazi fulani wenye kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni wametambua nini, na ni nini inaleta tatizo hilo?

5 Wazazi fulani Wakristo wenye kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni, wametambua kama urafiki wa watoto wao pamoja na Yehova umekuwa zaifu. Kwa sababu watoto wao hawaelewe muzuri mambo yenye yanafundishwa kwenye mikutano, mafundisho hayo hayawachochee kutenda. Pedro, mwenye alitoka Amerika Kusini na kuhamia Australia pamoja na familia yake, anasema hivi: “Mambo ya kiroho yanapaswa kugusa moyo na mawazo ya ndani.” [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.)​—Luka 24:32.

6 Wakati tunasoma habari fulani katika luga ingine, haiwezi kabisa kutugusa moyo kama vile ingetugusa moyo katika luga yetu. Pia, kwa sababu ni vigumu kuzungumuza katika luga ingine, hilo linaweza kutuchokesha sana na kuwa na matokeo ya mubaya juu ya ibada yetu kwa Yehova. Kwa hiyo, wakati tunaendelea kutia nguvu tamaa yetu ya kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni, tunapaswa pia kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova.​—Mathayo 4:4.

WALILINDA URAFIKI WAO PAMOJA NA YEHOVA

7. Namna gani Wababiloni walijaribu kulazimisha Danieli akubali desturi na dini yao?

7 Wakati Danieli na marafiki wake walipelekwa Babiloni, Wababiloni walijaribu kuwalazimisha wakubali desturi na dini yao. Namna gani? Waliwafundisha ‘luga ya Wakaldayo’ na wakawapatia majina ya Wababiloni. (Danieli 1:3-7) Jina lenye Danieli alipewa lilitokana na Beli, mungu mukubwa katika Babiloni. Kwa hiyo, inawezekana Mufalme Nebukadneza alipenda kufanya Danieli aamini kama mungu wa Babiloni alikuwa mwenye nguvu sana kuliko Yehova, Mungu wa Danieli.​—Danieli 4:8.

8. Danieli alifanya nini ili aendelee kutia nguvu urafiki wake pamoja na Yehova?

8 Katika Babiloni, Danieli alipewa vyakula vitamu vya mufalme. Lakini “aliazimia moyoni mwake” kama ataendelea kutii sheria ya Mungu. (Danieli 1:8) Kwa sababu aliendelea kujifunza “vitabu” vitakatifu, vyenye vilikuwa katika luga ya Kiebrania, aliendelea kutia nguvu urafiki wake pamoja na Yehova wakati alikuwa anaishi katika inchi ya kigeni. (Danieli 9:2) Kwa kweli, miaka karibu 70 kisha kuenda Babiloni, aliendelea kujulikana kwa jina lake la Kiebrania, Danieli.​—Danieli 5:13.

9. Muandikaji wa Zaburi ya 119 alikuwa na mawazo gani juu ya Neno la Mungu?

9 Mufano mwengine ni muandikaji wa Zaburi ya 119. Alipaswa kuvumilia wakati watu wa makao ya mufalme walikuwa wanasema mubaya juu yake. Lakini Neno la Mungu lilimutia nguvu, na jambo hilo lilimusaidia akuwe tofauti na wengine. (Zaburi 119:23, 61) Aliacha Neno la Mungu liguse kabisa moyo wake.​—Soma Zaburi 119:11, 46.

ENDELEA KUTIA NGUVU URAFIKI WAKO PAMOJA NA YEHOVA

10, 11. (a) Tunapaswa kuwa na kusudi gani wakati tunajifunza Neno la Mungu? (b) Namna gani tunaweza kutimiza kusudi letu? Toa mufano.

10 Hata kama tunaweza kuwa na mambo mengi ya kufanya katika kutaniko na kwenye kazi yetu, sisi wote tunapaswa kujipangia wakati wa kufanya funzo la pekee na ibada ya familia. (Waefeso 5:15, 16) Kusudi letu halipaswe kuwa tu kusoma habari nyingi ao kutayarisha maelezo ya kutoa kwenye mukutano. Kusudi letu linapaswa kuwa kuacha Neno la Mungu liguse moyo wetu na kutia nguvu imani yetu.

11 Ili kutimiza kusudi hilo, tunapaswa kuwa na usawaziko. Wakati tunajifunza, hatupaswe tu kufikiria mahitaji ya kiroho ya wengine, lakini tunapaswa kufikiria pia mahitaji yetu wenyewe ya kiroho. (Wafilipi 1:9, 10) Tunapaswa kujua kama wakati tunajitayarisha kwa ajili ya kazi ya kuhubiri, kwa ajili ya mikutano, ao wakati tunatayarisha hotuba fulani, hilo halimaanishe kama tutatumikisha kabisa-kabisa mambo yenye tunasoma. Kwa mufano, mutu mwenye kupika chakula katika restora anapaswa kuonja chakula hicho mbele ya kukipatia watu, lakini hawezi kuishi tu kwa chakula hicho cha kuonja. Ikiwa anapenda aendelee kuwa na afya ya muzuri, anapaswa kujipikia kwa ukawaida chakula chenye kujenga mwili. Vilevile, ikiwa tunapenda kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova, tunapaswa kujifunza Biblia kwa ukawaida. Kufanya hivyo kwa uangalifu kunatusaidia kutimiza mahitaji yetu wenyewe ya kiroho.

12, 13. Sababu gani ndugu na dada wengi wanaona kama ni muzuri kujifunza Biblia katika luga yao?

12 Ndugu na dada wengi wenye wanatumikia katika kutaniko la luga ya kigeni wanaona kama ni muzuri kujifunza Biblia kwa ukawaida katika ‘luga yao ya kizalikio.’ (Matendo 2:8) Hata wamisionere wanajua kama ili waendelee kuwa na nguvu kiroho wakati wanatumwa katika inchi ingine, hawapaswe tu kutegemea mambo yenye wanasikia kwenye mikutano.

13 Alain, mwenye alikuwa anajifunza luga ya Kiajemi (Perse) kwa miaka karibu munane, anasema hivi: “Wakati ninatayarisha mikutano katika luga ya Kiajemi, mara nyingi ninakaza tu akili yangu juu ya luga. Kwa sababu ninakaza zaidi akili yangu juu ya luga, mambo ya kiroho yenye ninasoma hayaguse kabisa moyo wangu. Ndiyo sababu ninajipangia wakati wa kujifunza Biblia na vichapo vingine katika luga yangu ya kizalikio.”

UGUSE MIOYO YA WATOTO WAKO

14. Wazazi wanapaswa kuhakikisha jambo gani, na sababu gani?

14 Wazazi Wakristo wanapaswa kuhakikisha kama kweli inagusa akili na mioyo yao. Fikiria mufano wa Serge na bibi yake Muriel, wenye walitumikia katika kutaniko la luga ya kigeni kwa zaidi ya miaka tatu. Walianza kuona kama mutoto wao mwanaume mwenye alikuwa na miaka 17, hakukuwa anapenda kuhubiri ao kuenda kwenye mikutano. Muriel anasema hivi: “Hakufurahia kuhuburi katika luga ingine hata kama zamani alikuwa anafurahia kuhubiri katika Kifaransa, luga yake ya kizalikio.” Serge anasema hivi: “Wakati tulitambua kama hali hiyo ilizuia mutoto wetu mwanaume kufanya maendeleo ya kiroho, tuliamua kurudia katika kutaniko letu la zamani.”

Muhakikishe kama kweli inagusa mioyo ya watoto wenu (Picha hii inapatana na fungu la 14, 15)

15. (a) Ni nini inaweza kusaidia wazazi waamue ikiwa wanapaswa kuhamia katika kutaniko lingine? (b) Andiko la Kumbukumbu la Torati 6:5-7 linatolea wazazi muongozo gani?

15 Ni nini inaweza kusaidia wazazi waamue ikiwa watahamia katika kutaniko lenye kutumia luga yenye watoto wao wanaelewa muzuri zaidi? Kwanza, wanapaswa kuamua ikiwa wako kabisa na wakati na uwezo wa kufundisha watoto wao wamupende Yehova na wakati huohuo kuwafundisha luga ya kigeni. Pili, wanaweza kutambua kama watoto wao hawapendi kuhubiri, kuenda kwenye mikutano, ao hata kutumikia katika kutaniko la luga ingine. Kwa hiyo, wazazi wanaweza kuamua kurudia katika kutaniko lenye kutumia luga yenye watoto wao wanaelewa muzuri zaidi. Kisha, wakati watoto watakuwa sasa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova, wazazi wanaweza kuamua kurudia katika kutaniko la luga ya kigeni.​—Soma Kumbukumbu la Torati 6:5-7.

16, 17. Ni nini imesaidia wazazi fulani wafundishe watoto wao juu ya Yehova?

16 Wazazi wengine wamepata njia mbalimbali za kufundisha watoto wao juu ya Yehova katika luga yao ya kizalikio na wanaendelea kuhuzuria mikutano katika kutaniko ao kikundi chenye kutumia luga ya kigeni. Charles ni baba mwenye kuwa na watoto tatu wanawake wenye miaka kati ya 9 na 13. Wanahuzuria mikutano katika kikundi chenye kutumia luga ya Lingala. Anasema hivi: “Tuliamua kufanya funzo na ibada ya familia pamoja na watoto katika luga yetu ya kizalikio. Lakini pia tulikuwa tunafanya vipindi vya mazoezi na michezo katika Lingala ili wajifunze luga hiyo wakati tunajifurahisha.”

Ujikaze kujifunza luga ya eneo na kutoa maelezo kwenye mikutano (Picha hii inapatana na fungu la 16, 17)

17 Kevin ni baba mwenye kuwa na watoto wawili wanawake; wa miaka tano na wa miaka munane. Anajikaza sana ili kuwafundisha kweli kwa sababu watoto hao hawajaanza kuelewa muzuri mambo yenye kufundishwa kwenye mikutano ya kutaniko hilo la luga ya kigeni. Anasema hivi: “Miye na bibi yangu tunafanya funzo la pekee pamoja na watoto wetu wawili katika Kifaransa, luga yao ya kizalikio. Pia, tulijiwekea mupango wa kuhuzuria mikutano katika luga ya Kifaransa mara moja kila mwezi, na tunatumia wakati wetu wa mapumuziko ili kuenda kwenye mikusanyiko yenye kufanywa katika luga yetu ya kizalikio.”

18. (a) Namna gani andiko la Waroma 15:1, 2 linaweza kukusaidia kukamata uamuzi muzuri wakati inaomba kusaidia watoto wako? (b) Wazazi fulani wametoa mapendekezo gani? (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.)

18 Kila familia inapaswa kuamua mambo ya maana zaidi juu ya watoto wao na juu ya urafiki wao pamoja na Yehova. [2] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) (Wagalatia 6:5) Muriel anasema kama yeye na bwana yake walipenda kabisa kuendelea kutumikia katika kutaniko la luga ya kigeni, lakini waliamua kutoka katika kutaniko hilo ili wasaidie mutoto mwanaume wao amupende Yehova zaidi. (Soma Waroma 15:1, 2.) Leo, Serge anaona kama walikamata uamuzi muzuri. Anasema hivi: “Wakati tu tulihamia katika kutaniko la Kifaransa, mutoto wetu mwanaume alifanya maendeleo ya kiroho na akabatizwa. Leo, ni painia wa kawaida. Anafikiria hata kurudia katika kikundi chenye kutumia luga ya kigeni!”

ACHA NENO LA MUNGU LIGUSE MOYO WAKO

19, 20. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda Neno la Mungu?

19 Yehova anapenda watu wote. Alifanya Biblia iandikwe katika luga nyingi ili “watu wa namna zote” wapate ujuzi wa kweli. (1 Timotheo 2:4) Anajua kama urafiki wetu pamoja naye utakuwa wenye nguvu wakati tunasoma Biblia katika luga yenye tunaelewa muzuri zaidi.

20 Sisi wote tunapaswa kujikaza sana ili tuendelee kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Tunaweza kufanya hivyo wakati tunajifunza Biblia kwa ukawaida katika luga yenye tunaelewa muzuri zaidi. Pia, tutaweza kusaidia watu wa familia yetu waendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, na tutaonyesha kama tunapenda kabisa Neno la Mungu.​—Zaburi 119:11.

[Maelezo ya Mwisho]

^ [1] (fungu la 5) Majina yamebadilishwa.

^ [2] (fungu 18) Ili kupata kanuni za Biblia zenye zinaweza kusaidia familia yako, soma habari yenye kichwa “Kuwalea Watoto Katika Nchi ya Kigeni​—Magumu na Thawabu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2002.

[Maulizo ya Funzo]