Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Unalinda Hekima Inayotumika’?

‘Unalinda Hekima Inayotumika’?

HADISI moja inasema kama kulikuwa kijana mumoja mwanaume mwenye aliishi katika kijiji cha mbali. Kijana huyo alikuwa masikini. Watu wenye kuishi katika muji walikuwa wanamucheka kwa sababu waliwaza kuwa ana akili kidogo. Wakati wageni walikuwa wanakuja, wakaaji fulani wa kijiji walikuwa wanamucheka mbele ya marafiki wao. Walikuwa wanatosha makuta mbili ya vichele, moja kubwa ya feza na ingine ndogo ya zahabu; ile ya zahabu ilikuwa na bei mara mbili kuliko ile ya feza. Walikuwa wanamuambia hivi: “Chagua yenye unapenda.” Kijana huyo alikuwa anachagua kichele cha feza na kuenda mbio.

Siku moja, mugeni fulani akamuuliza hivi: “Haujue kama kichele cha zahabu kiko na bei mara mbili kuliko kichele cha feza?” Kijana huyo akacheka kidogo na kusema hivi: “Ndiyo, ninajua.” Mugeni huyo akamuuliza hivi: “Sasa sababu gani unakamata kichele cha feza? Kama unakamata kile cha zahabu, kiko na bei mara mbili kuliko kile cha feza!” Kijana huyo akasema hivi: “Lakini, kama ninakamata kichele cha zahabu, watu wataacha kucheza pamoja na mimi. Unajua nimekusanya vichele ngapi vya feza?” Kijana huyo mwenye kuzungumuziwa katika hadisi hiyo alionyesha sifa yenye inaweza kuletea watu wenye kukomaa faida; sifa hiyo ni hekima yenye kutumika.

Biblia inasema hivi: ‘Linda hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri. Ndipo utakapotembea kwa usalama njiani mwako, na hata muguu wako hautagonga chochote.’ (Met. 3:21, 23) Kwa hiyo, kujua maana ya ‘hekima inayotumika’ na namna ya kuitumia ni ulinzi kwetu kabisa. Hilo linatusaidia tuepuke kujikwaa kiroho kwa kufanya ‘muguu’ wetu uendelee kuwa imara.

HEKIMA YENYE KUTUMIKA NI NINI?

Hekima yenye kutumika iko tofauti na ujuzi na uelewaji. Mutu mwenye kuwa na ujuzi anakusanya habari, ao mambo ya hakika. Mutu mwenye kuwa na uelewaji anaweza kuona namna jambo fulani la hakika linapatana na lingine. Mutu mwenye kuwa na hekima ana uwezo wa kuchanga ujuzi na uelewaji na kuvitumikisha katika njia yenye kufaa.

Kwa mufano, mutu fulani anaweza kwa muda mufupi kusoma na kuelewa kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Wakati anajifunza Biblia, anaweza kutoa majibu ya kweli. Anaweza kuanza kuenda kwenye mikutano ya kutaniko na hata kutoa maelezo ya muzuri. Mambo yote hayo yanaweza kuonyesha kama anaendelea kufanya maendeleo ya kiroho, lakini hilo linaonyesha kama amepata hekima? Hapana kabisa. Anaweza tu kuwa mutu mwenye kuwa na uwezo wa kuelewa mambo haraka. Lakini, ataanza kuwa na hekima wakati anatumikisha kweli, kwa kutumia ujuzi na uelewaji katika njia yenye kufaa. Ikiwa maamuzi yake yanaleta matokeo ya muzuri na kuonyesha kama aliyafikiria kwa uangalifu mbele ya wakati, hilo litaonyesha wazi kama amekuwa na hekima yenye kutumika.

Mathayo 7:24-27 inazungumuzia mufano wa Yesu wa wanaume wawili wenye walijenga nyumba zao. Mwanaume mumoja anaonyeshwa kuwa mwenye “busara.” Kwa sababu alifikiria mbele ya wakati mambo yenye yanaweza kutokea, alijenga nyumba yake kwenye mwamba (jiwe kubwa). Mwanaume huyo aliona mbali na alifikiri kwa njia yenye kufaa. Hakufikiri kama angejenga nyumba yake kwenye muchanga ili asitumie feza nyingi ao wakati murefu. Alifikiria kwa hekima matokeo ya muda murefu ya matendo yake. Kwa hiyo wakati upepo mukali ulikuja, nyumba yake haikuanguka. Sasa ulizo ni hili: Namna gani tunaweza kupata na kulinda sifa hiyo ya maana sana, ni kusema, hekima yenye kutumika?

NAMNA GANI NINAWEZA KUIPATA?

Kwanza, kumbuka kama Mika 6:9 inasema hivi: ‘Mutu mwenye hekima inayotumika ataliogopa jina la [Mungu].’ Kuogopa jina la Yehova kunamaanisha pia kumuheshimia. Hilo linamaanisha kuheshimia kwa njia yenye kufaa kile jina hilo linawakilisha, na hata kanuni zake. Ili uheshimie mutu fulani, unapaswa kujua namna anafikiri. Kisha, unaweza kumutumainia, kujifunza mambo fulani kupitia yeye, na kuiga matendo yake yenye hekima ili kupata pia matokeo ya muzuri. Ikiwa tunafikiria matokeo ya muda murefu yenye matendo yetu yatakuwa nayo juu ya urafiki wetu pamoja na Yehova na ikiwa tunakamata maamuzi yenye kutegemea kanuni zake, tutakuwa tumepata hekima yenye kutumika.

Pili, Methali 18:1 inasema hivi: ‘Mutu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe; atashindana na [atakataa] hekima yote inayotumika.’ Ikiwa hatuko waangalifu, tunaweza kujitenga sisi wenyewe na Yehova na watu wake. Ili kuepuka kujitenga, tunapaswa kupitisha wakati pamoja na watu wengine wenye kuogopa jina la Mungu na wenye kuheshimia kanuni zake. Ikiwa inawezekana kabisa, ni lazima tuende kwenye Jumba la Ufalme, na kukusanyika kwa ukawaida pamoja na ndugu na dada katika kutaniko. Wakati tuko kwenye mikutano, tunapaswa kufungua akili zetu na mioyo yetu na kuacha mambo yenye tunasikiliza yaguse mioyo yetu.

Zaidi ya hilo, ikiwa tunamwangia Yehova moyo wetu katika sala, tutamukaribia zaidi. (Met. 3:5, 6) Ikiwa tunafungua akili zetu na mioyo yetu wakati tunasoma Biblia na vichapo vyenye tengenezo la Yehova linatutolea, tunaona mbele ya wakati matokeo ya muda murefu ya matendo yetu, na tutajua namna ya kutenda. Tunapaswa pia kufungua mioyo yetu ili kusikiliza mashauri yenye ndugu wenye kukomaa wanatutolea. (Met. 19:20) Kwa hiyo, ‘hatutashindana na hekima yote inayotumika,’ lakini tutaendelea kutia nguvu sifa hiyo ya maana.

NAMNA GANI ITASAIDIA FAMILIA YANGU?

Hekima yenye kutumika inaweza kulinda familia nyingi. Kwa mufano, Biblia inatia moyo bibi ‘aheshimie sana’ bwana yake. (Efe. 5:33) Bwana anaweza kufanya nini ili bibi yake amuheshimie sana? Ikiwa anakaza ao analazimisha kwa ukali bibi yake amuheshimie, atapata matokeo ya muda mufupi. Ili kuepuka kukokotana, bibi ya bwana huyo anaweza kumuheshimia kwa kiasi fulani wakati iko pale. Lakini, atakuwa tayari kuheshimia bwana yake wakati haiko? Pengine hawezi kabisa kumuheshimia. Bwana anapaswa kufikiria mambo yenye yataleta matokeo ya muda murefu. Ikiwa anaonyesha sehemu mbalimbali za tunda la roho, kama vile upendo na upole, atafanya bibi yake amuheshimie sana. Kwa kweli, bibi Mukristo anapaswa kuheshimia bwana yake hata kama bwana hafanye kitu chochote ili kustahili heshima.​—Gal. 5:22, 23.

Biblia inasema pia kama bwana anapaswa kupenda bibi yake. (Efe. 5:28, 33) Ili bwana yake aendelee kumupenda, bibi anaweza kufikiri kama ni muzuri zaidi afiche bwana yake mambo fulani yenye hayafae yenye ana haki ya kujua. Lakini, hilo linaonyesha kabisa hekima yenye kutumika? Kisha, wakati anavumbua kama bibi yake alimuficha mambo fulani, hilo litakuwa na matokeo gani? Ataendelea kumupenda zaidi? Inaweza kuwa vigumu. Lakini, ikiwa bibi huyo anatafuta wakati wenye kufaa ili kuelezea kwa upole bwana yake mambo yenye hayafae, pengine bwana yake atamufurahia kwa sababu anaeleza mambo yote waziwazi. Kwa hiyo, ataendelea kumupenda zaidi.

Namna unatia watoto wako nizamu leo itafanya ikuwe vyepesi ao vigumu kuzungumuza nao wakati unaokuja

Watoto wanapaswa kuheshimia wazazi wao na kutiwa nizamu katika njia za Yehova. (Efe. 6:1, 4) Wazazi wanapaswa kufanya mengi zaidi juu ya mutoto wao kuliko tu kumuwekea sheria za kufuata ao kumupatia malipizi kwa sababu ya mwenendo mubaya. Muzazi mwenye kuwa na hekima yenye kutumika anasaidia mutoto wake aelewe sababu gani anapaswa kutii.

Kwa mufano, wazia kuwa mutoto fulani anatumia maneno yenye kumukosea muzazi wake adabu. Kufokea mutoto ao kumupatia malipizi bila kufikiri kunaweza kufanya asikie haya ao kumulazimisha abakie kimya. Lakini, anaweza kuweka kinyongo, na hilo linaweza kumusukuma ajitenge na wazazi wake.

Wazazi wenye kukomalisha hekima yenye kutumika watafikiria namna wanatia watoto wao nizamu na matokeo yenye hilo linaweza kuwa nayo juu ya watoto wakati unaokuja. Wazazi hawapaswe kutenda haraka kwa sababu tu wanajisikia mubaya. Pengine wakati wako peke yao, wanaweza kufikiri pamoja na mutoto kwa upole na upendo, na kumufasiria kama Yehova anamuomba aheshimie wazazi wake ili apate faida za milele. Kisha, wakati mutoto anaonyesha kama anaheshimia wazazi wake, atatambua kuwa anamuheshimia Yehova. (Efe. 6:2, 3) Kama wazazi wanatumia njia hiyo, wanaweza kugusa moyo wa mutoto wao. Ataona kama wazazi wake wanamuhangaikia kabisa, na ataendelea kuwaheshimia zaidi. Kwa hiyo, mutoto atakuwa tayari kuomba musaada wakati kunatokea mambo fulani ya maana.

Wazazi fulani wanaweza kuogopa kufanya mutoto wao ajisikie mubaya, kwa hiyo, wanaacha kumushauria ao kumupatia malipizi. Lakini, ni nini itatokea wakati mutoto atakomaa? Atamuogopa Yehova na kuelewa kama ni jambo la hekima kutii kanuni za Mungu? Atakuwa tayari kumuambia Yehova mambo yenye kuwa katika moyo na akili yake, ao ataacha kufanya mambo ya kiroho?​—Met. 13:1; 29:21.

Muchongaji muzuri anapangaka mbele ya wakati kitu chenye atachonga. Hachonge-chonge tu kitu fulani na kutumaini kama atapata matokeo ya muzuri. Wazazi wenye kuwa na hekima yenye kutumika wanatumia wakati mwingi ili kujifunza na kutumikisha kanuni za Yehova, kwa hiyo, wanaogopa jina lake. Wakati wanashikamana na Yehova na tengenezo lake, wanapata hekima yenye kutumika na wanaitumikisha ili kujenga familia yao.

Kila siku, tunakamata maamuzi yenye yanaweza kuwa na matokeo ya muda murefu katika maisha yetu. Kuliko kujibia mbio-mbio na kukamata maamuzi ya haraka-haraka, tunapaswa kutua kidogo na kufikiri. Fikiria kwa uangalifu matokeo ya muda murefu. Tafuta muongozo wa Yehova, na utumie hekima yenye kutoka kwake. Kwa hiyo, tutakuwa tumelinda hekima yenye kutumika, na itatupatia uzima.​—Met. 3:21, 22.