Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova

Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova

‘Imani ni . . . usibitisho [uhakikisho] ulio wazi wa mambo halisi [ya kweli-kweli] ingawa hayaonekane.’​—WAEBRANIA 11:1.

NYIMBO: 54, 125

1. Tunapaswa kujisikia namna gani juu ya imani yetu?

HAIKO watu wote ndio wako na imani. (2 Wathesalonike 3:2) Lakini Yehova anapatia imani wale wote wenye kumuabudu. (Waroma 12:3; Wagalatia 5:22) Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Yehova anatupatia imani!

2, 3. (a) Tunapata faida gani ikiwa tuko na imani? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

2 Yehova alitoa Mwana wake mupendwa Yesu, ili kila mutu mwenye anaonyesha imani katika yeye asamehewe zambi zake. Hilo linawezesha watu wakuwe marafiki wa Yehova na waishi milele. (Yohana 6:44, 65; Waroma 6:23) Yehova anatuonyesha wema kabisa! Hata kama tuko watenda-zambi na tunastahili kifo, Yehova aliona kama tulikuwa na uwezo wa kufanya mambo ya muzuri. (Zaburi 103:10) Alitusaidia tujifunze habari njema juu ya Yesu na zabihu yake ya ukombozi. Wakati tulianza kuwa na imani katika Yesu na kumufuata, hilo lilifanya tukuwe na tumaini la kupata uzima wa milele!​—Soma 1 Yohana 4:9, 10.

3 Lakini ni mambo gani mengine tunaweza kujifunza juu ya imani? Ikiwa tunajua tu mambo yenye Mungu ametufanyia na mambo yenye atafanya wakati unaokuja, ni kusema tuko na imani? Tuone basi mambo mengine yenye tunapaswa kufanya.

ONYESHA IMANI KATIKA ‘MOYO WAKO’

4. Ikiwa tuko na imani, itatuchochea kufanya nini?

4 Kuwa na imani katika Yehova na Yesu, haiko tu kujua mambo yenye wamefanya na yenye watatufanyia. Tunapenda pia kabisa kuishi kulingana na mambo yenye wametufundisha. Na tuko tayari kusaidia wengine wafikie kujua Yehova na Yesu. Mutume Paulo alisema hivi: ‘Ukitangaza waziwazi lile ‘neno lililo katika kinywa chako mwenyewe,’ kwamba Yesu ni Bwana, na kuonyesha imani moyoni mwako kwamba Mungu alimufufua kutoka kwa wafu, utaokolewa. Kwa maana kwa moyo mutu anaonyesha imani kwa ajili ya uadilifu, lakini kwa kinywa mutu anafanya tangazo la hazarani [mbele ya watu] kwa ajili ya wokovu.’​—Waroma 10:9, 10; 2 Wakorintho 4:13.

5. Sababu gani imani ni sifa ya maana sana, na tunapaswa kufanya nini ili tukuwe na imani yenye nguvu? Toa mufano.

5 Kwa kweli, ili kupata uzima wa milele katika dunia mupya ya Mungu, tunapaswa kuwa na imani na tunapaswa kuendelea kuifanya ikuwe yenye nguvu. Imani iko kama mumea. Tunapaswa kuendelea kuumwangia maji ili ukuwe na afya ya muzuri na uendelee kukomaa. Ikiwa hatuumwangie maji ya kutosha, unaweza kukauka na kufa. Vilevile, tunapaswa kuhakikisha kama imani yetu inaendelea kuwa na “afya” ya muzuri na inaendelea ‘kukua [kukomaa]’.​—Tito 2:2; 2 Wathesalonike 1:3; Luka 22:32; Waebrania 3:12.

BIBLIA INAFASIRIA MAANA YA IMANI

6. Andiko la Waebrania 11:1 linafasiria maana ya imani katika njia gani mbili?

6 Katika andiko la Waebrania 11:1, Biblia inafasiria maana ya imani. (Soma.) (1) Imani ni “ni tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa.” Kati ya mambo yenye ‘tunatumainia’ kuko pia ahadi za Mungu juu ya wakati unaokuja. Kwa mufano, tuko hakika kama mambo ya mubaya yataisha na kama kutakuwa dunia mupya. (2) Imani ni ‘usibitisho ulio wazi,’ ao uhakikisho wenye kusadikisha wa, ‘mambo halisi ingawa hayaonekane.’ Hata kama hatuwezi kuona na macho yetu, tunajua kama Yehova Mungu, Yesu Kristo, na malaika wako kabisa, na pia Ufalme wa mbinguni uko. (Waebrania 11:3) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko kabisa na imani katika ahadi za Mungu na katika mambo yenye hatuwezi kuona? Tunafanya hivyo kupitia namna tunatumia maisha yetu na kupitia maneno na matendo yetu.

7. Namna gani mufano wa Noa unatusaidia kuelewa maana ya kuwa na imani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Mufano wa Noa unatufundisha nini juu ya imani? Mutume Paulo alisema kama Noa, “baada ya kupewa onyo la kimungu la mambo ambayo yalikuwa bado hayajaonekana, alionyesha woga wa kimungu na kujenga safina kwa ajili ya kuiokoa nyumba yake.” (Waebrania 11:7) Kwa sababu Noa alikuwa na imani katika mambo yenye Yehova alimuambia, alijenga safina hiyo kubwa sana. Pengine majirani wake walimuuliza sababu gani alikuwa anajenga safina hiyo. Tuko hakika kama Noa hakukaa kimya. Biblia inasema kama Noa alikuwa ‘muhubiri wa uadilifu [haki].’ (2 Petro 2:5) Alionya watu kama Mungu angeleta garika ili kuharibu watu wabaya. Inawezekana aliwaambia kabisa mambo yenye Yehova alikuwa amemuambia. Yehova alimuambia hivi: “Mwisho wa wote wenye mwili umekuja mbele zangu, kwa maana dunia imejaa jeuri kwa sababu yao,” na ‘tazama, mimi ninaleta garika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu za uhai [uzima] ndani yao. Kila kitu kilicho duniani kitakata pumuzi.’ Kwa hiyo, inawezekana Noa aliambia kabisa watu mambo yenye walipaswa kufanya ili waokolewe. Yehova aliamuru hivi: “Nawe uingie ndani ya safina.”​—Mwanzo 6:13, 17, 18.

8. Yakobo alisema nini juu ya imani?

8 Yakobo pia aliandika juu ya imani. Inawezekana alifanya hivyo kisha tu mutume Paulo kuandikia Wakristo Waebrania. Yakobo aliandika hivi: ‘Nionyeshe imani yako bila matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.’ (Yakobo 2:18) Yakobo alionyesha kama ili tukuwe na imani, tunapaswa kufanya mambo mengi kuliko tu kuamini. Mashetani wanaamini kama kuna Mungu, hata hivyo, hawana imani katika Yehova. Lakini, wanamupinga sana. (Yakobo 2:19, 20) Kwa upande mwingine, ikiwa mutu fulani ana imani, atafurahisha Mungu kwa kufanya kazi nzuri, ao matendo ya muzuri. Abrahamu alifanya hivyo. Yakobo aliandika hivi: ‘Je, Abrahamu baba yetu hakutangazwa kuwa muadilifu kwa matendo baada ya kumutoa Isaka mwana wake juu ya mazabahu? Munaona kwamba imani yake ilitenda pamoja na matendo yake na kwa matendo yake imani yake ilikamilishwa.’ Kisha, Yakobo alikazia kama imani bila matendo ni ya bure. Alisema hivi: “Kama vile ambavyo mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo pia imani bila matendo imekufa.”​—Yakobo 2:21-23, 26.

9, 10. Kuonyesha imani katika Mwana, maana yake nini?

9 Kisha kupita miaka zaidi ya 30, Yohana aliandika Injili yake na barua tatu. Kama vile waandikaji wengine wa Biblia, Yohana alielewa maana ya imani. Yohana alitumia mara nyingi katika maandishi yake neno la Kigiriki lenye wakati fulani linatafsiriwa katika Kiswahili “kuonyesha imani.”

10 Kwa mufano, Yohana alifasiria hivi: ‘Yule anayemwamini [anaonyesha imani katika] Mwana ana uzima wa milele; yule asiyemutii Mwana hataona uzima, bali gazabu [hasira] ya Mungu inakaa juu yake.’ (Yohana 3:36) Ili kuonyesha imani katika Mwana, tunapaswa kutii Yesu. Kwa kweli, katika maandishi ya Yohana, tunaona kuwa Yesu alikuwa anasema mara nyingi kama ili kupata uzima wa milele, tunapaswa kuonyesha imani katika yeye na katika Baba yake.​—Yohana 3:16; 6:29, 40; 11:25, 26; 14:1, 12.

11. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa Yehova kwa sababu ametusaidia kujua kweli?

11 Yehova alitumia roho yake takatifu ili kutusaidia kuelewa kweli juu yake na juu ya Mwana wake na kutusaidia tuwaamini. (Soma Luka 10:21.) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa Yehova kwa ajili ya mambo yote yenye amefanya? Tunapaswa kuendelea kumushukuru Yehova kwa sababu anatusaidia tukuwe marafiki wake kupitia Yesu, ‘Wakili Mukubwa na Mukamilishaji wa imani yetu.’ (Waebrania 12:2) Na tunapaswa kuendelea kutia nguvu imani yetu kwa kusali sikuzote kwa Yehova na kujifunza Neno lake.​—Waefeso 6:18; 1 Petro 2:2.

Onyesha imani yako kwa kuhubiria wengine habari njema kila wakati unapata nafasi ya kufanya hivyo (Picha hii inapatana na fungu la 12)

12. Ikiwa tuko na imani, tutafanya nini?

12 Tunapaswa kuendelea kuonyesha kupitia matendo yetu kama tuko na imani yenye nguvu katika ahadi za Yehova. Kwa mufano, tunaendelea kuhubiria watu juu ya Ufalme wa Mungu na kuwasaidia wakuwe wanafunzi wa Yesu. Pia, tunaendelea kutendea “wote mema, na hasa [zaidi sana] wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Wagalatia 6:10) Na tunajikaza sana ili ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake’ kwa sababu hatupendi jambo lolote liharibu urafiki wetu pamoja na Yehova.​—Wakolosai 3:5, 8-10.

IMANI KWA MUNGU NI SEHEMU YA MUSINGI WETU

13. Sababu gani “imani kwa Mungu” ni ya maana sana? Namna gani Biblia inafasiria imani, na sababu gani?

13 Biblia inasema hivi: ‘Bila imani haiwezekane kamwe [hata kidogo] kumupendeza vema, kwa maana yule anayemukaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye anakuwa musawabishaji wa [mwenye kulipa] wale wanaomutafuta kwa bidii.’ (Waebrania 11:6) Biblia inaonyesha pia kama “imani kwa Mungu” ni jambo moja kati ya mambo ya kwanza Wakristo wanapaswa kuwa nayo. Ni sehemu ya ‘musingi’ wetu. (Waebrania 6:1) Lakini zaidi ya imani, tuko na lazima ya sifa zingine za maana ili tukuwe na urafiki pamoja na Yehova na kulinda urafiki huo.​—Soma 2 Petro 1:5-7; Yuda 20, 21.

14, 15. Sababu gani ni jambo la maana zaidi kuwa na upendo kuliko tu kuwa na imani?

14 Waandikaji wa Biblia walizungumuzia sana imani kuliko sifa zingine zote. Hilo linamaanisha kama imani ndiyo sifa ya maana zaidi yenye tunapaswa kuwa nayo?

15 Mutume Paulo alilinganisha imani na upendo. Aliandika hivi: “Ikiwa nina imani yote kuweza kuhamisha milima, lakini sina upendo, mimi si kitu.” (1 Wakorintho 13:2) Yesu alisema kama ‘amri iliyo kubwa katika Sheria’ ni kumupenda Mungu. (Mathayo 22:35-40) Upendo unatusaidia tukuwe na sifa zingine nyingi zenye kumupendeza Mungu. Kwa mufano, Biblia inasema kama upendo ‘unaamini mambo yote.’ Kwa hiyo, upendo utatusaidia kuamini, ao kuwa na imani katika, mambo yote yenye Mungu anatuambia katika Biblia.​—1 Wakorintho 13:4, 7.

16, 17. Biblia inasema nini juu ya imani na upendo? Kati ya sifa hizo mbili, ni sifa gani yenye kuwa ya maana zaidi, na sababu gani?

16 Imani na upendo ni sifa za maana sana, na mara nyingi waandikaji wa Biblia wanazungumuzia sifa hizo mbili pamoja. Mutume Paulo alitia ndugu zake moyo ‘wavae bamba la kifuani la imani na upendo.’ (1 Wathesalonike 5:8) Juu ya Yesu, Petro aliandika hivi: ‘Ninyi munamupenda, ingawa [hata kama] hamukumuona yeye kamwe. Ingawa hamumuone wakati wa sasa, bado munaonyesha imani katika yeye.’ (1 Petro 1:8) Yakobo aliuliza ndugu zake watiwa-mafuta hivi: ‘Mungu alichagua walio masikini kwa habari ya ulimwengu ili wakuwe matajiri katika imani na wariti wa ufalme, aliowaahidi wale wanaomupenda, sivyo?’ (Yakobo 2:5) Yohana aliandika kama amri ya Mungu ni kwamba ‘tukuwe na imani katika jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane.’​1 Yohana 3:23.

17 Lakini mutume Paulo aliandika pia hivi: “Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.” (1 Wakorintho 13:13) Wakati unaokuja, hatutakuwa tena na lazima ya kuwa na imani katika ahadi za Mungu juu ya dunia yake mupya kwa sababu ahadi hizo zitakuwa zimetimia. Tutakuwa na maisha ya muzuri sana yenye Biblia inazungumuzia. Lakini tutaendelea kuwa na lazima ya kupenda Mungu na watu. Kwa kweli, upendo wetu kwa Mungu na watu utaendelea kuongezeka milele.

YEHOVA AMEBARIKI IMANI YETU

18, 19. Kwa sababu watu wa Mungu wako na imani leo, hilo limekuwa na matokeo gani?

18 Watu wa Yehova wa wakati wetu wako na imani katika Ufalme wa Mungu na wanaunga mukono Ufalme huo. Na wanapendana. Wanafanya hivyo kwa sababu wanaacha roho takatifu ya Mungu iongoze maisha yao. (Wagalatia 5:22, 23) Hilo limekuwa na matokeo gani? Ndugu na dada zaidi ya milioni munane katika dunia yote wanaishi kwa amani na umoja katika makutaniko yao. Hilo linaonyesha wazi kama imani na upendo ni sifa zenye nguvu sana.

19 Ni Mungu wetu tu ndiye ametuwezesha tukuwe na umoja huo. Anastahili sifa kwa sababu ya jambo hilo. (Isaya 55:13) Tuko wenye shukrani kabisa kwa sababu amefanya tuweze ‘kuokolewa kupitia imani.’ (Waefeso 2:8) Yehova ataendelea kusaidia watu wengi zaidi wakuwe na imani kwake. Mwishowe, dunia yote itajaa watu wakamilifu, wenye haki, na wenye furaha ambao watamusifu Yehova milele!