Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Neno Lenye Lilikuwa na Maana Kubwa!

Neno Lenye Lilikuwa na Maana Kubwa!

‘MWANAMUKE.’ Wakati fulani Yesu alitumia neno hilo ili kuzungumuzia wanawake. Kwa mufano, wakati aliponya mwanamuke mulemavu mwenye kukunjama mugongo kwa miaka 18, alimuambia hivi: ‘Mwanamuke, umefunguliwa kutoka uzaifu wako.’ (Lu. 13:10-13) Hata Yesu alitumia neno hilo la kawaida na lenye lilionyesha adabu wakati wa zamani, wakati alizungumuza na mama yake. (Yoh. 19:26; 20:13) Lakini kulikuwa neno lingine lenye lilikuwa na maana kubwa kuliko kuonyesha tu adabu.

Wakati Biblia inazungumuzia wanawake fulani, inatumia neno lingine lenye kuonyesha wema na upole. Yesu alitumia neno hilo wakati alizungumuza na mwanamuke mwenye aliteseka kwa sababu ya kutokwa na damu kwa miaka 12. Namna mwanamuke huyo alimukaribia Yesu haikupatana kabisa na Sheria ya Mungu yenye ilisema kama mutu mwenye kuwa katika hali hiyo hakukuwa safi. Sheria ilisema kama alipaswa kujitenga na wengine kwa sababu ya hali yake. (Law. 15:19-27) Lakini alikuwa ameteseka sana. Kwa kweli, ‘alikuwa ameumizwa sana na matabibu [wanganga] wengi na alikuwa ametumia mali zake zote naye hakukuwa amefaidika bali, badala yake, hali yake ikakuwa mbaya zaidi.’—Mk. 5:25, 26.

Mwanamuke huyo alipita polepole katikati ya kikundi kikubwa cha watu, mupaka akafika nyuma ya Yesu na kugusa sehemu ya mwisho ya nguo yake ya inje. Na damu ikaacha kumutoka palepale! Mwanamuke huyo alifikiri kama ataondoka bila mutu kujua, lakini Yesu aliuliza hivi: “Ni nani aliyenigusa?” (Lu. 8:45-47) Kwa hiyo, mwanamuke huyo mwenye kuogopa na kutetemeka alianguka chini mbele ya Yesu na ‘akamuambia kweli yote.’—Mk. 5:33.

Ili kutuliza mwanamuke huyo, Yesu alimuambia hivi kwa upole: “Jipe moyo, binti yangu!” (Mt. 9:22) Watu wenye elimu ya mambo ya Biblia wanasema kama neno la Kiebrania na Kigiriki lenye kutafsiriwa “binti” linaweza kutumiwa kwa njia ya mufano ili kuonyesha “wema na upole.” Yesu alimutuliza zaidi kwa kumuambia hivi: ‘Imani yako imekuponya. Enda kwa amani, na ukuwe na afya njema kutokana na ugonjwa wako wenye kuhuzunisha.’—Mk. 5:34.

“Binti.” Ni hivyo Boazi, mwanaume tajiri Mwisraeli alimuita Ruthu Mumoabu. Yeye pia alikuwa na sababu ya kuogopa kwa kuwa alikuwa anaokota shayiri katika shamba la mwanaume mwenye hakukuwa anajua. Boazi alimuambia hivi: “Umesikia binti yangu.” Kisha akamuambia Ruthu aendelee kuokota shayiri katika mashamba yake. Ruthu alianguka chini mbele ya Boazi na kumuuliza sababu gani anamutendea kwa wema, hata kama yeye hakukuwa Mwisraeli. Ili kumutuliza zaidi, Boazi alimujibia hivi: ‘Nilipewa habari kamili juu ya yote ambayo umemufanyia mama-mukwe wako, [mujane Naomi] . . . Yehova na akupe sawabu [malipo] kwa sababu ya jinsi unavyotenda.’—Rut. 2:8-12.

Yesu na Boazi waliachia Wazee Wakristo mufano muzuri sana! Wakati fulani, wazee wanaweza kuzungumuza na dada Mukristo mwenye kuwa na lazima ya kutiwa moyo na kupewa musaada kutoka katika Maandiko. Kisha wazee kuomba Yehova muongozo katika sala na kusikiliza dada huyo kwa uangalifu, wataweza kumutuliza na kumutia moyo kwa kutumia Neno la Mungu.—Rom. 15:4.