Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vitu Vya Maana Sana Vya Historia Yetu

“Wahubiri wa Ufalme Katika Uingereza— Muamuke!!”

“Wahubiri wa Ufalme Katika Uingereza— Muamuke!!”

ULIKUWA mwaliko wa haraka na wenye kuwa wazi kabisa: “Wahubiri wa Ufalme Katika Uingereza—Muamuke!!” (Informateur, * ya Mwezi wa 12, 1937, chapa ya Londres) Kichwa hicho kidogo chenye kuchochea watu kufikiri kiliongezea hivi: “Hakuna Ongezeko Kubwa Katika Miaka Kumi.” Ili kuhakikisha jambo hilo, ukurasa wa kwanza ulikuwa na ripoti ya mahubiri ya miaka kumi kuanzia mwaka wa 1928 mupaka 1937.

MAPAINIA WENGI SANA?

Ni nini ilifanya wahubiri wapunguze bidii yao katika kazi ya kuhubiri katika Uingereza? Pengine makutaniko yalikuwa yamepoteza bidii, na wahubiri hawakuongeza utumishi wao. Tena biro ya tawi ilikuwa imeamua kama kulikuwa maeneo kwa ajili ya mapainia 200 tu, wenye walitumika katika maeneo ya mbali kuliko kutumika katika makutaniko. Kwa hiyo, tawi ilikuwa imeambia ndugu na dada wenye walipenda kufanya kazi ya upainia kwamba Uingereza haikuwa tena na maeneo ya kuhubiria, na iliwatia moyo waende kutumikia katika inchi zingine za Ulaya. Jambo la kufurahisha ni kwamba mapainia wengi wenye bidii walitoka Uingereza na kuhamia katika inchi kama vile Ufaransa hata kama walijua Kifaransa kidogo ao hawakujua luga hiyo.

“WANACHOCHEWA KUTENDA”

Kichapo Informateur cha mwaka wa 1937 kiliweka muradi mukubwa kwa ajili ya mwaka wa 1938: Kuhubiri saa milioni moja! Muradi huo ungetimizwa bila tatizo ikiwa wahubiri wangefanya saa 15 katika mahubiri kila mwezi na mapainia saa 110. Mapendekezo yalitia ndani kupanga mahubiri ya vikundi katika siku fulani za juma ili kuhubiri saa tano na kukazia sana kufanya marudio, zaidi sana katikati ya juma wakati wa mangaribi.

Mapainia wenye bidii walikazia kazi ya kuhubiri

Mabadiliko hayo yenye yalikazia tena kazi ya kuhubiri yalifurahisha wahubiri wengi. Dada Hilda Padgett, alikumbuka hivi: “Ulikuwa mualiko wa kutenda kutoka kwenye makao makubwa, wenye wengi kati yetu walikuwa wanangojea kwa hamu na wenye karibuni ungekuwa na matokeo ya muzuri sana.” * Dada Wallis alisema hivi: “Pendekezo la kuhubiri kwa saa tano katika siku fulani za juma, lilikuwa la muzuri sana! Ilikuwa furaha sana kupitisha muchana muzima katika kazi ya Bwana siku fulani za juma. . . . Wakati tulirudia tulikuwa pengine tunachoka, lakini tulikuwa na furaha kabisa!” Kijana Stephen Miller aliona kama iliomba kutenda haraka, na alitenda kulingana na mualiko huo. Alipenda kufanya hivyo wakati alikuwa na nafasi! Alikumbuka namna vikundi vya wahubiri wenye kutumia kinga zao walikuwa wanahubiri kwa siku nzima, na wakati wa mangaribi katika kipindi cha joto walikuwa wanapitisha hotuba zenye kurekodiwa. Walikuwa wanavaa pankarte na kufanya maandamano ya kutangaza habari njema na pia walihubiria watu katika barabara na kuwatolea magazeti.

Kichapo Informateur kilitoa pia mualiko huu wenye kupendeza: “Tuko na lazima ya jeshi la mapainia 1000.” Maagizo mapya juu ya eneo yalisema kama mapainia hawangetumika tena mbali na makutaniko lakini wangetumika pamoja na makutaniko ili kuyategemeza na kuyajenga kiroho. Joyce Ellis anakumbuka hivi: “Ndugu na dada wengi walianza kutambua kama wanapaswa kufanya kazi ya upainia.” Anasema hivi: “Hata kama nilikuwa na miaka 13 tu wakati huo, hilo ndilo nilipenda kufanya, nilipenda kufanya kazi ya upainia.” Alifikia muradi wake Mwezi wa 7, 1940, wakati alikuwa na miaka 15. Ndugu Peter, mwenye alifikia kuwa bwana ya Dada Joyce, alisikia mualiko huo, “Muamuke,” na ukamuchochea “aanze kufikiri juu ya kazi ya upainia.” Mwezi wa 6, 1940, wakati alikuwa na miaka 17, alitembeza kinga kwenye urefu wa kilometre 105 kuenda Scarborough ili kutumika katika mugawo wake mupya wa kazi ya upainia.

Cyril na Kitty Johnson walikuwa mufano wa mapainia wapya wenye kuwa na roho ya kujitoa. Waliamua kuuzisha nyumba yao na vitu vyao ili wapate feza za kuwategemeza katika utumishi wa wakati wote. Cyril aliacha kazi yake, na kisha mwezi moja walikuwa tayari kuanza kazi ya upainia. Alikumbuka hivi: “Tulikuwa hakika juu ya jambo hilo. Tulifanya hivyo kwa kujipendea na kwa furaha.”

NYUMBA ZA MAPAINIA ZINAFUNGULIWA

Wakati hesabu ya mapainia iliendelea kuongezeka sana, ndugu wenye kusimamia kazi ya kuhubiri walitafuta njia za kutegemeza jeshi hilo lenye lilikuwa linaongezeka. Jim Carr, mwenye alikuwa mutumishi wa eneo (sasa anaitwa mwangalizi wa muzunguko) katika mwaka wa 1938, alifuata pendekezo la kuanzisha nyumba za mapainia katika miji. Vikundi vya mapainia walitiwa moyo kuishi na kuhubiri pamoja, hilo lingewasaidia wasitumie feza nyingi. Katika muji wa Sheffield, walichukua nyumba kubwa ya kulipia, yenye ilisimamiwa na ndugu mwenye kukomaa kiroho. Kutaniko la eneo hilo lilichangia feza na vyombo mbalimbali. Jim alikumbuka hivi: “Kila mutu alijikaza sana ili mupango huo ukuwe na matokeo ya muzuri.” Mapainia kumi wenye bidii waliishi humo, na waliendelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho. “Walikuwa wanachunguza andiko [la siku] kila asubuhi wakati wa chakula,” na “mapainia walikuwa wanaenda kila siku katika eneo lao katika sehemu mbalimbali za muji.”

Hesabu ya mapainia iliongezeka sana katika Uingereza

Wahubiri na mapainia, wote walitenda kulingana na mualiko; kwa hiyo, walifikia muradi wa saa milioni moja katika mwaka wa 1938. Kwa kweli ripoti zinaonyesha kama kulikuwa ongezeko katika sehemu zote za mahubiri. Katika kipindi cha miaka 5 hesabu ya wahubiri katika Uingereza iliongezeka karibu mara tatu. Mabadiliko hayo yenye yalikazia kazi ya Ufalme yalipatia watu wa Yehova nguvu ya kupambana na miaka ya vita yenye ilikuwa mbele.

Leo, hesabu ya mapainia katika Uingereza inaongezeka tena, kadiri vita ya Mungu ya Har-Magedoni inakaribia. Kwa miaka kumi yenye imepita hesabu ya mapainia imeongezeka sana; Mwezi wa 10, 2015 hesabu ya mapainia ilikuwa 13224. Mapainia hao wanajua kabisa kama kufanya utumishi wa wakati wote ni njia moja ya kutumikisha muzuri zaidi maisha yao.

^ fu. 3 Ilifikia kuitwa Huduma Yetu ya Ufalme.

^ fu. 8 Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 1995, uku. 19-24, iko na habari juu ya maisha ya Dada Padgett.