Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | UTAKUBALI ZAWADI YA MUNGU YENYE KUWA KUBWA ZAIDI?

Zawadi ya Mungu Yenye Kuwa Kubwa Zaidi Itakuchochea Kufanya Nini?

Zawadi ya Mungu Yenye Kuwa Kubwa Zaidi Itakuchochea Kufanya Nini?

“Upendo alio nao Kristo hutulazimisha . . . Alikufa kwa ajili ya wote ili wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa kwa ajili yao.”2 Wakorintho 5:14, 15.

ZAWADI ya maana sana inapaswa kutulazimisha kuonyesha shukrani. Yesu alionyesha jambo hilo kisha kuponya wanaume kumi wenye walikuwa na ugonjwa mubaya ambao haukukuwa na dawa wakati huo. Mumoja kati ya wanaume hao kumi wenye Yesu aliponyesha ‘alirudi, akimutukuza Mungu kwa sauti kubwa.’ Yesu alisema hivi: “Wale kumi walitakaswa, sivyo? Basi, wako wapi wale wengine tisa?” (Luka 17:12-17) Jambo hilo linatufundisha nini? Jambo hilo linatufundisha kwamba tunaweza kusahau haraka mambo ya muzuri yenye wengine wanatufanyia.

Zawadi ya zabihu ya ukombozi ni tofauti na zawadi zingine. Hiyo ndiyo zawadi kubwa zaidi yenye imekwisha kutolewa. Kwa hiyo, unapaswa kufanya nini ili kuonyesha shukrani kwa jambo lenye Mungu amekufanyia?

  • Ujifunze juu ya Mutoaji. Zabihu ya ukombozi hailetee wanadamu uzima wa milele bila wao kufanya jambo lolote. Katika sala yake kwa Mungu, Yesu alisema hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Kama mutu anakuambia kwamba mutu fulani aliokoa uzima wako wakati ulikuwa mutoto, hautapenda kujua mengi zaidi juu ya mutu huyo na sababu gani alikuokoa? Yehova Mungu, mwenye alitoa zawadi ya zabihu ya ukombozi yenye kuokoa uzima, anataka ujue yeye ni nani na ukuwe rafiki yake. Biblia inatutia moyo hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.

  • Onyesha imani katika zabihu ya ukombozi. “Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele.” (Yohana 3:36) Namna gani tunaweza kuonyesha imani? Tunapaswa kuonyesha imani katika zabihu ya ukombozi kupitia matendo. (Yakobo 2:17) Matendo gani? Zawadi inakuwa yako wakati tu unaikubali. Kwa hiyo, unapaswa kukubali zabihu ya ukombozi. Namna gani? Ujifunze namna Mungu anapenda uishi, kisha uishi kulingana na mambo yenye unajifunza. * Umuombe Mungu akusamehe na akusaidie ukuwe na zamiri safi. Umukaribie Mungu ukiwa hakika kabisa kwamba wale wote wenye kuonyesha imani katika zabihu ya ukombozi watapata uzima wa milele katika amani, usalama, na watakuwa na maisha ya muzuri!—Waebrania 11:1.

  • Fika kwenye Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Yesu alianzisha tukio la kila mwaka la kutukumbusha mupango wa zabihu ya ukombozi. Alisema hivi kuhusu tukio hilo: ‘Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.’ (Luka 22:19) Mashahidi wa Yehova watafanya Ukumbusho wa kifo cha Yesu Siku ya Pili, Tarehe 11 Mwezi wa 4, 2017, kisha jua kutua. Kwenye programu hiyo yenye kufanya karibu saa moja, kutakuwa hotuba ambayo itafasiria maana ya kifo cha Yesu na namna kinaweza kutuletea faida leo na wakati unaokuja. Mwaka jana, watu karibu milioni 20 katika dunia yote walifika kwenye Ukumbusho. Tunafurahi kukualika ujiunge pamoja na sisi ili kuonyesha shukrani kwa zawadi kubwa zaidi ya Mungu.

^ fu. 7 Njia ya muzuri zaidi ya kujifunza juu ya Mungu na kumukaribia ni kujifunza Neno lake Biblia. Ili kujua namna ya kujifunza Biblia, zungumuza na Mashahidi wa Yehova ao fungua adresi yetu ya Internete, www.pr418.com.