Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Kuna siku kutakuwa haki ya kweli duniani?

Unaweza kujibu nini?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Pengine

Mambo Biblia inasema

“Najua vema kwamba Yehova atatimiza dai halali la mwenye kuteseka, hukumu ya maskini.” (Zaburi 140:12) Ufalme wa Mungu utaleta haki ya kweli duniani.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Mungu anaona ukosefu wa haki wenye kuwa duniani leo, na ataumaliza.​—Mhubiri 5:8.

  • Haki yenye kutoka kwa Mungu italeta amani na usalama duniani.​—Isaya 32:16-18.

Mungu anapendelea kikundi fulani cha watu?

Watu fulani wanaamini kwamba Mungu amebariki ao amelaani kikundi fulani cha watu; na wengine wanaamini kwamba Mungu anatendea watu wote kwa njia moja. Wewe unawaza nini?

Mambo Biblia inasema

‘Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’ (Matendo 10:34, 35) Mungu anaona watu wote kuwa sawa.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Biblia iko na “habari njema” kwa ajili ya ‘kila taifa na kabila na luga na watu.’​—Ufunuo 14:6.