Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Har-Magedoni ni nini?

Watu fulani wanaamini . . .

kwamba itakuwa kuharibiwa kwa dunia yote kupitia silaha za nyuklia ao kuharibiwa kwa mazingira. Unawaza namna gani?

Mambo Biblia inasema

Har-Magedoni ni mahali pa mufano kwa ajili ya “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote,” ni kusema, vita yake zidi ya watu waovu. ​—Ufunuo 16:14, 16.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Mungu hapigani vita ya Har-Magedoni ili kuharibu dunia, lakini anafanya hivyo ili wanadamu wasiiharibu.​—Ufunuo 11:18.

  • Vita ya Har-Magedoni itamaliza vita vyote.​—Zaburi 46:8, 9.

Inawezekana kuokoka vita ya Har-Magedoni?

Unaweza kujibu nini?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Pengine

Mambo Biblia inasema

‘Umati mukubwa’ wa watu kutoka mataifa yote utaokoka ‘ziki kubwa [ao, mateso makubwa],’ ambayo Har-magedoni itakuwa sehemu yake ya mwisho.​—Ufunuo 7:9, 14.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Mungu anapenda watu wengi kadiri inawezekana waokoke Har-Magedoni. Atalazimika kuua waovu kama tu hawabadilike.​—Ezekieli 18:32.

  • Biblia inaonyesha namna ya kuokoka Har-Magedoni.​—Sefania 2:3.