Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Umutegemee Yehova na Ufanye Mema’

‘Umutegemee Yehova na Ufanye Mema’

‘Umutegemee Yehova na ufanye mema . . . na utende kwa uaminifu.’ZABURI 37:3.

NYIMBO:133, 63

1. Wakati Yehova aliumba wanadamu, aliwapatia uwezo gani mbalimbali wa pekee?

WAKATI Yehova aliumba wanadamu, aliwapatia uwezo mbalimbali wa pekee. Alitupatia uwezo wa kufikiri wenye kutusaidia kumaliza magumu yetu na kufanya mipango kwa ajili ya wakati unaokuja. (Methali 2:11) Alitupatia nguvu ili tuweze kufanya mambo yenye tumepanga na kufikia miradi yetu. (Wafilipi 2:13) Alitupatia pia zamiri, ni kusema, uwezo wenye kuwa ndani yetu wa kujua mema na mabaya. Zamiri yetu inatusaidia tuepuke kufanya zambi na tuachane na makosa yetu.—Waroma 2:15.

2. Yehova anapenda tutumikishe uwezo wetu katika njia gani?

2 Yehova anapenda tutumie muzuri uwezo wetu. Sababu gani? Kwa sababu anatupenda na anajua kama tutakuwa na furaha wakati tunatumikisha zawadi zenye ametupatia. Kwa mufano, katika Maandiko ya Kiebrania, tunasoma hivi: ‘Mipango ya mwenye bidii bila shaka inaleta faida,’ na ‘yote ambayo mukono wako unapata kufanya yafanye kwa nguvu zako zote.’ (Methali 21:5; Mhubiri 9:10) Katika Maandiko ya Kigiriki, tunasoma hivi: “Basi, tukiwa na wakati unaofaa kwa ajili ya hilo, tuwatendee wote mema,” na ‘kadiri ambayo kila mumoja amepokea zawadi, muitumie katika kuhudumiana [kutumikiana].’ (Wagalatia 6:10; 1 Petro 4:10) Kwa kweli, Yehova anapenda tujikaze sana ili sisi wenyewe na wengine tupate faida.

3. Wanadamu wako na mipaka gani?

3 Yehova anapenda tutumikishe uwezo wetu, lakini anajua kama tuko na mipaka. Kwa mufano, hatuwezi kumaliza hali yetu ya kutokamilika, zambi, na kifo. (1 Wafalme 8:46) Pia, hatuwezi kuongoza watu wengine, kwa sababu kila mutu iko na uhuru wa kufanya maamuzi yake mwenyewe. Na hata kama tuko na ujuzi ao uzoefu mwingi sana, hatutakuwa sawa na Yehova hata siku moja.​—Isaya 55:9.

Wakati uko na magumu, ‘umutegemee Yehova na ufanye mema’

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Sikuzote, tunapaswa kumuacha Yehova atuongoze, na kuwa na tumaini kwamba atatutegemeza na kutufanyia mambo yenye hatuwezi kujifanyia sisi wenyewe. Lakini, Yehova anapenda pia tufikirie mambo yenye tunaweza kufanya ili kumaliza magumu yetu na kusaidia wengine. (Soma Zaburi 37:3.) Tunapaswa ‘kumutegemea Yehova na kufanya mema.’ Tunapaswa ‘kutenda kwa uaminifu.’ Namna gani tunaweza kufanya hivyo? Tuzungumuzie basi mufano wa Noa, Daudi, na watumishi wengine waaminifu wa Mungu wenye walimutegemea Yehova. Tutaona kama kulikuwa mambo yenye hawangeweza kufanya, lakini waliamua kukaza akili yao juu ya mambo yenye wangeweza kufanya.

WAKATI TUNAISHI KATI YA WATU WAOVU

5. Noa alikuwa katika hali gani? Eleza.

5 Noa aliishi katika ulimwengu wenye ‘ulijaa jeuri’ na mambo ya uasherati. (Mwanzo 6:4, 9-13) Hata kama alijua kuwa Yehova atafikia kuharibu ulimwengu huo muovu, Noa alihuzunika juu ya mambo yenye watu walikuwa wanafanya. Katika hali hiyo, Noa alitambua kama kulikuwa mambo yenye hangeweza kufanya, lakini alitambua pia kama kulikuwa mambo yenye angeweza kufanya.

Kupingwa katika kazi yetu ya kuhubiri (Picha hizi zinapatana na fungu la 6-9)

6, 7. (a) Noa hangeweza kufanya nini? (b) Namna gani tuko katika hali yenye kufanana na ile ya Noa?

6 Mambo yenye Noa hangeweza kufanya: Noa alihubiri kwa uaminifu ujumbe wa Yehova wa kuonya, lakini hangeweza kukaza watu wakubali ujumbe huo. Na hangeweza kufanya Garika ifike haraka sana. Noa alipaswa kuwa na tumaini kama Yehova angetimiza ahadi Yake ya kumaliza uovu, kwa kuamini kama Mungu angefanya hivyo kwa wakati wenye kufaa kabisa.—Mwanzo 6:17.

7 Sisi pia tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa mambo ya mubaya, na tunajua kama Yehova ameahidi kuharibu ulimwengu huu. (1 Yohana 2:17) Lakini mbele afanye hivyo, hatuwezi kukaza watu wakubali “habari njema ya Ufalme.” Na hatuwezi kufanya jambo lolote ili kufanya ‘ziki [taabu] kubwa ianze mbele ya wakati. (Mathayo 24:14, 21) Kama Noa, tunapaswa kuwa na imani yenye nguvu, na kutumaini kama Mungu atamaliza mambo yote ya mubaya hivi karibuni. (Zaburi 37:10, 11) Tuko hakika kama Yehova hataruhusu ulimwengu huu muovu uendelee hata kwa siku moja zaidi; atauharibu kwa wakati wake.—Habakuki 2:3.

8. Noa alikaza akili yake juu ya mambo gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Mambo yenye Noa angeweza kufanya: Kuliko kuvunjika moyo kwa sababu ya mambo yenye hangeweza kufanya, Noa alikaza akili yake juu ya mambo yenye angeweza kufanya. Noa alihubiri kwa uaminifu ujumbe wa Yehova wa kuonya. (2 Petro 2:5) Kazi hiyo ilimusaidia aendelee kuwa na imani yenye nguvu. Zaidi ya kazi ya kuhubiri, Noa alifuata maagizo ya Yehova juu ya kujenga safina.—Soma Waebrania 11:7.

9. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Noa?

9 Kama Noa, tuko na mengi ya kufanya “katika kazi ya Bwana.” (1 Wakorintho 15:58) Kwa mufano, tunaweza kusaidia katika kazi ya ujenzi na kutunza Majumba yetu ya Ufalme na Majumba yetu ya Mikusanyiko, kujitolea kufanya kazi kwenye mikusanyiko, kutumika kwenye biro ya tawi ao kwenye biro ya kutafsiri. Jambo la maana zaidi, tunaendelea kuwa na mengi ya kufanya katika kazi yenye inatia nguvu tumaini letu kwa ajili ya wakati unaokuja, ni kusema, kazi ya kuhubiri. Dada mumoja muaminifu alisema kama wakati anazungumuza na watu wengine juu ya baraka za Ufalme wa Mungu, anatambua kama watu hawana tumaini kabisa na wanaona kuwa magumu yao yataendelea milele. Kama vile dada huyo alisema, tuko na tumaini, na linakuwa lenye nguvu zaidi wakati tunazungumuza na watu juu ya tumaini hilo. Tumaini hilo linatusaidia tubakie katika mbio ya uzima!—1 Wakorintho 9:24.

WAKATI TUNAFANYA ZAMBI

10. Daudi alikuwa katika hali gani? Eleza.

10 Mufalme Daudi alikuwa mwanaume muaminifu, na Yehova alimupenda sana. (Matendo 13:22) Hata hivyo, Daudi alifanya uzinifu na Bath-sheba, hiyo ilikuwa zambi nzito. Jambo la mubaya zaidi, alitafuta kuficha zambi yake kwa kufanya mipango ili Uriya, bwana ya Bath-sheba, auawe kwenye vita. Pia, Daudi alimutuma Uriya na barua yenye kuwa na maagizo juu ya kifo chake mwenyewe! (2 Samweli 11:1-21) Mwishowe, zambi za Daudi zilijulikana. (Marko 4:22) Wakati jambo hilo lilitokea, Daudi alitenda namna gani?

Zambi za zamani (Picha hizi zinapatana na fungu la 11-14)

11, 12. (a) Kisha kufanya zambi, ni mambo gani yenye Daudi hangeweza kufanya? (b) Yehova atatufanyia mambo gani ikiwa tunatubu?

11 Mambo yenye Daudi hangeweza kufanya: Daudi hangeweza kubadilisha mambo yenye alikuwa amefanya. Kwa kweli, angepatwa na matokeo fulani ya zambi yake katika maisha yake yote. (2 Samweli 12:10-12, 14) Kwa hiyo, alipaswa kuwa na imani. Alipaswa kuwa na tumaini kama ikiwa angetubu kabisa, Yehova angemusamehe na kumusaidia avumilie matokeo ya matendo yake.

12 Kwa sababu hatukamilike, sisi wote tunafanya zambi. Lakini zambi fulani ziko nzito zaidi kuliko zingine, na wakati fulani tunaweza kushindwa kuepuka matokeo ya makosa yetu. Sisi pia tunaweza kupatwa na matokeo ya matendo yetu. (Wagalatia 6:7) Lakini tunatumainia ahadi ya Mungu kuwa ikiwa tunatubu, atatusaidia wakati tunapatwa na magumu, hata kama magumu hayo yametupata kwa sababu ya makosa yetu.​—Soma Isaya 1:18, 19; Matendo 3:19.

13. Namna gani Daudi alitengeneza urafiki wake pamoja na Yehova?

13 Mambo yenye Daudi angeweza kufanya: Daudi alipenda kutengeneza urafiki wake pamoja na Yehova. Namna gani alifanya hivyo? Daudi aliacha Yehova amusaidie. Kwa mufano, alikubali mashauri yenye Nathani, nabii wa Yehova, alimutolea. (2 Samweli 12:13) Pia, Daudi alisali kwa Yehova na kuungama zambi zake ili kuonyesha kabisa kama alipenda Yehova amukubali tena. (Zaburi 51:1-17) Kuliko kujilaumu sana kwa sababu ya makosa yake, Daudi alijifunza mambo fulani kupitia makosa hayo. Hakurudilia hata kidogo zambi hizo nzito. Kisha miaka fulani, alikufa akiwa mwanaume muaminifu, na Yehova anaendelea kumukumbuka hivyo.—Waebrania 11:32-34.

14. Mufano wa Daudi unaweza kutufundisha nini?

14 Mufano wa Daudi unaweza kutufundisha nini? Ikiwa tunafanya zambi nzito, tunapaswa kutubu kweli-kweli, kuungama zambi yetu kwa Yehova, na kumuomba atusamehe. (1 Yohana 1:9) Tunapaswa pia kuzungumuza na wazee, kwa sababu wanaweza kutusaidia kutengeneza urafiki wetu pamoja na Yehova. (Soma Yakobo 5:14-16.) Wakati tunakubali musaada wa Yehova, tunaonyesha kama tunatumainia ahadi yake ya kutusamehe. Zaidi ya hilo, tunapaswa kujifunza mambo fulani kupitia makosa yetu na kuendelea kumutumikia Yehova kwa moyo wote.—Waebrania 12:12, 13.

KATIKA HALI ZINGINE

Magonjwa (Picha hizi zinapatana na fungu la 15)

15 Pengine unaweza kufikiria watumishi wengine waaminifu wenye kuzungumuziwa katika Biblia wenye walitegemea Yehova na kuendelea kufanya mambo yenye waliweza kufanya katika hali ngumu. Kwa mufano, wakati fulani Hana hakuweza kuwa na watoto. Hangeweza kubadilisha hali hiyo. Lakini alitumaini kuwa Yehova angemufariji. Kwa hiyo, aliendelea kuabudu kwenye tabenakulo na kusali kwa Yehova na kumuambia mambo yenye yalikuwa katika moyo wake. (1 Samweli 1:9-11) Huo ni mufano muzuri zaidi kwetu! Wakati tuko na magonjwa fulani ao matatizo mengine yenye hatuwezi kumaliza, tunamutupia Yehova mahangaiko yetu na kutumaini kuwa atatuhangaikia. (1 Petro 5:6, 7) Na tunajikaza ili kupata faida kupitia mikutano ya Kikristo na programu zingine zenye tengenezo la Yehova linatutolea.—Waebrania 10:24, 25.

Watoto wenye wameacha kumutumikia Yehova (Picha hizi zinapatana na fungu la 16)

16. Mufano wa Samweli unaweza kufundisha wazazi nini?

16 Tuseme nini juu ya wazazi waaminifu wenye watoto wao wameacha kumutumikia Yehova? Nabii Samweli hangeweza kukaza watoto wake wanaume wenye kukomaa waendelee kuwa washikamanifu kwa Mungu. (1 Samweli 8:1-3) Alipaswa kuacha mambo katika mikono ya Yehova. Lakini, Samweli alifanya mambo yenye aliweza kufanya ili aendelee kuwa mushikamanifu kwa Mungu na kufurahisha Baba yake wa mbinguni. (Methali 27:11) Leo, wazazi wengi Wakristo wako katika hali kama hiyo. Wanatumaini kuwa, kama ule baba mwenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu wa mwana mupotevu, sikuzote Yehova anakuwa tayari kukaribisha watenda-zambi wenye kutubu. (Luka 15:20) Wakati huo-huo, wazazi wanaweza kukaza akili yao juu ya ushikamanifu wao kwa Yehova, na kutumaini kuwa mufano wao utachochea watoto wao wamurudilie Yehova.

Magumu ya kupata feza (Picha hizi zinapatana na fungu la 17)

17. Sababu gani mufano wa mujane masikini unatutia moyo?

17 Mufano mwengine wa muzuri ni wa mujane masikini wa wakati wa Yesu. (Soma Luka 21:1-4.) Hangeweza kufanya jambo lolote juu ya mambo ya udanganyifu yenye yalikuwa yanafanywa kwenye hekalu, na hangeweza kubadilisha hali yake ya umasikini. (Mathayo 21:12, 13) Lakini tumaini lake kwa Yehova lilimuchochea ategemeze ibada ya kweli. Alionyesha ukarimu na kutoa “sarafu [vichele] ndogo mbili,” na hizo ndizo feza zote zenye alikuwa nazo. Mwanamuke huyo muaminifu alionyesha kama anamutegemea Yehova kabisa. Alijua kama ikiwa anatia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza, Yehova angemupatia mambo yenye alikuwa nayo lazima. Vilevile, tunatumaini kuwa ikiwa tunatia Ufalme wa Mungu pa nafasi ya kwanza, Yehova atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima.​—Mathayo 6:33.

18. Toa mufano wa ndugu mumoja mwenye alikuwa na mawazo ya muzuri.

18 Leo, ndugu na dada wengi wanaonyesha tumaini kama hilo kwa Yehova kwa kukaza akili yao juu ya mambo yenye wanaweza kufanya kuliko kukazia mambo yenye hawawezi kufanya. Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Malcolm; ndugu huyo aliendelea kuwa muaminifu mupaka kifo chake katika mwaka wa 2015. Katika miaka mingi yenye yeye na bibi yake walimutumikia Yehova, walipata furaha na magumu pia. Alisema hivi: “Maisha ni magumu na mara nyingi hatujue yatakuwa namna gani wakati unaokuja. Lakini Yehova anawabariki wale wanaomutegemea.” Malcolm alitoa shauri gani? Alisema hivi: “Umuombe Yehova akusaidie ukuwe na bidii na upate matokeo ya muzuri katika kazi yake kadiri inawezekana. Kazia uangalifu yale unayoweza kufanya, wala si yale ambayo hauwezi kufanya.” *—Soma maelezo ya chini.

19. (a) Sababu gani andiko letu la mwaka wa 2017 ni lenye kufaa? (b) Namna gani utatumikisha andiko la mwaka wa 2017 katika maisha yako?

19 Ulimwengu huu muovu unaendelea ‘kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi,’ kwa hiyo tujue kama magumu yatakuwa mengi zaidi na zaidi. (2 Timotheo 3:1, 13) Kuliko wakati mwengine wowote, ni jambo la maana sana leo tuepuke kuhangaika sana juu ya magumu yetu. Lakini, tunapaswa kumutegemea zaidi Yehova na kukaza akili yetu juu ya mambo yenye tunaweza kufanya. Ndiyo sababu andiko letu la mwaka wa 2017 ni lenye kufaa. Linasema hivi: ‘Umutegemee Yehova na ufanye mema’!—Zaburi 37:3.

^ fu. 18 Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2013, ukurasa wa 17 mupaka wa 20.