Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anaongoza Watu Wake

Yehova Anaongoza Watu Wake

“Yehova hatakosa kukuongoza sikuzote.”—ISAYA 58:11.

NYIMBO: 152, 22

1, 2. (a) Namna gani Mashahidi wa Yehova wako tofauti na dini zingine? (b) Tutajifunza nini katika habari hii na ile yenye kufuata?

MARA nyingi watu wanauliza Mashahidi wa Yehova hivi: “Kiongozi wenu ni nani?” Wanauliza hivyo kwa sababu dini nyingi ziko na kiongozi fulani mwanaume ao mwanamuke. Lakini, sisi tunafurahi kusema kama Kiongozi wetu haiko mwanadamu mwenye hakamilike. Kiongozi wetu ni Yesu Kristo! Na anatii Yehova, Baba na Kiongozi wake.—Mathayo 23:10.

2 Pia kuko kikundi cha wanaume chenye kuitwa ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara,’ wenye kuongoza watu wa Mungu katika dunia leo. (Mathayo 24:45) Lakini namna gani tunajua kama Yehova ndiye anaongoza watu wake kupitia Mwana wake? Tutaona sababu tatu zenye kutuhakikishia jambo hilo. Na hata kama Yehova amekuwa akitumikisha wanadamu ili kuongoza watu wake, itaonekana wazi kama Yehova alikuwa na anaendelea kuwa kabisa Kiongozi wa watu wake.—Isaya 58:11.

ROHO TAKATIFU ILIWATIA NGUVU

3. Ni nini ilitia Musa nguvu ili aongoze taifa la Israeli?

3 Roho takatifu ilitia nguvu wanaume wenye Mungu alitumia ili kuongoza watu wake. Mungu alichagua Musa akuwe kiongozi wa Waisraeli. Ni nini ilimusaidia kutimiza mugawo huo wa maana sana? Yehova alipatia Musa “roho yake takatifu.” (Soma Isaya 63:11-14.) Kwa hiyo, Yehova alikuwa anaongoza kabisa watu wake kwa sababu ni roho yake ndiyo ilikuwa inasaidia Musa.

4. Ni nini ilihakikisha kama Musa alikuwa na roho ya Mungu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Watu wangeweza kuona kama Musa alikuwa na roho ya Mungu? Ndiyo! Roho takatifu ya Yehova ilipatia Musa uwezo wa kufanya miujiza na kujulisha jina la Mungu kwa Farao, Mutawala mwenye nguvu wa Misri. (Kutoka 7:1-3) Roho takatifu ilisaidia pia Musa kuwa kiongozi mwenye upendo na muvumilivu. Alikuwa tofauti sana na viongozi wakali na wenye kujipenda wenyewe wa inchi zingine! (Kutoka 5:2, 6-9) Ni wazi kwamba Yehova alikuwa amechagua Musa kuwa kiongozi wa watu wake.

5. Ni nani wengine wenye Yehova alipatia roho takatifu ili kuongoza watu wake?

5 Ni nani wengine wenye Yehova alipatia roho takatifu ili kuongoza watu wake? Biblia inasema hivi: “Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejaa roho ya hekima.” (Kumbukumbu la Torati 34:9) ‘Roho ya Yehova ikamufunika Gideoni.’ (Waamuzi 6:34) Na “roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu ya Daudi.” (1 Samweli 16:13) Wanaume hao wote walitegemea roho ya Mungu ili iwasaidie kufanya mambo yenye hawangeweza kufanya kwa nguvu yao wenyewe. (Yoshua 11:16, 17; Waamuzi 7:7, 22; 1 Samweli 17:37, 50) Ni wazi kwamba Yehova ndiye aliwapatia nguvu ya kufanya mambo makubwa, kwa hiyo, ni yeye tu ndiye alistahili kusifiwa.

6. Sababu gani Mungu alipenda watu wake waheshimie viongozi katika Israeli?

6 Waisraeli walipaswa kufanya nini wakati waliona kuwa roho ya Mungu ilikuwa imetia nguvu Musa, Yoshua, Gideoni, na Daudi? Walipaswa kuwaheshimia. Wakati watu walikuwa wananungunika juu ya Musa, Yehova aliuliza hivi: ‘Watu hawa wataendelea kunitendea bila heshima mupaka wakati gani?’ (Hesabu 14:2, 11) Ni wazi kwamba Yehova alichagua wanaume hao ili kuongoza watu wake. Wakati watu walitii wanaume hao, walikuwa wanamufuata kabisa Yehova kuwa Kiongozi wao.

MALAIKA WALIWASAIDIA

7. Namna gani malaika walisaidia Musa?

7 Malaika walisaidia wanaume wenye Mungu alitumia ili kuongoza watu wake. (Soma Waebrania 1:7, 14.) Mungu alitumia malaika ili kuongoza Musa. Kwanza, malaika mumoja ‘alimutokea katika muti wa miiba’ na kumupatia mugawo wa kukomboa Waisraeli na kuwaongoza. (Matendo 7:35) Pili, Mungu alitumia malaika ili kupatia Musa Sheria ya kufundisha Waisraeli. (Wagalatia 3:19) Tatu, Yehova alimuambia hivi: “Waongoze watu kwenda mahali nilipokuambia juu yake. Tazama! Malaika wangu ataenda mbele yako.” (Kutoka 32:34) Biblia haiseme kama Waisraeli waliona malaika anafanya mambo hayo. Lakini, namna Musa alifundisha na kuongoza watu, ilionyesha wazi kama malaika walimusaidia.

8. Namna gani malaika walisaidia Yoshua na Hezekia?

8 Malaika walisaidia nani wengine? Biblia inasema kama malaika mumoja, ‘mukubwa wa jeshi la Yehova,’ alisaidia Yoshua kupata ushindi katika vita yenye alipigana na Wakanaani. (Yoshua 5:13-15; 6:2, 21) Kisha, wakati Mufalme Hezekia alikuwa anaongoza watu wa Mungu, jeshi kubwa la Ashuru lilitafuta kuharibu Yerusalemu. Katika usiku mumoja, “malaika wa Yehova alitoka, akapiga na kuwaua watu 185000.”—2 Wafalme 19:35.

9. Hata kama wanaume wenye Mungu alitumia ili kuongoza hawakukuwa wakamilifu, Waisraeli walipaswa kufanya nini?

9 Malaika ni wakamilifu. Lakini, wanaume wenye walisaidia hawakukuwa wakamilifu. Kwa mufano, siku moja Musa hakumutukuza Yehova. (Hesabu 20:12) Yoshua hakumuuliza Mungu jambo la kufanya wakati Wagibeoni walitaka kufanya mapatano pamoja naye. (Yoshua 9:14, 15) Wakati fulani, Hezekia alikuwa na kiburi. (2 Mambo ya Nyakati 32:25, 26) Hata kama wanaume hao hawakukuwa wakamilifu, Waisraeli walipaswa kufuata muongozo wao. Waisraeli wangeweza kuona kama Yehova alikuwa anatumia malaika ili kutegemeza wanaume hao. Ni wazi kwamba Yehova alikuwa anaongoza watu wake.

NENO LA MUNGU LILIWAONGOZA

10. Namna gani Musa aliongozwa na Sheria ya Mungu?

10 Neno la Mungu liliongoza wanaume wenye Mungu alitumia ili kuongoza watu wake. Biblia inaita Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli kuwa “Sheria ya Musa.” (1 Wafalme 2:3) Lakini Biblia inaonyesha wazi kama Yehova ndiye alipatia Israeli Sheria hiyo. Na Musa pia alipaswa kuitii. (2 Mambo ya Nyakati 34:14) Kwa mufano kisha Yehova kumuambia ajenge tabenakulo, ‘Musa alifanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemuamuru. Alifanya vivyo hivyo.’—Kutoka 40:1-16.

11, 12. (a) Yoshua na wafalme wenye waliongoza watu wa Mungu walipaswa kufanya nini? (b) Namna gani Neno la Mungu liliongoza wanaume wenye waliongoza watu wa Mungu?

11 Yoshua alikuwa na sehemu ya Neno la Mungu wakati alichaguliwa kuwa kiongozi, na Yehova alimuambia hivi: ‘Nawe uisome kwa sauti ya chini muchana na usiku, upate kuangalia kufanya kulingana na yote ambayo yameandikwa ndani yake.’ (Yoshua 1:8) Wafalme wenye walifikia kuongoza watu wa Mungu walipaswa pia kusoma Sheria hiyo kila siku, kuandika kopi ya sheria hiyo, na kutii ‘maneno yote ya sheria hiyo na masharti [kanuni] hayo kwa kuyafanya.’—Soma Kumbukumbu la Torati 17:18-20.

12 Namna gani Neno la Mungu liliongoza wanaume wenye waliongoza watu wa Mungu? Fikiria mufano wa Mufalme Yosia. Kisha kupata Sheria ya Musa, mwandishi wa Yosia akaanza kumusomea Sheria hiyo. * (Soma maelezo ya chini.) ‘Mara tu mufalme alipoyasikia maneno ya kile kitabu cha ile sheria, akayararua [akayapasua] mavazi yake mara moja.’ Kisha, Neno la Mungu lilimuchochea Yosia kuharibu sanamu zote zenye zilikuwa katika inchi na kupanga kufanya Pasaka kubwa zaidi yenye ilikuwa haijafanywa hata kidogo. (2 Wafalme 22:11; 23:1-23) Kwa sababu Yosia na viongozi wengine waaminifu walifuata Neno la Mungu, walikuwa tayari kubadilisha muongozo wenye walikuwa wanatolea watu wa Mungu. Mabadiliko hayo yalisaidia watu wa Mungu wamutii.

13. Namna gani viongozi wa watu wa Mungu walikuwa tofauti na viongozi wa mataifa mengine?

13 Viongozi wa mataifa mengine waliongozwa na hekima ya wanadamu yenye kuwa na mipaka. Kwa mufano, viongozi Wakanaani na watu wao walifanya mambo ya mubaya sana, kama vile ngono kati ya watu wa familia moja, mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke, ngono kati ya mutu na munyama, kutoa watoto kuwa zabihu, na ibada ya sanamu. (Mambo ya Walawi 18:6, 21-25) Pia, viongozi Wababiloni na Wamisri hawakukuwa na sheria zilezile juu ya usafi zenye watu wa Mungu walikuwa nazo. (Hesabu 19:13) Lakini, watu wa Mungu wangeweza kuona namna viongozi wao waaminifu waliwatia moyo ili waendelee kufanya ibada yao ikuwe safi, wakuwe safi kimwili, na waepuke mambo machafu ya uasherati. Ni wazi kwamba Yehova alikuwa anawaongoza.

14. Sababu gani Yehova alipatia viongozi fulani wa watu wake malipizi?

14 Haiko wafalme wote wenye waliongoza watu wa Mungu ndio walifuata maagizo ya Mungu. Wafalme hao wenye kukosa uaminifu hawakumutii Mungu hata kidogo na walikataa kufuata muongozo wa roho takatifu ya Mungu, malaika zake, na Neno lake. Katika hali fulani, Yehova alipatia viongozi hao malipizi ao kuwatosha na kuweka wengine. (1 Samweli 13:13, 14) Kisha, Yehova aliweka mutu mwenye angekuwa kiongozi mukamilifu.

YEHOVA ANAWEKA KIONGOZI MUKAMILIFU

15. (a) Namna gani manabii walionyesha kuwa kiongozi mukamilifu alikuwa anakuja? (b) Kiongozi mukamilifu alikuwa nani?

15 Kwa mamia ya miaka, Yehova aliahidi kuwa angeweka kiongozi mukamilifu ili aongoze watu wake. Kwa mufano, Musa aliambia Waisraeli hivi: ‘Nabii kutoka katikati yako mwenyewe, kutoka kwa ndugu zako, kama mimi, ndiye ambaye Yehova Mungu wako atakuinulia. Ninyi munapaswa kumusikiliza yeye.’ (Kumbukumbu la Torati 18:15) Isaya alisema kuwa Mutu huyo angekuwa “kiongozi na kamanda.” (Isaya 55:4) Na Danieli aliandika juu ya Masiya, mwenye angekuwa “Kiongozi.” (Danieli 9:25) Mwishowe, Yesu Kristo alijionyesha mwenyewe kuwa “Kiongozi” wa watu wa Mungu. (Soma Mathayo 23:10.) Wanafunzi wa Yesu walikuwa tayari kumufuata, na waliamini kuwa yeye ndiye Yehova alichagua. (Yohana 6:68, 69) Ni nini iliwahakikishia kama Yesu Kristo alikuwa mutu mwenye Yehova angetumia ili kuongoza watu wake?

16. Ni nini ilionyesha kuwa Yesu alitiwa nguvu na roho takatifu?

16 Roho takatifu ilitia Yesu nguvu. Wakati Yesu alibatizwa, Yohana aliona “mbingu zikifunguka, na roho ikashuka juu yake kama njiwa.” Kisha tu hapo, ‘ile roho ikamushurutisha [ikamulazimisha] aende nyikani [katika jangwa].’ (Marko 1:10-12) Wakati Yesu alikuwa anafanya kazi ya kuhubiri katika dunia, roho ya Mungu ilimutia nguvu ya kufundisha na kufanya miujiza. (Matendo 10:38) Zaidi ya hilo, roho ya Mungu ilisaidia Yesu aonyeshe sifa kama vile upendo, shangwe, na imani yenye nguvu. (Yohana 15:9; Waebrania 12:2) Hakuna kiongozi mwengine mwenye alionekana waziwazi kabisa kuwa na roho takatifu ya Mungu kama yeye. Ni wazi kwamba Yehova alikuwa amemuchagua Yesu kuwa Kiongozi.

Namna gani malaika walisaidia Yesu kisha kubatizwa kwake? (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17. Malaika walifanya nini ili kumusaidia Yesu?

17 Malaika walimusaidia Yesu. Kisha tu Yesu kubatizwa, ‘malaika wakakuja na kuanza kumuhudumia [kumutumikia].’ (Mathayo 4:11) Muda mufupi tu mbele ya kifo chake, ‘malaika kutoka mbinguni akamutokea akamutia nguvu.’ (Luka 22:43) Yesu alijua kuwa Yehova angetuma malaika ili wamusaidie wakati wowote alikuwa na lazima ya musaada.​—Mathayo 26:53.

18, 19. Namna gani Neno la Mungu liliongoza maisha na mafundisho ya Yesu?

18 Neno la Mungu lilimuongoza Yesu. Kuanzia mwanzo wa kazi yake ya kuhubiri mupaka kifo chake kwenye muti wa mateso, Yesu aliacha Maandiko yamuongoze. Hata wakati alikaribia kufa, alizungumuzia unabii mbalimbali juu ya Masiya. (Mathayo 4:4; 27:46; Luka 23:46) Lakini, viongozi wa dini wa wakati huo walikuwa tofauti sana na Yesu. Hawakufuata Neno la Mungu kila wakati halikupatana na mafundisho yao. Yesu alitaja maneno ya Neno la Mungu wakati aliwaambia hivi: ‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, bali moyo wao umepelekwa mbali nami. Wao wananiabudu bure, kwa sababu wao wanafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’ (Mathayo 15:7-9) Yehova hangeweza hata kidogo kuchagua wanaume wenye hawakufuata Neno lake ili kuongoza watu wake.

19 Pia, Yesu alitumia Neno la Mungu wakati alifundisha wengine. Wakati viongozi wa dini walimupinga, hakutumia hekima yake mwenyewe ao uzoefu wake ili kuwajibia. Lakini, alitumia Maandiko ili kufundisha watu. (Mathayo 22:33-40) Pia, Yesu angeshangaza sana watu kwa kuwaelezea habari juu ya maisha yake ya mbinguni ao habari ya uumbaji wa ulimwengu. Lakini, kwa sababu alipenda Neno la Mungu alifurahia sana kuelezea wengine juu ya Neno hilo, na “akafungua akili zao ili kuifahamu maana ya Maandiko.”—Luka 24:32, 45.

20. (a) Namna gani Yesu alimupatia Yehova utukufu? (b) Namna gani mawazo ya Yesu yalikuwa tofauti na ya Herode Agripa wa Kwanza?

20 Hata kama wasikiliza wa Yesu walishangazwa na namna yake ya kuzungumuza, kila mara alikuwa anapatia utukufu Yehova, Mwalimu wake. (Luka 4:22) Wakati mwanaume mumoja tajiri alijaribu kupatia Yesu utukufu kwa kumuita “Mwalimu Mwema,” Yesu alikuwa munyenyekevu na alimuambia hivi: ‘Kwa nini unaniita mwema? Hakuna mutu aliye mwema, ila mumoja, Mungu.’ (Marko 10:17, 18) Lakini, Herode Agripa wa Kwanza mwenye alikuwa kiongozi wa Yudea, miaka munane hivi kisha hapo, alikuwa na mawazo yenye kuwa tofauti sana na ya Yesu! Siku moja, kwenye mukutano fulani wa pekee, Herode alivaa nguo ya kifalme yenye kupendeza sana na ya bei sana. Wakati watu walimuona na kumusikiliza, walisema hivi kwa sauti kubwa: “Ni sauti ya mungu, wala si ya mwanadamu!” Herode alipenda watu wamusifu. Lakini, ni nini ilitokea kisha? ‘Papo hapo malaika wa Yehova akamupiga, kwa sababu hakumupa Mungu utukufu; naye akakuliwa na wadudu akakata pumuzi.’ (Matendo 12:21-23) Ni wazi kwamba Yehova hakukuwa amemuchagua Herode kuwa kiongozi. Lakini, Yesu alionyesha wazi kwamba Mungu alikuwa amemuchagua, na kila mara alimutukuza Yehova kuwa Kiongozi Mukubwa Zaidi wa watu wake.

21. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

21 Yehova alipenda Yesu akuwe Kiongozi kwa miaka mingi. Kisha ufufuo wake, Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.” Aliongezea hivi: ‘Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mathayo 28:18-20) Lakini, kwa sababu Yesu iko mbinguni na haonekane, namna gani anaweza kuongoza watu wa Mungu katika dunia? Yehova angetumia nani ili kuwakilisha Yesu katika dunia? Na namna gani Wakristo wangeweza kutambua wanaume wenye Mungu anatumia ili kuongoza watu wake? Habari yenye kufuata itatoa majibu ya maulizo hayo.

^ fu. 12 Pengine Sheria hiyo ni ile yenye Musa mwenyewe aliandika.