Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Heshimia Wale Wenye Kustahili Heshima

Heshimia Wale Wenye Kustahili Heshima

“Kwake Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme na kwa Mwana-Kondoo kuwe na baraka na heshima na utukufu na nguvu milele na milele.”—UFUNUO 5:13.

NYIMBO: 9, 108

1. Sababu gani watu fulani wanastahili heshima, na tutajifunza nini katika habari hii?

NAMNA gani tunaheshimia watu? Tunafanya hivyo kwa kuwatendea kwa njia fulani ya pekee na kuwatii. Kwa kawaida, tunaheshimia wale wenye wamekwisha kufanya jambo lenye kustahili heshima ao wale wenye kuwa na mugawo ao cheo fulani cha maana. Katika habari hii, tutajua wale wenye tunapaswa kuheshimia na sababu gani.

2, 3. (a) Sababu gani Yehova anastahili kabisa kuheshimiwa? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Mwana-Kondoo mwenye kuzungumuziwa katika Ufunuo 5:13 ni nani, na sababu gani tunapaswa kumuheshimia?

2 Andiko la Ufunuo 5:13 linasema kama “Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme” na “Mwana-Kondoo” wanastahili heshima. “Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme” ni Yehova. Katika sura ya 4 ya kitabu cha Ufunuo, viumbe wa mbinguni wanatutolea sababu moja yenye kufanya Yehova, “Yule anayeishi milele na milele,” astahili kuheshimiwa. Wanasema hivi: “Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”—Ufunuo 4:9-11.

3 “Mwana-Kondoo” mwenye kuzungumuziwa katika Ufunuo 5:13 ni Yesu Kristo. Namna gani tunajua hilo? Wakati alikuwa katika dunia, Yesu aliitwa ‘Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye anaondolea mbali zambi ya ulimwengu.’ (Yohana 1:29) Ni mufalme gani mwingine mwenye amekwisha kutoa uzima wake kwa kupenda ili ukuwe zabihu ya ukombozi kwa ajili ya watu wenye anaongoza? Hiyo ni sababu ya muzuri kabisa yenye inafanya aheshimiwe. Yesu anastahili kuheshimiwa kwa sababu ‘yeye ni Mufalme wa wale wanaotawala wakiwa wafalme na Bwana wa wale wanaotawala wakiwa mabwana.’ (1 Timotheo 6:14-16) Pengine unajisikia kama viumbe wa mbinguni wenye wanaimba hivi: “Mwana-Kondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”—Ufunuo 5:12.

4. Sababu gani ni jambo la hekima tuheshimie Yehova na Kristo?

4 Andiko la Yohana 5:22, 23 linasema kama Yehova amemufanya Kristo kuwa muamuzi wa wanadamu wote. Hiyo ni sababu kubwa yenye inafanya Yesu astahili kuheshimiwa. Na wakati tunamuheshimia, tunamuheshimia pia Yehova. Wakati tunachagua kuheshimia Yesu na Baba yake, tunaweza kupata uzima wa milele.—Soma Zaburi 2:11, 12.

5. Sababu gani watu wote wanastahili kupewa heshima kwa kiasi fulani?

5 Wanadamu waliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu.’ (Mwanzo 1:27) Hilo linamaanisha kuwa watu wengi zaidi wako na uwezo wa kuonyesha sifa zenye kufanana na za Mungu. Kwa mufano, wanadamu wanaweza kuonyesha sifa kama vile upendo, wema, na huruma. Pia, wanadamu waliumbwa na zamiri, ni kusema, uwezo wa kujua mema ao mabaya, ukweli ao udanganyifu, mambo yenye kufaa ao yenye hayafae. (Waroma 2:14, 15) Watu wengi zaidi wanapenda mambo yenye kuwa safi na ya muzuri sana na wanapenda kuishi katika amani pamoja na wengine. Hilo halitushangaze, kwa sababu Yehova ni Mungu mwenye kupanga mambo muzuri na mwenye amani. Ni wazi kwamba wanadamu wote waliumbwa na uwezo wa kumuiga Yehova katika njia mbalimbali. Kwa hiyo, tunapaswa kuwaheshimia.​—Zaburi 8:5.

ONYESHA HESHIMA KATIKA NJIA YENYE KUFAA

6, 7. Namna gani Mashahidi wa Yehova wako tofauti na watu wengi wakati wanaonyesha wengine heshima?

6 Tunajua kama wanadamu wengine wanapaswa kuheshimiwa, lakini inaweza kuwa vigumu kujua ikiwa tutawaonyesha heshima ya namna gani, na kwa kiasi gani. Ni kwa sababu wanadamu wengi wenye hawakamilike wanachochewa sana na mawazo ya ulimwengu wa Shetani. Watu wengi wanaabudu wanaume ao wanawake. Kuliko kuwapatia heshima yenye Yehova anapenda wapate, watu wanawapatia wanadamu wengine heshima nyingi sana, kwa kuwatendea kama miungu. Wanaiga muvalio, mwenendo, na tabia za viongozi wa politike na wa dini, wachezaji wa michezo mbalimbali, wachezaji wa filme, na watu wengine wenye kujulikana sana.

7 Wakristo wa kweli wanajua kama itakuwa mubaya kuonyesha wanadamu heshima yenye kupita mipaka. Kati ya watu wote wenye wamekwisha kuishi, Yesu tu ndiye alituachia mufano mukamilifu wa kuiga. (1 Petro 2:21) Tunapaswa kukumbuka kama ‘wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.’ (Waroma 3:23) Hakuna mwanadamu mwenye anastahili kupewa ibada. Wakati tunaonyesha wanadamu heshima yenye kupita mipaka, hilo halimufurahishe Yehova.

8, 9. (a) Namna gani Mashahidi wa Yehova wanaona wakubwa wa serikali? (b) Ni wakati gani hatuwezi kutii wakubwa wa serikali?

8 Kuko watu fulani wenye tunapaswa kuheshimia ao kutii kwa sababu ya cheo chao. Kwa mufano, fikiria wakubwa wa serikali na mambo yenye wanafanya kwa ajili yako. Wanasaidia kuleta usalama mahali kwenye tunaishi na kutimizia raia wao mambo ya lazima. Kazi yao inaleta faida nyingi. Mutume Paulo alisema kama tunapaswa kuwaona wakubwa hao wa serikali kuwa “mamlaka zilizo kubwa.” Pia, alisema kama tunapaswa kutii sheria zao. Alisema hivi: ‘Muwape wote haki zao, yeye anayetaka kodi [taxe], kodi,’ na “yeye anayetaka heshima, heshima hiyo.”—Waroma 13:1, 7.

9 Sisi Mashahidi wa Yehova, tunajikaza sana kuonyesha wakubwa wa serikali kuwa tunawatii. Kwa kweli, kila inchi iko na desturi zake; kwa hiyo, mambo yenye viongozi wa serikali wanaweza kutuomba kufanya mahali fulani yanaweza kuwa tofauti mahali pengine. Hata hivyo, tunatii viongozi wa serikali wakati wanafanya kazi yao. Lakini, ikiwa wanatuomba tufanye jambo fulani lenye litafanya tukose kumutii Yehova, hatuwezi kufanya jambo hilo. Katika hali hizo, tunatii na kuheshimia Yehova kuliko watu.​—Soma 1 Petro 2:13-17.

10. Namna gani watumishi wa zamani wa Yehova walituachia mufano wa muzuri leo?

10 Mufano wa watumishi wa zamani wa Yehova wenye waliheshimia serikali na wakubwa wa serikali hizo, unaweza kutufundisha jambo fulani. Yosefu na Maria walituachia mufano muzuri. Wakati Waroma walipenda kujua hesabu ya watu wenye walikuwa wanaishi katika inchi, Yosefu na Maria walifanya safari ya kuenda Bethlehemu ili kujiandikisha hata kama Maria alikuwa karibu sana kuzaa. (Luka 2:1-5) Mutume Paulo ni mutu mwengine mwenye alionyesha mufano wa muzuri wa kuheshimia watawala wanadamu. Wakati alishitakiwa kwamba alifanya jambo fulani la mubaya, alijitetea kwa heshima mbele ya Mufalme Herode Agripa na mbele ya Festo, gavana wa jimbo la Yudea la Utawala wa Roma.​—Matendo 25:1-12; 26:1-3.

11, 12. (a) Sababu gani hatuonyeshe viongozi wa dini heshima ya pekee? (b) Ni nini ilitokea wakati Shahidi fulani wa inchi ya Austria aliheshimia mutu mumoja mwenye kufanya mambo ya politike?

11 Tuseme nini juu ya viongozi wa dini? Tunapaswa kuwaonyesha heshima ya pekee? Tunawaonyesha heshima yenye tunaonyesha watu wengine wote. Lakini itakuwa mubaya kuwaonyesha heshima ya pekee, hata kama wanapenda kupewa heshima hiyo. Sababu gani? Kwa sababu dini za uongo hazifundishe kweli juu ya Mungu na Neno lake, Biblia. Yesu alionyesha wazi tabia za walimu wa dini za uongo na aliwaita wanafiki na viongozi wabaya. (Mathayo 23:23, 24) Kwa upande mwingine, haitakuwa mubaya kutii na kuheshimia wakubwa wa serikali kwa njia fulani ya pekee. Kwa sababu ya kufanya hivyo, wametusaidia wakati fulani.

12 Mumoja kati ya wakubwa hao alikuwa Heinrich Gleissner, mwenye kufanya mambo ya politike wa inchi ya Austria (Autriche). Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, alikamatwa na Wanazi. Wakati alitiwa ndani ya treni ili kupelekwa katika kambi ya mateso, alikutana na Leopold Engleitner, Shahidi mwenye bidii wa inchi ya Austria. Ndugu Engleitner alimuelezea Heinrich Gleissner kwa heshima mambo yenye alikuwa anaamini. Gleissner, alisikiliza kwa uangalifu. Wakati vita ilimalizika, Gleissner alitumia cheo chake ili kusaidia mara kwa mara Mashahidi katika inchi ya Austria. Pengine unajua mifano mingine ya mambo ya muzuri yenye yametokea kwa sababu Wakristo waliheshimia wakubwa wa serikali.

ONYESHA WENGINE HESHIMA

13. Ni nani wenye tunapaswa kabisa kuheshimia, na sababu gani?

13 Tunapaswa kuheshimia ndugu na dada zetu. Zaidi sana ndugu wenye kuongoza, kama vile wazee, waangalizi wa muzunguko, ndugu wa Halmashauri ya Tawi, na ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza. (Soma 1 Timotheo 5:17.) Ndugu wote hao wanahangaikia mahitaji ya watu wa Mungu, na Biblia inazungumuzia watu hao kuwa “zawadi katika wanadamu.” (Waefeso 4:8) Kwa hiyo, tunapaswa kuwaheshimia bila kuangalia taifa lao, masomo yao, cheo chao, ao hali yao ya maisha. Wakristo wa kwanza walituachia mufano wa muzuri. Waliheshimia wanaume wenye walikuwa wanaongoza, na sisi pia tunafanya hivyo leo. Wakati tuko na wanaume hao, hatuwatendee kama malaika, ni kusema, kuwaona kuwa watu wa hali ya juu zaidi. Lakini tunawaheshimia na kuwatii kwa sababu ya kazi yao yenye bidii na unyenyekevu wao.​—Soma 2 Wakorintho 1:24; Ufunuo 19:10.

14, 15. Namna gani wazee Wakristo wako tofauti na viongozi wengi wa dini?

14 Wazee hao wako kama wachungaji wanyenyekevu. Hawapendi tuwatendee kama watu wenye kujulikana sana. Kwa hiyo, wako tofauti sana na viongozi wengi wa dini wa leo na viongozi wa dini wa wakati wa Yesu. Alisema juu yao hivi: ‘Wao wanapenda mahali penye kuonekana zaidi kwenye milo ya jioni [mangaribi] na viti vya mbele katika masinagogi na salamu katika masoko.’—Mathayo 23:6, 7.

15 Wazee wakristo wanatii maneno haya ya Yesu: “Musiitwe Rabi, kwa maana Mwalimu wenu ni mumoja, lakini ninyi nyote ni ndugu. Zaidi ya hayo, musimuite mutu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mumoja, Yule wa mbinguni. Wala musiitwe ‘viongozi,’ kwa maana Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo. Lakini aliye mukubwa zaidi katikati yenu lazima akuwe muhudumu [mutumishi] wenu. Yeyote yule anayejiinua atanyenyekezwa, na yeyote yule anayejinyenyekeza atainuliwa.” (Mathayo 23:8-12) Ikiwa wazee katika makutaniko ya dunia yote wako wanyenyekevu na wanatii maneno ya Yesu, ndugu na dada zao watawapenda, kuwatii na kuwaheshimia.

Wakati wazee wanatumika kwa unyenyekevu, ndugu na dada zao wanawapenda, na kuwaheshimia (Picha hizi zinapatana na fungu la 13-15)

16. Sababu gani tunapaswa kuendelea kujikaza sana ili kuonyesha wengine heshima?

16 Inaweza kutuomba wakati ili tujifunze namna ya kuonyesha wengine heshima. Wakristo wa kwanza walikuwa pia na tatizo hilo. (Matendo 10:22-26; 3 Yohana 9, 10) Lakini kufanya hivyo haiko kazi ya bure. Ikiwa tunaheshimia wengine namna Yehova anapenda tuwaheshimie, tutapata faida nyingi.

FAIDA ZA KUONYESHA WENGINE HESHIMA

17. Kuheshimia watu wenye kuwa na mamlaka kunaleta faida gani?

17 Wakati tunaheshimia watu wenye kuwa na mamlaka katika eneo letu, pengine wanaweza kabisa kutetea haki yetu ya kuhubiri. Wanaweza hata kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi yetu ya kuhubiri. Jambo hilo lilitokea katika inchi ya Ujerumani kumepita miaka mingi wakati painia mumoja mwenye kuitwa Birgit alienda kwenye masomo wakati binti yake alimaliza masomo ya musingi. Walimu walimuambia Birgit kama walikuwa wamefurahi sana kuwa na watoto Mashahidi kwenye masomo yao kwa miaka mingi. Waliona kuwa watoto Mashahidi walifanya masomo ikuwe nafasi ya muzuri zaidi. Birgit aliwaambia hivi: “Watoto wetu wanafundishwa kutii kanuni za Mungu za mwenendo muzuri, na pia kuwaheshimia walimu.” Mwalimu mumoja alisema kuwa ikiwa watoto wote walikuwa kama Mashahidi, kazi ya kufundisha ingekuwa mwepesi. Walikuwa na mawazo hayo ya muzuri juu ya watoto Mashahidi, na hilo lilifanya mumoja kati ya walimu hao ahuzurie mukusanyiko wetu mumoja kisha majuma fulani.

18, 19. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunaheshimia wazee?

18 Kanuni zenye kuwa katika Neno la Mungu zinaweza kutusaidia kuelewa namna ya kuheshimia wazee wa kutaniko. (Soma Waebrania 13:7, 17.) Tunaweza na tunapaswa kuwapongeza kwa kazi yao ngumu. Wakati tunatii muongozo wenye wanatutolea, hilo litawasaidia wazee watumike kwa furaha. Biblia inasema kama tunapaswa pia kuiga imani yao. Lakini hilo halimaanishe kama tunapaswa kujikaza kuiga kabisa-kabisa muvalio, namna ya kusema, na namna ya kufundisha ya muzee fulani “mwenye kujulikana sana.” Ikiwa tunafanya hivyo, itakuwa kama vile tuko tunafuata watu kuliko kumufuata Kristo. Tunapaswa kukumbuka kama wazee ni watu wenye hawakamilike kama sisi.

19 Wakati tunaheshimia wazee na kuepuka kuwatendea kama watu wenye kujulikana sana, hilo litawasaidia. Namna gani? Itakuwa mwepesi waendelee kuwa wanyenyekevu na waepuke kufikiri kuwa wao ni watu wa maana sana kuliko wengine ao kufikiri kuwa mambo yenye wanafanya ni yenye kufaa sikuzote.

20. Tunapata faida gani wakati tunaheshimia wengine?

20 Kuheshimia wengine kunatusaidia tuepuke kujipenda sisi wenyewe na kunatusaidia tuendelee kuwa wanyenyekevu wakati tunatendewa kwa njia fulani ya pekee. Pia, hilo linatulinda kwa sababu linatusaidia tuepuke kukwazika wakati mutu fulani mwenye tunaheshimia anafanya jambo fulani lenye kutuvunja moyo. Faida ingine ni kwamba hilo linafanya tuendelee kuwa na umoja katika tengenezo la Yehova. Tengenezo halipatie mwanadamu yeyote heshima yenye kuvuka mipaka, akuwe mutumishi wa Yehova ao hapana.

21. Tutapata faida gani ya maana zaidi wakati tunaonyesha wengine heshima?

21 Faida ya maana zaidi ya kuonyesha wengine heshima ni kwamba, wakati tunafanya hivyo tunamupendeza Mungu. Tutaendelea kufanya mambo yenye anapenda tufanye na kubakia waaminifu kwake. Kwa hiyo, Yehova anaweza kumujibia Shetani, mwenye anasema kama hakuna mutu mwenye anaweza kuwa muaminifu kwa Mungu. (Methali 27:11) Watu wengi zaidi katika ulimwengu hawajue namna ya kuonyesha wengine heshima katika njia yenye kufaa. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu tunajua namna ya kuonyesha heshima katika njia yenye kumupendeza Yehova!