Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utatia Moyo Wako Katika Mambo Yenye Kuandikwa?

Utatia Moyo Wako Katika Mambo Yenye Kuandikwa?

‘Mambo hayo . . . yaliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo.’—1 WAKORINTHO 10:11.

NYIMBO: 11, 61

1, 2. Sababu gani tutazungumuzia mifano ya wafalme ine wa Yuda?

IKIWA unaona mutu fulani anatereza nafasi fulani na kuanguka, pengine wewe pia utakuwa muangalifu kabisa wakati unatembea nafasi hiyo. Vilevile, wakati tunachunguza makosa yenye wengine wamefanya katika maisha yao, tunaweza kuepuka kufanya makosa kama yao. Kwa mufano, makosa ya watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia yanaweza kutufundisha mambo fulani.

2 Wafalme ine wa Yuda wenye tulizungumuzia katika habari yenye ilitangulia walimutumikia Yehova kwa moyo mukamilifu. Lakini waliendelea kufanya makosa mazito. Habari juu ya maisha yao ziliandikwa katika Biblia ili tuweze kufikiri sana juu ya habari hizo na kujifunza mambo ya maana. Mambo yenye yaliwapata yanaweza kutufundisha nini, na namna gani tunaweza kuepuka kufanya makosa kama yao?—Soma Waroma 15:4.

KUTEGEMEA HEKIMA YA MWANADAMU KUNALETA MUSIBA

3-5. (a) Hata kama Asa alimutumikia Yehova kwa moyo mukamilifu, alifanya makosa gani? (b) Ni nini pengine ilimufanya Asa ategemee wanadamu wakati alikuwa anapigana vita na Baasha?

3 Tuzungumuzie kwanza Asa. Alimutegemea Yehova wakati Waethiopia milioni moja walishambulia Yuda. Lakini, hakumutegemea Yehova wakati alipigana vita na Baasha, mufalme wa Israeli. Asa alipenda kumukataza Baasha kujenga Rama, muji wa maana wenye ulikuwa katika Israeli karibu na mupaka wa ufalme wa Yuda. (2 Mambo ya Nyakati 16:1-3) Asa aliamua kama ilikuwa muzuri apatie mufalme wa Siria rushwa (kata-midomo) ili amusaidie. Wakati Wasiria walishambulia miji ya Israeli, Baasha “mara moja akaacha kujenga Rama na kuikomesha [kuacha] kazi yake.” (2 Mambo ya Nyakati 16:5) Mwanzoni, pengine Asa alifikiri kuwa alikamata uamuzi wa muzuri.

4 Lakini Yehova alijisikia namna gani? Yehova hakufurahi kwa sababu Asa hakumutegemea, na alituma nabii Hanani ili amushaurie Asa. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 16:7-9.) Hanani alimuambia Asa hivi: “Tangu sasa na kuendelea kutakuwa na vita juu yako.” Asa alikamata muji wa Rama, lakini katika maisha yake yote, yeye na watu wake walipaswa kupigana vita nyingi.

5 Katika habari yenye ilitangulia, tulijifunza kuwa Yehova alipendezwa na Asa. Hata kama Asa hakukuwa mukamilifu, Mungu aliona kuwa Asa alimutumikia kwa moyo wake wote. (1 Wafalme 15:14) Hata hivyo, wakati Asa alikamata uamuzi wa mubaya, hangeepuka matokeo ya uamuzi wake. Sababu gani alijitegemea yeye mwenyewe na wanadamu wengine kuliko kumutegemea Yehova? Pengine Asa alifikiri kuwa angetumia ufundi wenye akili wa kijeshi ili kupata ushindi. Ao pengine alifuata mashauri ya mubaya yenye wengine walimutolea.

6. Makosa ya Asa yanaweza kutufundisha nini? Toa mufano.

6 Makosa ya Asa yanaweza kutufundisha nini? Katika hali zote, tunapaswa kumutegemea Yehova kuliko kutegemea mawazo yetu wenyewe. Tunapaswa kumuomba musaada, hata kama magumu yetu ni makubwa ao madogo. Ni muzuri kufikiria jambo hili: Wakati fulani tunajitegemea sisi wenyewe ili kujaribu kumaliza magumu fulani katika njia yenye tunaona kuwa ni ya muzuri zaidi? Ao kila mara tunafikiria kwanza mambo yenye Biblia inasema na kisha tunajaribu kutumia habari hizo ili kumaliza magumu yetu? Kwa mufano, fikiria kuwa watu wa familia yako wanakuzuia kuenda kwenye mukutano ao mukusanyiko fulani. Utamuomba Yehova akusaidie ili ujue jambo la kufanya katika hali hiyo? Ao pengine umefanya siku nyingi bila kuwa na kazi, kisha unapata mutu fulani mwenye anapenda kukupatia kazi. Utamuambia kama unapaswa kuenda kwenye mikutano kila juma na kuwa katika hatari ya kukosa kazi hiyo? Hata kama tunapatwa na magumu gani, tunapaswa kukumbuka shauri la muandikaji mumoja wa zaburi. Alisema hivi: ‘Umukabizi [umupatie] Yehova njia yako, na kumutegemea, naye mwenyewe atatenda.’—Zaburi 37:5.

NI NINI INAWEZA KUTOKEA IKIWA TUNACHAGUA MARAFIKI WABAYA?

7, 8. Yehoshafati alifanya makosa gani, na alipata matokeo gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Tuzungumuzie sasa mufano wa Yehoshafati, mutoto mwanaume wa Asa. Alikuwa na sifa nyingi za muzuri zenye zilimupendeza Yehova. Na wakati alimutegemea Yehova, alifanya mambo mengi ya muzuri. Lakini yeye pia alikamata maamuzi fulani ya mubaya. Kwa mufano, alifanya mipango ili mutoto wake mwanaume aoe mutoto mwanamuke mumoja wa Ahabu, mufalme mubaya. Kisha, Yehoshafati alijiunga na Ahabu ili kupigana vita na Wasiria, hata kama nabii Mikaya alimuonya asifanye hivyo. Katika vita hivyo, Wasiria walimushambulia Yehoshafati na kujaribu kumuua. (2 Mambo ya Nyakati 18:1-32) Wakati alirudia Yerusalemu, nabii Yehu alimuuliza hivi: ‘Je, waovu wanapaswa kupewa musaada, na je, unapaswa kuwapenda wale wanaomuchukia Yehova?’—Soma 2 Mambo ya Nyakati 19:1-3.

8 Je, mambo yenye yalimufikia Yehoshafati na mashauri ya nabii, yalimufundisha jambo fulani? Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, hakujifunza jambo lolote. Hata kama alikuwa angali anapenda Yehova na alipenda kumupendeza, Yehoshafati alifanya tena urafiki na mwanaume mwenye hakupenda kumuabudu Yehova. Mwanaume huyo alikuwa Mufalme Ahazia, mutoto mwanaume wa Ahabu. Yehoshafati na Ahazia walitengeneza mashua (bateaux) pamoja. Lakini mashua hizo ziliharibika mbele waanze kuzitumia.​—2 Mambo ya Nyakati 20:35-37.

9. Ni nini inaweza kutufikia ikiwa tunachagua marafiki wabaya?

9 Mambo yenye yalimufikia Yehoshafati yanaweza kutufundisha nini? Yehoshafati alifanya mambo yenye kuwa sawa na ‘alimutafuta Yehova kwa moyo wake wote.’ (2 Mambo ya Nyakati 22:9) Lakini alichagua kupitisha wakati pamoja na watu wenye hawakumuabudu Yehova, na hilo lilimuletea matatizo makubwa katika maisha yake. Kwa kweli, alikuwa karibu kuuawa. Ukumbuke mezali hii ya Biblia yenye kusema hivi: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana [anayefanya urafiki] na wajinga atapatwa na mabaya.” (Methali 13:20) Tunapenda kuzungumuza na wengine juu ya Yehova. Lakini, inaweza kuwa hatari kufanya urafiki wa sana pamoja na watu wenye hawamutumikie Yehova.

10. (a) Ikiwa tunapenda kuoa ao kuolewa, mufano wa Yehoshafati unaweza kutufundisha nini? (b) Tunapaswa kukumbuka nini?

10 Kwa mufano, ikiwa tunapenda kuoa ao kuolewa, mufano wa Yehoshafati unaweza kutufundisha nini? Pengine tunaweza kuanza kuwa na urafiki wa kimapenzi na mutu fulani mwenye hamupendi Yehova. Tunaweza kufikiri kuwa hatutapata mutu fulani mwenye tutaoana naye kati ya watu wa Mungu. Ao watu fulani wa jamaa yetu wanaweza kuendelea kutuambia kama ni lazima tuoe ao kuolewa mbele ya kukomaa sana. Ni kweli kwamba Yehova alituumba na tamaa ya kupenda na kupendwa. Hata hivyo, ikiwa hatuwezi kupata mutu mwenye kufaa wa kuoana naye, tunapaswa kufanya nini? Jambo moja lenye linaweza kutusaidia ni kufikiri sana juu ya mambo yenye yalimufikia Yehoshafati. Alimuomba Yehova muongozo sikuzote. (2 Mambo ya Nyakati 18:4-6) Lakini wakati alifanya urafiki pamoja na Ahabu, mutu mwenye hakumupenda Yehova, Yehoshafati alizarau shauri la Yehova. Yehoshafati alipaswa kukumbuka kama ‘macho yake [Yehova] yanaenda huku na huku duniani kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mukamilifu kumwelekea yeye.’ (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Sisi pia tunapaswa kukumbuka kama Yehova anapenda kutusaidia. Anaelewa hali yetu na anatupenda. Unaamini kuwa ikiwa unapenda kupata mutu wa kuoana naye, Mungu anajua hilo na kwamba atakusaidia? Ukuwe hakika kama atafanya hivyo wakati fulani!

Usifanye urafiki wa kimapenzi na mutu fulani mwenye hamuabudu Yehova (Picha hii inapatana na fungu la 10))

USIACHE MOYO WAKO UKUWE NA MAJIVUNO

11, 12. (a) Hezekia alifanya nini ili kuonyesha mambo yenye yalikuwa katika moyo wake? (b) Sababu gani Yehova alimusamehe Hezekia?

11 Mufano wa Hezekia unaweza kutufundisha nini? Yehova alimusaidia Hezekia kuona kabisa mambo yenye yalikuwa katika moyo wake. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 32:31.) Wakati Hezekia alikuwa mugonjwa, Mungu alimuambia kama angepona na alimutolea alama yenye kumuhakikishia jambo hilo. Yehova alifanya kivuli kirudie nyuma vipandio kumi. Kisha, inaonekana kuwa wakubwa kutoka Babiloni walipenda kujua mengi zaidi juu ya alama hiyo, na walituma wanaume kwa Hezekia ili kumuuliza juu ya jambo hilo. (2 Wafalme 20:8-13; 2 Mambo ya Nyakati 32:24) Yehova hakumuambia Hezekia namna ya kutendea wakubwa hao. Biblia inasema kama Yehova ‘akamuacha’ ili kuona ikiwa angefanya nini. Hezekia alionyesha wanaume hao kutoka Babiloni utajiri wote wenye alikuwa nao. Hilo lilionyesha mambo yenye yalikuwa katika moyo wa Hezekia. Namna gani?

12 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba Hezekia alianza kuwa na majivuno. Kwa hiyo, “hakurudisha kulingana na mema aliyotendewa.” Biblia haiseme sababu gani mawazo yake yalibadilika. Pengine ilikuwa kwa sababu alipata ushindi juu ya Waashuru ao kwa sababu Yehova alikuwa amemuponyesha. Ao pengine ni kwa sababu alikuwa amepata utajiri na kuwa mwenye kujulikana sana. Hata kama Hezekia alimutumikia Yehova kwa moyo mukamilifu, wakati fulani akaanza kuwa na majivuno na hilo halikumupendeza Yehova. Lakini mwishowe, “Hezekia akajinyenyekeza,” na Mungu alimusamehe.​—2 Mambo ya Nyakati 32:25-27; Zaburi 138:6.

13, 14. (a) Ni hali gani inaweza kuonyesha mambo yenye kuwa katika moyo wetu? (b) Tunapaswa kutenda namna gani wakati wengine wanatusifu?

13 Mufano wa Hezekia na makosa yenye alifanya, vinaweza kutufundisha nini? Ukumbuke kama Hezekia alitenda kwa majivuno kisha tu Yehova kumusaidia kupata ushindi juu ya Waashuru na kumuponyesha ugonjwa wake. Kwa hiyo, wakati tunapata matokeo ya muzuri katika jambo fulani ao wakati wengine wanatusifu, tutatenda namna gani? Namna tunatenda inaweza kuonyesha mambo yenye kuwa katika moyo wetu. Kwa mufano, ndugu fulani anaweza kuwa ametumika sana ili kutayarisha hotuba na kuitoa mbele ya wasikilizaji wengi. Watu wengi wanamusifu kwa hotuba yenye ametoa. Atatenda namna gani?

14 Tunapaswa kukumbuka sikuzote maneno haya ya Yesu. Alisema hivi: “Wakati mumefanya mambo yote muliyoagizwa, museme, ‘Sisi ni watumwa wasiofaa kitu. Jambo ambalo tumefanya ndilo tulilopaswa kufanya.’” (Luka 17:10) Ukumbuke kama wakati Hezekia alikuwa na majivuno, hakuonyesha shukrani juu ya namna Yehova alikuwa amemusaidia. Kwa hiyo, wakati wengine wanatusifu juu ya hotuba yenye tulitoa, ni nini inaweza kutusaidia tuendelee kuwa wanyenyekevu? Tunaweza kufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova ametufanyia. Na tunaweza kumushukuru juu ya namna ametusaidia. Kwa kweli, yeye ndiye ametupatia Biblia na roho yake takatifu ili kutusaidia kutoa hotuba hiyo.

UMUACHE YEHOVA AKUONGOZE WAKATI UNAKAMATA MAAMUZI

15, 16. Yosia alifanya jambo gani lenye lilimuletea kifo?

15 Mwishowe, mufano wa Yosia unaweza kutufundisha nini? Hata kama Yosia alikuwa mufalme muzuri, alifanya kosa lenye lilimuletea kifo. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 35:20-22.) Ni nini ilitokea? Yosia alianza kupigana vita na Neko, mufalme wa Misri, hata kama hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo. Kwa kweli, Neko mwenyewe alimuambia Yosia kama hakupenda kupigana vita naye. Biblia inasema kama maneno ya Neko ‘yalitoka kinywani mwa Mungu.’ Lakini Yosia alienda kupigana vita na akauawa. Sasa, sababu gani alipigana vita na Neko? Biblia haiseme.

16 Yosia alipaswa kutafuta kujua ikiwa mambo yenye Neko alikuwa amesema yalitoka kabisa kwa Yehova. Namna gani? Alipaswa kumuuliza Yeremia, nabii moja kati ya manabii wa Yehova. (2 Mambo ya Nyakati 35:23, 25) Pia, Yosia alipaswa kuchunguza mambo muzuri. Neko alikuwa anaenda Karkemishi ili kupigana vita na taifa lingine, hapana Yerusalemu. Na Neko hakujaribu kumutukana Yehova ao watu wake. Yosia hakufikiria kwa uangalifu mambo hayo mbele akamate uamuzi wake. Hilo linatufundisha jambo gani? Wakati tuko na magumu na tunapaswa kukamata uamuzi fulani, tunapaswa kwanza kufikiria mambo yenye Yehova anaweza kupenda tufanye.

17. Wakati tuko na magumu, namna gani tunaweza kuepuka kufanya kosa kama lile lenye Yosia alifanya?

17 Wakati tunapaswa kukamata uamuzi fulani, ni lazima tufikirie kwanza kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia na namna tunaweza kuzitumia. Katika hali fulani, tunaweza kupenda kutafuta habari zaidi katika vichapo vyetu ao hata kuomba muzee fulani mashauri. Anaweza kutusaidia kufikiri juu ya kanuni zingine za Biblia. Fikiria hali hii: Dada mumoja anaolewa na mutu mwenye haiko Shahidi. Anapanga siku fulani ili kuenda katika mahubiri. (Matendo 4:20) Lakini, siku hiyo bwana yake hapendi aende katika mahubiri. Anamuambia kama kumepita siku fulani hawapitishe wakati mwingi pamoja na kwamba anapenda waende pamoja nafasi fulani. Kwa hiyo, dada huyo anafikiria maandiko ya Biblia yenye yanaweza kumusaidia akamate uamuzi wenye hekima. Anajua kama anapaswa kumutii Mungu na kama Yesu alituamuru kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20; Matendo 5:29) Lakini anakumbuka pia kama bibi anapaswa kujitiisha kwa bwana yake na kama watumishi wa Mungu wanapaswa kuwa na usawaziko. (Waefeso 5:22-24; Wafilipi 4:5) Bwana yake anajaribu kumukataza kuenda katika mahubiri, ao anapenda tu apitishe wakati pamoja naye siku hiyo? Kwa sababu sisi ni watumishi wa Yehova, tunapenda kukamata maamuzi yenye kuwa na usawaziko na yenye kumupendeza.

UENDELEE KUWA NA MOYO MUKAMILIFU NA UPATE FURAHA

18. Unaweza kujifunza jambo gani wakati unafikiri sana juu ya mifano ya wafalme ine wa Yuda?

18 Wakati fulani, sisi pia tunaweza kufanya makosa kama ile yenye wafalme wa Yuda walifanya. Tunaweza (1) kutegemea mawazo yetu wenyewe, (2) kuchagua marafiki wabaya, (3) kuwa na majivuno, ao (4) kukamata maamuzi bila kwanza kufikiria mapenzi ya Mungu ni nini. Hata hivyo, hatuna sababu ya kufikiri kuwa hatuwezi kumupendeza Yehova hata kidogo. Anaona mambo ya muzuri yenye kuwa ndani yetu, kama vile aliona mambo ya muzuri yenye yalikuwa ndani ya wafalme hao ine. Pia, Yehova anaona namna tunamupenda sana na namna tunapenda sana kumutumikia kwa uaminifu. Kwa hiyo, ametupatia mifano yenye inaweza kutusaidia tuepuke kufanya makosa mazito. Basi, tufikiri sana juu ya watu hao wenye kuzungumuziwa katika Biblia na tumushukuru Yehova kwa sababu ametutolea mifano hiyo!