Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kusaidia Watoto wa “Wakaaji Wageni”

Namna ya Kusaidia Watoto wa “Wakaaji Wageni”

‘Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba nikuwe ninasikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.’—3 YOHANA 4.

NYIMBO: 88, 41

1, 2. (a) Watoto wengi wenye wamehamia katika inchi ingine wanapambana na magumu gani? (b) Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii?

JOSHUA anasema hivi: “Tangu utoto, nilizungumuza nyumbani na katika kutaniko luga ya wazazi wangu wenye wamehamia katika inchi ingine. Lakini kisha kuanza masomo, nilianza kupenda luga ya mahali tulikuwa tunaishi. Kisha miaka kidogo, nilianza kuzungumuza tu luga hiyo. Sikuelewa muzuri mikutano, na sikuona kuwa desturi ya wazazi wangu ilikuwa inanihusu.” Watoto wengi wako katika hali kama ya Joshua.

2 Leo, watu zaidi ya 240000000 wanaishi katika inchi ambamo hawakuzaliwa. Ikiwa uko muzazi mwenye amehamia katika inchi ingine, namna gani unaweza kutolea watoto wako nafasi ya muzuri zaidi ya kujifunza kumupenda Yehova na ‘kuendelea kutembea katika kweli’? (3 Yohana 4) Na namna gani wengine wanaweza kusaidia?

WAZAZI, MUKUWE MUFANO MUZURI

3, 4. (a) Namna gani wazazi wanaweza kuwa mufano muzuri kwa watoto wao? (b) Ni mambo gani yenye wazazi hawapaswe kutazamia kwa watoto wao?

3 Wazazi, mufano wenu ni wa maana sana ikiwa munapenda watoto wenu wakuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova na waishi milele. Wakati watoto wako wanaona kuwa ‘unatafuta kwanza Ufalme,’ wanajifunza kumutegemea Yehova ili awatimizie mahitaji yao ya kila siku. (Mathayo 6:33, 34) Utie utumishi wako kwa Yehova pa nafasi ya kwanza kuliko kutafuta vitu vingi zaidi vya kimwili. Ukuwe na maisha mepesi na uepuke kuwa na madeni. Utafute “hazina mbinguni,” ni kusema, kukubaliwa na Yehova, kuliko kutafuta feza ao “utukufu wa wanadamu.”—Soma Marko 10:21, 22; Yohana 12:43.

4 Uepuke kabisa kutumika sana mupaka unakosa wakati wa kuwa pamoja na watoto wako. Uwaambie kuwa unawafurahia wakati wanaamua kumutia Yehova pa nafasi ya kwanza kuliko kutafuta kujulikana sana ao kutafuta feza, iwe kwa ajili yao wenyewe ao kwa ajili yako. Uepuke kuwa na mawazo yenye hayafae kwamba watoto wanapaswa kusaidia wazazi wao wakuwe na maisha ya muzuri sana. Ukumbuke kama, “watoto hawapaswe kuweka akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi kwa ajili ya watoto wao.”—2 Wakorintho 12:14.

WAZAZI, MUJIKAZE KUMALIZA MATATIZO YA LUGA

5. Sababu gani wazazi wanapaswa kuzungumuza na watoto wao juu ya Yehova kwa ukawaida?

5 Kama vile Biblia ilitabiri, watu ‘kutoka katika luga zote za mataifa’ wanakuja katika tengenezo la Yehova. (Zekaria 8:23) Lakini ikiwa watoto wako hawaelewe muzuri luga yako, inaweza kuwa vigumu kwako kuwafundisha kweli. Watoto wako ndio wanafunzi wako Biblia wa maana sana, na wakati wanafikia ‘kupata ujuzi’ juu ya Yehova, hilo litawasaidia kupata uzima wa milele. (Yohana 17:3) Ili watoto wako wajue mafundisho ya Yehova, unapaswa “kuyasema” kwa ukawaida.—Soma Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.

6. Watoto wako wanaweza kupata faida gani wakati wanajifunza luga yako? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Pengine watoto wako watajifunza kwenye masomo na kutoka kwa wengine luga ya mahali munaishi. Lakini watajifunza luga yako wakati unazungumuza nao kwa ukawaida. Wakati watoto wako wanazungumuza luga yako, itakuwa mwepesi zaidi kwao kuzungumuza na wewe na kukuambia namna wanajisikia. Lakini kuko faida zingine. Wakati watoto wako wanazungumuza luga nyingi, hilo linapanua uwezo wao wa kufikiri na kuwasaidia waelewe mawazo ya wengine. Hilo linaweza pia kuwapatia nafasi ya kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova. Carolina mwenye wazazi wake walihamia katika inchi ingine, anasema hivi: “Kuwa katika kutaniko la luga ya kigeni kumeniletea furaha kubwa. Na ni jambo lenye kufurahisha kusaidia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri.”

7. Unaweza kufanya nini ikiwa kuko matatizo ya luga katika familia yako?

7 Lakini, wakati watoto wenye wamehamia katika inchi ingine pamoja na wazazi wao wanaendelea kujifunza desturi na luga ya eneo kwenye wanaishi, wamoja kati yao wanaweza kupoteza hamu ao hata uwezo wao wa kuzungumuza luga ya wazazi wao. Wazazi, ikiwa watoto wenu wako katika hali hiyo, munaweza kujifunza kwa kiasi fulani luga ya mahali kwenye munaishi? Itakuwa mwepesi zaidi kukomalisha watoto wako katika njia ya Kikristo ikiwa unaelewa mazungumuzo yao, mambo yao ya kujifurahisha, kazi zao za masomo na ikiwa unaweza kuzungumuza moja kwa moja na walimu wao. Ni kweli kwamba kujifunza luga ingine kunaomba wakati, bidii, na unyenyekevu. Lakini, hilo litakuwa na matokeo ya muzuri. Kwa mufano, ikiwa mutoto wako anakuwa kiziwi, hautajikaza kujifunza luga ya ishara ili kuzungumuza naye? Kwa kweli, mutoto mwenye kuzungumuza muzuri luga ingine anastahili kuhangaikiwa hivyo pia. *—Soma maelezo ya chini.

8. Namna gani unaweza kusaidia watoto wako ikiwa haujue kuzungumuza muzuri luga ya mahali kwenye munaishi?

8 Inaweza kuwa vigumu sana kwa wazazi fulani wenye walihamia katika inchi ingine kuzungumuza muzuri luga mupya ya watoto wao. Hilo linaweza kufanya ikuwe vigumu kwa wazazi kusaidia watoto wao kuelewa “maandishi matakatifu.” (2 Timotheo 3:15) Hata kama uko katika hali kama hiyo, unaweza kusaidia watoto wako wafikie kumujua na kumupenda Yehova. Muzee mumoja wa kutaniko mwenye kuitwa Shan alisema hivi: “Mama yetu mwenye alitukomalisha yeye mwenyewe, alikuwa na magumu ya kusema luga yenye tulikuwa tunaelewa muzuri, na mimi na dada zangu hatukukuwa tunasema muzuri luga yake. Lakini wakati tulikuwa tunamuona anajifunza, anasali, na kujikaza sana ili kuongoza ibada ya familia kila juma, tulielewa kuwa kufikia kumujua Yehova lilikuwa jambo la maana sana.”

9. Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wenye wako na lazima ya kujifunza katika luga mbili?

9 Watoto fulani wanaweza kuwa na lazima ya kujifunza juu ya Yehova katika luga mbili. Sababu gani? Kwa sababu wanazungumuza luga moja kwenye masomo na wanazungumuza luga ingine nyumbani. Kwa hiyo, wazazi fulani wanatumia vichapo, habari za kusikiliza tu, na video katika luga hizo mbili. Ni wazi kwamba, wazazi wenye wamehamia katika inchi ingine wanapaswa kujikaza sana ili kusaidia watoto wao wamukaribie Yehova.

MUNAPASWA KUWA KATIKA KUTANIKO LA LUGA GANI?

10. (a) Ni nani anapaswa kuamua ikiwa familia itakuwa katika kutaniko la luga gani? (b) Vichwa vya familia wanapaswa kufanya nini mbele ya kukamata uamuzi fulani?

10 Wakati “wakaaji wageni” wanaishi mbali na Mashahidi wenye kuzungumuza luga yao, wanaweza kuwa katika kutaniko lenye kutumia luga ya mahali wanaishi. (Zaburi 146:9) Lakini ikiwa kuko kutaniko lenye kutumia luga yao ya kizalikio, kichwa cha familia anapaswa kuamua ni kutaniko la luga gani lenye kufaa kabisa kwa ajili ya familia yake. Mbele ya kukamata uamuzi huo, anapaswa kufikiri sana na kusali juu ya jambo hilo. Atazungumuza pia na bibi yake na watoto wake. (1 Wakorintho 11:3) Atafikiria mambo gani? Ni kanuni gani za Biblia zenye zinaweza kumusaidia akamate uamuzi?

11, 12. (a) Namna gani luga inafanya watoto wapate ao wakose faida kwenye mikutano? (b) Sababu gani watoto fulani hawapendi kujifunza luga ya wazazi wao?

11 Wazazi wanapaswa kufikiria mambo yenye watoto wao wako nayo lazima kabisa. Zaidi ya saa kidogo tu ya kujifunza mafundisho ya Biblia kila juma kwenye mikutano, watoto wako na lazima ya mambo mengi zaidi ili waelewe muzuri kweli za Biblia. Lakini fikiria jambo hili: Ikiwa mikutano inafanywa katika luga yenye watoto wanaelewa muzuri, wanaweza kupata faida wakati wanahuzuria, pengine wanajifunza mambo mengi zaidi kuliko namna wazazi wao wanawazia. Inawezekana mambo hayatakuwa hivyo wakati watoto hawaelewe muzuri luga. (Soma 1 Wakorintho 14:9, 11.) Na pengine luga ya kizalikio ya mutoto haitabakia tu luga yenye itachochea mawazo yake na kugusa moyo wake. Kwa kweli, watoto fulani wanaweza kujifunza kutoa maelezo, migawo, na hotuba katika luga ya wazazi wao bila kueleza kabisa mawazo yao na namna wanajisikia katika moyo wao.

12 Pia, zaidi ya luga, kuko mambo mengine yenye yanaweza kuchochea moyo wa mutoto. Joshua mwenye tumekwisha kuzungumuzia alikuwa katika hali hiyo. Esther, dada yake, alisema hivi: “Watoto wadogo wanachochewa na luga, desturi na dini ya wazazi wao.” Ikiwa watoto wanaona kuwa desturi ya wazazi wao haiwahusu, hawawezi kuwa tayari kujifunza luga na dini ya wazazi wao. Wazazi wenye wamehamia katika inchi ingine wanaweza kufanya nini?

13, 14. (a) Sababu gani bibi na bwana fulani wenye kuishi katika inchi ingine walihamishia familia yao katika kutaniko la luga ya mahali kwenye wanaishi? (b) Wazazi walifanya nini ili waendelee kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova?

13 Wazazi Wakristo wanatia mahitaji ya watoto wao pa nafasi ya kwanza kuliko mambo yenye wanapenda sana. (1 Wakorintho 10:24) Samuel, baba ya Joshua na Esther, alisema hivi: “Mimi na bibi yangu tulichunguza watoto wetu ili kujua ni katika luga gani kweli inagusa mioyo yao, na tulisali kwa Mungu ili atupatie hekima. Hatukupata jibu lenye sisi tulikuwa tunapendelea. Lakini wakati tuliona kuwa hawakukuwa wanafaidika kabisa na mikutano katika luga yetu, tuliamua kuhamia katika kutaniko la luga ya mahali kwenye tulikuwa tunaishi. Sisi wote tulihuzuria mikutano pamoja na tulienda katika mahubiri kwa ukawaida. Tulialika marafiki wetu wa mahali kwenye tulikuwa tunaishi ili kula chakula pamoja na kutembelea mahali mbalimbali. Mambo hayo yote yalisaidia watoto wetu wafikie kujua ndugu na dada na wafikie kumujua Yehova, haiko tu kama Mungu wao lakini pia kama Baba yao na Rafiki yao. Tuliona kuwa hilo ndilo lilikuwa jambo la lazima sana kwao kuliko kujua muzuri luga yetu.”

14 Samuel anaongezea hivi: “Ili tuendelee kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova, mimi na bibi yangu tulihuzuria pia mikutano katika luga yetu. Tulikuwa na mambo mengi ya kufanya katika maisha, na tulichoka. Lakini tunamushukuru Yehova kwa kubariki bidii yetu na roho yetu ya kujitoa. Watoto wetu wote watatu wanamutumikia Yehova katika utumishi wa wakati wote.”

MAMBO YENYE VIJANA WANAWEZA KUFANYA

15. Sababu gani dada mumoja mwenye kuitwa Kristina aliona kuwa angefanya mengi zaidi katika kutaniko la luga ya mahali kwenye walikuwa wanaishi?

15 Wakati watoto wanakomaa, wanaweza kuona kama wanaweza kutumikia Yehova muzuri zaidi katika kutaniko la luga yenye wanaelewa muzuri. Ikiwa ni hivyo, wazazi wao hawapaswe kufikiri kuwa watoto wao wanawaachilia. Kristina anakumbuka hivi: “Nilijua mambo ya musingi ya luga ya wazazi wangu, lakini maneno yenye yalikuwa yanatumiwa kwenye mikutano yalikuwa magumu sana kwangu kuelewa. Wakati nilikuwa na miaka 12, nilihuzuria mukusanyiko mumoja wenye ulifanywa katika luga yenye tulikuwa tunatumia kwenye masomo. Kwa mara ya kwanza, nilielewa kuwa mambo yenye nilikuwa ninasikiliza yalikuwa kweli! Badiliko lingine la muzuri lilitokea wakati nilianza kusali katika luga yenye tulikuwa tunatumia kwenye masomo. Niliweza kumuambia Yehova mambo yote yenye kuwa katika moyo wangu!” (Matendo 2:11, 41) Wakati alieneza miaka 18, Kristina alizungumuza na wazazi wake na akaamua kuhamia katika kutaniko la luga ya mahali kwenye walikuwa wanaishi. Anasema hivi: “Kujifunza juu ya Yehova katika luga yenye tulikuwa tunatumia kwenye masomo, kulinichochea kufanya maendeleo.” Kristina akakuwa painia wa kawaida na iko na furaha sana.

16. Sababu gani Nadia anafurahi kwa sababu alibakia katika kutaniko la luga ya kigeni?

16 Kijana, unafikiri kama unapenda kuwa katika kutaniko la luga ya mahali kwenye unaishi? Ikiwa ni hivyo, ujiulize sababu gani. Ni kwa sababu kuhamia katika kutaniko hilo kunaweza kukusaidia umukaribie Yehova zaidi? (Yakobo 4:8) Ao ni kwa sababu haupendi wazazi wako waone mambo yote yenye unafanya ao kwa sababu haupendi kujikaza? Nadia, mwenye kutumikia sasa kwenye Beteli anasema hivi: “Wakati mimi na ndugu zangu tulikuwa vijana tulipenda kuhamia katika kutaniko la luga ya mahali tulikuwa tunaishi.” Lakini wazazi wake walijua kama hilo halingetia nguvu urafiki wa watoto wao pamoja na Yehova. Nadia anaongezea hivi: “Sasa tuko wenye shukrani kwa sababu wazazi wetu walijikaza sana ili kutufundisha luga yao na wakaamua tubakie katika kutaniko la luga ya kigeni. Hilo limefanya tukuwe na maisha ya muzuri na kutupatia nafasi nyingi za kusaidia wengine wamujue Yehova.”

NAMNA WENGINE WANAWEZA KUSAIDIA

17. (a) Ni nani Yehova alipatia daraka la kukomalisha watoto? (b) Namna gani wazazi wanaweza kupata musaada wa kufundisha watoto wao kweli?

17 Yehova amepatia wazazi daraka la kufundisha watoto wao kweli. Hakupatia wazazi wa baba na mama daraka hilo ao mutu mwengine yeyote. (Soma Methali 1:8; 31:10, 27, 28.) Hata hivyo, wazazi wenye hawajue luga ya mahali kwenye wanaishi wanaweza kuwa na lazima ya musaada ili kugusa mioyo ya watoto wao. Wakati wazazi hao wanaomba musaada, hilo halimaanishe kwamba wanajaribu kuepuka daraka la kukomalisha watoto wao. Lakini, hilo linaweza kuwasaidia kukomalisha watoto wao ‘katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Waefeso 6:4) Kwa mufano wazazi wanaweza kuomba wazee mashauri juu ya namna ya kufanya ibada ya familia na juu ya namna ya kupata marafiki wazuri kwa ajili ya watoto wao.

Wazazi na watoto wanapata faida wakati wanakuwa pamoja na ndugu na dada (Picha hii inapatana na fungu la 18, 19)

18, 19. (a) Namna gani Wakristo wengine wanaweza kusaidia vijana? (b) Wazazi wanapaswa kuendelea kufanya nini?

18 Ili kusaidia watoto wao, wazazi wanaweza kualika watu wa familia zingine wajiunge pamoja nao kwenye ibada yao ya familia mara kwa mara. Pia, vijana wengi wanajifunza mambo mengi kutoka kwa Wakristo wenzao wakati wanahubiri pamoja nao na wakati wanafanya mambo mengine pamoja. (Methali 27:17) Shan mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Ninakumbuka muzuri ndugu na dada wenye walinisaidia. Wakati walinisaidia kutayarisha migawo ya hotuba za wanafunzi kwa ajili ya mukutano, nilijifunza mengi sikuzote. Nilifurahia mambo ya kujifurahisha yenye tulifanya pamoja katika kikundi.”

19 Kwa kweli, wale wenye wazazi wanachagua ili kusaidia watoto wao wanapaswa kuwatia moyo sikuzote waheshimie wazazi wao. Wanaweza kufanya hivyo kwa kusema mambo ya muzuri juu ya wazazi na kwa kuepuka kuchukua daraka la wazazi la kukomalisha watoto wao. Pia, wale wenye kusaidia watoto wanapaswa kuepuka kuwa na mwenendo wowote wenye unaweza kukwaza wale wenye kuwa ndani ao inje ya kutaniko. (1 Petro 2:12) Hata kama wazazi wanaweza kuomba musaada kwa wengine, ni daraka lao kufundisha watoto wao kweli. Wanapaswa kujua musaada wenye Wakristo wengine wanatoa.

20. Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wakuwe watumishi wa Yehova?

20 Wazazi, musali kwa Yehova ili awasaidie, na mujikaze sana. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 15:7.) Muweke pa nafasi ya kwanza urafiki wa watoto wenu pamoja na Yehova kuliko mambo yenye munapenda. Mufanye yenu yote ili kuhakikisha kuwa Neno la Mungu linagusa mioyo ya watoto wenu. Muendelee kuwa na tumaini kuwa watoto wenu wanaweza kuwa watumishi wa Yehova. Wakati watoto wenu wanafuata Neno la Mungu na mufano wenu muzuri, mutajisikia kama mutume Yohana mwenye alisema hivi juu ya watoto wake wa kiroho: ‘Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba nikuwe ninasikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.’—3 Yohana 4.

^ fu. 7 Soma habari “Unaweza Kujifunza Lugha Nyingine!” katika Amuka! ya Mwezi wa 3, 2007, ukurasa wa 10-12.