Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Gayo Alisaidia Ndugu Zake

Namna Gayo Alisaidia Ndugu Zake

GAYO na Wakristo wengine wenye waliishi mwisho-mwisho wa mwaka kati ya 1 na 100, walipambana na magumu mbalimbali. Watu fulani wenye walikuwa wanaeneza mafundisho ya uongo walijaribu kuregeza na kugawanya makutaniko. (1 Yohana 2:18, 19; 2 Yohana 7) Mwanaume mumoja mwenye aliitwa Diotrefe alikuwa anaeneza “maneno maovu” juu ya mutume Yohana na wengine, alikuwa anakataa kukaribisha Wakristo wenye kusafiri, na alikuwa anajaribu kuchochea wengine wafuate mufano wake. (3 Yohana 9, 10) Hiyo ndiyo hali yenye ilikuwa wakati mutume Yohana alimuandikia Gayo. Barua hiyo yenye mutume huyo aliandika katika mwaka wa 98 inapatikana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo na inaitwa “Barua ya Tatu ya Yohana.”

Hata kama Gayo alipambana na magumu mengi, aliendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. Namna gani alionyesha kuwa alikuwa muaminifu? Sababu gani tunapenda kuiga mufano wa Gayo leo? Namna gani barua ya Yohana inaweza kutusaidia kufanya hivyo?

BARUA KWA RAFIKI MUPENDWA

Muandikaji wa barua ya Tatu ya Yohana anajiita kuwa ‘mwanaume muzee.’ Maneno hayo yalitosha ili kumusaidia Gayo mutoto wake wa kiroho mupendwa atambue kuwa barua hiyo ilikuwa ya mutume Yohana. Yohana anamuita hivi Gayo kwa furaha: ‘Mupendwa, ambaye mimi namupenda kweli.’ Kisha Yohana alionyesha kama anatumaini kuwa afya ya kimwili ya Gayo ilikuwa muzuri kama vile afya yake ya kiroho. Alikuwa na mawazo ya muzuri kabisa juu ya Gayo na alimupongeza kabisa!—3 Yohana 1, 2, 4.

Inawezekana kabisa kuwa Gayo alikuwa mwangalizi wa kutaniko, lakini barua hiyo haionyeshe waziwazi jambo hilo. Yohana alimusifu Gayo kwa sababu alikuwa anakaribisha ndugu hata kama hakukuwa anawajua. Yohana aliona kuwa hilo lilionyesha kuwa Gayo ni muaminifu, kwa sababu sikuzote sifa ya kukaribisha wageni inatambulisha watumishi wa Mungu.​—Mwanzo 18:1-8; 1 Timotheo 3:2; 3 Yohana 5.

Maneno ya shukrani ya Yohana juu ya ukaribishaji wenye Gayo alionyesha ndugu, yanaonyesha kwamba Wakristo wenye walikuwa wanatembelea makutaniko walikuwa wanapitia mahali kwenye Yohana alikuwa, na kwa kweli walikuwa wanamuelezea mambo yenye walikuwa wamejionea. Pengine wao ndio waliletea Yohana habari juu ya makutaniko hayo.

Kwa kweli, Wakristo wenye kusafiri wangependa kabisa kubakia pamoja na Wakristo wenzao. Nyumba za wageni zilikuwa zinasemwa mubaya sana, hali hazikukuwa za muzuri katika nyumba hizo, na zilijaa watu wenye mwenendo muchafu. Kwa hiyo, mahali iliwezekana, watu wenye kusafiri wenye hekima walikuwa wanabakia kwa marafiki wao; Wakristo wenye kusafiri walibakia kwa Wakristo wenzao.

“WALISAFIRI KWA AJILI YA JINA LAKE”

Yohana alimutia Gayo moyo aonyeshe tena sifa ya ukaribishaji-wageni, kwa sababu mutume Yohana alimuomba ‘aishugulikie safari ya hawa watu kwa namna inayomufaa Mungu.’ Katika hali hiyo, kushugulikia safari ya wageni kulimaanisha kuwatolea mambo yenye walikuwa nayo lazima ili waendelee na safari yao mupaka wafike mahali kwenye walikuwa wanaenda. Ilionekana wazi kama Gayo alikuwa tayari amefanyia hivyo wageni wengine, kwa sababu walikuwa wamemuletea Yohana habari ya muzuri juu ya upendo na imani yake.​—3 Yohana 3, 6.

Pengine wageni hao walikuwa wamisionere, watu wenye Yohana alituma, ao waangalizi wenye kusafiri. Iwe ni hivyo ao hapana, walisafiri kwa ajili ya habari njema. Yohana alisema hivi: “Kwa maana wao walisafiri kwa ajili ya jina lake.” (3 Yohana 7) Yohana alikuwa amezungumuzia Mungu (ona mustari wa 6), kwa hiyo maneno “kwa ajili ya jina lake” yanaonekana kuwa yanazungumuzia jina la Yehova. Kwa hiyo, ndugu walikuwa sehemu ya kutaniko la Kikristo na walipaswa kukaribishwa kwa furaha. Ndiyo sababu Yohana aliandika hivi: “Sisi tuna wajibu wa kuwakaribisha watu wa namna hiyo, ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 Yohana 8.

MUSAADA WA KUPIGANISHA HALI NGUMU

Yohana hakumuandikia Gayo ili kumushukuru tu. Alipenda pia kumusaidia apambane na tatizo fulani ngumu. Kwa sababu fulani, mutu mumoja katika kutaniko la Kikristo mwenye aliitwa Diotrefe hakukuwa anapenda kuonyesha sifa ya ukaribishaji-wageni kwa Wakristo wenye kusafiri. Na hata alijaribu kuzuia wengine kuonyesha ukaribishaji-wageni.​—3 Yohana 9, 10.

Kwa kweli, Wakristo waaminifu hawangependa kukaa na Diotrefe hata kama angewakaribisha. Alipenda kuwa na nafasi ya kwanza katika kutaniko, hakupokea kwa heshima jambo lolote kutoka kwa mutume Yohana, na alikuwa anaeneza maneno maovu juu ya mutume Yohana na juu ya wengine. Hata kama Yohana hakumuita hata kidogo kuwa mwalimu wa uongo, Diotrefe alikuwa anapinga mamlaka ya mutume Yohana. Tamaa ya Diotrefe ya kupenda kujulikana na tabia yake yenye haikukuwa ya Wakristo, vilileta mashaka juu ya ushikamanifu wake. Mufano wa Diotrefe unaonyesha namna watu wenye kupenda mambo makubwa na wenye kiburi wanaweza kujaribu kuleta mugawanyiko katika kutaniko. Kwa hiyo, Yohana aliambia Gayo maneno haya yenye yanahusu pia kila mumoja wetu: ‘Ukuwe muigaji, si wa yaliyo mabaya.’—3 Yohana 11.

SABABU YA MUZURI SANA YA KUFANYA MEMA

Tofauti na Diotrefe, Yohana alizungumuzia Mukristo mumoja mwenye kuitwa Demetrio kuwa ni mufano muzuri. Yohana aliandika hivi: “Demetrio ametolewa ushahidi . . . Kwa kweli, sisi, pia, tunatoa ushahidi,” juu yake, ‘nanyi munajua kwamba ushahidi tunaotoa ni wa kweli.’ (3 Yohana 12) Inawezekana Demetrio alikuwa na lazima ya musaada kutoka kwa Gayo, na pengine barua ya Tatu ya Yohana ilitumiwa ili kumutambulisha na kumupendekeza. Inawezekana kabisa kuwa Demetrio yeye mwenyewe ndiye alimupelekea Gayo barua hiyo. Kwa sababu alikuwa mutu mwenye Yohana alituma, ao pengine mwangalizi mwenye kusafiri, inawezekana Demetrio alikazia mambo yenye Yohana alikuwa ameandika.

Sababu gani Yohana alimutia Gayo moyo aendelee kuonyesha ukaribishaji-wageni hata kama tayari alikuwa anafanya hivyo? Yohana aliona lazima ya kuchochea ujasiri wa Gayo? Mutume Yohana aliogopa kuwa Gayo angesita kuonyesha sifa ya ukaribishaji-wageni kwa sababu Diotrefe alikuwa anajaribu kufukuza katika kutaniko Wakristo wenye walikuwa wanaonyesha sifa hiyo? Ikiwa ni hivyo ao hapana, Yohana alimuhakikishia Gayo kwamba ‘yeye ambaye anatenda mema anatokana na Mungu.’ (3 Yohana 11) Hiyo ni sababu ya muzuri sana ya kufanya mema na kuendelea kufanya hivyo.

Barua ya Yohana ilimuchochea Gayo aendelee kuonyesha ukaribishaji-wageni? Kwa sababu barua ya Tatu ya Yohana ilitiwa pamoja na vitabu vya Biblia ili kutia wengine moyo ‘wakuwe waigaji, si wa yaliyo mabaya,’ hilo linaonyesha kama ilifanya hivyo.

MAMBO YENYE TUNAJIFUNZA KATIKA BARUA YA TATU YA YOHANA

Hatujue mambo mengi zaidi juu ya Gayo, ndugu yetu mupendwa wa zamani. Lakini mambo madogo yenye tumeona juu ya maisha yake yanaweza kutufundisha mambo mengi ya maana.

Ni katika njia gani tunaweza “kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni”?

Kwanza, kwa kiasi fulani, wengi kati yetu tulijifunza kweli kupitia Wakristo waaminifu wenye walikuwa tayari kusafiri ili kutujulisha kweli hiyo. Kwa kweli, haiko Wakristo wote wa kutaniko la Kikristo leo ndio wanafanya safari ya mbali sana kwa sababu ya habari njema. Hata hivyo, kama vile Gayo, katika njia fulani tunaweza kutegemeza na kutia moyo wale wenye kusafiri, kama vile mwangalizi wa muzunguko na bibi yake. Ao tunaweza kuwa na uwezo wa kutoa musaada wenye kufaa kwa ndugu na dada wenye wamehamia katika maeneo mengine katika inchi yao, ao katika inchi ingine, ili kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kwa hiyo, tuendelee basi “kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni.”—Waroma 12:13; 1 Timotheo 5:9, 10.

Pili, hatupaswe kushangaa ikiwa watu fulani wanapinga mamlaka katika kutaniko leo, lakini hilo linatokea mara chache sana. Mamlaka ya Yohana yalipingwa; na mamlaka ya mutume Paulo pia yalipingwa. (2 Wakorintho 10:7-12; 12:11-13) Kwa hiyo, tunapaswa kutenda namna gani ikiwa watu fulani katika kutaniko wanatutendea hivyo? Paulo alimushauria Timotheo hivi: ‘Mutumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mupole kwa wote, mwenye sifa za kustahili kufundisha, akiendelea kujizuia chini ya uovu, akiwafundisha kwa upole wale wasio na mwelekeo unaofaa.’ Wakati tunaendelea kuwa na roho ya utulivu hata wakati tunachokozwa, watu fulani wenye kutuchambua wanaweza kubadilisha polepole mawazo yao. Na Yehova anaweza ‘kuwapa toba inayoongoza kwenye ujuzi sahihi juu ya kweli.’—2 Timotheo 2:24, 25.

Tatu, tunapaswa kuhangaikia na kupongeza Wakristo wenzetu wenye kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu kwa sababu wanaendelea kuwa waaminifu hata kama wanapambana na upinzani. Kwa kweli, mutume Yohana alimutia Gayo moyo na kumuhakikishia kuwa alikuwa anafanya mambo yenye kuwa sawa. Vilevile, wazee wanapaswa kufuata mufano wa mutume Yohana kwa kutia ndugu na dada zao moyo ili ‘wasizimie [wasichoke].’—Isaya 40:31; 1 Wathesalonike 5:11.

Kwa sababu barua ya Yohana kwa Gayo iko tu na maneno 219 katika Kigiriki, barua hiyo ndiyo kitabu kifupi zaidi katika Biblia. Lakini, iko na faida sana kwa Wakristo leo.