Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utamaliza Kukosa Kuelewana na Kuendeleza Amani?

Utamaliza Kukosa Kuelewana na Kuendeleza Amani?

YEHOVA MUNGU anatia moyo Wakristo wapende amani, waone amani kuwa jambo la maana sana katika maisha yao. Waabudu wa kweli wako na amani nyingi kwa sababu wanapenda kufanya amani. Hilo linafanya kutaniko la Kikristo livutie wale wenye wanapenda kupata mahali penye kuwa amani.

Kwa mufano, muchawi mumoja mwenye kujulikana sana katika Madagascar aliona namna Mashahidi wa Yehova walikuwa na amani. Alijiambia hivi: ‘Ikiwa wakati fulani nitapenda kuingia katika dini fulani, nitaingia katika dini hii.’ Kisha wakati fulani aliacha matendo yake ya uchawi, akachukua miezi fulani ili kufanya ndoa yake ipatane na maandiko, na akakuwa muabudu wa Yehova, Mungu wa amani.

Kama mwanaume huyo, kila mwaka maelfu ya watu wanapata katika kutaniko la Kikristo amani yenye walikuwa wanatamani sana. Lakini, Biblia inasema wazi kama ikiwa katika kutaniko kuna ‘wivu mukali na ugomvi,’ hilo linaweza kuharibu urafiki na kuvuruga amani. (Yak. 3:14-16) Jambo la kufurahisha ni kwamba Biblia inatutolea pia mashauri ya muzuri juu ya namna tunaweza kuepuka matatizo hayo na kuendeleza amani. Ili kujua namna ya kufanya hivyo, tuzungumuzie basi hali mbalimbali zenye kutokea katika maisha.

MATATIZO NA NAMNA YA KUYAMALIZA

“Sikukuwa ninaelewana na ndugu mumoja mwenye nilikuwa ninatumika naye. Siku moja wakati tulikuwa tunatombokeana, watu wawili walikuja mahali tulikuwa na wakaona namna tulikuwa tunatombokeana.”​—CHRIS.

“Dada mwenye nilizoea kuhubiri naye alivunja mara moja mipango yetu ya kuhubiri pamoja. Kisha akaacha kabisa kuzungumuza na mimi. Sikujua sababu gani.”​—JANET.

“Nilikuwa ninazungumuza na watu wawili kwenye telefone. Mumoja kati yao akatuaga, na nikafikiri kuwa amekwisha kukata telefone. Kisha nikaambia mutu wa pili mambo ya mubaya juu ya ule mutu wa kwanza, lakini mutu huyo wa kwanza alikuwa hajakata telefone.”​—MICHAEL.

“Katika kutaniko letu, mapainia wawili walianza kukosana. Painia mumoja alimutombokea sana ule mwingine. Mabishano yao yalikwaza wengine.”​—GARY.

Unaweza kuwaza kuwa matatizo hayo yalikuwa madogo-madogo. Lakini kila tatizo lingeweza kutokeza maumivu ya moyoni na ya kiroho kwa wale wenye walikosa kuelewana. Hata hivyo, utafurahi kujua kama ndugu na dada hao wote walifanya amani kwa sababu walifuata muongozo wa Biblia. Unafikiri ni miongozo gani ya Biblia yenye iliwasaidia kupata matokeo ya muzuri?

‘Musigombane njiani.’ (Mwa. 45:24) Yosefu alipatia ndugu zake shauri hilo wakati walikuwa wanarudia kwa baba yao. Maneno yake yalikuwa yenye hekima sana! Wakati mutu anashindwa kujizuia na anakasirika haraka, anaweza kufanya wengine pia wakuwe na hasira. Chris alifikia kuona kama uzaifu wake ulikuwa kiburi na kusita kukubali muongozo. Kwa sababu alipenda kubadilika, aliomba musamaha ndugu mwenye alikuwa amebishana naye na kisha akajikaza sana kuzuia hasira yake. Wakati ndugu huyo aliona namna Chris anajikaza kubadilika, yeye pia alifanya mabadiliko. Sasa wanafurahia kumutumikia Yehova pamoja.

‘Mipango inavunjika mahali ambapo hapana mazungumuzo ya siri.’ (Met. 15:22) Janet aliona kuwa alipaswa kuchukua shauri hilo kwa uzito. Aliamua ‘kuzungumuza’ na dada huyo mwengine. Wakati wa mazungumuzo yao, Janet aliomba kwa hekima dada mwenzake aeleze wazi-wazi mambo yenye yalimukwaza. Mwanzoni mazungumuzo yaliwaka moto kwa kadiri fulani, lakini hali iliendelea kuwa muzuri zaidi kadiri walizungumuzia tatizo lao kwa utulivu. Dada huyo alitambua kama alikuwa ameelewa mambo mubaya juu ya hali yenye haikuhusu hata dada Janet. Aliomba musamaha, na wanatumikia tena Yehova pamoja.

‘Ikiwa unaleta zawadi yako kwenye mazabahu na hapo ukumbuke kwamba ndugu yako ana jambo fulani juu yako, acha zawadi yako hapo mbele ya mazabahu, na uende zako; kwanza fanya amani yako pamoja na ndugu yako.’ (Mt. 5:23, 24) Inawezekana unakumbuka shauri hilo lenye Yesu alitoa katika Mahubiri ya Mulimani. Michael alijisikia mubaya sana wakati alitambua namna alikuwa amejiendesha mubaya. Aliazimia kujikaza sana ili kurudisha amani. Alionana na ndugu mwenye alikuwa amekwaza na akamuomba musamaha kwa unyenyekevu. Matokeo yalikuwa nini? Michael anasema hivi: “Ndugu yangu alinisamehe kabisa.” Wakakuwa marafiki tena.

‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.’ (Kol. 3:12-14) Kuhusu matatizo ya mapainia hao wawili wa muda murefu, muzee mumoja aliwasaidia kufikiri juu ya maulizo haya: ‘Sisi wawili tuko na haki ya kufanya wengine wakasirike kwa sababu ya matatizo yetu? Tuko kabisa na sababu ya kukosa kuvumiliana na kuendelea kumutumikia Yehova katika amani?’ Walikubali mashauri ya muzee huyo na wakayatumikisha. Sasa wanaelewana muzuri na wanahubiri pamoja habari njema.

Kutumikisha mashauri hayo ya Biblia yenye kuwa katika Wakolosai 3:12-14, ndilo jambo la kwanza lenye unaweza kufanya ikiwa mutu fulani anakukosea. Wengi wameona kama unyenyekevu unaweza kuwasaidia wasamehe na kusahau. Ikiwa kisha kujikaza kwa kadiri fulani, inaonekana kuwa unapaswa kufanya mengi zaidi, unaweza kutumia kanuni yenye kupatikana kwenye Mathayo 18:15? Mashauri ya Yesu yenye kuwa katika andiko hilo yanaonyesha hatua ya kufuata wakati mutu fulani anakosea sana mwengine. Lakini, kwa kawaida hiyo ni hatua yenye unaweza kufuata. Umuone ndugu ao dada yako na kwa upole na unyenyekevu ujikaze kuzungumuzia na kumaliza matatizo yenu.

Kwa kweli, Biblia inatutolea mashauri mengine yenye kufaa. Mengi kati ya mashauri hayo yanategemea sana kuonyesha sifa za ‘tunda la roho,’ ni kusema, ‘upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.’ (Gal. 5:22, 23) Kama vile mafuta yanasaidia mashini kufanya kazi muzuri, sifa hizo zinasaidia kufanya amani katika hali ya utulivu.

WATU WA UTU MBALIMBALI WANAFANYA KUTANIKO LIKUWE LENYE KUFURAHISHA

Utu ni tabia zenye kila mutu iko nazo na kila mutu iko na tabia zenye kuwa tofauti na za mwenzake; tabia hizo zinaweza kusaidia kufanya urafiki muzuri. Kuwa na tabia tofauti kunaweza pia kuleta hali ya kukosa kuelewana. Muzee mumoja mwenye uzoefu alitoa mufano huu: “Mutu mwenye kuwa na haya anaweza kushindwa kujisikia muzuri wakati iko pamoja na mutu mwenye kuchangamuka sana. Tofauti hiyo inaweza kuonekana kuwa haina maana, lakini inaweza kuleta matatizo makubwa.” Lakini, unafikiri kama watu wenye kuwa na utu tofauti kabisa hawawezi kuelewana? Tuone mufano wa mitume wawili. Petro alikuwa mutu wa namna gani? Unaweza kusema kama alikuwa mutu mwenye kusema mawazo yake waziwazi na mwenye kutenda haraka-haraka. Halafu Yohana? Inaonekana kuwa Yohana alikuwa mwenye kuhangaikia wengine na mwenye kufikiri kwanza mbele ya kusema ao kufanya jambo fulani. Kuko sababu fulani zenye zinaweza kutufanya tukuwe na mawazo hayo juu ya mitume hao wawili. Inaonekana kuwa walikuwa na utu wenye kuwa tofauti. Hata hivyo, walitumika muzuri pamoja. (Mdo. 8:14; Gal. 2:9) Kwa hiyo, inawezekana Wakristo wenye kuwa na tabia zenye kuwa tofauti watumike pamoja leo.

Pengine, katika kutaniko lako kuko ndugu mwenye maneno na matendo yake yanakukasirisha. Lakini, unajua kama Kristo alikufa kwa ajili ya mutu huyo na unapaswa kumuonyesha upendo. (Yoh. 13:34, 35; Rom. 5:6-8) Kwa hiyo, kuliko kukataa kufanya urafiki pamoja naye ao kujaribu kumuepuka, ujiulize hivi: ‘Ndugu yangu anafanya jambo fulani lenye halipatane na Maandiko? Anatumia ujanja ili kujaribu kunifanya nijisikie mubaya? Ao tuko tu na tabia zenye kuwa tofauti?’ Pia, ulizo la maana sana ni hili: ‘Iko na sifa gani za muzuri zenye ninaweza kuiga?’

Ulizo hilo la mwisho ni la maana sana. Ikiwa mutu huyo ni mwenye kusema mingi lakini wewe uko mutu wa kimya, fikiria namna ni vyepesi kwake kuanzisha mazungumuzo katika mahubiri. Unaweza kumuomba muhubiri pamoja naye na kuona mambo yenye unaweza kujifunza kutoka kwake. Ikiwa anazoea kuonyesha wengine ukarimu, lakini wewe unaonekana kuwa muchoyo, unaweza kumuiga ili kuona furaha yenye kutokana na kutoa kwa kusaidia wale wenye kuzeeka, wagonjwa, ao wenye kuwa katika uhitaji. Wazo kubwa ni kwamba, hata kama muko na utu tofauti, wewe na ndugu yako munaweza kuwa marafiki ikiwa munakazia sifa za muzuri. Inawezekana kama hilo halitafanya mukuwe marafiki wa sana, lakini linaweza kuwasaidia mukaribiane na kufanya kuwe na amani kati yenu na katika kutaniko lote.

Inawezekana Euodia na Sintike walikuwa na utu tofauti. Lakini mutume Paulo aliwatia moyo ‘wakuwe na akili moja katika Bwana.’ (Flp. 4:2) Utajikaza pia kufanya hivyo na kuendeleza amani?

USIRUHUSU KUKOSA KUELEWANA KUENDELEE

Kama vile magugu ao majani ya mubaya yenye kuota katika shamba la maua, mawazo ya mubaya juu ya wengine yanaweza kuongezeka zaidi ikiwa hatuyaondoe. Wakati kinyongo kinakomaa sana katika moyo wa mutu, hilo linaweza hata kuharibu amani katika kutaniko. Ikiwa tunapenda Yehova na ndugu na dada zetu, tutafanya yetu yote tusiharibu ao kupunguza amani ya watu wa Mungu kwa sababu ya utu wetu wenye kuwa tofauti.

Ikiwa unajinyenyekeza na kujikaza kufanya amani, unaweza kupata matokeo ya muzuri sana

Wakati tunazungumuzia matatizo ya kukosa kuelewana tukiwa na kusudi la kufanya amani, tunaweza kushangaa kuona matokeo ya muzuri yenye tutapata. Fikiria mufano wa Shahidi mumoja. Alisema hivi: “Niliona kuwa dada fulani alikuwa ananitendea kama mutoto. Hilo lilinisumbua sana. Kadiri hasira yangu juu yake iliendelea kuongezeka, nilianza kumujibia bila adabu. Niliwaza hivi: ‘Kwa sababu hanionyeshe heshima yenye ninastahili, na mimi pia sitamuheshimia.’”

Kisha Shahidi huyo alianza kufikiria matendo yake mwenyewe. Alisema hivi: “Nilianza kuona uzaifu wangu mwenyewe na nikajisikia kuwa sifae kabisa. Nilitambua kuwa nilipaswa kubadilisha mawazo yangu. Kisha kusali kwa Yehova juu ya jambo hilo, niliuzia dada huyo zawadi ndogo na nikamuandikia barua fupi ili kumuomba musamaha kwa sababu ya tabia yangu ya mubaya. Tulikumbatiana na kusikilizana kuwa tutasahau tatizo hilo. Hatujakuwa na matatizo mengine tangu hapo.”

Watu wako na lazima sana ya amani. Lakini wakati wanaona kuwa cheo ao heshima yao iko katika hatari, wengi wanaanza kutenda katika njia yenye haiwezi kuleta amani. Watu wengi wenye hawamuabudu Yehova wanafanya hivyo, lakini waabudu wa Yehova wanapaswa kulinda amani na umoja. Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika hivi: ‘Nawasihi [nawaomba] ninyi mutembee kwa kuustahili mwito mulioitiwa, mukiwa na unyenyekevu kamili wa akili na upole, mukiwa na ustahimilivu, mukivumiliana katika upendo, mukijitahidi [mukijikaza] sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’ (Efe. 4:1-3) “Kifungo [hicho] chenye kuunganisha cha amani” ni cha maana sana. Tuendelee basi kutia nguvu kifungo hicho na tuazimie kumaliza matatizo yoyote yenye yanaweza kutokea kati yetu.