Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Busara Yako na Ibarikiwe!”

“Busara Yako na Ibarikiwe!”

DAUDI mwenye aliishi katika Israeli ya zamani alisema maneno hayo ili kumusifu mwanamuke mumoja mwenye alikuja kukutana naye. Jina lake lilikuwa Abigaili. Ni nini ilimuchochea Daudi amusifu, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?

Daudi alikutana na mwanamuke huyo mwenye kuolewa wakati alikuwa anakimbia Mufalme Sauli. Abigaili alikuwa bibi ya Nabali, mwanaume tajiri mwenye alikuwa anafugia wanyama wake wengi katika eneo la milima la kusini mwa Yuda. Daudi na wanaume wake walikuwa kama ‘ukuta kuzunguka’ wachungaji na wanyama wa Nabali. Kisha Daudi alituma wajumbe kwa Nabali ili kumuomba chakula ‘chochote ambacho mukono wake unaweza kupata.’ (1 Sam. 25:8, 15, 16) Ombi hilo halikukosa usawaziko hata kidogo, kwa kufikiria namna Daudi na watu wake walikuwa wamelinda mali ya Nabali.

Lakini Nabali, mwenye jina lake linamaanisha “Mutu Asiye na Akili” ao “Mupumbavu,” alikuwa anatenda kulingana na jina lake. Alijibu kwa ukali na kwa matukano, na kukataa ombi la Daudi. Kwa hiyo, Daudi alijitayarisha kuenda kumupatia Nabali malipizi kwa sababu ya jibu lake lenye ukali na lenye kukosa akili. Nabali na watu wa nyumba yake wangepewa malipizi kwa sababu ya upumbavu wake.​—1 Sam. 25:2-13, 21, 22.

Wakati Abigaili alijua matokeo ya mubaya ya tendo hilo lenye lilikuwa linapangwa, Abigaili alitenda kwa ujasiri. Kwa heshima, alimulilia Daudi kwa kukazia urafiki wake pamoja na Yehova. Na akatoa chakula kingi kwa Daudi, mwenye angekuwa mufalme mupya, na kwa wanaume wake. Daudi alitambua kuwa Yehova alikuwa ametumia mwanamuke huyo ili kumuzuia asifanye jambo lenye lingemufanya akuwe na kosa mbele ya Mungu. Daudi aliambia Abigaili hivi: “Busara yako na ibarikiwe, nawe ubarikiwe, ambaye umenizuia leo nisiingie katika hatia [deni] ya damu.”​—1 Sam. 25:18, 19, 23-35.

Kwa kweli, hatupendi hata kidogo kuwa kama Nabali, kwa kukosa shukrani kwa ajili ya mambo mazuri yenye wengine wanatufanyia. Pia, wakati tunaona hali fulani inaanza kuwa mubaya, ni muzuri tujikaze sana ili kuizuia. Kwa kweli, tunaweza kujisikia kama muandikaji mumoja wa zaburi mwenye aliambia Mungu hivi: “Unifundishe . . . kuwa na akili na ujuzi.”​—Zab. 119:66.

Wengine wanaweza kuona matendo yetu yenye hekima ao busara. Iwe wanasema ao hapana, wanaweza kujisikia kama Daudi mwenye alisema hivi: “Busara yako na ibarikiwe!”