Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uko Tayari Kungojea kwa Uvumilivu?

Uko Tayari Kungojea kwa Uvumilivu?

‘Ninyi pia muonyeshe subira.’​—YAK. 5:8.

NYIMBO: 78, 139

1, 2. (a) Ni nini inaweza kutufanya tuulize: ‘Mupaka wakati gani’? (b) Sababu gani mifano ya watumishi waaminifu wa zamani inaweza kututia moyo?

‘MUPAKA wakati gani?’ Manabii waaminifu Isaya na Habakuki waliuliza ulizo hilo. (Isa. 6:11; Hab. 1:2) Wakati alikuwa anaandika Zaburi ya 13, Mufalme Daudi aliuliza pia hivi mara ine: ‘Mupaka wakati gani?’ (Zab. 13:1, 2) Hata Bwana wetu Yesu Kristo aliuliza ulizo hilo wakati alikuwa anazungukwa na watu wenye hawakukuwa na imani. (Mt. 17:17) Kwa hiyo, hatupaswe kushangaa ikiwa sisi pia tunafikia kuuliza ulizo hilo wakati fulani.

2 Ni nini inaweza kutufanya tuulize: ‘Mupaka wakati gani?’ Pengine tumetendewa bila haki kwa njia fulani. Ao pengine tunavumilia magumu yenye kuletwa na uzee na magonjwa ao mikazo ya kuishi katika “nyakati [hizi] za hatari” zenye kuwa ‘ngumu kushugulika nazo.’ (2 Tim. 3:1) Ao pengine tabia za mubaya za watu wenye kutuzunguka zinatuchokesha. Hata iwe ni kwa sababu gani, ni jambo lenye kutia moyo kabisa kujua kuwa watumishi waaminifu wa zamani wa Yehova waliuliza pia ulizo hilo lenye linaweza kutokea katika akili zetu, na Mungu hakuwakaripia kwa sababu ya kuuliza ulizo hilo!

3. Ni nini inaweza kutusaidia wakati tunapatwa na magumu?

3 Lakini ni nini inaweza kutusaidia wakati tunapatwa na magumu kama hayo katika maisha yetu? Mwanafunzi Yakobo, ndugu ya Yesu, aliongozwa na roho takatifu ili kutuambia hivi: ‘Muonyeshe subira, akina ndugu, mupaka kuwapo kwa Bwana.’ (Yak. 5:7) Kwa kweli, sisi wote tuko na lazima ya kuonyesha subira ao kungojea. Lakini kuwa na sifa hiyo yenye kutoka kwa Mungu kunatia ndani nini?

KUNGOJEA MAANA YAKE NINI?

4, 5. (a) Sifa ya kungojea inatia ndani nini? (b) Namna gani mwanafunzi Yakobo anafasiria kungojea? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Kulingana na Biblia, sifa ya ustahimilivu ao ya kungojea inatokana na roho takatifu; bila musaada wa Mungu, wanadamu wenye hawakamilike hawawezi kungojea namna inaombwa. Sifa ya kungojea ni zawadi kutoka kwa Mungu, na kuonyesha sifa hiyo ni njia ya maana ya kuonyesha kuwa tunamupenda. Kungojea kunaonyesha pia kuwa tunapenda wengine. Kukosa kungojea kunafanya upendo wetu ukuwe zaifu; lakini kungojea kunatia nguvu upendo huo. (1 Kor. 13:4; Gal. 5:22) Sifa ya kungojea inatia ndani sifa zingine za maana za Kikristo. Kwa mufano, inapatana sana na sifa ya uvumilivu, yenye inatusaidia kupiganisha magumu na wakati huohuo tunaendelea kuwa na mawazo yenye kufaa. (Kol. 1:11; Yak. 1:3, 4) Kungojea kunaweza pia kutia ndani kuteseka bila kulipiza kisasi na kuendelea kuwa imara hata kutokee nini. Tena, Biblia inatuomba tuelewe kuwa tuko na lazima ya kuwa tayari kungojea. Sifa hiyo ya kungojea inakaziwa katika Yakobo 5:7, 8. (Soma.)

5 Sababu gani tunapaswa kuwa tayari kuelewa kuwa tuko na lazima ya kungojea Yehova atende? Yakobo analinganisha hali yetu na hali ya mulimaji. Hata kama mulimaji anatumika sana ili kupanda mimea yake, hana uwezo juu ya hali ya hewa ao kukomaa kwa mimea. Hawezi kufanya wakati upite haraka. Anaelewa kuwa anapaswa kungojea kwa uvumilivu ‘matunda yenye samani ya inchi.’ Vilevile, kuko mambo mengi yenye hatuwezi kufanya ao kuzuia wakati tunangojea Yehova atimize ahadi zake. (Mk. 13:32, 33; Mdo. 1:7) Kama mulimaji, tunapaswa kungojea kwa uvumilivu.

6. Mufano wa nabii Mika unaweza kutufundisha nini?

6 Hali zenye tunapambana nazo leo zinafanana na hali zenye zilikuwa wakati wa nabii Mika. Aliishi wakati wa utawala wa mufalme mubaya Ahazi; wakati huo watu walikuwa wanafanya mambo ya udanganyifu ya kila aina. Kwa kweli, watu walikuwa wamekuwa na ufundi wa kufanya “lililo baya.” (Soma Mika 7:1-3.) Mika alielewa kuwa hangeweza kubadilisha hali hizo. Kwa hiyo, angeweza kufanya nini? Anatuambia hivi: ‘Mimi, nitaendelea kumutazamia Yehova. Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea Mungu wa wokovu wangu. Mungu wangu atanisikia.’ (Mika 7:7) Kama Mika, sisi pia tunapaswa kuwa na ‘mutazamo wa kungojea,’ ni kusema, kungojea kwa uvumilivu.

7. Sababu gani tunapaswa kufanya mengi zaidi kuliko tu kungojea Yehova atimize ahadi zake?

7 Ikiwa tuko na imani kama ya Mika tutakuwa tayari kumungojea Yehova. Hali yetu haiko kama ya mufungwa mwenye anangojea katika gereza hukumu yake ya kifo. Analazimishwa kungojea, na hangojee kwa hamu tukio hilo. Hali yetu ni tofauti kabisa! Tuko tayari kungojea Yehova kwa sababu tunajua kama atatimiza ahadi yake ya kutupatia uzima wa milele kwa wakati muzuri na wenye kufaa kabisa! Kwa hiyo, ‘tunavumilia kikamili na kuwa wenye ustahimilivu pamoja na shangwe.’ (Kol. 1:11, 12) Lakini, wakati tunangojea hatupaswe kulalamika na kunungunika kuwa Yehova hatende haraka; kufanya hivyo hakutamufurahisha Mungu wetu.​—Kol. 3:12.

WATU WAAMINIFU WENYE WALIONYESHA SIFA YA KUNGOJEA

8. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunatafakari juu ya mifano ya wanaume na wanawake wa zamani?

8 Tutakuwa tayari zaidi kungojea ikiwa tunakumbuka wanaume na wanawake wa zamani wenye walingojea Yehova atimize ahadi zake. (Rom. 15:4) Wakati tunatafakari juu ya mifano yao, ni muzuri tukumbuke walipaswa kungojea kwa muda gani, sababu gani walikuwa tayari kungojea, na walipata baraka gani kwa sababu ya kungojea.

Abrahamu alipaswa kungojea miaka mingi mbele wajukuu wake Esau na Yakobo wazaliwe (Picha hii inapatana na fungu la 9, 10)

9, 10. Abrahamu na Sara walipaswa kungojea Yehova kwa muda gani?

9 Fikiria mufano wa Abrahamu na Sara. Wako kati ya ‘wale ambao kupitia imani na subira wanaziriti ahadi.’ Maandiko yanatuonyesha kuwa “baada ya Abrahamu kuonyesha subira,” Yehova alimuahidi kuwa angemubariki na kuzidisha uzao wake. (Ebr. 6:12, 15) Sababu gani Abrahamu alipaswa kuonyesha sifa ya kungojea? Kwa kifupi, ni kwa sababu kungepita muda murefu ili ahadi hiyo itimie. Agano lenye Yehova alifanya pamoja na Abrahamu lilianza kufanya kazi tarehe 14 Mwezi wa Nisani, 1943 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Ni wakati huo ndio yeye na Sara pamoja na watu wa nyumba yao walivuka Muto Efrati na kuingia katika Inchi ya Ahadi. Kisha, Abrahamu alipaswa kungojea miaka 25 mbele mutoto wake Isaka azaliwe katika mwaka wa 1918, na alipaswa kungojea miaka ingine 60 mbele wajukuu wake Esau na Yakobo wazaliwe katika mwaka wa 1858 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu.​—Ebr. 11:9.

10 Inchi yenye Abrahamu aliriti ilikuwa na ukubwa gani? Biblia inatuambia hivi: ‘Bado [Yehova] hakumupa [Abrahamu] uriti wowote ndani yake, hapana, hata upana wa . . . muguu; bali aliahidi kumupa hiyo kuwa miliki, na uzao wake baada yake, alipokuwa bado hana mutoto.’ (Mdo. 7:5) Wazao wake walifikia kupangwa na kuwa taifa lenye lingeriti inchi hiyo kisha kupita miaka 430 tangu Abrahamu avuke Muto Efrati.​—Kut. 12:40-42; Gal. 3:17.

11. Sababu gani Abrahamu alikuwa tayari kungojea Yehova, na atapata baraka gani kwa sababu ya kungojea?

11 Abrahamu alikuwa tayari kungojea kwa uvumilivu, kwa sababu sifa yake ya kungojea ilitegemea imani yake kwa Yehova. (Soma Waebrania 11:8-12.) Abrahamu alifurahia kungojea, hata kama hakuona utimizo wote wa ahadi hiyo wakati alikuwa angali muzima. Lakini fikiria furaha yenye Abrahamu atakuwa nayo wakati atafufuliwa katika dunia paradiso. Atashangaa kuona namna Biblia ilizungumuzia sana maisha yake na wazao wake. * Fikiria namna atafurahi kuelewa kwa mara ya kwanza daraka la maana lenye alikuwa nalo katika utimizo wa kusudi la Yehova juu ya uzao wenye uliahidiwa! Kwa kweli, ataona kuwa alifanya muzuri sana kungojea kwa muda murefu.

12, 13. Sababu gani Yosefu alipaswa kungojea, na alikuwa na mawazo gani ya muzuri?

12 Yosefu wa kizazi cha Abrahamu alionyesha pia kuwa alikuwa tayari kungojea. Alitendewa mubaya sana bila haki kwa njia mbalimbali. Kwanza, ndugu zake walimuuzisha ili akuwe mutumwa wakati alikuwa na miaka 17 hivi. Kisha alishitakiwa kwa uongo kuwa alitaka kulala kinguvu bibi ya mukubwa wake, na akafungwa katika vyuma katika gereza. (Mwa. 39:11-20; Zab. 105:17, 18) Kuliko kubarikiwa kwa sababu ya matendo yake ya muzuri, ilionekana kuwa alikuwa anapewa malipizi. Lakini, kisha miaka 13, mambo yote yalibadilika haraka. Alifunguliwa katika gereza na kupewa cheo cha mutu wa pili mwenye mamlaka zaidi katika Misri.​—Mwa. 41:14, 37-43; Mdo. 7:9, 10.

13 Yosefu alikuwa na hasira kwa sababu ya kutendewa kwa ukosefu huo wote wa haki? Aliacha kumutumainia Yehova, Mungu wake? Hapana. Ni nini ilimusaidia Yosefu angojee kwa uvumilivu? Ni imani yake kwa Yehova. Aliona mukono wa Yehova katika mambo hayo yote. Hilo linaonekana katika maneno yenye aliambia ndugu zake. Aliwaambia hivi: ‘Musiogope, kwa maana, je, mimi niko mahali pa Mungu? Kwa upande wenu, ninyi mulikuwa na uovu akilini mwenu kunielekea mimi. Mungu alikuwa na wema akilini kwa kusudi la kutenda kama ilivyo leo hii ili kuhifazi hai [kuponyesha uzima wa] watu wengi.’ (Mwa. 50:19, 20) Mwishowe, Yosefu alitambua kuwa alifanya muzuri sana kungojea.

14, 15. (a) Sababu gani sifa ya Daudi ya kungojea ni ya pekee? (b) Ni nini ilisaidia Daudi angojee kwa uvumilivu?

14 Mufalme Daudi alitendewa pia bila haki kwa njia nyingi. Wakati alikuwa angali kijana, Daudi alichaguliwa na Yehova ili afikie kuwa mufalme wa Israeli. Lakini alipaswa kungojea miaka 15 hivi mbele akuwe mufalme juu ya kabila lake. (2 Sam. 2:3, 4) Katika wakati fulani wa kipindi hicho, Mufalme Sauli mwenye kukosa uaminifu, alimutafuta Daudi ili kumuua. * Kwa hiyo, Daudi alilazimika kuishi kama mukimbizi, wakati fulani katika inchi ingine na wakati mwingine ndani ya mashimo katika jangwa. Hata wakati Sauli alifikia kuuawa katika vita, Daudi alilazimika kungojea tena ingine miaka saba ili afikie kupewa ufalme juu ya taifa lote la Israeli.​—2 Sam. 5:4, 5.

15 Sababu gani Daudi alikuwa tayari kungojea kwa uvumilivu? Anatupatia jibu katika zaburi ileile kwenye aliuliza mara ine, ‘Mupaka wakati gani?’ Alisema hivi: ‘Nami nimezitegemea fazili zako zenye upendo; moyo wangu na ushangilie katika wokovu wako. Nitamuimbia Yehova, kwa maana amenitendea kwa njia ya kunipa sawabu [baraka].’ (Zab. 13:5, 6) Daudi alitumainia upendo mushikamanifu wa Yehova. Kwa furaha, alingojea kwa hamu kukombolewa, na alifikiria namna Yehova alikuwa amemubariki. Kwa kweli, Daudi aliona kuwa ilikuwa muzuri kungojea baraka za Yehova.

Kuhusu kuonyesha sifa ya kungojea, Yehova hatazamie tufanye jambo lenye yeye mwenyewe haiko tayari kufanya

16, 17. Namna gani Yehova Mungu na Yesu Kristo wanatuwekea mufano muzuri sana juu ya kuwa tayari kungojea?

16 Kuhusu kuonyesha sifa ya kungojea, Yehova hatazamie tufanye jambo lenye yeye mwenyewe haiko tayari kufanya. Ametuwekea mufano mukubwa zaidi wa kuwa tayari kungojea. (Soma 2 Petro 3:9.) Yehova amekuwa akingojea kwa uvumilivu kwa maelfu ya miaka ili mashitaka yenye yalitokezwa katika shamba la Edeni yafikie kujibiwa kabisa. Yehova anangojea kwa uvumilivu na ‘kuendelea kutarajia’ wakati wenye jina lake litatakaswa kabisa. Hilo litaleta baraka nyingi sana kwa ajili ya wale ‘wanaoendelea kumutarajia [kumungojea].’​—Isa. 30:18.

17 Yesu pia amekuwa tayari kungojea. Hata kama alishinda jaribu la ushikamanifu hapa duniani na kumutolea Baba yake samani ya zabihu yake ya ukombozi katika mwaka wa 33, alipaswa kungojea mupaka mwaka wa 1914 ili aanze kutawala. (Mdo. 2:33-35; Ebr. 10:12, 13) Ni mupaka mwisho wa Utawala wake wa Miaka Elfu, ndio maadui wake wote wataharibiwa kabisa. (1 Kor. 15:25) Atakuwa amengojea kwa muda murefu kabisa, lakini tunaweza kuwa hakika kuwa kungojea hivyo kutakuwa na matokeo ya muzuri.

NINI ITATUSAIDIA?

18, 19. Ni nini itatusaidia kuwa tayari kungojea kwa uvumilivu?

18 Kwa kweli, kila mumoja wetu anapaswa kuwa tayari kungojea. Lakini, ni nini itatusaidia kufanya hivyo? Usali kwa Mungu na kumuomba roho yake takatifu. Kumbuka kuwa sifa ya ustahimilivu ni sehemu ya tunda la roho takatifu. (Efe. 3:16; 6:18; 1 Tes. 5:17-19) Umuombe Yehova akusaidie kuvumilia na kuendelea kungojea.

19 Kumbuka pia mambo yenye yalimusaidia Abrahamu, Yosefu, na Daudi wangojee Yehova atimize ahadi zake. Ilikuwa imani yao kwa Yehova na kutumainia namna yake ya kutenda. Hawakujifikiria tu wao wenyewe na mambo yenye kuwapendeza. Wakati tunafikiria matokeo ya muzuri yenye walipata, sisi pia tutachochewa kuonyesha sifa ya kungojea.

20. Kila mumoja wetu anapaswa kuazimia kufanya nini?

20 Kwa hiyo, hata kama tunapatwa na majaribu na magumu, tumeazimia kuonyesha ‘mutazamo wa kungojea.’ Ni kweli kwamba, wakati fulani tunaweza kuuliza hivi: ‘Mupaka wakati gani, Ee Yehova?’ (Isa. 6:11) Lakini kupitia nguvu ya roho takatifu ya Mungu, kila mumoja wetu ameazimia kusema maneno haya ya Yeremia: ‘Yehova ni fungu langu . . . Ndiyo sababu nitaonyesha mutazamo wa kumungojea.’​—Omb. 3:21, 24.

^ fu. 11 Sura 15 hivi za kitabu cha Mwanzo zinazungumuzia maisha ya Abrahamu. Pia, waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo wanamutaja Abrahamu zaidi ya mara 70.

^ fu. 14 Hata kama Yehova alimukataa Sauli kisha tu kutawala kwa miaka mbili hivi, alimuruhusu aendelee kutawala kwa miaka ingine 38, mupaka wakati alikufa.​—1 Sam. 13:1; Mdo. 13:21.