Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Amani ya Mungu . . . Inazidi Fikira Zote’

‘Amani ya Mungu . . . Inazidi Fikira Zote’

“Amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu.”​—FLP. 4:7.

NYIMBO: 76, 141

1, 2. Ni matukio gani yenye yalifanya Paulo na Sila wafungwe katika Filipi? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

NI KARIBU katikati ya usiku. Katika muji wa Filipi, wamisionere wawili, Paulo na Sila, wako katika sehemu ya ndani zaidi ya gereza. Miguu yao inafungwa na migongo yao ingali na maumivu kwa sababu wametoka tu kupigwa. (Mdo. 16:23, 24) Mambo yalitendeka haraka sana! Bila kuonywa walikuwa wamepelekwa kinguvu katika soko na kikundi cha watu wenye hasira ili wasambe mbele ya tribinali yenye iliitishwa haraka. Manguo yenye walikuwa wanavaa yalipasuliwa, na walipigwa sana fimbo. (Mdo. 16:16-22) Walitendewa bila haki kabisa! Kwa sababu Paulo alikuwa raia wa Roma, alipaswa kusambishwa kwa njia yenye kufaa. *

2 Wakati Paulo anakaa katika giza, anafikiria matukio ya siku hiyo. Anafikiri juu ya watu wa muji wa Filipi. Tofauti na miji mingine yenye Paulo amekwisha kutembelea, watu wa muji huo hawana hata sinagogi la Wayahudi. Ili kuabudu, Wayahudi walipaswa kukusanyika inje ya milango ya muji pembeni ya muto. (Mdo. 16:13, 14) Ni kwa sababu katika muji huo hakukuwa hata wanaume 10 Wayahudi, hesabu yenye iliombwa ili kuanzisha sinagogi? Watu wa Filipi wanajivunia sana kuwa na uraia wa Roma hata kama ni uraia wenye hauko kamili ao wa sehemu tu. (Mdo. 16:21) Pengine ndio sababu Wayahudi hao hawafikiri hata kuwa Paulo na Sila wanaweza kuwa raia wa Roma. Iwe ni hivyo ao hapana, walifungwa katika gereza bila sababu.

3. Sababu gani inawezekana kuwa Paulo alichanganyikiwa wakati alifungwa katika gereza, lakini alitenda namna gani?

3 Pengine Paulo anafikiria pia matukio ya miezi fulani yenye ilikuwa imepita. Alikuwa upande mwingine wa Bahari ya Aegea, katika Asia Ndogo. Wakati Paulo alikuwa huko, roho takatifu ilimuzuia mara kwa mara kuhubiri katika maeneo fulani. Ilikuwa kama vile roho takatifu ilikuwa inamusukuma aende mahali pengine. (Mdo. 16:6, 7) Lakini wapi? Alipewa jibu katika maono wakati alikuwa katika muji wa Troa. Paulo aliambiwa hivi: “Vuka uingie Makedonia.” Kwa sababu alionyeshwa wazi mapenzi ya Yehova, Paulo alikubali mara moja mualiko huo. (Soma Matendo 16:8-10.) Lakini, nini ilitokea kisha hapo? Kisha tu kufika Makedonia, alifungwa katika gereza! Sababu gani Yehova aliruhusu jambo hilo limufikie Paulo? Angefanya muda gani katika gereza? Hata kama maulizo hayo yalihangaisha sana akili ya Paulo, hakuruhusu yavunje imani yake ao kumaliza furaha yake. Yeye na Sila walianza ‘kusali na kumusifu Mungu kwa wimbo.’ (Mdo. 16:25) Amani ya Mungu ilituliza mioyo yao na akili zao.

4, 5. (a) Namna gani hali yetu inaweza kuwa kama ile ya Paulo? (b) Namna gani hali ya Paulo ilibadilika bila kutazamia?

4 Kama Paulo, pengine wakati fulani katika maisha yako uliona kuwa ulikuwa unafuata muongozo wa roho takatifu ya Mungu, lakini mambo hayakutendeka namna ulitazamia. Ulipatwa na magumu fulani, ao ulijikuta katika hali za mupya zenye zilikuomba ufanye mabadiliko makubwa katika maisha yako. (Mhu. 9:11) Wakati unakumbuka, pengine unajiuliza sababu gani Yehova aliruhusu mambo fulani yakufikie. Ikiwa ni hivyo, ni nini inaweza kukusaidia kuendelea kuvumilia na kumutumainia Yehova kabisa? Ili kupata jibu, tuzungumuzie tena Paulo na Sila.

5 Wakati Paulo na Sila wanaendelea kuimba nyimbo za sifa, matukio mbalimbali yenye hayakutazamiwa kabisa yanaanza kutokea. Mara moja, kunatokea tetemeko kubwa. Milango ya gereza inafunguka. Vitu vyote vyenye vilikuwa vinafunga wafungwa vinafunguka. Paulo anazuia mulinzi wa gereza kujiua. Mulinzi wa gereza na familia yake yote wanabatizwa. Asubuhi sana, waamuzi wa muji wanatuma polisi ili wafungue Paulo na Sila na kuwaomba waondoke katika muji kwa amani. Kisha, wakati wanatambua kuwa Paulo na Sila ni raia wa Roma, waamuzi wa muji wanaona kuwa wamekosea sana, kwa hiyo wanakuja wao wenyewe kuwasindikiza wanaume hao wawili ili waondoke. Lakini Paulo na Sila wanaenda kwanza kuaga dada Lidia, mwenye alikuwa ametoka tu kubatizwa. Pia, walitumia nafasi hiyo ili kutia nguvu ndugu na dada. (Mdo. 16: 26-40) Mambo yalibadilika haraka sana!

‘INAZIDI FIKIRA ZOTE’

6. Tutazungumuzia sasa nini?

6 Matukio hayo yanatufundisha nini? Yehova anaweza kufanya mambo yenye hatutazamie; kwa hiyo, hatupaswe kuhangaika wakati tunapambana na magumu. Bila shaka, tukio hilo liligusa sana Paulo, kama vile inaonekana katika maneno yenye alifikia kuandikia ndugu wa Filipi juu ya mahangaiko na amani ya Mungu. Tuzungumuzie basi maneno ya Paulo yenye kupatikana katika Wafilipi 4:6, 7. (Soma.) Kisha, tutazungumuzia mifano ingine fulani yenye kuwa katika Maandiko yenye kuonyesha namna Yehova alifanya mambo yenye haikutazamiwa. Mwishowe, tutazungumuzia namna “amani ya Mungu” inaweza kutusaidia kuvumilia na kumutumainia Yehova kabisa.

7. Paulo alikazia somo gani wakati aliandikia ndugu wa Filipi? Na mambo yenye aliandika yanaweza kutufundisha nini?

7 Bila shaka wakati ndugu wa Filipi walisoma barua yenye Paulo aliwaandikia, walikumbuka mambo yenye yalikuwa yamemufikia na namna hakuna hata mumoja wao mwenye alitazamia kuwa Yehova angetenda namna alitenda. Paulo alipenda kuwafundisha nini? Kwa kweli, alipenda kuwafundisha kuwa wasihangaike. Wasali na kisha watapata amani ya Mungu. Paulo aliwaambia kuwa ‘amani ya Mungu . . . inazidi fikira zote.’ Hilo linamaanisha nini? Watafsiri fulani wanatafsiri maneno hayo kuwa “inapita matumaini yote” ao “inapita mipango yote ya mwanadamu.” Kwa kweli, Paulo alikuwa anasema kuwa “amani ya Mungu” ni ya ajabu zaidi kuliko namna tunaweza kuwazia. Kwa hiyo, hata kama sisi wanadamu, tunaweza kuona kuwa hakuna namna ya kumaliza matatizo yetu, Yehova yeye anaona na anaweza kufanya mambo yenye hatutazamie.​—Soma 2 Petro 2:9.

8, 9. (a) Hata kama Paulo alitendewa bila haki katika Filipi, matukio hayo yalikuwa na matokeo gani ya muzuri? (b) Sababu gani ndugu katika Filipi wangeweza kukamata maneno ya Paulo kwa uzito?

8 Wakati ndugu wa Filipi walikuwa wanafikiria mambo yenye yalikuwa yamemupata Paulo miaka kumi yenye ilikuwa imepita, walipaswa kutiwa nguvu. Mambo yenye Paulo aliandika yalikuwa ya kweli. Hata kama Yehova aliruhusu ukosefu huo wa haki utendeke, hilo lilifikia ‘kutetea na kusibitisha kisheria habari njema.’ (Flp. 1:7) Waamuzi hao wa muji wangefikiri kwanza mbele ya kufanya jambo lolote juu ya kutaniko mupya la Kikristo katika muji huo. Pengine kwa sababu Paulo alisema kuwa yeye ni raia wa Roma, hilo lilimusaidia Luka, mwangalizi mwenzake mwenye kusafiri aweze kubakia Filipi kisha Paulo na Sila kuondoka. Kwa hiyo, Luka angeweza kusaidia sana Wakristo wapya katika muji huo.

9 Bila shaka, wakati ndugu wa Filipi walisoma barua ya Paulo, walijua kuwa maneno hayo hayakuwa ya mutu fulani mwenye alisoma sana mwenye kukaa mahali fulani katika biro. Paulo alipatwa na magumu makali sana; lakini, alionyesha kuwa alikuwa na “amani ya Mungu.” Wakati Paulo aliandikia ndugu hao, alikuwa amefungwa huko Roma. Lakini aliendelea kuonyesha kuwa alikuwa na “amani ya Mungu.” ​—Flp. 1:12-14; 4:7, 11, 22.

‘MUSIHANGAIKE JUU YA KITU CHOCHOTE’

10, 11. Tunapaswa kufanya nini wakati tunahangaika sana juu ya tatizo fulani, na tunaweza kutazamia nini?

10 Ni nini inaweza kutusaidia ili tusihangaike juu ya kitu chochote na tukuwe na “amani ya Mungu”? Maneno yenye Paulo aliwaandikia Wafilipi yanaonyesha kuwa dawa ya mahangaiko ni sala. Kwa hiyo, wakati tuko na mahangaiko, tunapaswa kusali sana. (Soma 1 Petro 5:6, 7.) Wakati unasali, ukuwe na imani kabisa kwa Yehova, na ujue kuwa anakuhangaikia. Usali kwake kwa “kutoa shukrani,” juu ya baraka zenye umepata. Tumaini letu kwake litatiwa nguvu wakati tunakumbuka kuwa anaweza ‘kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunayoomba ao tunayofikiri.’​—Efe. 3:20.

11 Kam vile Yehova alitendea Paulo na Sila katika Filipi, tunaweza kushangazwa na jambo lenye anaweza kutufanyia. Pengine halitakuwa jambo la ajabu, lakini litakuwa sikuzote jambo lenye tuko nalo lazima. (1 Kor. 10:13) Kwa kweli, hilo halimaanishe kuwa tutafunga tu mikono na kungojea Yehova atengeneze mambo ao amalize tatizo fulani. Tunapaswa kutenda kulingana na sala zetu. (Rom. 12:11) Matendo yetu yataonyesha uaminifu wetu, na kupatia Yehova sababu fulani ya kutubariki. Lakini, wakati huohuo, tunapaswa kukumbuka kuwa Yehova anaweza kutufanyia zaidi ya maombi, mipango, na mambo yenye tunatazamia. Wakati fulani anafanya mambo fulani yenye hatutazamie. Tuzungumuzie basi habari fulani zenye kuwa katika Biblia zenye kutia nguvu imani yetu katika uwezo wa Yehova wa kutufanyia mambo yenye hatutazamie.

MIFANO YA WATU WENYE YEHOVA ALIFANYIA MAMBO YENYE HAWAKUTAZAMIA

12. (a) Mufalme Hezekia alifanya nini wakati Senakeribu mufalme wa Ashuru alimuogopesha? (b) Namna Yehova alimaliza tatizo hilo, inatufundisha nini?

12 Biblia inazungumuzia mifano mingi yenye kuonyesha namna Yehova alifanya mambo yenye watu hawakutazamia. Mufalme Hezekia aliishi wakati wenye Senakeribu mufalme wa Ashuru, alishambulia Yuda na kukamata miji yote yenye kuta, lakini hakukamata tu muji wa Yerusalemu. (2 Fal. 18:1-3, 13) Kisha, Senakeribu alipenda sasa kukamata pia Yerusalemu. Mufalme Hezekia alifanya nini wakati alipambana na hali hiyo yenye kuogopesha? Alisali kwa Yehova na kuomba mashauri kwa Isaya, nabii wa Yehova. (2 Fal. 19:5, 15-20) Pia, Hezekia alijikaza kuonyesha usawaziko kwa kulipa vitu vyenye Senakeribu alimulazimisha kulipa. (2 Fal. 18:14, 15) Kisha Hezekia alifanya mipango fulani ya kusaidia ikiwa muji unazungukwa kwa muda murefu. (2 Nya. 32:2-4) Lakini namna gani tatizo hilo lilimalizwa? Yehova alituma malaika mumoja mwenye aliua maaskari 185  000 wa Senakeribu katika usiku mumoja. Kwa kweli, Hezekia hakutazamia hata kidogo kuwa jambo hilo lingetendeka!​—2 Fal. 19:35.

Mambo yenye yalimufikia Yosefu yanaweza kutufundisha nini?​—Mwa. 41:42 (Picha hii inapatana na fungu la 13)

13. (a) Mambo yenye yalimufikia Yosefu, yanatufundisha nini? (b) Namna gani jambo lenye halikutazamiwa lilitokea katika maisha ya Sara, bibi ya Abrahamu?

13 Fikiria mufano wa kijana Yosefu, mutoto wa Yakobo. Wakati alikuwa katika gereza moja katika Misri, je, Yosefu alifikiria kuwa angewekwa kuwa mutu wa pili mwenye mamlaka zaidi katika inchi hiyo ao kuwa Yehova angemutumia ili kuokoa familia yake wakati wa njaa kubwa? (Mwa. 40:15; 41:39-43; 50:20) Kwa kweli, mambo yenye Yehova alifanya yalipita mambo yote yenye Yosefu alikuwa anatazamia. Fikiria pia Sara tate (nkambo) ya Yakobo, baba ya Yosefu. Sara alitazamia kuwa Yehova angemuwezesha kuzaa mutoto wake mwenyewe, kuliko tu kuwa na mutoto wa mutumwa wake mwanamuke? Kuzaliwa kwa Isaka kulipita mambo yote yenye Sara angeweza kuwazia.​—Mwa. 21:1-3, 6, 7.

14. Tunaweza kuwa hakika kuwa Yehova atatufanyia nini?

14 Lakini, hatutazamie kuwa Yehova ataondoa kwa njia ya muujiza magumu yetu yote mbele ya ulimwengu mupya wenye ameahidi ufike; na hatumuombe afanye mambo ya ajabu katika maisha yetu. Lakini, tunajua kuwa Mungu mwenye alisaidia watumishi wake kwa njia za ajabu ni Yehova, Mungu wetu. (Soma Isaya 43:10-13.) Kuwa hakika juu ya jambo hilo, kunatusaidia kuwa na imani kwake. Tunajua kuwa anaweza kufanya jambo lolote lenye kuhitajiwa ili kututia nguvu ili tutimize mapenzi yake. (2 Kor. 4:7-9) Habari hizo zenye kuwa katika Biblia zinatufundisha nini? Mufano wa Hezekia, Yosefu, na wa Sara unaonyesha kuwa Yehova anaweza kutusaidia kupata ushindi juu ya jambo fulani lenye tunaona kuwa hatuwezi kushinda ikiwa tunaendelea kuwa waaminifu kwake.

Yehova anaweza kutusaidia kupata ushindi juu ya jambo fulani lenye tunaona kuwa hatuwezi kushinda ikiwa tunaendelea kuwa waaminifu kwake

15. Ni nini itatusaidia kuendelea kuwa na “amani ya Mungu,” na hilo linawezekana namna gani?

15 Namna gani tunaweza kuendelea kuwa na “amani ya Mungu” wakati tunapambana na magumu? Ni kwa kuendelea kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova, Mungu wetu. Urafiki huo unawezekana tu “kwa njia ya Kristo Yesu,” mwenye alitoa uzima wake kuwa zabihu ya ukombozi. Mupango wa zabihu ya ukombozi ni moja kati ya kazi za ajabu za Baba yetu. Yehova anatumia zabihu ya ukombozi ili kusamehe zambi zetu, na hilo linatusaidia kuwa na zamiri safi na kumukaribia.​—Yoh. 14:6; Yak. 4:8; 1 Pet. 3:21.

ITALINDA MIOYO YETU NA NGUVU ZETU ZA AKILI

16. Tutapata matokeo gani wakati tunapata “amani ya Mungu”? Toa mufano.

16 Tunapata matokeo gani wakati tunapata “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote”? Maandiko yanatoa jibu kwa kusema kama ‘italinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.’ (Flp. 4:7) Neno la zamani lenye kutafsiriwa “kulinda” lilitumiwa katika jeshi. Lilizungumuzia kikundi cha askari wenye walipewa kazi ya kulinda muji wenye kuzungukwa na kuta wakati wa zamani. Muji wa Filipi ulikuwa hivyo. Wakaaji wa Filipi walilala salama usiku kwa sababu walijua kuwa maaskari walikuwa wanalinda milango ya muji wao. Vilevile, wakati tuko na “amani ya Mungu,” mioyo yetu na akili zetu zinatulia. Tunajua kama Yehova anatuhangaikia na anataka tukuwe na maisha ya muzuri. (1 Pet. 5:10) Kujua hilo kunatusaidia tusihangaike sana na tusivunjike moyo.

17. Ni nini itatusaidia tumutumainie kabisa Yehova wakati wa ziki kubwa?

17 Hivi karibuni wanadamu watapambana na ziki kubwa zaidi yenye haitatokea tena katika dunia. (Mt. 24:21, 22) Hatujue kabisa-kabisa ni mambo gani yatapata kila mumoja wetu. Lakini, hatupaswe kuhangaika sana. Hata kama hatujue mambo yote yenye Yehova atafanya, tunamujua Mungu wetu. Namna alitendea watumishi wake waaminifu wa zamani inaonyesha kuwa hata kutokee nini, sikuzote Yehova atatimiza kusudi lake, na wakati fulani anafanya hivyo kwa njia yenye haitazamiwe. Kila wakati Yehova anatufanyia hivyo, tunaweza kujionea kwa njia ingine “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”

^ fu. 1 Inawezekana kuwa Sila alikuwa pia raia wa Roma.​—Mdo. 16:37.