Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari juu ya Maisha ya Watu

Kuvumilia Wakati wa Magumu Kunaleta Baraka

Kuvumilia Wakati wa Magumu Kunaleta Baraka

OFISA mumoja wa KGB * aliniambia hivi kwa ukali: “Uko baba mubaya sana. Umeacha bibi yako mwenye kuwa na mimba na mutoto wako mudogo mwanamuke. Nani atawasaidia kupata chakula na kuwatunza? Kataa kazi yako na utarudia nyumbani!” Nilijibia hivi: “Hapana sikuacha familia yangu. Mulinifunga! Na nilifanya kosa gani?” Ofisa huyo alijibia hivi: “Kuwa Shahidi ndiyo kosa kubwa zaidi.”

Mazungumuzo hayo yalifanywa katika mwaka wa 1959 katika gereza moja katika muji wa Irkutsk, Urusi. Ninataka kuwaelezea sababu gani mimi na bibi yangu Maria, tulikuwa tayari ‘kuteseka kwa ajili ya uadilifu’ na namna tulibarikiwa kwa sababu ya kubakia waaminifu.​—1 Pet. 3:13, 14.

Nilizaliwa katika Ukrainia katika mwaka wa 1933 katika kijiji cha Zolotniki. Katika mwaka wa 1937, dada ya mama yangu pamoja na bwana yake walitoka Ufaransa na kuja kututembelea; walikuwa Mashahidi wa Yehova. Na walituachia vitabu Governement na Délivrance, vyenye vilichapishwa na Shirika Watch Tower. Wakati baba yangu alisoma vitabu hivyo, imani yake katika Mungu ilichochewa tena. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba katika mwaka wa 1939 aligonjwa sana, lakini mbele akufe aliambia mama yangu hivi: “Hii ndio kweli. Uifundishe watoto.”

SIBERIA, ENEO MUPYA LA KUHUBIRIA

Katika Mwezi wa 4, 1951, wakubwa wa serikali walianza kuhamisha Mashahidi wengi kutoka mangaribi mwa Muungano wa Sovieti na kuwatuma Siberia. Mimi na mama yangu na Grigory mudogo yangu mwanaume tulihamishwa kutoka Mangaribi mwa Ukrainia. Kisha kusafiri kilometre zaidi ya 6000 katika treni, tulifika katika muji wa Tulun katika Siberia. Majuma mbili kisha hapo, Bogdan kaka yangu mukubwa, alifika katika kambi moja katika muji wa Angarsk wenye ulikuwa karibu. Alikuwa amehukumiwa miaka 25 ya kazi ngumu.

Mimi, mama yangu, na Grigory, tulihubiri makao ya watu yenye yalikuwa pembeni ya Tulun, lakini tulipaswa kuwa waangalifu. Kwa mufano, tulikuwa tunauliza hivi: “Kuko mutu mwenye anapenda kuuzisha ngombe?” Wakati tulipata mutu mwenye kuwa na ngombe ya kuuzisha, tulizungumuza na mutu huyo namna ngombe iliumbwa kwa njia ya ajabu sana. Na bila kukawia, tulianza kuzungumuza naye juu ya Muumbaji. Wakati huo, gazeti moja la ulimwengu liliandika kuwa Mashahidi wa Yehova wanauliza juu ya ngombe lakini wanatafuta kondoo! Na tulipata watu wenye kuwa mufano wa kondoo! Tulifurahia kujifunza Biblia pamoja na watu wanyenyekevu na wakaribishaji-wageni katika eneo hilo lenye lilikuwa halijahubiriwa. Leo, katika muji wa Tulun kuko kutaniko lenye kuwa na wahubiri zaidi ya 100.

NAMNA IMANI YA MARIA ILIJARIBIWA

Bibi yangu Maria, alijifunza kweli katika Ukrainia katikati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu. Wakati alikuwa na miaka 18, ofisa mumoja wa KGB alijaribu kumuchochea afanye uasherati naye, lakini alikataa kabisa jambo hilo. Siku moja wakati Maria alirudia nyumbani, alikutana mwanaume huyo analala kwenye kitanda chake. Maria alikimbia. Ofisa huyo alikasirika na alimuogopesha kuwa atamufunga kwa sababu yeye ni Shahidi, na kwa kweli, katika mwaka wa 1952, Maria alihukumiwa miaka kumi katika gereza. Alijisikia kama Yosefu mwenye alifungwa kwa sababu aliendelea kuwa mushikamanifu. (Mwa. 39:12, 20) Mutu mwenye alikuwa anatembeza motokari yenye ilitosha Maria kwenye tribinali na kumupeleka katika gereza, alimuambia hivi: “Usiogope. Watu wengi wanaenda katika gereza lakini wanarudia na heshima yao yote.” Maneno hayo yalimutia nguvu.

Kuanzia mwaka 1952 mupaka mwaka wa 1956, Maria aliombwa kutumika katika kambi ya kazi ngumu karibu na muji wa Gorkiy (sasa unaitwa Nizhniy Novgorod) katika Urusi. Alilazimishwa kuongoa miti hata wakati wa baridi sana. Afya yake iliharibika, lakini katika mwaka wa 1956 aliachiliwa na alienda Tulun.

KUWA MBALI SANA NA BIBI YANGU NA WATOTO WANGU

Wakati ndugu mumoja katika Tulun aliniambia kuwa dada fulani alikuwa anakuja, nilitumia kinga yangu na kuenda mahali penye bisi ilikuwa inasimama ili kukutana naye na kumusaidia kubeba mizigo yake. Wakati nilikutana na Maria, nilimupenda mara moja. Iliniomba kujikaza sana ili kumufanya anipende pia, lakini niliweza kufanya hivyo. Tulioana katika mwaka wa 1957. Kisha mwaka moja, Irina, mutoto wetu mwanamuke alizaliwa, lakini, furaha ya kuwa pamoja naye ilifupishwa. Katika mwaka wa 1959, nilifungwa kwa sababu ya kuchapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia. Nilifanya miezi sita hivi katika chumba cha gereza mimi mwenyewe. Ili kuendelea kuwa na amani ya moyoni wakati huo, kila mara nilisali, niliimba nyimbo za Ufalme, na kuwazia namna ningeweza kuhubiri ikiwa ninaachiliwa.

Wakati nilikuwa ninaishi katika kambi ya kazi ngumu katika mwaka wa 1962

Katika gereza, wakati nilikuwa ninaulizwa maulizo, mupelelezi alisema hivi kwa sauti kubwa: “Hivi karibuni, tutawaponda kama vile mutu anaponda panya kwenye udongo!” Nilijibia hivi: “Yesu alisema kuwa habari njema ya Ufalme ITAHUBIRIWA katika mataifa yote, na hakuna mutu mwenye anaweza kuzuia jambo hilo.” Kisha, mupelelezi huyo alibadilisha ufundi wake na kujaribu kunishawishi kukana imani yangu, kama vile nilieleza mwanzoni. Wakati hakuweza kuniogopesha ao kunishawishi, nilihukumiwa miaka saba ya kazi ngumu katika kambi moja karibu na muji wa Saransk. Wakati nilikuwa ninapelekwa katika kambi hiyo, nilijulishwa kuwa Olga, mutoto wetu wa pili mwanamuke, alikuwa amezaliwa. Hata kama bibi yangu na watoto wangu wanawake walikuwa mbali, nilifarijiwa kujua kuwa mimi na Maria tulikuwa tumebakia washikamanifu kwa Yehova.

Maria na watoto wetu wanawake, Olga na Irina, katika mwaka wa 1965

Mara moja kwa mwaka Maria alisafiri na kuja Saransk ili kunitembelea, hata kama safari ya kutoka Tulun na kurudia ilikuwa inachukua siku 12 kwa treni. Kila mwaka alikuwa ananiletea viatu vya mupya vya aina ya buti. Alificha ndani ya viatu hivyo, magazeti ya mupya ya Munara wa Mulinzi. Mwaka mumoja ulikuwa wa pekee sana kwa sababu Maria alikuja na watoto wetu wadogo wawili. Wazia namna nilifurahi sana kwa sababu ya kuwaona na kuwa pamoja nao!

MAENEO MAPYA NA MAGUMU MAPYA

Katika mwaka wa 1966, nilifunguliwa kutoka katika kambi ya kazi ngumu na sisi wote tulihamia katika muji wa Armavir, karibu na Bahari Nyeusi. Watoto wetu wanaume Yaroslav na Pavel walizaliwa katika muji huo.

Kisha muda mufupi, maofisa wa KGB walianza kuchunguza nyumba yetu ili kutafuta vichapo vyenye kutegemea Biblia. Walitafuta kila mahali, hata mahali pa kuwekea ngombe chakula. Wakati fulani, maofisa, walitokwa sana jasho kwa sababu ya joto, na nguo zao zilikuwa zinajaa vumbi. Maria aliwasikilia huruma, kwa sababu walikuwa tu wanatii maagizo. Aliwapatia maji ya matunda na kuwaletea brosse ya nguo, beseni ya maji, na nguo za kujipanguza. Kisha, wakati mukubwa wa KGB alifika, maofisa walimuambia namna walikuwa wametendewa muzuri. Wakati waliondoka, mukubwa huyo alituonyesha sura ya kicheko na kutuaga. Tulifurahi kuona matokeo ya muzuri yenye tunaweza kupata wakati tunajikaza ‘kuendelea kuushinda uovu kwa wema.’​—Rom. 12:21.

Hata kama walikuwa wanachunguza nyumba yetu, tuliendelea kuhubiri katika Armavir. Tulisaidia pia kutia nguvu kikundi kidogo cha wahubiri katika muji wenye kuwa karibu wa Kurganinsk. Niko na furaha sana kujua kuwa leo kuko makutaniko sita katika muji wa Armavir na makutaniko ine katika muji wa Kurganinsk.

Katika miaka mingi, wakati fulani hatukutumikia Yehova namna tulipaswa kumutumikia. Lakini tuko wenye shukrani kwa Yehova kwa sababu alitumia ndugu waaminifu ili kuturekebisha na kututia nguvu kiroho. (Zab. 130:3) Ilikuwa pia jaribu kubwa kutumika pamoja na watu wa KGB wenye walijiingiza katika kutaniko bila sisi kutambua jambo hilo. Walionekana kuwe wenye bidii na walikuwa wanahubiri sana. Hata wamoja wao walipewa madaraka katika tengenezo. Lakini, kisha wakati fulani tulivumbua walikuwa nani kabisa.

Katika mwaka wa 1978, wakati Maria alikuwa na miaka 45, alipata tena mimba. Kwa sababu alikuwa na ugonjwa wa moyo wa muda murefu, wanganga waliogopa kuwa angekufa na walijaribu kumusadikisha atoshe mimba hiyo. Maria alikataa. Kwa hiyo, wanganga fulani walimufuata kila mahali katika hospitali na kujaribu kumutoboa dawa yenye ingefanya azae mbele ya miezi kuenea. Ili kulinda mutoto mwenye alikuwa katika tumbo, Maria alikimbia hospitali.

Maofisa wa KGB walituamuru tuondoke katika muji. Tulihamia katika kijiji kimoja karibu na muji wa Tallinn katika Estonia, yenye ilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti. Tofauti na namna wanganga walikuwa wamewazia, Maria alizaa Vitaly, mutoto mwanaume mwenye afya ya muzuri.

Kisha, tulitoka Estonia na tukahamia Nezlobnaya, kusini mwa Urusi. Tulihubiri kwa uangalifu katika miji jirani kwenye watu walizoea kufanyia mapumuziko; miji hiyo ilitembelewa na watu kutoka katika inchi yote. Walikuja kwa sababu za matunzo, lakini wamoja walirudia wakiwa na tumaini la uzima wa milele!

KUSAIDIA WATOTO WETU WAMUPENDE YEHOVA

Tulijikaza kufundisha watoto wetu wamupende Yehova na wakuwe na hamu ya kumutumikia. Mara kwa mara tulialika katika nyumba yetu ndugu wenye wangechochea watoto wetu kiroho. Mugeni mumoja mwenye alizoea kututembelea alikuwa mudogo yangu Grigory, mwenye alikuwa mwangalizi wa muzunguko kuanzia mwaka wa 1970 mupaka 1995. Familia yote ilifurahi wakati alikuwa anatutembelea kwa sababu alikuwa mwenye furaha na alikuwa mwenye kuchekesha. Wakati tulikuwa na wageni, mara nyingi tulicheza michezo ya Biblia, na watoto wetu walifikia kupenda historia za Biblia.

Watoto wangu wanaume na bibi zao.

Kutoka kushoto kuenda kuume, nyuma: Yaroslav, Pavel, Jr., Vitaly

Mbele: Alyona, Raya, Svetlana

Katika mwaka wa 1987, Yaroslav, mutoto wetu mwanaume, alihamia katika muji wa Riga katika Latvia, kwenye aliweza kuhubiri waziwazi zaidi. Lakini wakati alikataa kufanya kazi ya jeshi, alihukumiwa mwaka moja na nusu katika gereza na alipelekwa katika gereza kenda mbalimbali. Mambo yenye nilikuwa nimemuambia juu ya maisha yangu katika gereza yalimusaidia kuvumilia. Kisha, alianza kufanya kazi ya upainia. Katika mwaka wa 1990, kijana wetu Pavel, mwenye alikuwa na miaka 19, alitaka kuenda kufanya kazi ya upainia katika Sakhalin, kisiwa kimoja chenye kuwa kaskazini mwa japani. Mwanzoni hatukupenda aende. Kulikuwa tu wahubiri 20 katika kisiwa chote, na kisiwa hicho kilikuwa kwenye umbali wa kilometre zaidi ya 9000 kutoka mahali tulikuwa tunaishi. Lakini mwishowe tulikubali, na ulikuwa uamuzi muzuri. Katika kisiwa hicho watu walikubali ujumbe wa Ufalme. Kisha miaka kidogo, kulikuwa makutaniko munane. Pavel alitumikia katika Sakhalin mupaka mwaka wa 1995. Wakati huo, Vitaly, mutoto wetu mwanaume wa mwisho ndiye tu alikuwa amebakia nyumbani. Tangu wakati alikuwa mutoto alipenda kusoma Biblia. Wakati alikuwa na miaka 14, alianza kufanya kazi ya upainia, na nilifanya kazi ya upainia pamoja naye kwa miaka mbili. Huo ulikuwa wakati muzuri sana. Wakati alikuwa na miaka 19, Vitaly aliondoka nyumbani ili kuenda kutumikia mugawo wa painia wa pekee.

Katika mwaka 1952, ofisa wa KGB aliambia Maria hivi: “Kana imani yako ao ufungwe katika gereza miaka kumi. Wakati utatoka katika gereza utakuwa umezeeka na utakuwa peke yako.” Lakini mambo hayakuwa hivyo kabisa. Tuliona upendo wa Yehova, Mungu wetu mushikamanifu, wa watoto wetu, na wa watu wengi wenye tumepata pendeleo la kusaidia wajue kweli. Mimi na Maria tulifurahi kutembelea mahali penye watoto wetu walikuwa wanatumikia. Tuliona shukrani ya wale wenye watoto wetu walisaidia kujua kweli.

NIKO MWENYE SHUKRANI KWA SABABU YA WEMA WA YEHOVA

Katika mwaka wa 1991, kazi ya Mashahidi wa Yehova ilikubaliwa na sheria. Uamuzi huo uliongeza bidii katika kazi kuhubiri. Hata kutaniko letu liliuza bisi ili tuweze kusafiri katika miji na vijiji jirani kila mwisho wa juma.

Mimi pamoja na bibi yangu katika mwaka wa 2011

Niko mwenye furaha kwa sababu Yaroslav na bibi yake Alyona, na Pavel na bibi yake Raya, wanatumikia kwenye Beteli, na Vitaly na bibi yake yake Svetlana, wanafanya kazi ya muzunguko. Irina, mutoto wetu mwanamuke mukubwa na familia yake wanaishi Ujerumani. Bwana yake Vladimir, na watoto wake watatu wanaume wote ni wazee wa kutaniko. Olga, mutoto wetu mwingine mwanamuke anaishi katika Estonia na mara kwa mara ananiita. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, Maria, bibi yangu mupendwa alikufa katika mwaka wa 2014. Ninangojea kwa hamu sana kumuona tena wakati wa ufufuo! Sasa ninaishi katika muji wa Belgorod, na ndugu wananitegemeza sana hapa.

Miaka yenye nimefanya katika utumishi wa Yehova imenifundisha kuwa ili kuendelea kuwa washikamanifu inaomba kujikaza sana, lakini amani ya moyo yenye Yehova anatupatia kwa sababu ya ushikamanifu huo ni hazina kubwa sana. Baraka zenye mimi na Maria tulipata kwa sababu ya kuendelea kuwa imara ni nyingi sana kuliko namna ningeweza kuwazia. Mbele ya kuanguka kwa Muungano wa Sovieti katika mwaka wa 1991, kulikuwa tu wahubiri zaidi ya 40 000. Leo, kuko wahubiri zaidi ya 400 000 katika inchi zenye zamani zilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti! Sasa niko na miaka 83, na ninaendelea kuwa muzee wa kutaniko. Sikuzote Yehova amenitegemeza, na hilo limenipatia nguvu ya kuvumilia. Kwa kweli, Yehova amenibariki sana.​—Zab. 13:5, 6.

^ fu. 4 Katika luga ya Kirusi, KGB ni kifupi cha Shirika la Usalama wa Kitaifa la Sovieti.