Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kweli Hailete, “Amani, Bali Upanga”

Kweli Hailete, “Amani, Bali Upanga”

‘Musifikiri nilikuja kuleta amani duniani; nilikuja kuleta, si amani, bali [lakini] upanga.’​—MT. 10:34.

NYIMBO: 125, 135

1, 2. (a) Tunaweza kufurahia amani gani leo? (b) Ni nini inatuzuia kupata amani kabisa-kabisa leo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

SISI wote tunapenda kuwa na maisha yenye amani, bila mahangaiko. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Yehova anatupatia “amani ya Mungu,” ni kusema, utulivu wa moyoni wenye unaweza kutulinda ili tusikuwe na mawazo yenye kuhangaisha akili! (Flp. 4:6, 7) Kwa sababu tumejitoa kwa Yehova, tunafurahia pia kuwa na “amani pamoja na Mungu,” ni kusema, urafiki muzuri pamoja naye.​—Rom. 5:1.

2 Lakini, wakati wenye Mungu ataleta amani kabisa-kabisa haujafika. Katika siku hizi za mwisho zenye kuwa ngumu kushugulika nazo, watu wengi hawapendi kuelewana na wanapenda mabishano. (2 Tim. 3:1-4) Sisi Wakristo tunapaswa kupigana vita ya kiroho na Shetani na mafundisho ya uwongo yenye anachochea. (2 Kor. 10:4, 5) Lakini jambo lenye linaweza kutia zaidi amani yetu katika hatari ni watu wa jamaa yetu wenye hawako Mashahidi. Wamoja wanaweza kuchekelea ao kuzarau mambo yenye tunaamini, wanaweza kusema kuwa tunagawanya familia, ao kutuogopesha kuwa watatukataa ikiwa hatuache imani yetu. Namna gani tunapaswa kuona upinzani wa watu wa familia? Namna gani tunaweza kupambana muzuri na magumu yenye upinzani huo unaleta?

NAMNA GANI TUNAPASWA KUONA UPINZANI WA WATU WA FAMILIA?

3, 4. (a) Mafundisho ya Yesu yanaleta matokeo gani? (b) Ni wakati gani ingekuwa vigumu zaidi kumufuata Yesu?

3 Yesu alijua kuwa mafundisho yake yangegawanya watu na kwamba wale wenye kumufuata wangekuwa na lazima ya ujasiri ili waendelee kumufuata hata kama wanapingwa. Upinzani huo ungetia katika hatari amani kati ya watu wa familia. Yesu alisema hivi: ‘Musifikiri nilikuja kuleta amani duniani; nilikuja kuleta, si amani, bali upanga. Kwa maana nilikuja kuleta mugawanyiko, mutu kumupinga baba yake, binti kumupinga mama yake, muke aliye muchanga kumupinga mama-mukwe wake. Kwa kweli, adui za mutu watakuwa watu wa nyumbani kwake mwenyewe.’​—Mt. 10:34-36.

4 Wakati Yesu alisema ‘Musifikiri nilikuja kuleta amani,’ alimaanisha kuwa wamoja kati ya wasikilizaji wake walipaswa kufikiria matokeo ya kumufuata. Ujumbe wake ungeleta mugawanyiko kati ya watu. Kwa kweli, kusudi la Yesu lilikuwa kutangaza ujumbe wa kweli wa Mungu, lakini haiko kuharibu uhusiano kati ya watu. (Yoh. 18:37) Hata hivyo, ingekuwa vigumu kushikamana kwa uaminifu na mafundisho ya Kristo, ikiwa marafiki wa sana wa mutu ao watu wa familia yake wangekataa kweli.

5. Wanafunzi wa Yesu wamepatwa na nini?

5 Yesu alionyesha kuwa maumivu yenye kuletwa na upinzani wa watu wa familia ingekuwa kati ya mateso yenye wanafunzi wake wangepaswa kuvumilia. (Mt. 10:38) Ili kuonyesha kuwa wanastahili kuwa wanafunzi wa Kristo, wanafunzi wake wamelazimika kuvumilia kuzarauliwa na kuchukiwa na watu wa familia zao. Lakini, wamepata mambo mengi zaidi ya ile yenye wamepoteza.​—Soma Marko 10:29, 30.

6. Tunapaswa kukumbuka nini ikiwa watu wa jamaa yetu wanatupinga kwa sababu tunamuabudu Yehova?

6 Hata wakati watu wa jamaa yetu wanatupinga kwa sababu tunamuabudu Yehova, tunaendelea kuwapenda, lakini tunapaswa kukumbuka kuwa upendo wetu kwa Mungu na Kristo ndio unapaswa kuwa pa nafasi ya kwanza. (Mt. 10:37) Tunapaswa kujua pia kwamba Shetani atajaribu kutumia upendo wetu kwa watu wa familia yetu ili kuvunja ushikamanifu wetu. Tuzungumuzie basi hali fulani zenye kufanya watu wa familia yetu watupinge na tuone namna tunaweza kupambana muzuri na hali hizo.

BIBI AO BWANA MWENYE HAIKO SHAHIDI

7. Namna gani unapaswa kuona hali yako ikiwa bibi ao bwana yako haiko Shahidi?

7 Biblia inasema kuwa wale wenye kufunga ndoa ‘watakuwa na ziki [taabu] katika mwili wao.’ (1 Kor. 7:28) Ikiwa uko na bibi ao bwana mwenye haiko Shahidi, unaweza kupata mahangaiko zaidi katika ndoa yako. Lakini, ni jambo la maana uone hali yako kama vile Yehova anaiona. Anaonyesha kuwa hatuwezi kutengana ao kuvunja ndoa yetu kwa sababu tu bibi ao bwana yetu hamutumikie Yehova. (1 Kor. 7:12-16) Hata kama pengine bwana mwenye haiko Shahidi hahangaikie mambo ya kiroho, bibi anapaswa kumuheshimia kwa sababu ya daraka lake la kuwa kichwa cha familia. Vilevile, bwana Mukristo anapaswa kutendea kwa upole na upendo bibi yake mwenye haiko Shahidi.​—Efe. 5:22, 23, 28, 29.

8. Unaweza kujiuliza maulizo gani ikiwa bibi ao bwana yako anajaribu kuweka mipaka juu ya ibada yako?

8 Tuseme nini ikiwa bibi ao bwana yako anakuwekea mipaka juu ya ibada yako kwa Yehova? Kwa mufano, bwana ya dada mumoja alimuambia kuwa anaweza kuhubiri siku fulani tu katika juma. Ikiwa uko katika hali hiyo, ujiulize hivi: ‘Bibi ao bwana yangu ananiomba niache kumuabudu Mungu? Ikiwa ni hapana, ninaweza kukubali ombi lake?’ Kuwa na usawaziko kunaweza kukusaidia uepuke matatizo ya kukosa kuelewana katika ndoa juu ya mambo madogo-madogo.​—Flp. 4:5.

9. Namna gani Wakristo wanaweza kufundisha watoto wao waheshimie muzazi mwenye haiko Shahidi?

9 Inaweza kuwa vigumu sana kufundisha watoto wako ikiwa bibi ao bwana yako haiko Shahidi. Kwa mufano, unapaswa kufundisha watoto wako kutii amri hii ya Biblia: ‘Muheshimu baba yako na mama yako.’ (Efe. 6:1-3) Lakini utafanya nini ikiwa bibi ao bwana yako hafuate kanuni za juu za mwenendo za Biblia? Uonyeshe mufano kwa kuheshimia bibi ao bwana yako. Kazia sifa zake za muzuri, na umuonyeshe shukrani. Uepuke kusema mambo ya mubaya juu ya bibi ao bwana yako mbele ya watoto wako. Lakini, uwafasirie kuwa kila mutu anapaswa kuchagua ikiwa atamutumikia Yehova ao hapana. Mwenendo muzuri wa watoto unaweza kuchochea muzazi mwenye haiko Shahidi akubali ibada ya kweli.

Fundisha watoto wako kweli ya Biblia kila wakati inawezekana kufanya hivyo (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10. Namna gani wazazi Wakristo wanafundisha watoto wao kweli ya Biblia katika familia ambamo bibi ao bwana haiko Shahidi?

10 Wakati fulani bibi ao bwana mwenye haiko Shahidi anaweza kuomba watoto wafanye sikukuu za kipagani ao wafundishwe mafundisho ya dini ya uwongo. Bwana fulani wanaweza kukataza bibi Mukristo kufundisha watoto Biblia. Hata hivyo, bibi Mukristo anapaswa kufanya yake yote ili kufundisha watoto kweli ya Biblia. (Mdo. 16:1; 2 Tim. 3:14, 15) Kwa mufano, bwana ya bibi mwenye kuwa Shahidi anaweza kumukataza kuwa na programu ya kujifunza Biblia na watoto wake wadogo ao kuwapeleka kwenye mikutano. Bibi ataheshimia maamuzi yake, lakini anaweza kuelezea watoto wake imani yake wakati nafasi inajitokeza, kwa kufanya hivyo wanaweza kujifunza juu ya Yehova na kanuni zake za mwenendo. (Mdo. 4:19, 20) Kwa kweli, watoto wake watafikia kukamata uamuzi wao wenyewe juu ya mambo ya ibada.​—Kum. 30:19, 20. *

WATU WA JAMAA WENYE WANAPINGA IBADA YA KWELI

11. Ni nini inaweza kutokeza matatizo kati yako na watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi?

11 Pengine mwanzoni, hatukuambia watu wa familia yetu kuwa tumeanza kujifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova. Lakini, kadiri imani yetu iliendelea kukomaa, tuliona kuwa ni jambo la lazima kuwaelezea mambo yenye tunaamini. (Mk. 8:38) Ikiwa musimamo wako wa ujasiri umetokeza matatizo kati yako na watu wa jamaa yako wenye hawako Mashahidi, fikiria mambo fulani yenye unaweza kufanya ili kupunguza matatizo na kuendelea kuwa mushikamanifu.

12. Sababu gani watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi wanaweza kutupinga? Lakini namna gani tunaweza kuonyesha kuwa tunajitia pa nafasi yao?

12 Ujitie pa nafasi ya watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi. Hata kama tunaweza kufurahia sana kweli za Biblia zenye tumejifunza, watu wa jamaa yetu wanaweza kuwaza kuwa tumedanganywa ao tumeingia katika kikundi kidogo cha kidini. Wanaweza kufikiri kuwa hatuwapendi tena kwa sababu hatufanye tena sikukuu pamoja nao. Hata wanaweza kuogopa kuwa tutapatwa na jambo fulani la mubaya wakati tutakufa. Tunapaswa kujitia pa nafasi yao kwa kujaribu kuwaelewa na kuwasikiliza kwa uangalifu ili kujua mambo yenye kuwahangaisha kabisa. (Met. 20:5) Mutume Paulo alijikaza kuelewa “watu wa namna zote” ili awahubirie habari njema; kufanya hivyo kunaweza kutusaidia pia.​—1 Kor. 9:19-23.

13. Namna gani tunapaswa kuzungumuza na watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi?

13 Uzungumuze kwa upole. Biblia inasema hivi: ‘Maneno yenu na yakuwe yenye neema sikuzote.’ (Kol. 4:6) Tunapaswa kuomba Yehova roho yake takatifu ili itusaidie kuonyesha sifa za tunda la roho wakati tuko tunazungumuza na watu wa jamaa yetu. Hatupaswe kubishana juu ya mafundisho yote ya uwongo ya dini yao. Ikiwa maneno ao matendo yao yanatukwaza, tunaweza kuiga mufano wa mitume. Paulo aliandika hivi: “Tunapotukanwa, tunabariki; tunapoteswa, tunavumilia tunapoharibiwa sifa, tunasihi.”​—1 Kor. 4:12, 13.

14. Kuendelea kuwa na mwenendo muzuri kunaleta faida gani?

14 Uendelee kuwa na mwenendo muzuri. Hata kama maneno ya upole yanaweza kusaidia kupambana na upinzani wa watu wa jamaa, mwenendo wetu muzuri unaweza kuwa na matokeo mazuri hata zaidi. (Soma 1 Petro 3:1, 2, 16.) Kupitia mufano wako, usaidie watu wa jamaa yako waone kuwa Mashahidi wa Yehova wako na ndoa zenye furaha, wanahangaikia watoto wao, wako na mwenendo safi, na wako na furaha katika maisha. Hata kama watu wa jamaa yetu hawatafikia kukubali kweli, tunaweza kuwa na furaha kwa sababu tunamupendeza Yehova kwa kubakia waaminifu kwake.

15. Namna gani tunaweza kufikiria mbele ya wakati hali zenye zinaweza kuleta mabishano?

15 Upange mbele ya wakati. Fikiria hali zenye zinaweza kutokeza mabishano, na ufikirie namna ya kutenda. (Met. 12:16, 23) Dada mumoja wa Australia anasema hivi: “Baba-mukwe wangu alikuwa anapinga sana kweli. Mbele ya kumuita ili kujua hali yake, mimi na bwana yangu tulikuwa tunasali ili Yehova atusaidie kujibia kwa upole wakati anazungumuza na sisi kwa hasira. Tulikuwa tunatayarisha habari za kuzungumuzia ili tuendelee kuzungumuza kama marafiki. Ili kuepuka mazungumuzo marefu yenye mara nyingi yangeongoza kwenye mabishano makali juu ya mambo ya dini, tuliweka mipaka juu ya muda wa kuzungumuza naye.”

16. Namna gani unaweza kushinda mawazo ya kujisikia kuwa umekosea watu wa jamaa yako?

16 Kwa kweli, hauwezi kuepuka hali zote za kukosa kuelewana na watu wa jamaa yako wenye hawako Mashahidi. Hali hizo za kukosa kuelewana zinaweza kukufanya ujisikie kuwa uko na makosa, zaidi sana kwa sababu unapenda sana watu wa jamaa yako na umejikaza sikuzote kuwafurahisha. Ikiwa unajisikia hivyo, ujikaze kutia ushikamanifu wako kwa Yehova pa nafasi ya kwanza kuliko upendo wako kwa watu wa familia yako. Musimamo kama huo unaweza kusaidia watu wa jamaa yako waelewe kuwa kutumikia Yehova ni jambo la maana sana. Hata hivyo, ukumbuke kuwa hauwezi kukaza mutu yeyote akubali kweli. Lakini, kupitia mufano wako, uwasaidie waone faida za kutii kanuni za Yehova. Kama vile Mungu wetu mwenye upendo anakupatia nafasi ya kuchagua kumutumikia, anawapatia wao pia nafasi ya kufanya hivyo.​—Isa. 48:17, 18.

WAKATI MUTU WA FAMILIA ANAMUACHA YEHOVA

17, 18. Ni nini inaweza kukusaidia kuvumilia ikiwa mutu wa familia yako anamuacha Yehova?

17 Wakati mutu wa familia anatengwa na kutaniko ao anajitenga yeye mwenyewe, hilo linaweza kuhuzunisha sana. Namna gani tunaweza kupambana na huzuni hiyo?

18 Uendelee kuwa na programu ya muzuri ya mambo ya kiroho. Utie nguvu hali yako ya kiroho kwa kusoma Biblia kwa ukawaida, kutayarisha na kuhuzuria mikutano ya Kikristo, kufanya kazi ya kuhubiri, na kusali ili kuomba Mungu akupatie nguvu ya kuvumilia. (Yuda 20, 21) Utafanya nini ikiwa unajisikia kuwa haufanye hivyo kwa moyo wako wote, na kuwa unaendelea kujisikia tu mubaya? Usichoke! Kuwa na programu ya muzuri ya mambo ya kiroho kunaweza kukusaidia kuzuia mawazo yako. Fikiria mambo yenye yalimufikia muandikaji wa Zaburi ya 73. Wakati fulani alikuwa na mawazo ya mubaya na yalimuhangaisha sana, lakini aliweza kubadilisha mawazo yake wakati aliingia mahali pa kufanyia ibada ya Mungu. (Zab. 73:16, 17) Kumutumikia Yehova kwa uaminifu kunaweza pia kukusaidia kufanya hivyo.

19. Namna gani unaweza kuonyesha kuwa unaheshimia mupango wa Yehova wa kutoa nizamu?

19 Uheshimie nizamu ya Yehova. Mupango huo unaweza kuleta matokea ya muzuri sana na ya muda murefu kwa wote, na kwa mutenda-zambi pia, hata kama unahuzunisha kwanza. (Soma Waebrania 12:11.) Kwa mufano, Yehova anatuamuru ‘tuache kuchangamana [kushirikiana]’ na watenda zambi wenye hawatubu. (1 Kor. 5:11-13) Hata kama tuko na huzuni nyingi katika moyo, tunapaswa kuepuka kuzungumuza kwa ukawaida na mutu wa familia mwenye ametengwa na kutaniko, iwe kupitia telefone, ujumbe kwenye telefone, barua, ao kupitia Internete.

20. Tunaweza kuendelea kuwa na tumaini gani?

20 Uendelee kuwa na tumaini. Upendo ‘unatumaini mambo yote,’ kwa hiyo, tunaweza kuendelea kutumainia kuwa wale wenye wamemuacha Yehova watamurudilia. (1 Kor. 13:7) Ikiwa unaona mambo yenye kuonyesha kuwa moyo wa mutu wa familia yako unaanza kubadilika, unaweza kusali kwa ajili yake ili apate nguvu kupitia Maandiko na akubali mualiko huu wa Yehova: “Rudi kwangu.”​—Isa. 44:22.

21. Unapaswa kufanya nini ikiwa watu wa familia yako wanakupinga kwa sababu unamufuata Yesu?

21 Yesu alisema kuwa ikiwa tunapenda sana mwanadamu yeyote kuliko yeye, hatustahili kuwa wanafunzi wake. Lakini, alikuwa hakika kuwa wanafunzi wake wangekuwa na ujasiri wa kuendelea kuwa washikamanifu kwake hata kama watu wa familia zao wanawapinga. Ikiwa kumufuata Yesu kumeleta “upanga” katika familia yako, umutegemee Yehova ili akusaidie kupambana muzuri na magumu hayo. (Isa. 41:10, 13) Upate basi furaha kwa kujua kwamba Yehova na Yesu wanapendezwa na wewe na kwamba watabariki uaminifu wako.

^ fu. 10 Ili kupata maelezo mengine juu ya namna ya kufundisha watoto katika familia ambamo bibi ao bwana haiko Shahidi, ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi, wa tarehe 15 Mwezi wa 8, 2002.