Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maono ya Zekaria​—Yanakuhusu Namna Gani?

Maono ya Zekaria​—Yanakuhusu Namna Gani?

‘Murudi kwangu, . . . nami nitarudi kwenu.’​—ZEK. 1:3.

NYIMBO: 120, 117

1-3. (a) Watu wa Yehova walikuwa katika hali gani wakati Zekaria alianza kutoa unabii? (b) Sababu gani Yehova aliomba watu wake ‘wamurudilie’?

KITABU cha kukunjwa chenye kuruka, mwanamuke mwenye kufungwa katika chombo fulani chenye kufanana na kitunga, na wanawake wenye kuruka katika anga wenye kuwa na mabawa kama ya ndege fulani mwenye kuitwa korongo; picha hizo zenye kushangaza zinazungumuziwa katika kitabu cha Zekaria. (Zek. 5:1, 7-9) Sababu gani Yehova alimutolea nabii wake maono hayo yenye kushangaza? Waisraeli walikuwa katika hali gani wakati huo? Namna gani habari ya Zekaria juu ya maono hayo inatuhusu leo?

2 Mwaka wa 537 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, ulikuwa mwaka wa furaha kwa watu wa Yehova wenye kujitoa kwake. Kisha kufanya miaka 70 katika uhamisho, waliachiliwa kutoka katika Babiloni. Mwanzoni, walianza kufanya kazi ya kurudisha ibada ya kweli katika Yerusalemu kwa furaha sana. Katika mwaka wa 536, musingi wa hekalu uliwekwa. Wakati huo watu walikuwa ‘wanapaaza sauti kubwa, na sauti hiyo ikasikiwa hata mbali sana.’ (Ezra 3:10-13) Lakini, bila kukawia kazi yao ya kujenga ikaanza kupingwa. Watu walivunjika moyo kwa sababu ya magumu na matatizo mengi; kwa hiyo, waliacha kujenga hekalu na wakaanza kuhangaikia nyumba zao wenyewe na kulima mashamba yao. Miaka kumi na sita kisha kuwekwa kwa musingi, kazi ya kujenga hekalu la Yehova ilikuwa imesimama. Watu wa Mungu walipaswa kukumbushwa kuwa walipaswa kumurudilia Yehova na kuacha kutia mambo yao ya pekee pa nafasi ya kwanza. Yehova alipenda wamuabudu tena bila kuogopa, na kwa moyo wao wote.

3 Ili kusaidia watu wake wakumbuke sababu kubwa yenye ilifanya wakombolewe kutoka katika Babiloni, Mungu alituma nabii Zekaria katika mwaka wa 520, mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Jina Zekaria lenye kumaanisha “Yehova amekumbuka,” lingewafanya wakumbuke kweli fulani ya maana. Hata kama walikuwa wamesahau matendo ya wokovu ya Yehova, Mungu alikuwa angali anawakumbuka. (Soma Zekaria 1:3, 4.) Kwa upendo, aliwahakikishia kuwa atawasaidia kurudisha ibada safi, lakini aliwaonya pia kabisa kama hatakubali ibada yenye haitolewe kwa moyo wote. Tuone basi namna Yehova aliwachochea kutenda kupitia maono ya sita na ya saba ya Zekaria. Pia, maono hayo yanaweza kutufundisha nini leo?

HUKUMU YA MUNGU JUU YA WALE WENYE KUIBA

4. Zekaria aliona nini katika maono yake ya sita, na sababu gani kitabu cha kukunjwa kilikuwa kimeandikwa kwenye sehemu zote mbili? (Ona picha ya 1 kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Sura ya 5 ya kitabu cha Zekaria inaanza na maono yenye kushangaza. (Soma Zekaria 5:1, 2.) Zekaria anaona kitabu cha kukunjwa chenye kuruka katika anga, chenye kuwa na urefu wa karibu metre 9 na upana wa karibu metre 4 na nusu! Kimefunguliwa, na kiko tayari kusomwa. Kiko na ujumbe wa hukumu, wenye kujaza sehemu zote mbili za kitabu hicho cha kukunjwa. (Zek. 5:3) Kwa kawaida, kitabu cha kukunjwa kiliandikwa kwenye sehemu moja tu, kwa hiyo, ni wazi kuwa kitabu hicho cha kukunjwa kiko na ujumbe muzito na wa maana sana.

Wakristo wanapaswa kuepuka aina yoyote ya wizi (Picha hii inapatana na fungu la 5-7)

5, 6. Namna gani Yehova anaona aina yoyote ya wizi?

5 Soma Zekaria 5:3, 4. Watu wote watatoa hesabu mbele za Yehova, lakini zaidi sana watu wenye kubeba jina lake. Wale wenye kumupenda Yehova wanajua kuwa aina yoyote ya wizi ‘inashambulia [inachafua] jina la Mungu [wao].’ (Met. 30:8, 9) Watu fulani wanaweza kufikiri kuwa haiko mubaya kuiba ikiwa wako na sababu ya muzuri ya kufanya hivyo, lakini mwizi anatia pa nafasi ya kwanza tamaa yake ya pupa kuliko Mungu, na anaona vitu vya kimwili kuwa vya maana zaidi. Anazarau sheria ya Mungu, anazarau Yehova na jina lake na kuona kuwa jina hilo halina maana yoyote.

6 Uliona kuwa Zekaria 5:3, 4 inaonyesha kuwa ‘laana . . . ingeingia katika nyumba ya mwizi . . . nayo ingekaa katikati ya nyumba yake na kuiangamiza’? Hakuna kitu chenye kinaweza kumuzuia Yehova kutimiza hukumu yake. Yehova anaweza kufunua na kuhukumu matendo yoyote ya mubaya kati ya watu wake. Hata kama mutu anaweza kuficha wizi wake kwa wenye mamlaka, wafanyakazi, wazee, ao wazazi, hawezi kuuficha kwa Mungu mwenye anatuhakikishia kuwa kila aina ya wizi utafunuliwa. (Ebr. 4:13) Ni jambo lenye kufurahisha sana kuwa pamoja na watu wenye wanajikaza sikuzote kuwa waaminifu “katika mambo yote”!​—Ebr. 13:18.

7. Namna gani tunaweza kuepuka laana yenye kuwa katika kitabu cha kukunjwa chenye kuruka katika anga?

7 Yehova anachukia aina zote za wizi. Tunaona kuwa ni pendeleo kuishi kulingana na kanuni za juu za mwenendo za Yehova, kwa kuendelea kuwa na mwenendo wenye hauchafue jina lake katika njia yoyote. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuepuka hukumu ya Yehova juu ya wale wenye wanavunja sheria yake kwa makusudi.

TUTIMIZE NENO LETU “SIKU BAADA YA SIKU”

8-10. (a) Kiapo ni nini? (b) Mufalme Sedekia alishindwa kutimiza kiapo gani?

8 Ujumbe wenye kuandikwa kwenye kitabu hicho cha kukunjwa unaonya pia wale wenye ‘kufanya kiapo katika jina la Mungu kwa uwongo.’ (Zek. 5:4) Kiapo ni maneno yenye mutu anasema ili kuhakikisha kuwa jambo fulani ni kweli ao ahadi ya pekee yenye anatoa ili kusema kuwa atafanya ao hatafanya jambo fulani.

9 Ni jambo nzito sana kufanya kiapo katika jina la Yehova. Mufalme wa mwisho katika Yerusalemu alifanya hivyo. Sedekia aliapa kwa jina la Yehova kwamba ataendelea kuwa mutumishi mushikamanifu wa mufalme wa Babiloni. Lakini, Sedekia hakutimiza kiapo chake. Kwa hiyo, Yehova alisema maneno haya ya hukumu juu yake: ‘Kama ninavyoishi, . . . mahali pa mufalme aliyemuweka kuwa mufalme yule aliyekizarau kiapo chake na ambaye alilivunja agano lake, [Sedekia] atakufa pamoja naye katikati ya Babiloni.’​—Eze. 17:16.

10 Mufalme Sedekia alikuwa ameapa kwa jina la Mungu, kwa hiyo, Yehova alitazamia kuwa alipaswa kutimiza kiapo chake. (2 Nya. 36:13) Lakini, Sedekia alitafuta musaada kwa Misri ili kujaribu kutoka chini ya utawala wa Wababiloni, hata hivyo Misri haikuweza kumusaidia.​—Eze. 17:11-15, 17, 18.

11, 12. (a) Ni naziri gani yenye kuwa ya maana zaidi? (b) Namna gani naziri yetu ya kujitoa kwa Mungu inahusu maisha yetu ya kila siku?

11 Yehova anasikiliza pia ahadi zenye tunatoa. Anachukua kwa uzito naziri zetu, na tunapaswa kuzitimiza ili tukubaliwe naye. (Zab. 76:11) Kati ya ahadi zote zenye tunatoa, ahadi ya maana zaidi ni ile yenye tunatoa wakati tunajitoa kwa Yehova. Kujitoa kwa Mungu ni naziri nzito ya kumutumikia Yehova katika maisha yetu yote hata kutokee nini.

12 Namna gani tunaweza kuonyesha kuwa tunatimiza naziri yetu ya kujitoa kwa Mungu? Namna tunatenda wakati wa majaribu makubwa ao madogo inapaswa kuonyesha kwamba tunachukua kwa uzito ahadi yetu ya kumusifu Yehova “siku baada ya siku.” (Zab. 61:8) Kwa mufano wakati mutu fulani kwenye kazi ao kwenye masomo anatutongoza, tunaona jambo hilo kuwa nafasi ya ‘kupendezwa na njia [za Yehova]’ kwa kukataa kishawishi hicho? (Met. 23:26) Ikiwa watu wa familia yetu hawako Mashahidi, tunamuomba Yehova atusaidie kuendelea kuonyesha sifa za Kikristo hata kama pembeni yetu hakuna mutu mwengine mwenye kujikaza kufanya hivyo? Tunasali kila siku kwa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo na kumushukuru kwa kutupatia pendeleo la kuwa kati ya watu wake na kwa upendo wake? Tunajikaza kuwa na wakati wa kusoma Biblia kila siku? Kwa njia fulani, tuliahidi kuwa tutafanya mambo hayo. Sivyo? Tunaonyesha utii wakati tunafanya mambo hayo. Kufanya ibada yetu kwa bidii kunaonyesha kuwa tunamupenda Yehova na tumejitoa kabisa kwake. Ibada yetu kwa Yehova ni sehemu ya maisha yetu, haiko ya desturi tu. Kutimiza ahadi yetu ni kwa faida yetu wenyewe; uaminifu wetu utatusaidia kuwa na maisha ya muzuri wakati unaokuja.​—Kum. 10:12, 13.

13. Maono ya sita ya Zekaria yanatufundisha nini?

13 Maono ya sita ya Zekaria yametusaidia kuona kama wale wenye kumupenda Yehova wanapaswa kuepuka aina yoyote ya wizi na viapo vya uwongo. Tumeona pia kuwa hata kama Waisraeli walifanya makosa mengi, Yehova hakuwaacha. Alielewa magumu yenye walipambana nayo kwa sababu walikuwa wamezungukwa na maadui. Anatuwekea mufano kwa kutimiza ahadi zake, na atatusaidia tutimize ahadi zetu. Njia moja yenye anatumia ili kutusaidia ni kwa kututolea tumaini kuwa karibuni atamaliza uovu wote katika dunia yote. Maono yenye kufuata ya Zekaria yanahakikisha tumaini hilo la muzuri.

UOVU ‘UNAWEKWA MAHALI PENYE UNAPASWA KUWA’

14, 15. (a) Zekaria anaona nini katika maono ya saba? (Ona picha ya 2 kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Mwanamuke mwenye kuwa ndani ya chombo hicho anafananisha nini? Sababu gani malaika anafunika chombo hicho?

14 Kisha kuona kitabu cha kukunjwa chenye kuruka katika anga, malaika anaambia Zekaria hivi: “Inua macho yako.” Maono yake ya saba yatafunua nini? Sasa, anaona chombo cha kupimia chenye kuitwa “efa” kinatokea. (Soma Zekaria 5:5-8.) Chombo hicho chenye kufanana na kitunga cha ukubwa wa kadiri, kiko na kifuniko cha muviringo chenye kutengenezwa na majiwe fulani ya bei yenye kuitwa risasi. Wakati kifuniko kinaondolewa, Zekaria anaona ‘mwanamuke fulani amekaa ndani.’ Malaika anasema kuwa mwanamuke mwenye kuwa ndani ya chombo hicho ni “Uovu.” Wazia namna Zekaria aliogopa wakati aliona mwanamuke huyo anajaribu kutoka katika chombo hicho! Lakini, mara moja malaika anamurudisha ndani na kufunika chombo hicho kwa kifuniko chake chenye kuwa na uzito. Hilo linamaanisha nini?

15 Sehemu hiyo ya maono inaonyesha kuwa Yehova hataruhusu uovu wa aina yoyote kati ya watu wake. Atahakikisha kuwa unawekwa katika chombo na kuondolewa haraka. (1 Kor. 5:13) Malaika anatuhakikishia jambo hilo kwa kurudisha tena kifuniko juu ya chombo hicho.

Yehova ameahidi kufanya ibada yake iendelee kuwa safi (Picha hii inapatana na fungu la 16-18)

16. (a) Chombo hicho kinafanywa nini? (Ona picha ya 3 kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Wanawake wenye kuwa na mabawa wanapeleka wapi chombo hicho?

16 Kisha kunatokea wanawake wawili wenye kuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. (Soma Zekaria 5:9-11.) Wanawake hao wako tofauti kabisa na mwanamuke mwenye kuwa katika chombo hicho! Wanawake hao wanatumia mabawa yao ili kushuka na kuchukua chombo hicho chenye kuwa na “Uovu.” Wanamupeleka wapi? Uovu unapelekwa katika ‘inchi ya Shinari,’ ni kusema, Babiloni. Sababu gani walipeleka chombo hicho katika Babiloni?

17, 18. (a) Sababu gani Shinari ni mahali penye “Uovu” unapaswa kuwa? (b) Tunapaswa kuazimia kufanya nini juu ya uovu?

17 Kwa Waisraeli wa siku za Zekaria, Shinari ilikuwa mahali penye kufaa pa kuweka uovu. Zekaria na Wayahudi wenzake wangeweza kuhakikisha kuwa Babiloni ilikuwa nafasi ya uovu katika siku zao. Walikuwa wamekomalia katika muji huo wenye kujaa uchafu na ibada ya sanamu, walipaswa kujikaza sana kila siku ili kupinga roho ya ulimwengu huo wa wapagani. Maono hayo yalipaswa kuwatuliza sana, na kuwahakikishia kuwa Yehova angefanya ibada yake iendelee kuwa safi!

18 Lakini, maono hayo yalikumbusha pia Wayahudi daraka lao la kuendelea kulinda safi ibada yao kwa Yehova. Uovu hauwezi na hautaruhusiwa kuingia kwa uficho ao kukaa kati ya watu wa Yehova. Kisha kuingia katika tengenezo safi la Mungu lenye upendo na lenye kutoa ulinzi, tuko na daraka la kuendelea kulinda usafi huo. Tunachochewa kuendelea kufanya tengenezo hilo likuwe safi? Uovu wa aina yoyote haupaswe kupatikana katika paradiso yetu ya kiroho.

WATU SAFI WANAMULETEA YEHOVA HESHIMA

19. Maono ya Zekaria yenye kushangaza sana yanatufundisha nini leo?

19 Maono ya sita na ya saba ya Zekaria ni onyo kubwa kwa wale wenye wanaendelea kufanya matendo ya udanganyifu, yanatukumbusha kuwa Yehova hataachilia watu wenye kufanya mambo ya mubaya. Watumishi wake wenye kumuabudu kwa moyo wote wanapaswa kuchukia kabisa mambo maovu. Maono hayo yanatuhakikishia pia kuwa ikiwa tunafanya yetu yote ili tukubaliwe na Mungu na kupata ulinzi wake, hatutapatwa na laana ya kifo. Lakini, Yehova atatubariki kabisa. Bidii yetu yenye tunafanya ili tuendelee kuwa safi katika ulimwengu wenye kujaa uovu italeta matokeo ya muzuri. Tunaweza kuwa hakika kwamba tunaweza kupata ushindi kwa musaada wa Yehova! Lakini namna gani tunaweza kuwa hakika kuwa ibada ya Yehova itaendelea kuwa safi katika ulimwengu huu wenye kujaa mambo ya mubaya? Nini inatuhakikishia kuwa Yehova atalinda tengenezo lake kadiri ziki kubwa inakaribia? Tutajibia maulizo hayo katika habari yenye kufuata.