Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Taji na Magari ya Kukokotwa Vinawalinda

Taji na Magari ya Kukokotwa Vinawalinda

‘Nayo yatatukia​—bila shaka ikiwa mutaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.’​—ZEK. 6:15.

NYIMBO: 17, 136

1, 2. Kwenye mwisho wa maono ya saba ya Zekaria, hali ya Wayahudi ilikuwa namna gani katika Yerusalemu?

WAKATI maono ya saba ya Zekaria yanaisha, nabii anakuwa na mambo mengi ya kufikiria. Yehova alikuwa amehakikisha kuwa atahukumu watu wenye kutenda kwa udanganyifu kwa sababu ya matendo yao ya mubaya. Kwa kweli, ahadi hiyo ilimutia nguvu Zekaria. Lakini, mambo yalikuwa hayajabadilika kabisa. Udanganyifu na matendo mengine ya mubaya yalikuwa yangali yanafanywa. Na kazi ya kujenga hekalu la Yehova katika Yerusalemu ilikuwa haijakaribia kumalizika. Sababu gani Wayahudi waliacha haraka sana kazi yao yenye Mungu alikuwa amewapatia? Walirudia Yerusalemu ili kufanya tu maisha yao ikuwe ya muzuri zaidi?

2 Zekaria alijua kuwa wanaume na wanawake wenye walirudia Yerusalemu walikuwa wenye imani. Ni wao ndio ‘Mungu wa kweli aliiamusha roho’ yao ili waache maisha yao ya muzuri na biashara yao. (Ezra 1:2, 3, 5) Waliacha inchi yenye walikuwa wanajua ili wahamie katika inchi yenye wengi kati yao walikuwa hawajaona hata kidogo. Kazi ya kujenga upya hekalu la Yehova ilikuwa jambo la maana, ndiyo sababu Wayahudi hao walifanya safari hiyo yenye magumu ya kilometre 1600 hivi kwa kupitia katika njia yenye milima na majiwe-majiwe.

3, 4. Wayahudi wenye walirudia katika Yerusalemu, walipambana na magumu gani?

3 Wazia safari hiyo ndefu ilikuwa ya namna gani. Wakati Wayahudi walikuwa katika safari hiyo, bila shaka walifikiria kwa saa nyingi makao yao mapya. Walikuwa wamesikia namna muji wa Yerusalemu ulikuwa wenye kupendeza sana zamani. Wale wenye walikuwa na miaka mingi zaidi kati yao, walikuwa wameona utukufu wa hekalu la zamani. (Ezra 3:12) Ikiwa ulisafiri pamoja nao, ungejisikia namna gani wakati ungeona kwa mara ya kwanza Yerusalemu, makao yako ya mupya? Ungehuzunika wakati ungeona majengo yenye kubomoka yenye kuzungukwa na majani? Ungelinganisha kuta mbili kubwa zenye nguvu za Babiloni na kuta za Yerusalemu zenye kubomoka, zenye kuwa na tundu kubwa-kubwa mahali kwenye milango na minara ya walinzi ilikuwa hapo zamani? Lakini, watu hawakuvunjika moyo. Walikuwa wameona mukono wa Yehova wenye kuokoa katika safari yao ndefu ya kurudia nyumbani. Kisha tu kufika, jambo la kwanza lenye walifanya lilikuwa kujenga mazabahu mahali penye hekalu la zamani lilikuwa, na wakaanza kumutolea Yehova zabihu kila siku. (Ezra 3:1, 2) Mwanzoni walikuwa na furaha sana, na ilionekana kuwa hakuna kitu chenye kingeweza kuwavunja moyo.

4 Zaidi ya kujenga upya hekalu, Waisraeli walipaswa kujenga upya miji yao. Walipaswa kutengeneza nyumba zao, kulima mashamba, na kukulisha watu wa familia zao. (Ezra 2:70) Kazi yenye walikuwa nayo ilionekana kuwa ya mingi sana. Kisha, bila kukawia kukatokea upinzani mukubwa. Hata kama mwanzoni walitenda bila kuogopa, upinzani wenye ulifanya miaka 15 uliwavunja moyo. (Ezra 4:1-4) Habari ya mubaya zaidi ilitokea katika mwaka wa 522 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati mufalme wa Perse alikataza kazi ya kujenga katika Yerusalemu. Ilionekana kuwa muji huo hautajengwa tena.​—Ezra 4:21-24.

5. Namna gani Yehova aliwasaidia watu wake?

5 Yehova alijua jambo lenye watu wake walikuwa nalo lazima. Mungu alipatia Zekaria maono ya mwisho ili kuhakikishia Wayahudi kuwa anawapenda na anapendezwa na kazi yenye walikuwa wamekwisha kufanya na kuwahakikishia kuwa atawalinda ikiwa wangeanza tena kufanya kazi yake. Kuhusu kazi ya kujenga upya hekalu, Yehova aliahidi hivi: ‘Nayo yatatukia​—bila shaka ikiwa mutaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.’​—Zek. 6:15.

JESHI LA MALAIKA

6. (a) Maono ya munane ya Zekaria yanaanza namna gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Sababu gani kila farasi iko na rangi yake?

6 Pengine maono ya munane ya Zekaria ndiyo yenye kutia nguvu zaidi imani. (Soma Zekaria 6:1-3.) Wazia mambo yenye Zekaria aliona: “Kutoka katikati ya milima . . . ya shaba,” magari ine ya kukokotwa na farasi inatokea, inawezekana yenye kustahili kwa ajili ya vita. Farasi wenye kukokota magari ni wenye rangi tofauti. Hilo lingesaidia kutofautisha waendeshaji wake. Zekaria aliuliza hivi: “Magari haya ni nini?” (Zek. 6:4) Sisi pia tunapenda kujua kwa sababu maono hayo yanatuhusu kabisa.

Yehova anaendelea kutumia malaika zake ili kulinda na kutia nguvu watu wake

7, 8. (a) Milima hiyo mbili inafananisha nini? (b) Sababu gani milima hiyo ni ya shaba?

7 Katika Biblia, milima inaweza kufananisha ufalme, ao serikali. Milima yenye kutajwa katika maono ya Zekaria inafanana na milima mbili yenye kuzungumuziwa katika unabii wa Danieli. Mulima moja unafananisha utawala wa Yehova wa ulimwengu wote muzima na wa milele. Mulima mwingine unafananisha Ufalme wa Kimasiya wenye kuongozwa na Yesu. (Dan. 2:35, 45) Tangu Yesu awekwe kuwa Mufalme katika mwaka wa 1914, milima hiyo mbili imekuwa na daraka la pekee katika kutimiza mapenzi ya Mungu duniani.

8 Sababu gani milima hiyo ni ya shaba? Kama zahabu, shaba ni majiwe ya bei sana. Yehova alitoa maagizo kuwa majiwe hayo yenye kungaa yatumiwe katika ujenzi wa tabenakulo na kisha katika ujenzi wa hekalu la Yerusalemu. (Kut. 27:1-3; 1 Fal. 7:13-16) Kwa hiyo, inafaa kabisa kusema kuwa milima hiyo mbili ya mufano inatukumbusha uzuri wa utawala wa Yehova wa ulimwengu wote muzima na Ufalme wa Kimasiya, wenye utatolea wanadamu wote usalama na baraka.

9. Waendeshaji wa magari ya kukokotwa na farasi ni nani, na wako na mugawo gani?

9 Tuzungumuzie sasa magari yenye kukokotwa na farasi. Magari hayo na waendeshaji wake wanafananisha nini? Waendeshaji wa magari hayo ya kukokotwa na farasi ni malaika, pengine vikundi fulani vya malaika. (Soma Zekaria 6:5-8.) Wanatoka “mbele za Bwana wa dunia yote” na wako na mugawo fulani wa pekee wa kutimiza. Wamepewa mugawo gani? Magari ya kukokotwa na farasi na waendeshaji wake wanatumwa waende kulinda maeneo fulani ya pekee. Daraka lao ni kulinda watu wa Yehova, zaidi sana ili wasishambuliwe na ‘inchi ya kaskazini,’ ni kusema, Babiloni. Yehova angehakikisha kuwa Babiloni haingefanya tena watu wake wakuwe watumwa. Kwa kweli, hilo lilipaswa kufariji sana wale wenye walikuwa wanajenga hekalu katika siku za Zekaria! Hawangepaswa kuogopa mashambulizi kutoka kwa maadui wao.

10. Maono ya Zekaria juu ya magari ya kukokotwa na farasi na waendeshaji wake, yanahakikishia nini watu wa Mungu leo?

10 Kama wakati wa Zekaria, Yehova anaendelea kutumia malaika zake ili kulinda na kutia nguvu watu wake. (Mal. 3:6; Ebr. 1:7, 14) Tangu wakati Israeli la kiroho lilikombolewa kutoka katika utumwa wa mufano wa Babiloni Mukubwa katika mwaka wa 1919, ibada safi imeendelea kuenea hata kama kumekuwa upinzani mukubwa. (Ufu. 18:4) Kwa sababu malaika wanatulinda, hatupaswe kuogopa kuwa tengenezo la Yehova litaingia tena katika utumwa fulani wa kiroho. (Zab. 34:7) Lakini, tunaweza kuwa hakika kuwa watumishi wa Mungu katika dunia yote wataendelea kuwa na hali ya muzuri ya kiroho. Wakati tunafikiri juu ya maono hayo ya Zekaria, tuko hakika kuwa tuko salama katika ulinzi wa milima hiyo mbili.

11. Sababu gani hatupaswe kuogopa mashambulizi ya wakati unaokuja juu ya watu wa Mungu?

11 Hivi karibuni viongozi wa politike wa ulimwengu wa Shetani wataungana ili kujaribu kuharibu watu wa Mungu. (Eze. 38:2, 10-12; Dan. 11:40, 44, 45; Ufu. 19:19) Unabii wa Ezekieli unaeleza kuwa majeshi hayo yanafunika inchi kama mawingu na yanakuja kutushambulia kwa hasira, na yanakuja kwenye farasi. (Eze. 38:15, 16) * Tunapaswa kuogopa? Hapana kabisa! Tuko na jeshi lenye kuwa upande wetu. Wakati huo wa magumu wakati wa ziki kubwa, majeshi ya malaika wa Yehova yatakuja pamoja ili kulinda watu wa Mungu na kuharibu wale wenye kupinga haki yake ya kutawala. (2 Tes. 1:7, 8) Hiyo itakuwa siku ya furaha kabisa! Lakini ni nani mwenye kuongoza jeshi la Yehova la mbinguni?

YEHOVA ANAVALISHA KUHANI TAJI ILI AKUWE MUFALME

12, 13. (a) Zekaria anaambiwa afanye nini? (b) Namna gani tunajua kuwa mwanaume mwenye kuitwa Chipukizi anafananisha Yesu Kristo? Eleza.

12 Zekaria alipewa maono munane yenye yeye mwenyewe tu alikuwa anaona. Sasa anashiriki katika tendo la kiunabii ili kutia moyo wale wenye kutengeneza upya hekalu la Mungu. (Soma Zekaria 6:9-12.) Zekaria anaambiwa akusanye feza na zahabu kutoka kwa Heldai, Tobaya, na Yedaya; watu watatu wenye wamefika kutoka Babiloni, na atengeneze “taji la fahari [lenye utukufu]” kwa kutumia michango hiyo. (Zek. 6:11) Je, Zekaria anaambiwa avalishe taji hilo Gavana Zerubabeli wa kabila la Yuda na muzao wa Daudi? Hapana. Watu wenye walikuwa wanaangalia walipaswa kushangaa sana wakati aliweka taji hilo juu ya kichwa cha Kuhani Mukubwa, Yoshua.

13 Kwa sababu Kuhani Mukubwa Yoshua alivalishwa taji, hilo lilimufanya akuwe mufalme? Hapana, Yoshua hakukuwa katika kizazi cha Mufalme Daudi, kwa hiyo, hakustahili kuwa mufalme. Wakati alivalishwa taji, hilo lilikuwa na maana ya kiunabii, lilionyesha kuwa mutu fulani angekuwa kuhani na mufalme milele wakati wenye kuja. Kuhani mukubwa mwenye anafanywa kuwa mufalme anaitwa Chipukizi. Maandiko yanaonyesha waziwazi kuwa Chipukizi huyo ni Yesu Kristo.​—Isa. 11:1; Mt. 2:23.

14. Yesu anafanya kazi gani kwa sababu yeye ni Mufalme na Kuhani Mukubwa?

14 Kwa sababu yeye ni Mufalme na Kuhani Mukubwa, Yesu ni kiongozi wa jeshi la mbinguni la Yehova. Kwa hiyo, anatumika sana ili watu wa Mungu kwa ujumla waishi katika usalama hata kama wanaishi katika ulimwengu huu wenye chuki. (Yer. 23:5, 6) Hivi karibuni, Yesu atapata ushindi juu ya mataifa ili kuunga mukono haki ya Mungu ya kutawala na kulinda watu wa Yehova. (Ufu. 17:12-14; 19:11, 14, 15) Lakini, mbele ya kufanya hukumu hiyo, Chipukizi iko na kazi kubwa ya kufanya.

ATAJENGA HEKALU

15, 16. (a) Ni kazi gani ya kurudisha na kusafisha yenye imefanywa katika siku zetu, na ni nani amefanya kazi hiyo? (b) Hali itakuwa namna gani kwenye mwisho wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu?

15 Zaidi ya kufanywa kuwa Mufalme na Kuhani Mukubwa, Yesu alipewa kazi ya ‘kujenga hekalu la Yehova.’ (Soma Zekaria 6:13.) Katika siku zetu, kazi ya Yesu ya kujenga hekalu imetia ndani kukomboa waabudu wa kweli kutoka katika Babiloni Mukubwa na kurudisha kutaniko la Kikristo katika mwaka wa 1919. Aliweka pia ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ ili aongoze kazi katika viwanja vya duniani vya hekalu kubwa la kiroho. (Mt. 24:45) Yesu pia ameendelea kutumika sana ili kusafisha watu wa Mungu na kuwasaidia wamutolee Yehova ibada safi.​—Mal. 3:1-3.

16 Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu, Yesu na wafalme na makuhani wenzake 144000 watasaidia wanadamu waaminifu wafikie ukamilifu. Wakati watatimiza jambo hilo, waabudu wa kweli tu wa Yehova ndio watakuwa katika dunia yenye itakuwa imesafishwa. Mwishowe, ibada ya kweli itarudishwa kabisa!

USAIDIE KATIKA KAZI YA KUJENGA

17. Yehova alihakikishia tena Wayahudi jambo gani, na ujumbe wake ulikuwa na matokeo gani juu yao?

17 Ujumbe wa Zekaria ulikuwa na matokeo gani juu ya Wayahudi wa siku zake? Yehova alikuwa amewahakikishia kuwa atawasaidia wafanye kazi kwa usalama na kuwalinda. Kwa sababu aliwahakikishia kuwa hekalu lingejengwa, hilo lilipaswa kuwapatia tena tumaini. Lakini, namna gani hesabu kidogo ya watu ingeweza kutimiza kazi hiyo kubwa sana? Maneno yenye Zekaria alisema kisha hapo, yaliondoa woga na mashaka yote. Zaidi ya kutegemezwa na watu waaminifu kama vile Heldai, Tobaya, na Yedaya, Mungu alisema kuwa watu wengine wengi ‘wangekuja na kujenga katika hekalu la Yehova.’ (Soma Zekaria 6:15.) Kwa sababu walikuwa hakika kuwa Mungu atawasaidia, mara moja Wayahudi walitenda na kuanza tena kazi yao ya kujenga hata kama ilikuwa imekatazwa. Bila kukawia Yehova aliondoa kizuizi chenye kuwa kama mulima, ni kusema, kizuizi cha mufalme wa Perse, na hekalu likamalizika kujengwa katika mwaka wa 515 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. (Ezra 6: 22; Zek. 4: 6, 7) Lakini maneno ya Yehova yanazungumuzia mambo makubwa zaidi yenye kutendeka katika siku zetu.

Yehova hawezi kusahau hata kidogo upendo wenye tunamuonyesha! (Picha hizi zinapatana na fungu la 18, 19)

18. Namna gani andiko la Zekaria 6:15 linaendelea kutimia leo?

18 Leo mamilioni ya watu wanaingia katika ibada safi, na moyo wao unawachochea kuchangia ‘vitu vyao vyenye samani,’ ni kusema, wakati wao, nguvu yao, na mali yao ili kutegemeza hekalu kubwa la kiroho la Yehova. (Met. 3:9) Namna gani tunaweza kuwa hakika kuwa Yehova anapendezwa na mambo yenye tunafanya ili kutegemeza kwa ushikamanifu ibada yake? Ukumbuke kuwa Heldai, Tobaya, na Yedaya walileta vyombo kwa ajili ya taji lenye Zekaria alifanya. Taji hilo lilitumiwa kama “ukumbusho,” wa muchango wao kwa ajili ya ibada ya kweli. (Zek. 6:14) Vilevile, Yehova hawezi kusahau hata kidogo kazi yetu na upendo wetu kwake. (Ebr. 6:10) Yehova atavikumbuka milele.

19. Maono ya Zekaria yanapaswa kuwa na matokeo gani juu yetu leo?

19 Mambo yote yenye yametimizwa kwa ajili ya ibada safi katika siku hizi za mwisho ni ushuhuda wenye kuonyesha baraka za Yehova na uongozi wa Kristo. Tuko katika tengenezo lenye kuwa imara, salama, na la milele. Kusudi la Yehova juu ya ibada safi ‘litatukia’ ao litatimia. Upendezwe na nafasi yako kati ya watu wa Yehova, na ‘kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako.’ Kwa kufanya hivyo, unaweza kubakia katika ulinzi wa Mufalme wetu na Kuhani Mukubwa na waendeshaji wa mbinguni wa magari ya kukokotwa na farasi. Utegemeze ibada ya kweli kwa moyo wako wote. Wakati unafanya hivyo, unaweza kuwa hakika kuwa Yehova wa majeshi atakulinda katika wakati wenye kubakia wa siku hizi za mwisho, na kwa umilele wote!

^ fu. 11 Ili kupata habari zaidi, ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 5, 2015, uku. 29-30.