Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ninajua Atafufuka”

“Ninajua Atafufuka”

Rafiki yetu anapumuzika, lakini ninafunga safari kuenda huko ili kumuamusha kutoka usingizini.’​YOH. 11:11.

NYIMBO: 142129

1. Martha alikuwa hakika juu ya jambo gani kuhusu ndugu yake? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

MARTHA, rafiki wa sana wa Yesu na mwanafunzi wake, alikuwa na huzuni sana. Ndugu yake Lazaro alikuwa amekufa. Kuko jambo fulani lenye lingepunguza huzuni yake? Ndiyo. Yesu alimuhakikishia hivi: “Ndugu yako atafufuka.” Pengine hilo halikumaliza huzuni yake yote; lakini, Martha aliamini maneno ya Yesu. Alisema hivi: “Ninajua atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” (Yoh. 11:20-24) Alikuwa hakika kuwa hilo lingetokea wakati wenye kuja. Kisha Yesu akafanya muujiza. Akamufufua Lazaro siku ileile.

2. Sababu gani unapenda kuwa na uhakika kama Martha?

2 Hatuna sababu ya kuamini kuwa Yesu ao Baba yake watafanya muujiza kama huo kwa ajili yetu leo. Lakini, kama Martha, uko hakika kwamba mupendwa wako atafufuliwa wakati wenye kuja? Pengine ni bwana ao bibi yako, ao mama yako, baba yako, ao ni tate (nkambo) yako mupendwa ndiye amekufa. Ao uko na huzuni kwa sababu mutoto wako amekufa. Unatamani sana kukumbatia, kuzungumuza, na kucheka pamoja na mupendwa wako. Jambo la kufurahisha ni kwamba, kama Martha, uko na sababu ya muzuri ya kusema hivi: ‘Ninajua kuwa mupendwa wangu atafufuka.’ Lakini ni muzuri kila Mukristo afikirie sababu gani iko hakika juu ya jambo hilo.

3, 4. Namna gani pengine imani ya Martha ilitiwa nguvu na mambo yenye Yesu alikuwa amefanya?

3 Inawezekana kuwa Martha mwenye alikuwa anaishi karibu na Yerusalemu, hakuona namna Yesu anafufua mutoto wa mujane mumoja karibu na muji wa Naini katika Galilaya. Lakini, pengine alisikia habari juu ya ufufuo huo. Na inawezekana pia alisikia habari juu ya namna Yesu alifufua mutoto mwanamuke wa Yairo. Watu wenye walikuwa katika nyumba yao “walijua [kama] alikuwa amekufa.” Lakini, Yesu alichukua mukono wa mutoto huyo mwenye alikuwa amekufa na kusema hivi: ‘Musichana, inuka!’ Na akaamuka mara moja. (Lu. 7:11-17; 8:41, 42, 49-55) Martha na dada yake Maria, walikuwa wanajua kama Yesu alikuwa na uwezo wa kuponyesha wagonjwa. Ndiyo sababu, waliwaza kwamba ikiwa Yesu angekuwa hapo, Lazaro hangekufa. Sasa kwa sababu rafiki mupendwa wa Yesu alikuwa amekufa, Martha alikuwa na tumaini gani? Ona kwamba Martha alisema kuwa Lazaro atafufuka wakati wenye kuja, katika “siku ya mwisho.” Sababu gani alikuwa hakika juu ya jambo hilo? Na sababu gani unaweza kuwa hakika kuwa kutakuwa ufufuo wakati wenye kuja na pengine wapendwa wako watafufuliwa pia?

4 Uko na sababu za muzuri za kuwa na uhakika huo. Wakati tutakuwa tunazungumuzia sababu fulani, unaweza kuvumbua katika Neno la Mungu mambo yenye hauzoee kufikiria juu ya ufufuo na yatatia nguvu tumaini lako la kuona tena mupendwa wako.

MATUKIO YENYE KULETA TUMAINI!

5. Sababu gani Martha alikuwa hakika kuwa Lazaro atafufuliwa?

5 Ona kwamba Martha hakusema: ‘Ninatumaini kuwa ndugu yangu atafufuka.’ Alisema hivi: “Ninajua atafufuka.” Martha alikuwa hakika kwa sababu ya miujiza yenye pengine alikuwa amejifunza hata mbele Yesu aanze kazi yake ya kuhubiri. Alikuwa amejifunza juu ya miujiza hiyo nyumbani kwao na kwenye sinagogi wakati alikuwa kijana. Pengine unafikiria habari tatu zenye kuwa katika Maandiko.

6. Martha alikuwa amejifunza juu ya muujiza gani?

6 Ufufuo wa kwanza ulifanyika katika kipindi chenye Mungu alikuwa anamupatia nabii wake Eliya nguvu ili afanye miujiza. Katika Sarefathi, muji wa Foinike wenye ulikuwa pembeni ya bahari, mujane masikini alimuonyesha nabii Eliya ukaribishaji-wageni. Kisha kwa muujiza Mungu aliendelea kuongeza unga na mafuta yake, ili yeye na mutoto wake waendelee kuishi. (1 Fal. 17:8-16) Kisha, mutoto wake aligonjwa na akakufa. Eliya alimusaidia mwanamuke huyo. Wakati Eliya aligusa maiti, alisali hivi: ‘Ee Yehova, Mungu wangu, tafazali, irudishe nafsi [uzima] ya mutoto huyu ndani yake.’ Na jambo hilo likatokea! Mungu alisikia sala ya Eliya, na mutoto huyo akafufuka. Huo ndio ulikuwa ufufuo wa kwanza wenye kuzungumuziwa katika Biblia. (Soma 1 Wafalme 17:17-24.) Kwa kweli, Martha alikuwa amejifunza juu ya tukio hilo la ajabu.

7, 8. (a) Elisha alifanya nini ili kumaliza huzuni ya mwanamuke mumoja? Eleza. (b) Muujiza wa Elisha unaonyesha nini juu ya Yehova?

7 Ufufuo wa pili wenye kuzungumuziwa katika Maandiko ulifanywa na nabii Elisha mwenye alichukua nafasi ya nabii Eliya. Mwanamuke mumoja Mwisraeli katika Shunemu mwenye kujulikana sana na mwenye hakukuwa anazaa, alionyesha Elisha ukaribishaji-wageni kwa njia ya pekee. Kupitia nabii Elisha, Mungu alimubariki mwanamuke huyo pamoja na bwana yake mwenye kuzeeka kwa kuwawezesha kuzaa mutoto mwanaume. Kisha kupita miaka fulani, mutoto huyo akakufa. Wazia huzuni nyingi yenye mama huyo alikuwa nayo. Bwana yake alimuruhusu kufanya safari ya kilometre 30 hivi ili kumuona Elisha kwenye Mulima Karmeli. Nabii Elisha alimutuma Gehazi mutumishi wake awatangulie Shunemu. Gehazi hakuweza kufufua mutoto huyo. Kisha mama huyo mwenye alikuwa na huzuni alifika pamoja na Elisha.​—2 Fal. 4:8-31.

8 Wakati alifika katika Shunemu, Elisha alisali karibu na mwili wa mutoto huyo. Kwa muujiza, mutoto huyo akafufuka na mama yake akafurahi sana! (Soma 2 Wafalme 4:32-37.) Pengine alikumbuka maneno yenye Hana mwenye zamani hakukuwa na uwezo wa kuzaa alisema katika sala wakati alileta Samweli ili atumike katika tabenakulo, alisema hivi: ‘Yehova . . . anashusha mupaka katika Kaburi, na Yeye anainua.’ (1 Sam. 2:6) Kwa kweli, kwa kufufua kabisa mutoto huyo katika Shunemu, Mungu alionyesha uwezo wake wa kufufua watu.

9. Ni ufufuo gani wa tatu wenye kuzungumuziwa katika Biblia? Eleza.

9 Jambo lingine la kushangaza lilitokea kisha kifo cha Elisha. Elisha alikuwa nabii kwa miaka zaidi ya 50, na kisha ‘akashikwa na ugonjwa ambao . . . ulimuua.’ Kisha, wakati mwili wa Elisha ulikuwa umebakia mifupa tu, kikundi cha maadui kilikuja katika inchi. Waisraeli fulani walikuwa wanaenda kuzika mwanaume fulani. Kwa sababu walikuwa wanakimbia maadui wao, walitupa mwanaume huyo mwenye kufa katika kaburi ambamo mulikuwa mifupa ya Elisha. Biblia inasema hivi: ‘Mutu yule alipoigusa mifupa ya Elisha, akawa hai [muzima] mara moja na kusimama kwa miguu yake.’ (2 Fal. 13:14, 20, 21) Fikiria namna habari hizo za ufufuo zingeweza kumutia moyo sana Martha! Kwa kweli, Mungu iko na uwezo juu ya kifo. Habari hizo zinapaswa kukufundisha nini? Bila shaka zinapaswa kukusadikisha kuwa Mungu iko na nguvu nyingi sana yenye haina mipaka.

MATUKIO YA WAKATI WA MITUME

10. Petro alifanya nini wakati dada mumoja Mukristo alikufa?

10 Pia, Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, yanazungumuzia ufufuo mbalimbali wenye watumishi wa Mungu walifanya. Yanazungumuzia ufufuo wenye Yesu alifanya wakati alikuwa inje ya muji wa Naini na wakati alikuwa katika nyumba ya Yairo. Mutume Petro alifanya ufufuo mwingine, alimufufua mwanamuke mumoja Mukristo mwenye aliitwa Dorkasi (Tabitha). Petro aliingia mahali penye mwili wake ulikuwa umewekwa, na akasali wakati alikuwa karibu na mwili huo. Kisha akasema hivi: “Tabitha, inuka!” Akafufuka palepale, na Petro akamuweka mbele ya Wakristo wenzake “akiwa hai.” Tukio hilo lilikuwa lenye kusadikisha sana na likafanya ‘wengi wamwamini Bwana.’ Wangeweza kutoa ushahidi juu ya Bwana, na zaidi sana juu ya uwezo wa Yehova wa kufufua wafu.​—Mdo. 9:36-42.

11. Luka alieleza jambo gani lenye lilipata kijana mumoja, na hilo lilikuwa na matokeo gani juu ya wengine?

11 Wengine walijionea ufufuo mwengine. Wakati mumoja Paulo alikuwa katika mukutano fulani katika chumba cha juu katika Troa; sasa ni sehemu ya kaskazini-mangaribi mwa Uturuki. Paulo alizungumuza mupaka katikati ya usiku. Kijana mwanaume mwenye aliitwa Eutiko alikuwa anasikiliza, na alikuwa anakaa kwenye dirisha. Lakini alianza kusinzia na akaanguka chini kutoka kwenye gorofa ya tatu. Pengine munganga Luka ndiye alikuwa wa kwanza kufika mahali penye Eutiko alikuwa na akachunguza hali yake: Eutiko hakuumia tu ao kupoteza akili, lakini alikuwa amekufa! Paulo alishuka chini na akakumbatia mwili huo, na kisha akasema maneno haya yenye kushangaza: “Nafsi yake imo ndani yake.” Hilo lilipaswa kugusa sana mioyo ya watu wenye walijionea jambo hilo! Kwa sababu walijionea namna Paulo anafufua mutu, “wakafarijiwa kupita kiasi.”​—Mdo. 20:7-12.

TUMAINI LENYE KUWA HAKIKA

12, 13. Kulingana na ufufuo mbalimbali wenye tumezungumuzia, tunaweza kujiuliza maulizo gani?

12 Habari zenye tumezungumuzia zinapaswa kukupatia jambo fulani lenye Martha alikuwa nalo. Jambo hilo ni, uhakika kuwa Mungu wetu mwenye alitupatia uzima iko na uwezo wa kufufua watu. Inafurahisha kujua kama watumishi waaminifu wa Mungu, kama vile Eliya, Yesu, ao Petro, kila mumoja wao alikuwa hapo wakati ufufuo ulitendeka, wakati Yehova alikuwa anafanya miujiza. Lakini tunaweza kusema nini juu ya wale wenye walikufa katika vipindi vingine? Ikiwa katika kipindi fulani Mungu hakukuwa anafufua watu, wanaume na wanawake waaminifu wangeweza kutumainia kuwa Mungu atafufua watu wakati wenye kuja? Wangeweza kuwa hakika kama Martha mwenye alisema: “Ninajua [ndugu yangu] atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho”? Sababu gani aliamini jambo hilo, na sababu gani wewe pia unaweza kuamini?

13 Kwa kweli, Neno la Mungu lenye liliongozwa na roho yake, liko na habari mbalimbali zenye kuonyesha kama watumishi washikamanifu wa Yehova walijua kama kutakuwa ufufuo wakati wenye kuja. Tuzungumuzie mifano fulani.

14. Habari juu ya Abrahamu inaweza kutufundisha nini juu ya ufufuo?

14 Fikiria jambo lenye Mungu aliambia Abrahamu afanye juu ya Isaka, muriti mwenye alikuwa amengojea kwa miaka mingi. Yehova alisema hivi: ‘Tafazali, muchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayemupenda sana, Isaka, . . . umutoe kama toleo la kuteketezwa.’ (Mwa. 22:2) Fikiria namna Abrahamu alijisikia kwa sababu ya amri hiyo. Yehova alikuwa ameahidi kuwa kupitia uzao wa Abrahamu mataifa yote yangebarikiwa. (Mwa. 13:14-16; 18:18; Rom. 4:17, 18) Pia, Yehova alisema kuwa baraka hiyo ingekuja “kupitia Isaka.” (Mwa. 21:12) Lakini, jambo hilo lingetimia namna gani ikiwa Abrahamu angemuua Isaka kwa kumutoa kama zabihu? Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kueleza kuwa Abrahamu aliamini kama Mungu angeweza kumufufua Isaka. (Soma Waebrania 11:17-19.) Biblia haiseme kuwa Abrahamu alifikiri kuwa ikiwa anatii, Isaka angefufuliwa kisha saa kidogo, kisha siku moja, ao juma moja. Abrahamu hakujua ni wakati gani mutoto wake angefufuliwa. Lakini, alikuwa na tumaini kuwa Yehova angemufufua Isaka.

15. Ayubu alikuwa na tumaini gani?

15 Ayubu pia alingojea ufufuo wa wakati wenye kuja. Alijua kuwa ikiwa muti unakatwa unaweza kuota tena na kuwa kama mumea mupya. Lakini hilo haliwezi kutendeka kwa mwanadamu. (Ayu. 14:7-12; 19:25-27) Ikiwa mutu anakufa hawezi kujifufua mwenyewe kutoka katika kaburi na kuishi tena. (2 Sam. 12:23; Zab. 89:48) Kwa kweli, hilo halikumaanisha kuwa Mungu hangeweza kufufua mutu. Ayubu aliamini kuwa wakati fulani Yehova angemukumbuka. (Soma Ayubu 14:13-15.) Ayubu hangeweza kujua kabisa-kabisa ni wakati gani. Lakini, aliamini kuwa yule mwenye alianzisha uzima wa mwanadamu angemukumbuka na kumufufua.

16. Namna gani malaika mumoja alimutia Danieli moyo?

16 Mutumishi mwingine muaminifu mwenye kuzungumuziwa katika Maandiko ya Kiebrania ni Danieli. Alimutumikia Mungu kwa ushikamanifu kwa miaka mingi na Yehova alimutegemeza. Wakati fulani, malaika mumoja alimuita Danieli kuwa ‘mutu mwenye kutamanika sana,’ na akamuambia ‘akuwe na amani’ na ‘akuwe na nguvu.’​—Dan. 9:22, 23; 10:11, 18, 19.

17, 18. Danieli alipewa ahadi gani juu ya wakati wenye kuja?

17 Danieli alikuwa na miaka karibu 100 na alikuwa karibu kufa. Na pengine alikuwa anafikiria wakati wake wenye kuja. Danieli angeishi tena? Ndiyo kabisa! Kwenye mwisho wa kitabu cha Danieli, kuko maneno haya yenye Mungu alimuhakikishia: ‘Enda zako kuelekea ule mwisho; nawe utapumuzika.’ (Dan. 12:13) Muzee Danieli alijua kuwa watu wenye kufa wanapumuzika, na hakuna “utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi.” Karibuni, Danieli angeenda humo. (Mhu. 9:10) Lakini hiyo haingekuwa mwisho wake. Alipewa tumaini la wakati wenye kuja.

18 Malaika aliendelea kumuambia Danieli hivi: “Utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.” Hakuambiwa tarehe gani ao kisha muda gani jambo hilo lingetokea. Danieli angekufa na kupumuzika. Lakini, wakati malaika alimuambia Danieli kuwa ‘atasimama kwa ajili ya fungu lake’ wakati wenye kuja, hilo lilionyesha wazi ahadi ya ufufuo wa wakati wenye kuja, muda murefu kisha yeye kufa. Hilo lingetokea “mwishoni mwa zile siku.” Biblia Habari Njema inatafsiri hivi ahadi hiyo yenye Danieli alipewa: “Utasimama na wakati huo utakapotimia utafufuka na kupata tuzo [zawadi] lako.”

Kama Martha, unaweza kuwa na uhakika juu ya ufufuo (Picha hizi zinapatana na fungu la 19, 20)

19, 20. (a) Namna gani mambo yenye tumezungumuzia yanapatana na maneno yenye Martha aliambia Yesu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

19 Kwa kweli, Martha alikuwa na sababu ya kuwa hakika kuwa ndugu yake muaminifu Lazaro, “atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” Ahadi yenye Danieli alipewa na jibu lenye uhakika lenye Martha alijibia Yesu, vinapaswa kupatia Wakristo uhakika leo kuwa kutakuwa ufufuo.

20 Tumeona kama matukio ya kweli kabisa ya zamani yanahakikisha kwamba ufufuo unaweza kufanyika, watu wenye wamekufa wanaweza kuishi tena. Na wanaume na wanawake wenye walimutumikia Mungu walikuwa na tumaini kuwa kutakuwa ufufuo wakati wenye kuja. Lakini, kuko jambo lolote lenye kuonyesha kwamba ufufuo unaweza kufanyika muda murefu kisha kuahidiwa? Ikiwa ni ndiyo, hilo litatupatia sababu ingine ya kuwa na tumaini kama Martha kuwa kutakuwa ufufuo wakati wenye kuja. Lakini, ufufuo utafanyika wakati gani? Tutazungumuzia mambo hayo katika habari yenye kufuata.