Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wazazi​—Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na “Hekima kwa Ajili ya Wokovu”

Wazazi​—Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na “Hekima kwa Ajili ya Wokovu”

‘Tangu utoto muchanga umeyajua maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu.’​—2 TIM. 3:15.

NYIMBO: 141134

1, 2. Sababu gani wazazi fulani wanaweza kuwa na wasiwasi wakati watoto wao wanapenda kujitoa kwa Yehova na kubatizwa?

MAELFU ya wanafunzi wa Biblia wanajitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa. Wengi kati yao ni vijana wenye wamekomalia katika kweli na wenye wamechagua maisha ya muzuri zaidi. (Zab. 1:1-3) Ikiwa uko muzazi Mukristo, kwa kweli, unangojea kwa hamu siku yenye mutoto wako atabatizwa.​—Linganisha na 3 Yohana 4.

2 Lakini, unaweza kuwa na wasiwasi. Pengine umeona vijana fulani wanabatizwa lakini kisha wanakuwa na mashaka juu ya faida ya kuishi kulingana na kanuni za Mungu. Na hata wamoja wameacha kweli. Kwa hiyo, unaweza kuwa na wasiwasi kuwa mutoto wako ataanza kumutumikia Yehova lakini kisha anaacha na kupoteza upendo wenye alikuwa nao mwanzoni juu ya kweli. Anaweza kuwa kama Wakristo wa kwanza-kwanza wa kutaniko la Efeso wenye Yesu aliambia hivi: ‘Mumeacha upendo muliokuwa nao mwanzoni.’ (Ufu. 2:4) Namna gani unaweza kujikaza kuepuka magumu hayo na kusaidia mutoto wako “akue [ao, akomae] kufikia wokovu”? (1 Pet. 2:2) Ili kujibia ulizo hilo, tuzungumuzie mufano wa Timotheo.

“UMEYAJUA MAANDISHI MATAKATIFU”

3. (a) Namna gani Timotheo alifikia kuwa Mukristo, na namna gani alitumikisha mambo yenye alijifunza? (b) Paulo aliandikia Timotheo juu ya mambo gani tatu kuhusu kujifunza?

3 Mutume Paulo alitembelea Listra kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 47 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Inawezekana ni wakati huo ndio Timotheo alijua mafundisho juu ya Ukristo. Hata kama wakati huo inawezekana Timotheo alikuwa angali kijana sana, alikuwa anatumikisha mambo yenye alijifunza. Kisha miaka mbili, akaanza kusafiri pamoja na Paulo. Kisha kupita miaka 16 hivi, Paulo aliandikia Timotheo hivi: ‘Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini, ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza haya na kwamba tangu utoto muchanga umeyajua maandishi matakatifu [Maandiko ya Kiebrania], ambayo yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.’ (2 Tim. 3:14, 15) Ona kwamba Paulo anataja (1) kujua maandishi matakatifu, (2) kushawishiwa kuamini mambo yenye mutu amejifunza na (3) kuwa na hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.

4. Ni vyombo gani vyenye umeona kuwa vyenye faida wakati unafundisha watoto wako wadogo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Kwa sababu wewe ni muzazi Mukristo unapenda mutoto wako ajifunze maandishi matakatifu, yenye yanafanyizwa leo na Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kulingana na uwezo wao, hata watoto wadogo wanaweza kujifunza mambo ya musingi juu ya watu na matukio yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Tengenezo la Yehova limetoa vyombo mbalimbali vyenye wazazi wanaweza kutumia ili kusaidia watoto wao. Unajua vyombo fulani vyenye kupatikana katika luga yenu? Kumbuka kuwa mutoto wako iko na lazima ya kujua mafundisho yenye kuwa katika Biblia ili akuwe na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova.

‘KUSHAWISHIWA KUAMINI’

5. (a) ‘Kushawishiwa kuamini,’ maana yake nini? (b) Tunajua namna gani kuwa Timotheo alishawishiwa kuamini habari njema juu ya Yesu?

5 Ni jambo la lazima kujua maandishi matakatifu. Lakini, haitoshe tu kufundisha watoto juu ya watu na matukio yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Timotheo ‘alishawishiwa kuamini’ pia. Katika Kigiriki, maneno hayo yanamaanisha “kuwa hakika juu ya” ao “kusadikishwa na kukubali kuwa jambo fulani ni kweli.” Timotheo alijua Maandiko ya Kiebrania tangu wakati alikuwa mutoto. Lakini, kisha wakati fulani alisadikishwa na ushuhuda wenye kuonyesha wazi kuwa Yesu alikuwa Masiya. Ao tunaweza kusema kuwa ujuzi wake ulitia nguvu imani yake. Kwa kweli, imani ya Timotheo juu ya habari njema ilikuwa yenye nguvu sana mupaka akafikia kuwa mwanafunzi mwenye kubatizwa na akaanza kutumika pamoja na Paulo katika kazi ya umisionere.

6. Namna gani unaweza kusaidia watoto wako washawishiwe kuamini mambo yenye wanajifunza katika Neno la Mungu?

6 Namna gani unaweza kusaidia watoto wako watie nguvu imani yao ili washawishiwe kuamini kama Timotheo? Kwanza, ukuwe muvumilivu. Inaomba wakati ili mutu akuwe na imani yenye nguvu; na kwa sababu wewe unaamini jambo fulani haimaanishe kuwa mutoto wako pia ataamini jambo hilo. Kila mutoto anapaswa kutumia ‘nguvu zake za kufikiri’ ili kutia nguvu imani yake juu ya kweli ya Biblia. (Soma Waroma 12:1.) Wewe muzazi uko na daraka la maana sana la kumusaidia kufanya hivyo, zaidi sana wakati mutoto wako anauliza maulizo. Tuzungumuzie mufano mumoja.

7, 8. (a) Namna gani baba mumoja Mukristo anaonyesha uvumilivu wakati anafundisha mutoto wake? (b) Namna gani umetambua kuwa ni jambo la maana kuonyesha uvumilivu kama huo?

7 Thomas, baba ya mutoto mwanamuke wa miaka 11 anaeleza hivi: “Wakati fulani mutoto wangu ananiuliza, ‛Inawezekana kuwa Yehova alitumia mageuzi ili kutokeza uzima katika dunia?’ ao, ‛Sababu gani hatujiunge na wengine, kwa mufano, kwa kufanya uchaguzi ili kujaribu kufanya mambo yakuwe muzuri zaidi?’ Wakati fulani ninapaswa kuzuia ulimi wangu ili nisitoe jibu la moja kwa moja. Jambo lenye kusadikisha mutu haiko kweli ya moja kwa moja yenye unamuelezea. Lakini, ni mambo madogo-madogo yenye kusadikisha.”

8 Thomas anajua pia kwamba inaomba kuwa muvumilivu wakati unafundisha. Kwa kweli, uvumilivu ni sifa ya maana kwa Wakristo wote. (Kol. 3:12) Thomas anajua kama inaomba wakati na inaomba kuzungumuza na mutoto wake mara kwa mara. Anapaswa kufikiri naye kupitia maandiko ili aamini kabisa mambo yenye anajifunza. Thomas anasema hivi: “Zaidi sana kuhusu mambo ya maana, mimi na bibi yangu tunapenda kujua ikiwa mutoto wetu anaamini kabisa mambo yenye anajifunza na ikiwa anayaona kuwa yenye kupatana na akili. Ni muzuri ikiwa anauliza maulizo. Kusema kweli, ninaweza kuwa na wasiwasi ikiwa anakubali jambo fulani bila kuuliza maulizo.”

9. Namna gani unaweza kusaidia mutoto wako aamini Neno la Mungu?

9 Ikiwa wazazi wanafundisha watoto wao kwa uvumilivu, pole kwa pole watoto wataanza kuelewa “upana na urefu na kimo na kina” cha imani. (Efe. 3:18) Tunaweza kuwafundisha mambo yenye kupatana na miaka yao na uwezo wao. Kadiri wanaendelea kuwa na imani yenye nguvu juu ya mambo yenye wanajifunza, itakuwa vyepesi zaidi kwao kutetea imani yao mbele ya wengine, kutia ndani wanafunzi wenzao. (1 Pet. 3:15) Kwa mufano, watoto wako wanaweza kufasiria mambo yenye Biblia inasema juu ya hali ya watu wenye kufa? Wanakubali kabisa mafasirio ya Biblia juu ya jambo hilo? * Kwa kweli, unapaswa kuwa muvumilivu ili kusaidia mutoto wako aamini Neno la Mungu, lakini utapata matokeo ya muzuri.​—Kum. 6:6, 7.

10. Kufundisha kunatia ndani jambo gani la maana?

10 Bila shaka mufano wako ni wa maana pia ili kusaidia watoto wako wakuwe na imani yenye nguvu. Stephanie, mama mwenye kuwa na watoto watatu wanawake, anasema hivi: “Tangu wakati watoto wangu walikuwa wadogo, ninajiuliza hivi, ‘Ninaelezea watoto wangu sababu gani niko hakika kuwa Yehova iko, niko hakika juu ya upendo wake, na kuwa kanuni zake ni zenye kuwa sawa? Watoto wangu wanaweza kuona waziwazi kuwa ninamupenda Yehova kabisa?’ Siwezi kutazamia watoto wangu washawishiwe kuamini ikiwa mimi siamini.”

‘KUWA MWENYE HEKIMA KWA AJILI YA WOKOVU’

11, 12. Hekima ni nini, na tunajua namna gani kuwa haitegemee miaka yenye mutu iko nayo?

11 Kama vile tumeona, Timotheo alikuwa (1) na ujuzi wa Maandiko na (2)  alisadiki mambo yenye alijifunza. Lakini Paulo alimaanisha nini wakati alisema kuwa maandishi matakatifu yangemufanya Timotheo akuwe na “hekima kwa ajili ya wokovu”?

12 Kitabu Étude Perspicace des Écritures, Buku la 2, kinafasiria kuwa, katika Biblia, hekima inatia ndani “uwezo wa kutumia muzuri ujuzi na uelewaji ili kumaliza magumu fulani, kuepuka ao kuzuia hatari fulani ao kufikia miradi fulani ao kushauria wengine wafanye hivyo. Ni kinyume cha ujinga.” Biblia inasema kuwa ‘Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa muvulana [ao, mutoto].’ (Met. 22:15) Kwa hiyo, inafaa kusema kuwa hekima, kinyume cha ujinga, inaweza kuwa jambo moja lenye kuonyesha kuwa mutu amekomaa kiroho. Mutu anakuwa mwenye kukomaa kiroho kwa sababu ya kumuogopa Yehova kwa njia yenye kufaa na kuwa tayari kutii amri zake, haiko kwa sababu ya miaka yake.​—Soma Zaburi 111:10.

13. Namna gani kijana anaweza kuonyesha kama iko na hekima kwa ajili ya wokovu?

13 Vijana wenye kukomaa kiroho “hawarushwe huku na huku kama kwa mawimbi na kuchukuliwa huku na huku” na tamaa zao ao na mikazo ya vijana wenzao. (Efe. 4:14) Lakini wanafanya maendeleo ili wakuwe na “nguvu zao za ufahamu [zenye] zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.” (Ebr. 5:14) Wanaonyesha kuwa wanaendelea kukomaa kiroho kwa kukamata maamuzi yenye hekima, hata wakati wazazi wao ao watu wengine wenye kukomaa hawako pamoja nao. (Flp. 2:12) Hekima ya aina hiyo ni ya maana kwa ajili ya wokovu. (Soma Methali 24:14.) Namna gani unaweza kusaidia watoto wako wakuwe na hekima hiyo? Kwanza kabisa, uhakikishe kuwa unaelezea watoto wako kanuni zenye kutegemea Biblia. Kupitia maneno na mufano wako, uwasaidie waone kuwa unaishi kulingana na kanuni zenye kuwa katika Neno la Mungu.​—Rom. 2:21-23.

Sababu gani ni jambo la maana muzazi aendelee kujikaza? (Picha hizi zinapatana na fungu la 14-18)

14, 15. (a) Kijana mwenye anapenda kubatizwa anapaswa kufikiria mambo gani mazito? (b) Namna gani unaweza kusaidia watoto wako wafikiri juu ya baraka za kutii sheria za Mungu?

14 Lakini haitoshe tu kuambia watoto wako mambo yenye kuwa mazuri na yale yenye kuwa mabaya. Ni muzuri pia uwasaidie wafikirie maulizo kama vile: ‘Sababu gani Biblia inakataza mambo yenye yanaweza kuonekana kuwa yenye kufurahisha? Ni nini inanihakikishia kuwa kanuni za Biblia ni zenye kuniletea faida sikuzote?’​—Isa. 48:17, 18.

15 Ikiwa mutoto wako anaonyesha kuwa anapenda kubatizwa, unapaswa kumusaidia kufikiri juu ya jambo lingine; iko na mawazo gani juu ya madaraka yenye mutu anakuwa nayo wakati anakuwa Mukristo. Atapata baraka gani? Atapata magumu gani? Namna gani baraka zenye atapata ni nyingi kuliko magumu? (Mk. 10:29, 30) Hayo ni maulizo yenye yanaweza kutokea kisha kubatizwa. Kwa hiyo, ni jambo la maana kufikiria mambo hayo mbele ya kuchukua uamuzi huo muzito. Ikiwa unasaidia watoto wako kufikiri sana juu ya baraka za kutii na matokeo ya mubaya ya kukosa kutii, hilo linaweza kuwasaidia wakuwe hakika kuwa kanuni za Biblia zitawaletea faida sikuzote.​Kum. 30:19, 20.

WAKATI KIJANA MWENYE KUBATIZWA ANAKUWA NA MASHAKA

16. Wazazi wanapaswa kufikiria nini ikiwa imani ya mutoto mwenye amekwisha kubatizwa inaanza kuwa zaifu?

16 Utafanya nini ikiwa mutoto wako anaanza kuwa na mashaka muda fulani kisha kubatizwa? Kwa mufano, kijana mwenye kubatizwa anaweza kuanza kuvutiwa na vitu vya ulimwengu ao anaweza kuanza kuwa na mashaka juu ya faida ya kuishi kulingana na kanuni za Biblia. (Zab. 73:1-3, 12, 13) Muzazi, ujue kwamba namna unashugulikia mashaka hayo ya mutoto wako inaweza kumusaidia aendelee kumutumikia Yehova ao inaweza kumufanya aache kumutumikia. Ujikaze ili usibishane sana na mutoto wako juu ya jambo hilo, iwe hajafikia miaka ya ujana ao ni kijana. Muradi wako unapaswa kuwa kumuonyesha kuwa unamupenda na kumujulisha kama unapenda kumusaidia.

17, 18. Ikiwa kijana anaanza kuwa na mashaka, namna gani wazazi wanaweza kumusaidia?

17 Kwa kweli, kijana mwenye amebatizwa amejitoa kabisa kwa Yehova. Kujitoa kwa Mungu ni ahadi ya kumupenda na kutia mapenzi yake pa nafasi ya kwanza. (Soma Marko 12:30.) Yehova anachukua ahadi hiyo kwa uzito, na kila mutu mwenye ameitoa anapaswa kuichukua kwa uzito. (Mhu. 5:4, 5) Kwa wakati wenye kufaa na kwa upole, umukumbushe mutoto wako mambo hayo. Lakini, mbele ya kufanya hivyo ujifunze habari mbalimbali zenye tengenezo la Yehova limetoa kwa ajili ya wazazi. Kufanya hivyo kunaweza kutoa sababu za musingi zenye kukazia kwamba kujitoa kwa Yehova ni jambo nzito na baraka zenye anaweza kupata kwa sababu amejitoa kwa Yehova na kubatizwa.

18 Kwa mufano, mashauri mazuri yanaweza kupatikana katika nyongeza yenye kichwa “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza,” kwenye mwisho wa kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1. Inasema hivi: “Usikate kauli kwamba kijana wako ameikataa imani yako. Mara nyingi, huenda kukawa na sababu nyingine.” Inaweza kuwa ni kwa sababu ya mukazo wa vijana wenzake. Pia, pengine ni kwa sababu ya kujisikia kuwa peke yake ao kuona kuwa vijana wengine Wakristo wanafanya maendeleo mazuri zaidi ya kiroho. Nyongeza hiyo inasema tena hivi: “Kumbuka kwamba, mambo kama haya hayahusiane na mafundisho ya imani yako. Kwa sasa, yanahusiana sana na hali zinazofanya iwe vigumu kujizoeza imani.” Kisha nyongeza hiyo inatoa mapendekezo mbalimbali juu ya namna muzazi Mukristo anaweza kusaidia kijana mwenye imani yake inaanza kuwa zaifu.

19. Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wakuwe na “hekima kwa ajili ya wokovu”?

19 Muzazi, uko na daraka kubwa na pendeleo la kukomalisha watoto wako ‘katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4) Kama vile tumeona, haitoshe tu kuwafundisha yale yenye Biblia inasema, lakini pia inaomba kuwasaidia watie nguvu imani yao juu ya mambo yenye wanajifunza. Kwa kweli, wako na lazima ya imani yenye nguvu ili iwachochee wajitoe kwa Yehova na kumutumikia kwa moyo wote. Basi, Neno la Yehova, na roho yake, na bidii yenu nyinyi wazazi visaidie watoto wenu wakuwe na “hekima kwa ajili ya wokovu.”

^ fu. 9 Misaada ya kujifunza yenye kichwa “Biblia Inafundisha Kabisa Nini?” ni vyombo vya muzuri sana kwa ajili ya vijana na watu wazima vya kuwasaidia kuelewa na kufasiria kweli za Biblia. Unaweza kupata misaada hiyo kwenye jw.org katika luga nyingi. Fungua kwenye sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > VYOMBO VYA KUSAIDIA KUJIFUNZA BIBLIA.