Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1 Inasaidia Kuepuka Matatizo

1 Inasaidia Kuepuka Matatizo

Biblia inasema kuwa mashauri yenye inatoa yameongozwa na roho ya Mungu na ni ‘yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.’ (2 Timotheo 3:​16) Ni kweli? Tuone namna hekima ya Biblia imesaidia watu fulani kuepuka matatizo makubwa zaidi ya maisha mbele yawatawale.

KUNYWA POMBE KUPITA KIASI

Delphine, mwenye tulizungumuzia katika habari yenye imepita, aliona kuwa mahangaiko yake yalikuwa yanamusukuma kunywa pombe kupita kiasi. Biblia haikataze kunywa pombe kwa kiasi, lakini inasema hivi: ‘Usikuwe kati ya watu wanaokunywa divai mno [ao, sana].’ (Methali 23:20) Kunywa pombe kupita kiasi kumetokeza matatizo makubwa ya afya, kumevunja na kuharibu uhusiano kati ya watu, na kila mwaka, mamilioni ya watu wanapatwa na kifo cha mbele ya wakati. Watu wanaweza kuepuka mengi kati ya matatizo hayo ikiwa wanafuata mashauri yenye hekima ya Biblia.

Delphine alifanya hivyo. Sasa, anasema hivi: “Nilitambua kama pombe haikukuwa inanisaidia kumaliza mahangaiko yangu. Nilitumikisha mashauri yenye hekima yenye kuwa katika Wafilipi 4:​6, 7, yenye inasema hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali [ao, lakini] . . . maombi yenu na yajulishwe Mungu.’ Kila usiku wakati nilianza kuwaza sana na kuwa na mahangaiko mengi, nilisali kwa Yehova. Nilimuambia namna nilikuwa ninanijisikia, kutia ndani kasirani, huzuni, na hali yangu ya kuvunjika moyo, na nilimulilia ili anisaidie nijue namna gani ninaweza kuwa na mawazo ya muzuri zaidi. Kila asubui, nilihakikisha kuwa nimeachana kabisa na mawazo hayo ya mubaya. Tabia hiyo ya kusali kwa Yehova ilinisaidia nikaze akili yangu juu ya mambo yenye niko nayo kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye sina. Niliamua kuwa sitakunywaka pombe tena. Kwa sababu amani yenye nilipata ilikuwa ya maana sana, sikupenda kuipoteza.”

MWENENDO MUCHAFU

Mwenendo muchafu ni moja kati ya mambo yenye yanaletea mutu huzuni mwingi na magumu. Lakini kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia kuepuka matatizo kama hayo kwa kuzungumuzia mambo fulani makubwa yenye yanaweza kutokeza matatizo hayo; kwa mufano, tabia ya kuchezea mutu kimapenzi na kuangalia pornografia. Mwanaume mumoja mwenye kuitwa Samuel anasema, “Ilikuwa mwepesi sana kuchezea mutu kimapenzi. Wakati fulani sikukuwa ninapendezwa na mutu huyo, lakini ningeweza kuona kuwa alikuwa ananipenda; na hilo lilifanya tuchezeane kimapenzi.” Samuel alitambua kuwa alikuwa anashtakiwa kwamba alikuwa anachezeana kimapenzi mara nyingi; hata wakati hilo halikukuwa katika akili yake. Kwa hiyo, mwishowe aliamua kuchezeana kimapenzi kimakusudi. Lakini tabia hiyo ilimusumbua sana. Sasa anasema hivi: “Ilikuwa tabia ya mubaya, kwa sababu ilinifanya nikomalishe tamaa ya kujipenda mwenyewe.”

Samuel alisoma habari moja yenye kuhusu vijana yenye inapatikana kwenye site ya Internete jw.org. Na alifikiri juu ya andiko la Methali 20:11, lenye linasema hivi: ‘Muvulana [ao, mutoto mwanaume] anajitambulisha kama utendaji wake ni safi na munyoofu [ao, wenye kufaa].’ Namna gani andiko hilo lilimusaidia? Samuel alitambua kuwa tabia yake ya kuchezeana kimapenzi haikukuwa safi wala yenye kufaa. Sasa anasema hivi: “Nilielewa pia kama kijana mwenye anachezeana kimapenzi iko anakomalisha sifa zenye zinaongoza mutu akuwe bwana ao bibi mubaya. Nilianza kufikiria namna bibi mwenye nitaoa atajisikia ikiwa ananiona ninachezea mwanamuke mwingine kimapenzi. Hilo lilinisaidia nitambue kuwa tabia hiyo ni yenye kuumiza. Haiko kwa sababu ni mwepesi kuchezeana kimapenzi ndio inafanya tabia hiyo ikuwe ya muzuri.” Samuel alibadilika. Kuepuka kuchezeana kimapenzi kumemusaidia pia aepuke mwenendo muchafu.

Antonio alikuwa hata katika hatari kubwa ya kuangukia katika mwenendo muchafu: Alipenda sana kuangalia pornografia. Hata kama alikuwa ameoa mwanamuke mwenye alipenda sana, alitambua kama ameanza kutawaliwa na tabia ya kuangalia pornografia tena na tena. Anasema kuwa kufikiri juu ya andiko la 1 Petro 5:8 kulimusaidia kabisa. Andiko hilo linasema hivi: ‘Mutunze akili zenu, mukuwe wenye kulinda [ao, mukuwe macho]. Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kumumeza mutu.’ Antonio anaeleza hivi: “Picha za pornografia ziko kila mahali katika ulimwengu huu, na picha hizo zinaweza kubakia kwa wakati murefu katika akili yetu. Andiko hilo lilinisaidia kabisa nifikiri juu ya ule mwenye anatokeza majaribu hayo ya kuangalia pornografia. Nilipaswa kujifunza kukumbuka haraka kuwa picha hizo chafu zilitoka kwa Shetani. Sasa, ninajua kuwa ni Yehova tu ndiye anaweza kunisaidia ‘nitunze akili yangu na nikuwe mwenye kulinda’ ili niweze kuvuta picha hizo katika akili yangu, moyo wangu, na katika ndoa yangu.” Antonio alipata musaada wenye alikuwa nao lazima, na mwishowe aliachana na tabia yake ya mubaya. Hilo limemusaidia aepuke hata matatizo makali zaidi.

Ni wazi kwamba, Biblia inatoa mashauri yenye kufaa yenye yanaweza kutusaidia tuepuke matatizo makubwa. Lakini tuseme nini juu ya matatizo yenye yamekwisha kututawala na yenye yanaonekana kuwa hayaishe? Tuone basi namna Neno la Mungu linaweza kutusaidia kumaliza matatizo kama hayo.

Muongozo wenye kufaa wenye Biblia inatoa unaweza kutusaidia kuepuka matatizo fulani