Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Una Maoni Gani?

Una Maoni Gani?

Je, Biblia inaweza kukusaidia uwe rafiki ya Mungu?

BAADHI YA WATU WANAAMINI . . .

kwamba hawawezi kuwa rafiki za Mungu kwa sababu wanahisi wao si safi au ni wenye dhambi. Wengine husema kwamba Mungu hatujali. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI

Mungu “ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.” (Methali 3:32) Tukimtii Mungu, tutakuwa rafiki zake.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

  • Mungu anataka kuwa Rafiki yetu.—Yakobo 4:8.

  • Akiwa Rafiki yetu, Mungu yuko tayari kutusaidia na kutusamehe.—Zaburi 86:5.

  • Rafiki za Mungu hupenda mambo anayopenda na kuchukia mambo anayochukia.—Waroma 12:9.