Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajimu na Kutabiri Matukio​—Vinatusaidia Kujua Wakati Wenye Kuja?

Unajimu na Kutabiri Matukio​—Vinatusaidia Kujua Wakati Wenye Kuja?

UNAJIMU

Unajimu ni aina fulani ya uaguzi yenye kutegemea imani ya kuwa nyota, mwezi, na sayari vinachochea sana maisha ya watu katika dunia. Watu wenye kufanya unajimu wanasema kama mupangilio wa vitu hivyo katika anga wakati mutu anazaliwa uko na matokeo juu ya tabia za mutu huyo na wakati wake wenye kuja.

Hata kama unajimu ulianzia katika Babiloni ya zamani, watu wengi leo wangali wanapenda kutumia ufundi huo. Kulingana na uchunguzi wenye ulifanywa mwaka wa 2012 katika États-Unis, mutu mumoja juu ya watu tatu alisema kama ufundi huo wa kutumia nyota ili kutabiri mambo kuhusu maisha ya mutu ulikuwa “aina fulani ya sayansi,” na watu 10 juu ya watu 100 walisema kama ulikuwa “kabisa sayansi.” Je, ni kweli? Hapana. Tuone sababu gani.

  • Sayari na nyota hazina nguvu yoyote yenye inaweza kuchochea maisha ya watu kama vile watu wenye kufanya unajimu wanasema.

  • Mara nyingi wanatabiri mambo kwa ujumla hivi kwamba yanaweza kutumiwa kwa mutu yeyote.

  • Leo, hesabu zenye watu wenye kufanya unajimu wanafanya zinategemea mawazo ya zamani yenye kusema kama sayari zinazunguka dunia. Lakini, ni sayari ndizo zinazunguka jua.

  • Mambo yenye kutabiriwa kwa ajili ya mutu mumoja kwa watu tofauti wenye kufanya unajimu hayapatane.

  • Unajimu unapanga watu kwenye kila moja ya alama 12, ao alama za makundi ya nyota za unajimu, kulingana na tarehe yao ya kuzaliwa. Kwa sababu uhusiano wa dunia na makundi ya nyota umebadilika hatua kwa hatua katika kipindi cha mamia ya miaka, tarehe zenye zilihusiana na alama za makundi ya nyota hazipatane tena na makundi ya nyota kwenye alama hizo za nyota zilipata majina yazo wakati jua inapita katika makundi hayo ya nyota. Watu wanasema kama alama za makundi ya nyota zinafunua mambo fulani juu ya tabia ya mutu.

Lakini kusema kweli, watu wenye walizaliwa tarehe ileile hawakuwake na tabia zenye kufanana; tarehe ya mutu haifunue jambo lolote juu ya tabia yake. Kuliko kuona watu vile wako kabisa, watu wenye kufanya unajimu wanahukumu mwenendo na tabia ya mutu kupitia mambo ya kuwazia-wazia tu. Je, hiyo haiko aina fulani ya ubaguzi?

KUTABIRI MATUKIO

Tangu zamani, watu wameenda kwa wale wenye kutabiri matukio ili wawasaidie kujua mambo ya wakati wenye kuja. Watu fulani wenye kutabiri matukio walitafuta maana katika vitu kama vile sehemu za ndani za munyama na za mutu ao namna jogoo anakula mbegu. Wengine walitabiri mambo kwa kutumia majani ya chai ao masalio ya kahawa (café) yenye kuoza. Leo watu wanatumia karata, kitu chenye kuwa kama kioo, na njia zingine ili kuwasaidia kujua wakati wenye kuja wa mutu fulani. Je, kutabiri matukio ni njia yenye kutegemeka ya kujua wakati wenye kuja? Hapana kabisa. Tufikirie basi jambo hilo.

Fikiria tatizo la kukosa upatano katika mambo yenye wanatabiri. Mara nyingi, njia zenye watu tofauti wenye kutabiri matukio wanatumia ili kutabiri matukio zinapingana. Hata kama ni njia ileile moja ndiyo inatumiwa, mambo yenye yanatabiriwa hayapatane. Kwa mufano, ikiwa mutu fulani anauliza watu wawili wenye kutabiri matukio wamuambie mambo ya wakati wenye kuja kwa kutumia karata zilezile, kwa kawaida jibu halipaswe kuwa tofauti. Lakini mara nyingi haiko hivyo.

Watu wameanza kuwa na mashaka juu ya nia ya watu wenye kutabiri matukio na njia zenye wanatumia. Wachambuzi wanasema kama karata na kioo ni vyombo tu vyenye vinawategemeza na kwamba mutu mwenye kutabiri matukio anajifunza matendo ya mutu na kutabiri kulingana na matendo hayo. Kwa mufano, mutu mwenye kutabiri matukio mwenye uzoefu anaweza kuuliza maulizo mbalimbali na kuona kwa uangalifu namna mutu iko anasema ao kutenda ili kupata kile kinaweza kufunua jambo fulani juu ya mutu huyo. Mutu mwenye kutabiri matukio anafikia kujisifu kuwa amejua mambo ya mutu na hali mbalimbali wakati ni mutu huyo ndiye alifunua mambo yake mwenyewe bila kujua. Kwa sababu watu wamefikia kuwatumainia, waaguzi fulani wamefikia kupata feza nyingi kutoka kwa wale wenye kuja kuwaona.

MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA

Unajimu na kutabiri matukio vinafanya watu waamini kama mambo yenye kutupata leo yamekwisha kupangwa. Lakini ni kweli? Biblia inasema kama tuko na uwezo wa kuchagua mambo ya kuamini ao mambo yenye tunapenda kufanya na kama maamuzi yenye tunafanya yako na matokeo juu ya wakati wetu wenye kuja.​—Yoshua 24:15.

Waabudu wa Mungu wako na sababu ingine ya kukataa unajimu na kutabiri matukio​—Mungu hakubali aina yoyote ya uaguzi. Biblia inasema hivi: ‘Asipatikane ndani yako yeyote . . . anayefanya uaguzi, mwenye kufanya uchawi ao yeyote anayetafuta ishara za bahati ao mulozi, ao anayefunga wengine kwa kuwatakia maovu ao yeyote anayetafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo ao mujuzi wa kubashiri [ao, kutabiri] matukio ao yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu. Kwa maana kila mutu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova.’ *​—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

^ fu. 17 Jina la ule mwenye kuwa “Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”​—Zaburi 83:18.