“Wapole Wataimiliki Dunia”
Wengi wetu tumeshuhudia haki ikipotoshwa na kuona watu wazuri, wasio na hatia wakikandamizwa na waovu. Je, kuna wakati ambapo hakutakuwa na ukosefu wa haki na uovu?
Biblia inatupatia jibu na mwongozo katika Zaburi ya 37. Chunguza majibu yake kuhusu maswali haya muhimu.
Tunapaswa kuwaonaje wale wanaotukandamiza?—Mstari wa 1, 2.
Ni nini kitakachowapata waovu?—Mstari wa 10.
Maisha yatakuwaje baadaye kwa wale wanaotenda mema?—Mstari wa 11, 29.
Tunapaswa kufanya nini sasa?—Mstari wa 34.
Zaburi ya 37, ambayo iliongozwa na roho ya Mungu, inaeleza waziwazi kwamba wale ‘wanaomtumaini Yehova na kufuata njia yake’ watakuwa na maisha mazuri wakati ujao. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia ujifunze Biblia na kujua hatua unazoweza kuchukua ili wewe na wapendwa wako mfurahie tumaini hilo.