Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hivi Karibuni, Mungu Atamaliza Mateso Yote

Hivi Karibuni, Mungu Atamaliza Mateso Yote

“Ee Yehova, nililie musaada mupaka wakati gani, lakini wewe hausikie? Nitakuomba musaada kwa sababu ya jeuri mupaka wakati gani, lakini wewe hauingilie kati?” (Habakuki 1:2, 3) Hayo ni maneno ya Habakuki, mwanaume muzuri mwenye alikubaliwa na Mungu. Ombi lake lilionyesha kama alikosa imani? Hapana kabisa! Mungu alimuhakikishia Habakuki kwamba alikuwa na wakati wenye aliweka ili kumaliza mateso.​—Habakuki 2:2, 3.

Wakati wewe ao mutu mwenye unapenda iko anateseka, ni mwepesi kusema mara moja kama Mungu anakawia kutenda, na kama alipaswa kutenda sasa. Hata hivyo, Biblia inatuhakikishia hivi: “Yehova hakawie kuhusiana na ahadi yake, kama vile watu fulani wanaona kukawia, lakini yeye ni muvumilivu kuwaelekea ninyi kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.”​—2 Petro 3:9.

MUNGU ATATENDA WAKATI GANI?

Hivi karibuni! Yesu alisema kama kizazi fulani cha pekee kingejionea hali nyingi za pekee zenye kuonyesha kama tunaishi siku za mwisho za “mupangilio wa mambo.” (Matayo 24:3-42) Utimizo wa unabii wa Yesu katika siku zetu unaonyesha kama Mungu iko karibu kutenda. *

Lakini, namna gani Mungu atamaliza mateso yote? Wakati Yesu alikuwa katika dunia, alionyesha kama Mungu iko na nguvu ya kumaliza mateso ya wanadamu. Fikiria mifano fulani kuhusu jambo fulani.

Misiba ya Asili: Wakati Yesu na mitume wake walikuwa wanasafiri kwenye Bahari ya Galilaya, kulitokea zoruba kali yenye ilifanya mashua ikaribie kuzama. Lakini Yesu alionyesha kama yeye na Baba yake wanaweza kuzuia nguvu za asili. (Wakolosai 1:15, 16) Yesu alisema tu: “Nyamaza! Tulia!” Matokeo yalikuwa nini? “Upepo ukatulia na kukakuwa utulivu mukubwa.”​—Marko 4:35-39.

Magonjwa: Yesu alijulikana muzuri kuwa alikuwa na uwezo wa kuponyesha vipofu na vilema, na pia wote wenye kifafa, ukoma, ao kila namna ingine ya uzaifu. “Akaponyesha wote wenye walikuwa wagonjwa.”​—Matayo 4:23, 24; 8:16; 11:2-5.

Upungufu wa Chakula: Yesu alitumia nguvu zenye alipewa na Baba yake ili kuzidisha chakula kidogo na kukitolea watu. Biblia inasema kama wakati wa utumishi wake, alikulisha mara mbili maelfu ya watu.​—Matayo 14:14-21; 15:32-38.

Kifo: Nguvu ya Yehova ya kuondoa kifo inaonyeshwa wazi kupitia ufufuo tatu wenye kuzungumuziwa katika Biblia wenye Yesu alifanya. Mumoja kati ya watu wenye Yesu alifufua alikuwa amekufa kumepita siku ine.​—Marko 5:35-42; Luka 7:11-16; Yohana 11:3-44.

^ fu. 5 Ili kupata habari zaidi juu ya siku za mwisho, ona sura ya 9 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza kukichukua bila kulipa ku www.pr418.com