Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unamujua Yehova Kama Vile Noa, Danieli, na Ayubu Walimujua?

Unamujua Yehova Kama Vile Noa, Danieli, na Ayubu Walimujua?

‘Watu wenye mwelekeo wa ubaya hawawezi kuelewa hukumu [ao, haki], lakini wale wanaomutafuta Yehova wanaweza kuelewa kila jambo.’​—MET. 28:5.

NYIMBO: 126, 150

1-3. (a) Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa waaminifu kwa Mungu katika siku hizi za mwisho? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

KADIRI siku hizi za mwisho zinakaribia mwisho wake, watu wabaya wanaendelea ‘kuchipuka kama majani.’ (Zab. 92:7) Kwa hiyo, hatuwezi kushangaa kuona namna watu wengi wanakataa kufuata kanuni za Mungu za mwenendo. Katika ulimwengu huu, namna gani tunaweza kuwa “watoto kuhusiana na ubaya” lakini “watu wazima katika nguvu [zetu] za uelewaji”?​—1 Kor. 14:20.

2 Jibu linapatikana katika andiko letu la musingi; sehemu moja ya andiko hilo inasema hivi: ‘Wale wanaomutafuta Yehova wanaweza kuelewa kila jambo,’ ni kusema, kila jambo lenye wako nalo lazima ili kumufurahisha. (Met. 28:5) Mawazo kama hayo yanapatikana katika andiko la Methali 2:7, 9 lenye kusema kama Yehova ‘anawawekea wanyoofu [ao, waaminifu] hazina ya hekima inayotumika.’ Kwa hiyo, wenye haki wanaweza “kuelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.”

3 Noa, Danieli, na Ayubu walifikia kuwa na hekima hiyo. (Eze. 14:14) Ni hivyo pia kuhusu watu wa Mungu leo. Halafu wewe? ‘Unaelewa kila jambo’ lenye uko nalo lazima ili kumufurahisha Yehova? Ujuzi wa kweli ndio jambo kubwa lenye linaweza kukusaidia. Katika habari hii tutazungumuzia (1) namna Noa, Danieli, na Ayubu walifikia kumujua Mungu, (2) namna ujuzi huo uliwaletea faida, na (3) namna tunaweza kuwa na imani kama yao.

NOA ALITEMBEA PAMOJA NA MUNGU KATIKA ULIMWENGU MUBAYA

4. Namna gani Noa alifikia kumujua Yehova, na namna gani ujuzi wa kweli ulimusaidia?

4 Namna gani Noa alifikia kumujua Yehova? Tangu zamani sana, wanaume na wanawake wenye imani wamejifunza juu ya Mungu kupitia njia tatu: kwanza, kwa kuangalia uumbaji wenye kuonekana, pili, kupitia wanadamu wengine wenye kumuogopa Mungu, na tatu, kwa kujionea namna anawabariki wakati wanaishi kulingana na kanuni zake. (Isa. 48:18) Wakati alikuwa anaangalia uumbaji, Noa angeweza kuona ushuhuda wenye kuonyesha kama Mungu iko kabisa, na angeweza pia kuona sifa zake nyingi zenye hazionekane, kama vile “nguvu zake za milele na Uungu” wake. (Rom. 1:20) Kwa hiyo, Noa hakumuamini tu Mungu, lakini pia alikomalisha imani yenye nguvu katika Mungu.

5. Namna gani Noa alifikia kujua kusudi la Mungu juu ya wanadamu?

5 Imani ‘inafuata jambo lililosikiwa.’ (Rom. 10:17) Namna gani Noa alisikia habari juu ya Yehova? Bila shaka, alijifunza mambo mengi kupitia watu wa jamaa yake. Kati ya watu hao kuko Lameki, baba yake, mwenye aliishi wakati mumoja na Adamu kwa kipindi fulani. (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) Kuko pia Methusela, tate yake, na Yaredi, tate ya Methusela. Yaredi aliishi mupaka wakati Noa alikuwa na miaka 366. * (Lu. 3:36, 37) Pengine Noa alijifunza kupitia wanaume hao na inawezekana kupitia bibi zao pia juu ya namna maisha ya wanadamu yalianza, kusudi la Mungu kwamba wanadamu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa wajaze dunia, na uasi wenye ulitokea katika shamba la Edeni; na Noa angeweza kujionea matokeo ya uasi huo. (Mwa. 1:28; 3:16-19, 24) Kwa kweli, mambo yenye Noa alijifunza yaligusa moyo wake, na yalimuchochea amutumikie Mungu.​—Mwa. 6:9.

6, 7. Namna gani tumaini lilitia nguvu imani ya Noa?

6 Tumaini linatia nguvu imani. Fikiria namna Noa alijisikia wakati alijua kama jina lake lenye pengine linamaanisha “pumuziko; faraja” lilitoa tumaini! (Mwa. 5:29) Lameki aliongozwa na roho ya Mungu ili kusema hivi: “Huyu [Noa] atatuletea faraja katika . . . maumivu ya mikono yetu yanayoletwa na udongo ambao Yehova amelaani.” Noa alikuwa na tumaini katika Mungu. Kama Abeli na Enoko wenye waliishi mbele yake, alikuwa na imani katika “uzao” wenye ungeponda kichwa cha nyoka.​—Mwa. 3:15.

7 Hata kama pengine Noa hakuelewa kabisa-kabisa maana ya unabii wenye kuwa katika Mwanzo 3:15, kwa kweli, alielewa kama unabii huo ulitoa tumaini la wokovu. Zaidi ya hilo, ahadi hiyo yenye ilitolewa katika shamba la Edeni inapatana na ujumbe wenye Enoko alitangaza; alitabiri pia hukumu ya Mungu juu ya watu wabaya. (Yuda 14, 15) Ujumbe wa Enoko wenye utakuwa na utimizo wake wa mwisho kwenye Har-Magedoni, bila shaka ulitia nguvu imani na tumaini la Noa!

8. Namna gani ujuzi wa kweli juu ya Mungu ulimulinda Noa?

8 Namna gani ujuzi wa kweli juu ya Mungu ulimuletea Noa faida? Ujuzi wa kweli ulimupatia Noa imani na hekima kutoka kwa Mungu; sifa hizo zilimulinda asipatwe na hatari, zaidi sana hatari ya kiroho. Kwa mufano, kwa sababu Noa “alitembea pamoja na Mungu wa kweli,” hakutembea ao hakujiunga na watu wenye hawakumuogopa Mungu. Hakudanganywa na mashetani wenye walivaa miili ya wanadamu, wenye kwa kweli walishangaza wanadamu wenye hawakukuwa na imani, na pengine hata watu walifikia kuanza kuwaabudu. (Mwa. 6:1-4, 9) Pia, Noa alijua kama Mungu alikuwa ameambia wanadamu wazae na wajaze dunia. (Mwa. 1:27, 28) Kwa hiyo, alijua kwamba ngono kati ya wanawake na mashetani hao wenye walivaa miili ya wanadamu, haikukuwa jambo la kawaida na ilikuwa mubaya. Hilo lilionekana kuwa kweli wakati walifikia kuzaa watoto wenye hawakukuwa wa kawaida. Kisha wakati fulani, Mungu alimuonya Noa kwamba angeleta garika katika dunia. Imani ya Noa katika onyo hilo ilimuchochea kujenga safina, na kwa kufanya hivyo aliokoa familia yake.​—Ebr. 11:7

9, 10. Namna gani tunaweza kuiga imani ya Noa?

9 Namna gani tunaweza kukomalisha imani kama ya Noa? Jambo kubwa lenye linaweza kutusaidia ni kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, kuweka katika moyo wetu mambo yenye tunajifunza, na kuacha ujuzi huo utufinyange na kutuongoza. (1 Pet. 1:13-15) Kisha imani na hekima kutoka kwa Mungu vitatulinda kutokana na njia za Shetani zenye ujanja na kutokana na roho ya ulimwengu. (2 Kor. 2:11) Roho hiyo inachochea watu wapende jeuri na mwenendo mubaya. Na inachochea watu wafuatie tamaa za mwili. (1 Yoh. 2:15, 16) Inaweza hata kuchochea watumishi wa Mungu wenye kuwa zaifu kiroho wazarau ushuhuda wenye kuonyesha kama siku kubwa ya Yehova iko karibu. Ona kwamba wakati Yesu alilinganisha siku zetu na siku za Noa, hakukazia jeuri na mwenendo mubaya, lakini alikazia hatari ya kukengeuka kiroho.​—Soma Mathayo 24:36-39.

10 Ujiulize hivi: ‘Maisha yangu yanaonyesha kama ninamujua Yehova kabisa? Imani yangu inanichochea kuishi kulingana na kanuni za haki za Mungu na kuzielezea wengine?’ Majibu yako yanapaswa kuonyesha kama wewe pia ‘unatembea pamoja na Mungu wa kweli.’

DANIELI ALIONYESHA HEKIMA KUTOKA KWA MUNGU KATIKA BABILONI YA WAPAGANI

11. (a) Kijana Danieli alishikamana na Mungu; hilo linaonyesha nini juu ya namna alilelewa? (b) Unapenda kuiga sifa gani za Danieli?

11 Namna gani Danieli alifikia kumujua Yehova? Kwa kweli, Danieli alifundishwa muzuri na wazazi wake; walimufundisha kumupenda Yehova na Neno lake. Zaidi ya hilo, Danieli alionyesha upendo huo katika maisha yake yote. Hata wakati alizeeka, aliendelea kuchunguza Maandiko. (Dan. 9:1, 2) Sala ya Danieli yenye kutoka moyoni na yenye kuonyesha unyenyekevu wake yenye kupatikana katika Danieli 9:3-19, inaonyesha wazi kama alimujua Mungu muzuri sana, na alijua namna Mungu alitendea Waisraeli. Unaweza kutumia wakati fulani ili kusoma na kutafakari juu ya sala hiyo, na kuchunguza kwa uangalifu mambo yenye sala hiyo inakufundisha juu ya Danieli.

12-14. (a) Namna gani Danieli alionyesha hekima kutoka kwa Mungu? (b) Namna gani Mungu alibariki ushikamanifu na ujasiri wa Danieli?

12 Namna gani ujuzi wa kweli juu ya Mungu ulimuletea Danieli faida? Maisha katika Babiloni ya wapagani yalileta majaribu makubwa kwa Wayahudi waaminifu. Kwa mufano, Yehova aliambia hivi Wayahudi: ‘Mutafute amani kwa ajili ya jiji ambamo nimewapeleka ninyi uhamishoni.’ (Yer. 29:7) Lakini, wakati huohuo, aliwaomba wamuabudu yeye tu kwa moyo wao wote. (Kut. 34:14) Ni nini ilimusaidia Danieli akuwe na usawaziko juu ya mambo hayo mawili? Hekima ya Mungu ilimusaidia aelewe kanuni yenye kuonyesha kama utii wetu kwa viongozi wa ulimwengu unapaswa kuwa na mipaka. Miaka mingi kisha hapo, Yesu alifundisha kanuni hiyohiyo.​—Lu. 20:25.

13 Fikiria jambo lenye Danieli alifanya wakati sheria fulani ya serikali iliomba watu wote wasisali kwa mungu ao mwanadamu fulani lakini wasali kwa mufalme tu kwa siku 30. (Soma Danieli 6:7-10.) Danieli angeweza kutoa visababu kwa kusema hivi: ‘Ni siku 30 tu!’ Lakini hakuruhusu sheria ya mufalme imuzuie kufanya mambo yenye Maandiko yalimuomba kufanya. Kwa kweli, angeweza kusali kwa siri ili watu wasimuone. Lakini alijua kama watu walizoea kumuona wakati alikuwa anasali kila siku. Kwa hiyo, hata kama hilo lingetia maisha yake katika hatari, Danieli aliendelea kusali nafasi kwenye watu wangeweza kumuona ili wasifikiri kuwa alikuwa ameacha kumutumikia Yehova.

14 Yehova alibariki uamuzi wa Danieli wenye kuonyesha ushikamanifu na ujasiri kwa kumulinda kwa njia ya muujiza ili asiuawe na simba. Kwa kweli, hilo lilifikia kutoa ushahidi muzuri sana juu ya Yehova; ushahidi huo ulifika mupaka katika maeneo ya mbali zaidi ya Utawala wa Wamedi na Waperse!​—Dan. 6:25-27.

15. Namna gani tunaweza kukomalisha imani kama ya Danieli?

15 Namna gani tunaweza kukomalisha imani kama ya Danieli? Jambo kubwa lenye linaweza kutusaidia haiko kusoma tu Neno la Mungu, lakini pia ‘kuelewa maana’ yake. (Mt. 13:23) Tunapenda kujua mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali, hilo linatia ndani kuelewa kanuni za Biblia. Kwa hiyo, tunapaswa kutafakari juu ya mambo yenye tunasoma. Pia ni jambo la maana kusali kwa ukawaida kwa moyo wote, zaidi sana wakati tunapambana na majaribu ao magumu mengine. Wakati tunasali kwa imani ili tupate hekima na nguvu, Yehova atatupatia mambo hayo kwa ukarimu.​—Yak. 1:5.

AYUBU ALITUMIKISHA KANUNI ZA MUNGU WAKATI WA MUZURI NA WA MAGUMU

16, 17. Namna gani Ayubu alifikia kuwa na ujuzi wa kweli juu ya Mungu?

16 Namna gani Ayubu alifikia kumujua Yehova? Ayubu hakukuwa Mwisraeli. Lakini, alikuwa mutu wa jamaa ya mbali ya Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na Yehova alikuwa amefunuliwa wanaume hao mambo mbalimbali juu yake na juu ya kusudi lake kwa wanadamu. Kwa njia fulani, Ayubu alijua mambo mengi juu ya kweli hizo za maana. (Ayu. 23:12) Ayubu alisema hivi: “Nimesikia habari zako.” (Ayu. 42:5) Zaidi ya hilo, Yehova mwenyewe alisema kama Ayubu alisema mambo ya kweli juu yake.​—Ayu. 42:7, 8.

Wakati tunaangalia uumbaji wenye kuonekana, tunaona sifa za Mungu zenye hazionekane, na hilo linatia nguvu imani yetu (Picha hii inapatana na fungu la 17)

17 Kupitia uumbaji wenye kuonekana, Ayubu aliona pia sifa nyingi za Mungu zenye hazionekane. (Ayu. 12:7-9, 13) Kisha, Elihu na Yehova walitumia mambo fulani ya uumbaji ili kumukumbusha Ayubu kuwa mwanadamu ni wa hali ya chini sana kwa kulinganishwa na Mungu. (Ayu. 37:14; 38:1-4) Maneno ya Yehova yaligusa moyo wa Ayubu kwa sababu alisema hivi kwa unyenyekevu: ‘Nimepata kujua kwamba unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna wazo lolote ambalo hauwezi kulifikia. . . . Ninatubu katika mavumbi na majivu.’​—Ayu. 42:2, 6.

18, 19. Namna gani Ayubu alionyesha kama alimujua Yehova kabisa?

18 Namna gani ujuzi juu ya Mungu ulimuletea Ayubu faida? Ayubu alielewa muzuri sana kanuni za Mungu. Alimujua Yehova kabisa, na alitenda kulingana na ujuzi huo. Kwa mufano, Ayubu alijua kama hangeweza kusema kama anamupenda Mungu na wakati huohuo kutendea mubaya mwanadamu mwenzake. (Ayu. 6:14) Hakujiona kuwa wa maana kuliko wengine, lakini alihangaikia watu wote kwa upendo, iwe matajiri ao maskini. Alisema hivi: “Je, si yeye Mumoja tu aliyetufanya sisi katika tumbo la uzazi?” (Ayu. 31:13-22) Hata wakati Ayubu alikuwa tajiri na mwenye kujulikana, hakuruhusu mambo hayo yamufanye akuwe na kiburi na kujiona kuwa wa maana kuliko wengine. Alikuwa tofauti kabisa na watu wengi wenye kuwa na mamlaka na utajiri katika ulimwengu huu!

19 Ayubu aliepuka aina yote ya kuabudu sanamu, hata katika moyo wake. Alijua kama ibada ya uwongo, kutia ndani kufuatia utajiri wa kimwili, ingekuwa kumukana “Mungu wa kweli aliye juu.” (Soma Ayubu 31:24-28.) Aliona ndoa kuwa ahadi takatifu kati ya mwanaume na mwanamuke. Alifanya hata agano na macho yake ili asiangalie mwanamuke kwa njia yenye haifae. (Ayu. 31:1) Ukumbuke kwamba wakati huo Mungu alikuwa anaachilia wanaume waoe wanawake wengi. Kwa hiyo, Ayubu angeweza kuoa bibi wa pili ikiwa angependa. * Lakini, alifuata mufano wa ndoa yenye Mungu alianzisha katika shamba la Edeni, na kufanya mufano huo kuwa sheria kwake. (Mwa. 2:18, 24) Miaka 1600 hivi kisha hapo, Yesu Kristo alifundisha wasikilizaji wake wafuate kanuni hiyohiyo juu ya ndoa na mwenendo muzuri juu ya ngono.​— Mt. 5:28; 19:4, 5.

20. Namna gani ujuzi wa kweli juu ya Yehova na kanuni zake vinatusaidia kuchagua marafiki wazuri na mambo ya kujifurahisha yenye kufaa?

20 Namna gani tunaweza kukomalisha imani kama ya Ayubu? Tena, jambo kubwa lenye linaweza kutusaidia, ni kuwa na ujuzi wa kweli juu ya Yehova na kuacha ujuzi huo utuongoze katika sehemu zote za maisha yetu. Kwa mufano, Biblia inasema kama Yehova anachukia ‘mutu yeyote anayependa jeuri,’ na inatuonya pia juu ya kufanya urafiki pamoja “na watu wasiosema kweli.” (Soma Zaburi 11:5; 26:4.) Maandiko hayo yanakufundisha nini juu ya mawazo ya Mungu? Kujua mambo hayo kunapaswa kuwa na matokeo gani juu ya mambo yenye unatia pa nafasi ya kwanza, namna unatumia Internete, na namna unachagua marafiki na mambo ya kujifurahisha? Majibu yako yanaweza kukusaidia kujua ikiwa unamujua Yehova kwa kadiri gani. Ili kuendelea kuwa na mwenendo muzuri katika ulimwengu huu muovu, tunapaswa kuzoeza ‘nguvu zetu za ufahamu’ ili tuweze kutofautisha mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa; lakini pia mambo ya hekima na yenye haiko ya hekima.​—Ebr. 5:14; Efe. 5:15.

21. Ni nini itatusaidia “kuelewa kila jambo” lenye tuko na lazima ya kujua ili kumufurahisha Baba yetu wa mbinguni?

21 Kwa sababu Noa, Danieli, na Ayubu walimutafuta Yehova kwa moyo wao wote, aliwasaidia wamupate. Aliwasaidia “kuelewa kila jambo” lenye walikuwa nalo lazima ili kumupendeza. Kwa hiyo, walifikia kuwa mifano ya uadilifu, na walikuwa na maisha yenye furaha kabisa. (Zab. 1:1-3) Kwa hiyo, ujiulize hivi, ‘Ninamujua Yehova muzuri kama vile Noa, Danieli, na Ayubu walimujua?’ Kwa kweli, nuru ya kiroho yenye imeongezeka, inaweza kukusaidia kumujua muzuri hata zaidi! (Met. 4:18) Kwa hiyo, uchimbe kabisa katika Neno la Mungu. Ufikiri sana juu ya Neno hilo. Na umuombe Mungu roho yake takatifu. Kisha utamukaribia zaidi Baba yako wa mbinguni. Ikiwa unafanya hivyo, utatenda kwa utambuzi na hekima katika ulimwengu wa leo wenye kujaa watu wenye hawamuogope Mungu.​—Met. 2:4-7.

^ fu. 5 Enoko, baba ya tate ya Noa, yeye pia ‘aliendelea kutembea pamoja na Mungu wa kweli.’ Lakini, alikufa miaka 69 hivi mbele Noa azaliwe.​—Mwa. 5:23, 24.

^ fu. 19 Tunaweza kusema hivyo pia kuhusu Noa. Alikuwa tu na bibi mumoja, hata kama watu walianza kuwa na bibi wengi muda mufupi kisha uasi kutokea katika Edeni.​—Mwa. 4:19.