Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Hotuba za Watu Wote Zinaeneza Habari Njema Katika Irelandi

Hotuba za Watu Wote Zinaeneza Habari Njema Katika Irelandi

WAKATI mashua inakaribia, sehemu ya bahari yenye kuingia katika inchi kavu yenye kuitwa Belfast Lough, kikundi kidogo cha watu wenye kusafiri wenye kusimama inje katika mashua wanaona milima yenye kuwa na majani wakati mwangaza wa asubuhi unatokea. Ilikuwa Mwezi wa 5, 1910. Kati ya wasafiri hao kulikuwa Charles Taze Russell, hiyo ilikuwa safari yake ya tano ya kuja katika Irelandi. Mbele ya Ndugu Russell kulikuwa mashua mbili kubwa-kubwa zenye zilikuwa zinatengenezwa, ni kusema, Titanic yenye ilifikia kuzama na mashua ingine yenye iliitwa Olympic. * Pembeni na mahali hapo pa kutengenezea mashua, Wanafunzi fulani wa Biblia, walikuwa wanasimama mahali penye mashua zinazoea kusimama, ili kungojea Charles Russell afike.

Miaka 20 hivi mbele ya hapo, Ndugu Russell alitafuta njia ya muzuri ya kutangaza habari njema katika dunia yote, kwa hiyo, aliamua kufanya safari mbalimbali za kuenda inje ya Amerika. Katika safari yake ya kwanza alitembelea inchi ya Irelandi, katika Mwezi wa 7, 1891. Wakati alikuwa katika mashua yenye kuitwa City of Chicago, aliona namna jua linashuka wakati walikuwa wanakaribia inchi kavu katika muji wa Queenstown, na pengine alikumbuka mambo yenye wazazi wake walimuambia juu ya inchi yao ya kizalikio. Wakati Ndugu Russell na wasafiri wenzake walikuwa wanapita katika miji yenye kuwa safi na vijiji vyenye kupendeza, walitambua kama inchi hiyo ilikuwa shamba lenye kuwa “tayari na lenye kungojea kuvunwa.”

Ndugu Russell alitembelea Irelandi mara saba. Kwa sababu watu walipendezwa wakati wa safari yake ya kwanza, hilo lilifanya mamia ya watu na wakati fulani maelfu ya watu wakuje kumusikiliza wakati alikuwa anatembelea tena inchi hiyo. Kufikia wakati wa safari yake ya pili, katika Mwezi wa 5, 1903, magazeti ya ulimwengu yalikuwa yanafanya matangazo juu ya hotuba za watu wote katika Belfast na Dublin. Russell alieleza kama “wahuzuriaji walisikiliza kwa uangalifu sana” hotuba yenye kichwa “Ahadi Yenye Kufungwa kwa Kiapo” juu ya imani ya Abrahamu na baraka za wakati wenye kuja kwa ajili ya wanadamu.

Kwa sababu watu wengi walipendezwa, Russell alitembelea tena Irelandi wakati wa safari yake ya tatu katika Ulaya. Ndugu tano walimusalimia wakati alifika mahali penye mashua zinazoea kusimama katika Belfast, ilikuwa asubuhi moja Mwezi 4, 1908. Hotuba yenye ilikuwa imefanyiwa matangazo, yenye kichwa, “Kupinduliwa kwa Milki ya Shetani,” ilichochea “wahuzuriaji wenye kupendezwa karibu 300” mangaribi ya siku hiyo. Mupinzani mumoja kati ya watu hao alinyamazishwa bila kukawia kupitia namna Maandiko yalikuwa yanatumiwa kwa ufundi. Katika Dublin mupinzani mukubwa, O’Connor, mwandishi wa Association chrétienne de jeunes gens, alijaribu kuchochea wasikilizaji zaidi ya 1000 wapinge Wanafunzi wa Biblia. Ni jambo gani lilitokea?

Turudie nyuma na kuwazia katika akili yetu mambo yenye pengine yalitokea kwenye tukio hilo. Mwanaume mumoja mwenye alipenda kupata kweli ya Biblia aliamua kuhuzuria hotuba ya watu wote yenye ilifanyiwa matangazo katika gazeti la The Irish Times. Pengine alijikaza sana ili kupata nafasi ya kukaa katika jumba lenye kujaa sana watu. Mwanaume huyo anasikiliza kwa uangalifu musemaji mwenye kuwa na nywele mweupe na ndevu za murefu mwenye kuvaa koti ndefu la mweusi. Wakati musemaji huyo anatoa hotuba, anatembea-tembea kwenye jukwaa, anafanya ishara, anafasiria maandiko mbalimbali yenye kupatana, na kufungua masikio ya mwanaume huyo ili aelewe kweli za Biblia. Hata bila kutumia chombo cha kuongeza sauti, sauti ya musemaji huyo inafika katika jumba lote, na wahuzuriaji wanamusikiliza kwa uangalifu kwa saa moja na nusu. Wakati wa kipindi cha maulizo na majibu, O’Connor na marafiki wake wanamupinga, lakini anatetea muzuri kabisa ujumbe kwa kutumia Biblia. Wasikilizaji wanakubaliana naye na kupiga mikono. Wakati kunakuwa utulivu, mwanaume huyo mwenye kupendezwa anakaribia ndugu ili ajue mengi zaidi. Watu wengi wenye walijionea mambo hayo, walisema kwamba watu wengi walijifunza kweli katika njia hiyo.

Ndugu Russell aliondoka New York katika Mwezi wa 5, 1909 katika mashua yenye kuitwa Mauretania ili kutembelea Irelandi kwa mara ya ine. Alienda pamoja na Ndugu Huntsinger, mwenye alikuwa mwandishi ili wakati wangekuwa wanasafiri katika bahari aweze kumuambia habari za kuandika katika Munara wa Mulinzi. Hotuba ya watu wote ya Ndugu Russell katika Belfast ilichochea watu 450 wa eneo hilo, kati yao watu 100 hivi walisimama kwa sababu ya kukosa mahali pa kukaa katika jumba.

Ndugu Russell iko katika mashua Lusitania

Safari yake ya tano, yenye tulizungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii, ilikuwa hivyo pia. Kisha kutoa hotuba ya watu wote katika Dublin, mwanateolojia mumoja mwenye kujulikana sana, mwenye aliletwa na O’Connor alipata majibu ya Maandiko juu ya maulizo yake, na wasikilizaji walifurahi sana. Siku yenye ilifuata wasafiri waliingia katika mashua moja ya kutembea haraka ya poste ili kuenda Liverpool na kuingia katika mashua yenye ilijulikana sana yenye kuitwa Lusitania ili kuenda New York. *

Hotuba ya watu wote inafanyiwa matangazo katika gazeti la The Irish Times, tarehe 20 Mwezi wa 5, 1910

Hotuba za watu wote zilifanyiwa pia matangazo wakati wa safari ya sita na ya saba ya Ndugu Russell katika mwaka wa 1911. Katika Mwezi wa 4 Wanafunzi wa Biblia 20 katika Belfast walikaribisha watu 2000 wenye walikuja kusikiliza hotuba yenye kichwa “Uzima kisha kifo.” O’Connor alikuja katika Dublin pamoja na kiongozi mwingine wa dini mwenye aliuliza maulizo, lakini wasikilizaji walifurahia sana majibu ya Maandiko na wakapiga mikono. Katika Mwezi wa 10 na Mwezi wa 11 wa mwaka uleule miji mingine ilitembelewa na watu wengi walihuzuria. O’Connor na watu 100 wenye kuleta muvurugo walijaribu kuvuruga tena mukutano mumoja katika Dublin, lakini wasikilizaji waliunga musemaji mukono kwa furaha.

Hata kama Ndugu Russell ndiye alizoea kutoa hotuba za watu wote, alikubali kama “hakuna mwanadamu mwenye kuwa wa maana sana,” kwa sababu “kazi hii haiko ya mwanadamu; ni kazi ya Mungu.” Matangazo juu ya hotuba za watu wote yenye yalifanywa mbele ya Mikutano ya Watu Wote, yalitokeza nafasi za muzuri za kufundisha kweli za Maandiko. Kulikuwa matokeo gani? Hotuba za watu wote zilisaidia kueneza habari njema, na makutaniko yaliongezeka katika miji mingi katika inchi ya Irelandi.​—Kutoka katika vitu vya maana vya historia yetu vya Uingereza.

^ fu. 3 Kisha miaka mbili Titanic ilizama.

^ fu. 9 Lusitania ilizama mahali penye mashua inazoea kusimama kusini mwa Irelandi katika Mwezi wa 5, 1915.