Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yakobo alifikia kuwa katika kizazi chenye kilitokeza Masiya kwa sababu aliuza haki ya Esau ya kuwa muzaliwa wa kwanza?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Katika Israeli ya zamani, kizazi chenye kuongoza kwa Masiya kilipitishwa tu kupitia haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza?

Wakati fulani tumesema kuwa mambo yalikuwa hivyo. Jambo hilo lilionekana kuwa linapatana na andiko la Waebrania 12:16. Andiko hilo linasema kuwa Esau ‘hakusamini mambo matakatifu’ na ‘alitoa [kwa Yakobo] haki zake za kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na mulo mumoja.’ Ilionekana kuwa andiko hilo linaonyesha kuwa wakati Yakobo alipata ‘haki zake za kuwa muzaliwa,’ akakuwa pia katika ya kizazi chenye kilitokeza Masiya.​—Mt. 1:2, 16; Lu. 3:23, 34.

Lakini, kisha kuchunguza tena habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, tumeona kuwa mwanaume hakupaswa tu akuwe muzaliwa wa kwanza ili kuwa katika kizazi chenye kingetokeza Masiya. Fikiria ushuhuda fulani:

Muzaliwa wa kwanza wa Yakobo (Israeli), alikuwa Rubeni mwenye bibi yake Lea alizaa. Kisha muzaliwa wake wa kwanza kwa Raheli, bibi yake mwenye alipenda sana, alikuwa Yosefu. Wakati Rubeni alijiendesha mubaya, Yosefu akapewa haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza. (Mwa. 29:31-35; 30:22-25; 35:22-26; 49:22-26; 1 Nya. 5:1, 2) Lakini Masiya hakutokea katika kizazi cha Rubeni ao katika kizazi cha Yosefu. Alitokea katika kizazi cha Yuda, mutoto wa ine wa Lea.​—Mwa. 49:10.

Luka 3:32 inataja majina tano ya watu wenye walikuwa katika kizazi chenye kilifikia kutokeza Masiya. Kila mwanaume anaonekana kuwa alikuwa muzaliwa wa kwanza. Boazi akamuzaa Obedi, na Obedi alikuwa baba ya Yese.​—Rut. 4:17, 20-22; 1 Nya. 2:10-12.

Hata hivyo, Daudi mutoto wa Yese hakukuwa muzaliwa wa kwanza. Alikuwa wa mwisho kati ya watoto wanaume munane. Lakini, Masiya alitokea katika kizazi cha Daudi. (1 Sam. 16:10, 11; 17:12; Mt. 1:5, 6) Vilevile mutu mwingine mwenye alikuwa katika kizazi hicho alikuwa Sulemani hata kama hakukuwa muzaliwa wa kwanza wa Daudi.​—2 Sam. 3:2-5.

Hilo halimaanishe kama kuwa muzaliwa wa kwanza haikukuwa jambo la maana. Muzaliwa wa kwanza alikuwa na cheo cha kuheshimika na mara nyingi yeye ndiye angefikia kusimamia familia. Pia, ni yeye ndiye mwana mwenye alipewa sehemu mbili za uriti.​—Mwa. 43:33; Kum. 21:17; Yos. 17:1.

Lakini mutoto mwengine angeweza kupewa haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza. Abrahamu alimufukuza Ishmaeli, na akamupatia Isaka haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza. (Mwa. 21:14-21; 22:2) Na kama vile tumeona, haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza ya Rubeni ilipewa Yosefu.

Sasa tuchunguze tena andiko la Waebrania 12:16 lenye linasema hivi: ‘Kusiwe na muasherati wala yeyote asiyesamini mambo matakatifu, kama Esau, ambaye alitoa haki zake za kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na mulo mumoja.’ Mutume Paulo alipenda kuzungumuzia jambo gani?

Hapa, Paulo hakukuwa anazungumuzia juu ya watu wenye kuwa katika kizazi chenye kilitokeza Masiya. Alikuwa tu ametoka kushauria Wakristo ‘wafanyie miguu yao mapito yaliyonyooka.’ Kwa kufanya hivyo, hawangekosa kupata ‘fazili zisizostahiliwa za Mungu,’ jambo la kuhuzunisha ni kwamba wangezikosa ikiwa wangeanza kufanya mambo ya uasherati. (Ebr. 12:12-16) Ikiwa wangefanya hivyo, wangekuwa kama Esau. Alishindwa ‘kusamini mambo matakatifu,’ na kwa njia ya moja kwa moja alifuatia mambo ya kimwili.

Esau aliishi wakati wa zamani, na pengine mara kwa mara alikuwa na pendeleo la kutoa zabihu. (Mwa. 8:20, 21; 12:7, 8; Ayu. 1:4, 5) Lakini, kwa sababu Esau aliona mambo kwa njia ya kimwili, aliacha mapendeleo kama hayo kwa sababu ya chakula. Pengine alipenda kuepuka mateso yenye yalikuwa yametabiriwa kuwa yangepata wazao wa Abrahamu. (Mwa. 15:13) Esau alionyesha pia kuwa anapenda mambo za kimwili, na akakosa kuheshimia mambo matakatifu, kwa kuoa wanawake wawili wapagani na hilo lililetea sana uchungu wazazi wake. (Mwa. 26:34, 35) Alikuwa tofauti kabisa na Yakobo mwenye alijikaza kuoa mwanamuke mwenye kuabudu Mungu wa kweli!​—Mwa. 28:6, 7; 29:10-12, 18.

Kwa hiyo, tunaweza kusema nini juu ya kizazi chenye kilitokeza Yesu, Masiya? Wakati fulani kizazi hicho kilipitishwa kwa muzaliwa wa kwanza, lakini haikuwa hivyo kila mara. Wayahudi walijua jambo hilo na walilikubali, kwa sababu walikubali kuwa Kristo alipaswa kutokea katika kizazi cha Daudi, mutoto wa mwisho wa Yese.​—Mt. 22:42.