Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umujue Adui Yako

Umujue Adui Yako

‘Hatukose kuzijua mbinu [ao, ujanja] zake [Shetani].’​—2 KOR. 2:11.

NYIMBO: 150, 32

1. Kisha Adamu na Eva kufanya zambi, Yehova alisema nini juu ya adui yetu?

ADAMU alijua kama nyoka haiwezi kusema. Kwa hiyo, wakati alijua kama nyoka ilisema na Eva, pengine Adamu alitambua kabisa kama ni kiumbe fulani wa roho ndiye alisema na Eva. (Mwa. 3:1-6) Adamu na Eva hawakujua kiumbe huyo wa roho alikuwa nani. Lakini, Adamu aliamua kujiunga na adui huyo ili kumupinga Baba yake wa mbinguni mwenye upendo. (1 Tim. 2:14) Bila kukawia, Yehova alianza kutoa maelezo mengi juu ya adui huyo muovu na akaahidi kama mwishowe ataharibiwa. Lakini Yehova alionya kama mbele aharibiwe, kiumbe huyo wa roho mwenye alizungumuza kupitia nyoka, angepinga wale wote wenye kumupenda Mungu.​—Mwa. 3:15.

2, 3. Pengine sababu gani Yehova hakufunua mambo mengi juu ya Shetani mbele ya kuja kwa Masiya?

2 Yehova hajatuambia hata kidogo jina la pekee la malaika huyo mwenye alimupinga. * (Ona maelezo ya chini.) Yehova alionyesha muasi huyo alikuwa nani kisha kupita miaka 2500 tangu uasi kutokea katika Edeni. (Ayu. 1:6) Anajulikana kuwa “Shetani,” jina lenye kumaanisha “Mupinzani.” Jina Shetani linapatikana katika vitabu vitatu tu vya Maandiko ya Kiebrania, ni kusema, 1 Mambo ya Nyakati, Ayubu, na Zekaria. Sababu gani Maandiko hayakuzungumuzia sana adui huyo mbele ya kuja kwa Masiya?

3 Yehova hakutia katika Maandiko ya Kiebrania maelezo mengi juu ya Shetani na mambo yenye anafanya. Kwa kweli, kusudi la Maandiko ya Kiebrania lilikuwa kusaidia watu watambue Masiya na kumufuata. (Lu. 24:44; Gal. 3:24) Wakati Masiya alifika, Yehova alimutumia yeye na wanafunzi wake ili kufunua mambo mengi yenye tunajua juu ya Shetani na malaika wenye walijiunga naye. * (Ona maelezo ya chini.) Hilo linafaa kwa sababu Yehova atatumia Yesu na Wakristo watiwa mafuta ili kumuharibu Shetani na wale wenye kumuunga mukono.​—Rom. 16:20; Ufu. 17:14; 20:10.

4. Sababu gani hatupaswe kumuogopa Shetani?

4 Mutume Petro alieleza kama Shetani Ibilisi ni kama “simba anayenguruma,” na Yohana alimuita kuwa “nyoka” na ‘joka mukubwa.’ (1 Pet. 5:8; Ufu. 12:9) Lakini hatupaswe kuogopa Ibilisi. Nguvu zake ziko na mipaka. (Soma Yakobo 4:7.) Yehova, Yesu, na malaika waaminifu wanatulinda. Kwa musaada wao, tunaweza kupinga maadui wetu. Hata hivyo, tuko na lazima ya kujua majibu ya maulizo haya matatu ya maana: Shetani iko na nguvu kwa kadiri gani? Namna gani anajaribu kudanganya watu? Na ni mambo gani yenye hawezi kufanya? Tujibie basi maulizo hayo na tuone mambo yenye tunaweza kujifunza.

SHETANI IKO NA NGUVU KWA KADIRI GANI?

5, 6. Sababu gani serikali za wanadamu haziwezi kuleta mabadiliko yenye wanadamu wako nayo lazima kabisa?

5 Malaika wengi walijiunga na Shetani katika kumuasi Mungu. Mbele ya Garika, Shetani alichochea malaika fulani kati yao wafanye ngono na wanawake. Biblia inaeleza jambo hilo kwa njia ya mufano wakati inasema kwamba joka huyo mukubwa alikokota pamoja naye sehemu ya tatu ya nyota wa mbinguni. (Mwa. 6:1-4; Yuda 6; Ufu. 12:3, 4) Wakati malaika hao waliacha familia ya Mungu, walijitia chini ya uongozi wa Shetani. Hatupaswe kufikiri kama malaika hao wenye waliasi hawapangwe muzuri. Katika ulimwengu wa roho wenye hauonekane, Shetani ameanzisha serikali yake yenye kuiga Ufalme wa Mungu. Amejifanya kuwa mufalme, na amepanga mashetani, amewapatia mamlaka, na amewafanya kuwa viongozi wa ulimwengu.​—Efe. 6:12.

6 Shetani anatumia tengenezo lake ili kuongoza serikali zote za wanadamu. Tunaweza kuwa hakika juu ya jambo hilo, kwa sababu alimuonyesha Yesu “falme zote za dunia inayokaliwa,” na alimuambia hivi: ‘Nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, na yeyote ninayetaka mimi ninamupatia.’ (Lu. 4:5, 6) Lakini, serikali nyingi zinafanyia wanainchi wao mambo mazuri, na viongozi fulani wanapenda kabisa kusaidia watu. Hata hivyo, hakuna kiongozi mwanadamu mwenye anaweza kuleta mabadiliko yenye tuko nayo lazima kabisa.​—Zab. 146:3, 4; Ufu. 12:12.

7. Zaidi ya kutumia serikali, namna gani Shetani anatumia dini za uongo na mambo ya biashara ya ulimwengu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Shetani na mashetani wake wanatumia pia dini za uongo na mambo ya biashara ya ulimwengu ili ‘kuipotosha [kudanganya] dunia nzima inayokaliwa,’ ao wanadamu wote. (Ufu. 12:9) Shetani anatumia dini za uongo ili kueneza habari za uongo juu ya Yehova, na amejaribu hata kuficha jina la Mungu. (Yer. 23:26, 27) Kwa hiyo, watu fulani wenye kuwa na moyo muzuri wenye wanafikiri kama wanamuabudu Mungu, kwa kweli, wanaabudu mashetani. (1 Kor. 10:20; 2 Kor. 11:13-15) Pia, Shetani anatumia mambo ya biashara ya ulimwengu ili kueneza uongo. Kwa mufano, ulimwengu huu unafundisha watu kama feza na vitu vya kimwili vinaleta furaha. (Met. 18:11) Wale wenye kuamini uongo huo wanatumia maisha yao yote ili kutumikia “Utajiri” kuliko kumutumikia Mungu. (Mt. 6:24) Hata kama hapo zamani walikuwa wanamupenda Mungu, upendo wao juu ya vitu vya kimwili unakuwa nguvu mupaka upendo wao kwa Mungu unapotea.​—Mt. 13:22; 1 Yoh. 2:15, 16.

8, 9. (a) Tunaweza kujifunza mambo gani mawili juu ya matendo ya Adamu, Eva, na malaika wenye waliasi? (b) Sababu gani kujua kama Shetani anatawala ulimwengu ni jambo la muzuri kwetu?

8 Kuko mambo mbili ya maana yenye tunaweza kujifunza kutokana na matendo ya Adamu na Eve, na malaika wenye waliasi. Kwanza, tunajifunza kama kuko pande mbili tu na tunapaswa kuchagua upande moja. Tunaweza kuwa upande wa Yehova ao wa Shetani. (Mt. 7:13) Pili, tunajifunza kama wale wenye wanajiunga na Shetani wanapata tu faida zenye kuwa na mipaka. Adamu na Eva walipata nafasi ya kujiamulia wao wenyewe mema na mabaya. Na mashetani walipata mamlaka fulani juu ya serikali za wanadamu. (Mwa. 3:22) Lakini, kuchagua upande wa Shetani kunaleta matokeo ya mubaya sikuzote. Hakuna faida za kweli kabisa!​—Ayu. 21:7-17; Gal. 6: 7, 8.

9 Sababu gani kujua kama Shetani anatawala ulimwengu ni jambo la muzuri kwetu? Kunatusaidia kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya serikali na kunatuchochea kuhubiri habari njema. Tunajua kama Yehova anapenda tuheshimie serikali. (1 Pet. 2:17) Anapenda tutii sheria za serikali hizo ikiwa hazipinge kanuni zake. (Rom. 13:1-4) Lakini tunajua pia kama tunapaswa kuepuka kabisa kuunga mukono chama fulani cha politike ao kiongozi fulani mwanadamu. (Yoh. 17:15, 16; 18:36) Kwa sababu tunaelewa kama Shetani anajaribu kuficha jina la Yehova na kumuharibishia sifa, tunajikaza sana ili kufundisha watu kweli juu ya Mungu wetu. Tunajivunia kuitwa kwa jina lake na kulitumia. Kumupenda Mungu ni jambo la maana sana kuliko kupenda feza ao vitu vya kimwili.​—Isa. 43:10; 1 Tim. 6:6-10.

NAMNA GANI SHETANI ANAJARIBU KUDANGANYA WATU?

10-12. (a) Namna gani pengine Shetani alitumia mutego ili kujaribu malaika fulani? (b) Namna malaika hao walitenda inatufundisha nini?

10 Shetani anatumia njia zenye matokeo ili kudanganya watu. Ili kuwachochea wafanye mambo yenye anapenda, anatumia mitego ili kuwajaribu na wakati fulani anajaribu kuwaogopesha.

11 Shetani alitumia mitego ili kujaribu hesabu kubwa ya malaika. Pengine aliwatazama kwa muda murefu ili ajue ni mambo gani yenye yangeweza kuwaingiza katika jaribu. Malaika fulani waliangukia katika mutego na wakafanya ngono pamoja na wanawake. Watoto wao walikuwa warefu na wanene na walitendea kwa jeuri watu wenye waliwazunguka. (Mwa. 6:1-4) Zaidi ya kutumia uasherati ili kujaribu malaika hao, pengine Shetani aliwaahidi pia kama wangekuwa na mamlaka juu ya wanadamu wote. Kwa kufanya hivyo, pengine Shetani alikuwa anajaribu kuzuia utimizo wa unabii wa Yehova juu ya ‘uzao wa mwanamuke.’ (Mwa. 3:15) Lakini Yehova hakuruhusu jambo hilo litokee. Alileta Garika yenye iliharibu mipango yoyote kama hiyo ya Shetani na mashetani wake.

Shetani anatumia mutego wa mambo ya uasherati, majivuno yenye haifae, na mambo ya uchawi ili kututega (Picha hizi zinapatana na fungu la 12, 13)

12 Habari hiyo inatufundisha nini? Mambo ya uasherati na kiburi ni aina ya mitego yenye inabana watu wengi. Malaika wenye walijiunga na Shetani walikuwa wamepitisha miaka mingi mbinguni pamoja na Mungu mwenyewe! Lakini, wengi kati yao waliacha tamaa za mubaya zikomae ndani yao, na tamaa hizo zikakuwa zenye nguvu sana. Tunapaswa kukumbuka sikuzote kwamba hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi, tamaa za mubaya zinaweza kukomaa katika moyo wetu. (1 Kor. 10:12) Ndiyo sababu tunapaswa kuchunguza mara kwa mara moyo wetu na kuondoa mawazo yoyote machafu na kiburi!​—Gal. 5:26; soma Wakolosai 3:5.

13. Ni mutego wa aina gani ingine wenye Shetani anatumia, na namna gani tunaweza kuepuka mutego huo?

13 Mutego wa aina ingine wenye Shetani anatumia ni kuchochea watu wapende kujua habari juu ya mambo ya uchawi. Leo, anajaribu kuchochea watu wapendezwe na mashetani kwa kutumia dini za uongo na mambo ya kujifurahisha. Filme, michezo ya video, na aina zingine za mambo ya kujifurahisha, vinaweza kufanya mambo ya uchawi yaonekane kuwa yenye kufurahisha. Namna gani tunaweza kuepuka mutego huo? Hatupaswe kutazamia kama tengenezo la Yehova litatupatia liste ya mambo ya kujifurahisha yenye kuwa ya muzuri na yenye kuwa ya mubaya. Tunapaswa kuzoeza zamiri yetu ili tuweze kukamata maamuzi ya muzuri yenye kutegemea kanuni za Yehova. (Ebr. 5:14) Na ikiwa upendo wetu kwa Mungu hauna “unafiki,” tutakamata maamuzi yenye hekima. (Rom. 12:9) Munafiki hatende kulingana na mambo yenye anasema. Kwa hiyo wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninafuata kanuni zilezile zenye ninaambia wengine wafuate? Wanafunzi wangu wa Biblia ao watu wengine wenye ninarudilia katika mahubiri, wanaweza kuwaza nini ikiwa wanaona mambo ya kujifurahisha yenye ninachagua?’ Wakati tunafuata kanuni zilezile zenye tunaambia wengine wafuate, itakuwa mwepesi kwetu kuepuka mutego wa Shetani.​—1 Yoh. 3:18.

Shetani anajaribu kutuogopesha kwa kutumia serikali ili kukataza kazi yetu, kwa kutumia mukazo kutoka kwa wanafunzi wenzetu, na upinzani kutoka kwa watu wa familia (Picha hizi zinapatana na fungu la 14)

14. Namna gani Shetani anaweza kujaribu kutuogopesha, na namna gani tunaweza kubakia imara?

14 Pia Shetani anajaribu kutuogopesha ili tuvunje ushikamanifu wetu kwa Yehova. Kwa mufano, anaweza kuchochea serikali zikataze kazi yetu ya kuhubiri. Anaweza pia kuchochea wafanyakazi wenzetu ao wanafunzi wenzetu watucheke kwa sababu tunafuata kanuni za Biblia. (1 Pet. 4:4) Shetani anaweza hata kuchochea watu wa familia yenye wenye hawako Mashahidi, wenye wanaweza kuwa na nia ya muzuri, lakini wenye wanaweza kujaribu kutukataza kuhuzuria mikutano. (Mt. 10:36) Tunaweza kufanya nini ili kupinga mutego wa Shetani wa kutuogopesha? Mashambulizi hayo hayapaswe kutushangaza kwa sababu tunajua kama Shetani anapigana vita pamoja na sisi. (Ufu. 2:10; 12:17) Pia, tunapaswa kukumbuka shitaka la Shetani: Anasema kama tunamutumikia Yehova wakati tu hali iko muzuri na kama tutamukataa Mungu wakati magumu yanatokea. (Ayu. 1:9-11; 2:4, 5) Kwa hiyo, tunapaswa kumuomba Yehova sikuzote ili atupatie nguvu. Ukumbuke kama Yehova hatatuacha hata kidogo.​—Ebr. 13:5.

MAMBO YENYE SHETANI HAWEZI KUFANYA

15. Shetani anaweza kutukaza kufanya jambo lolote lenye hatupendi kufanya? Eleza.

15 Shetani hawezi kukaza watu wafanye jambo lolote yenye hawapendi kufanya. (Yak. 1:14) Watu wengi katika ulimwengu hawajue kama wanaunga mukono upande wa Shetani. Lakini wakati mutu anajifunza kweli, anapaswa kuchagua ikiwa atakuwa upande wa Yehova ao wa Shetani. (Mdo. 3:17; 17:30) Ikiwa tunaazimia kumutii Mungu, Shetani hawezi kuvunja ushikamanifu wetu.​—Ayu. 2:3; 27:5.

16, 17. (a) Ni jambo gani lingine lenye Shetani na mashetani wake hawawezi kufanya? (b) Sababu gani hatupaswe kuogopa kusali kwa sauti kwa Yehova?

16 Kuko mambo mengine yenye Shetani na mashetani wake hawawezi kufanya. Kwa mufano, Biblia haiseme hata kidogo kama wanaweza kujua mambo yenye kuwa katika akili yetu ao katika moyo wetu. Yehova na Yesu tu ndio wanaweza kufanya hivyo. (1 Sam. 16:7; Mk. 2:8) Kwa hiyo, tunapaswa kuogopa kama ikiwa tunasema kwa sauti ao kusali kwa sauti Shetani na mashetani wake watasikia mambo yenye tunasema na kutumia mambo hayo ili kutushambulia? Hapana! Sababu gani? Fikiria ulinganifu huu: Hatuogope kufanya mambo ya muzuri katika utumishi wetu kwa Yehova kwa sababu tu Shetani anaweza kutuona. Vilevile, hatupaswe kuogopa kusali kwa sauti kwa sababu tu Shetani anaweza kutusikia. Pia, Biblia iko na mifano mingi yenye kuonyesha kama watumishi wa Mungu walisali kwa sauti, na haiseme hata kidogo kama waliogopa kuwa Ibilisi angewasikia. (1 Fal. 8:22, 23; Yoh. 11:41, 42; Mdo. 4:23, 24) Ikiwa tunajikaza kusema na kufanya mambo yenye Mungu anapenda tufanye, tunaweza kuwa hakika kama Yehova hatamuruhusu Shetani atufanyie mambo yenye yanaweza kutuangamiza milele.​—Soma Zaburi 34:7.

17 Tunapaswa kujua adui yetu, lakini hatupaswe kumuogopa. Hata kama hatukamilike, kwa musaada wa Yehova, tunaweza kupata ushindi juu ya Shetani! (1 Yoh. 2:14) Ikiwa tunamupinga, atatukimbia. (Yak. 4:7; 1 Pet. 5:9) Leo, inaonekana kama Shetani anashambulia zaidi sana vijana. Namna gani wanaweza kupinga mashambulizi ya Shetani? Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.

^ fu. 2 Biblia inataja majina ya pekee ya malaika fulani. (Amu. 13:18; Dan. 8:16; Lu. 1:19; Ufu. 12:7) Inasema pia kama Yehova alipatia kila nyota jina. (Zab. 147:4) Kwa hiyo, inapatana na akili kufikiri kama Yehova alipatia pia malaika wote majina, kutia ndani ule mwenye alifikia kuwa Shetani.

^ fu. 3 Jina “Shetani” linapatikana mara 18 katika Maandiko ya Kiebrania; lakini linapatikana zaidi ya mara 30 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.