Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mukusanyiko wa wilaya katika Nyzhnya Apsha, Ukrainia, 2012

Mavuno Mengi!

Mavuno Mengi!

YESU alitabiri kama wanafunzi wake wangefurahia mavuno mengi katika wakati huu wa mwisho. (Mt. 9:37; 24:14) Fikiria namna maneno yake yanatimia kwa njia ya peke katika eneo la Transcarpathia, Ukrainia. Katika miji tatu jirani katika eneo hilo, kuko makutaniko 50 yenye kuwa na wahubiri zaidi ya 5400. * Kwa kweli, kulingana na jumla ya watu wenye kuishi katika miji hiyo tatu, mutu mumoja kati ya watu ine ni Shahidi wa Yehova!

Watu wako namna gani katika eneo hilo? Ndugu mumoja wa eneo hilo mwenye kuitwa Vasile, anasema hivi: “Hapa watu wanaheshimia Biblia, wanapenda haki, wako na familia zenye kuungana sana, na wanajikaza kabisa kusaidiana.” Anaongezea hivi: “Hawakubaliane sikuzote na mambo yenye tunaamini. Lakini wakati unawaonyesha jambo fulani kutoka katika Biblia, wanasikiliza kwa uangalifu.”

Kwa kweli, ndugu na dada wako na magumu fulani ya pekee wakati wanahubiri katika eneo hilo lenye kuwa na wahubiri wengi, lakini watu wa kuhubiriwa ni wachache. Kwa mufano, kutaniko moja liko na wahubiri 134 lakini kuko tu nyumba 50 za watu katika eneo la kutaniko hilo! Namna gani wahubiri wanajipatanisha na hali hiyo?

Ndugu na dada wengi wanajitoa ili kuhubiri katika maeneo yenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri. Ndugu mumoja mwenye kuwa na miaka 90 mwenye kuitwa Ionash, anasema hivi: “Katika eneo la kutaniko letu muhubiri mumoja anapaswa kuhubiri nyumba mbili. Nilikuwa ninahubiri katika kijiji na nilisafiri pia karibu kilometre 160 ili kuenda katika eneo lenye halijapewa muhubiri fulani, na huko nilihubiria watu katika luga ya Kihungaria. Lakini hivi karibuni, afya yangu iliharibika zaidi na siwezi tena kufanya hivyo.” Wahubiri wanapaswa kujitoa ili kusaidia katika maeneo mengine. Ionash anasema hivi: “Ili kupata treni, nilipaswa kuamuka saa 10 ya asubui na nilihubiri mupaka saa 12 ya mangaribi wakati treni inafanya safari ya kurudia nyumbani. Nilifanya hivyo mara mbili ao mara tatu katika juma.” Anaona kama bidii yake ilikuwa na matokeo ya muzuri? Anasema hivi: “Nilipata furaha kubwa katika aina hiyo ya utumishi. Nilikuwa na pendeleo la kusaidia familia moja yenye ilikuwa katika eneo la mbali kujifunza kweli.”

Ni kweli kwamba, haiko watu wote katika makutaniko ya eneo hilo ndio wako na uwezo wa kufanya safari ya kuenda mbali. Lakini wote, kutia ndani wahubiri wenye kuzeeka, wanajikaza kuhubiri eneo lote la kutaniko lao. Matokeo ni kwamba katika mwaka wa 2017, jumla ya watu wenye walihuzuria Ukumbusho katika miji hiyo tatu, ilizidi mara mbili hivi hesabu ya wahubiri; ao ilikuwa nusu ya watu wote wenye kuwa katika miji hiyo. Bila shaka, hata iwe tunatumikia wapi, kungali “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 Kor. 15:58.

^ fu. 2 Majina ya miji hiyo ni Hlybokyy Potik, Serednye Vodyane, na Nyzhnya Apsha.