Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unatafuta Kukubaliwa na Nani?

Unatafuta Kukubaliwa na Nani?

“Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu na upendo wenye mulionyesha kwa ajili ya jina lake.”​—EBR. 6:10.

NYIMBO: 39, 30

1. Sisi wote tumezaliwa na tamaa gani?

UNAJISIKIA namna gani wakati mutu fulani mwenye unajua na kuheshimia anasahau jina lako ao, hata jambo la mubaya zaidi, anakosa kukutambua? Jambo hilo linaweza kuvunja moyo sana. Sababu gani? Kwa sababu kila mumoja wetu alizaliwa na tamaa ya kupenda wengine wamukubali. Lakini, kuliko tu kujua sisi ni nani, tunapenda wafanye mengi zaidi. Tunapenda wajue sisi ni watu wa namna gani na mambo yenye tumetimiza.​—Hes. 11:16; Yob. 31:6.

2, 3. Namna gani tunaweza kutumia mubaya tamaa yetu ya kupenda wengine watukubali? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Lakini kama hatuko waangalifu, tunaweza kutumia mubaya tamaa hiyo ya kupenda wengine watukubali yenye tunazaliwa nayo. Ulimwengu wa Shetani unaweza kutufanya tutafute kujulikana sana na kuwa watu wa maana. Wakati tunafanya vile, hatumupatie Yehova, Baba yetu wa mbinguni, heshima na ibada yenye anastahili.​—Ufu. 4:11.

3 Wakati wa Yesu, viongozi fulani wa dini walikuwa na mawazo ya mubaya kuhusu kutambuliwa. Yesu alionya wanafunzi wake hivi: “Mufanye angalisho na waandishi wenye wanapenda kutembea-tembea wakiwa wamevaa kanzu, na wanapenda salamu katika masoko, na kukaa kwenye viti vya muzuri zaidi katika masinagogi na wanapenda nafasi za heshima zaidi kwenye chakula cha mangaribi.” Aliongeza hivi: “Hao watapokea hukumu kali zaidi.” (Lu. 20:46, 47, maelezo ya chini) Lakini, Yesu alimusifu mujane maskini mwenye alitoa feza mbili za vichele zenye samani kidogo sana, hata kama pengine hakuna mutu mwingine mwenye alitambua jambo hilo. (Lu. 21:1-4) Kwa kweli, mawazo ya Yesu juu ya kutambuliwa yalikuwa tofauti sana na ya wengine. Habari hii itatusaidia tuendelee kuwa na mawazo ya muzuri kuhusu kutambuliwa, mawazo yenye Yehova Mungu anataka tukuwe nayo.

AINA YA MUZURI ZAIDI YA KUKUBALIWA

4. Ni aina gani ya kukubaliwa yenye kuwa ya muzuri zaidi, na sababu gani?

4 Ni aina gani ya kukubaliwa yenye kuwa ya muzuri zaidi? Haiko aina ya kukubaliwa yenye watu wengi wanatafuta kupata kwa kusoma masomo ya juu, kupata matokeo ya muzuri katika biashara, ao kujulikana sana katika mambo ya kujifurahisha ya ulimwengu huu. Paulo alifasiria aina ya muzuri zaidi ya kukubaliwa wakati alisema hivi: “Sasa kwa kuwa mumemujua Mungu ao, tofauti na hilo, kwa kuwa Mungu amewajua ninyi, sababu gani munarudilia tena mambo ya musingi yenye kuwa zaifu na yenye hayana maana na munataka kuyatumikia tena?” (Gal. 4:9) Ni pendeleo la muzuri sana kujulikana na Mungu, Mutawala Mukubwa Zaidi wa ulimwengu wote! Yehova anajua sisi ni nani, anatupenda, na anataka tumukaribie. Yehova alituumba ili tukuwe marafiki wake.​—Muh. 12:13, 14.

5. Tunapaswa kufanya nini ili Mungu atujue?

5 Tunajua kama Musa alikuwa rafiki ya Yehova. Wakati fulani alimuomba Yehova hivi: “Nijulishe njia zako.” Yehova alimujibu hivi: “Nitafanya pia jambo hilo lenye unaomba, kwa sababu umekubaliwa mbele ya macho yangu na ninakujua wewe kwa jina.” (Kut. 33:12-17) Yehova anaweza pia kutujua kipekee. Lakini, tunapaswa kufanya nini ili tukuwe marafiki wa Yehova? Tunapaswa kumupenda na kutoa maisha yetu kwake.​—Soma 1 Wakorinto 8:3.

6, 7. Ni nini inaweza kutufanya tupoteze urafiki wetu pamoja na Yehova?

6 Hata hivyo, tunapaswa kuendelea kulinda urafiki wetu wa maana sana pamoja na Baba yetu wa mbinguni. Kama Wakristo wa kwanza-kwanza katika Galatia, tunapaswa kuacha kutumikia “mambo ya musingi yenye kuwa zaifu na yenye hayana maana” yenye ulimwengu huu unatoa, kama vile, utajiri na kujulikana sana. (Gal. 4:9) Wakristo hao katika Galatia walikuwa wamekwisha kumujua Mungu, na Mungu alikuwa amekwisha kuwajua. Lakini Paulo alisema kama Wakristo hao walikuwa ‘wanarudilia tena’ mambo yenye hayana maana. Ni kama vile alikuwa anawauliza hivi: ‘Sababu gani mulirudia nyuma na kuanza kutumikia tena mambo yaleyale ya upumbavu na yenye hayana maana?’

7 Je, jambo hilo linaweza kutufikia sisi pia? Ndiyo. Kama Paulo, pengine wakati tulijua kweli, tulikataa kukubaliwa na ulimwengu wa Shetani. (Soma Wafilipi 3:7, 8.) Pengine tuliacha nafasi za kusoma masomo ya juu kwa bure, kazi za muzuri, na nafasi za kupata feza nyingi. Ao pengine tungejulikana sana ao kuwa matajiri kwa sababu tuko na uwezo fulani wa kizalikio katika mambo ya muziki ao michezo. Lakini, tulikataa mambo hayo yote. (Ebr. 11:24-27) Kama tunahuzunika kwa sababu ya maamuzi hayo yenye tulikamata na kuwaza kama maisha yetu yangekuwa muzuri zaidi ikiwa tungefuatia mambo hayo, inaweza kuwa kukosa hekima sana! Mawazo hayo yanaweza kutufanya turudilie mambo ya ulimwengu huu, ni kusema, mambo yenye tayari tulikuwa tumeona kuwa “zaifu na yenye hayana maana.”

TIA NGUVU TAMAA YAKO YA KUPENDA KUKUBALIWA NA YEHOVA

8. Ni nini itatia nguvu tamaa yetu ya kupenda kukubaliwa na Yehova?

8 Tunaweza kufanya nini ili tamaa yetu ya kupenda kukubaliwa na Yehova ikuwe yenye nguvu zaidi kuliko tamaa ya kupenda kukubaliwa na ulimwengu? Tunapaswa kukumbuka mambo mbili ya maana. Kwanza, sikuzote Yehova anaonyesha kama anakubali wale wenye kumutumikia kwa uaminifu. (Soma Waebrania 6:10; 11:6) Yehova anaona watumishi wake wote waaminifu kuwa wa maana sana, kwa hiyo, anaona kama inaweza kuwa “ukosefu wa haki” kusahau mumoja kati yao. Sikuzote, Yehova anajua “wenye kuwa wake.” (2 Ti. 2:19) “Anajua njia ya wenye haki” na anajua namna ya kuwaokoa.​—Zb. 1:6; 2 Pe. 2:9.

9. Namna gani Yehova ameonyesha kama anakubali watu wake? Toa mifano.

9 Wakati fulani, Yehova ameonyesha katika njia za pekee sana kama anakubali watu wake. (2 Ny. 20:20, 29) Kwa mufano, fikiria namna Yehova aliokoa watu wake kwenye Bahari Nyekundu wakati jeshi lenye nguvu la Farao lilikuwa linawafuatilia. (Kut. 14:21-30; Zb. 106:9-11) Tukio hilo lilikuwa lenye kushangaza sana; watu katika eneo hilo walikuwa wangali wanalizungumuzia miaka 40 kisha jambo hilo kutokea. (Yos. 2:9-11) Inatia moyo sana kukumbuka namna Yehova alipenda watu wake na kutumia nguvu zake ili kuwaokoa wakati wa zamani, kwa sababu hivi karibuni Gogu wa Magogu atatushambulia. (Eze. 38:8-12) Wakati huo, tutafurahi sana kwa sababu tulitafuta kukubaliwa na Mungu kuliko kukubaliwa na ulimwengu.

10. Ni jambo lingine gani lenye tunapaswa kukumbuka?

10 Jambo la pili lenye tunapaswa kukumbuka ni hili: Yehova anaweza kuonyesha kama anatukubali katika njia zenye hatuwazie hata kidogo. Kama watu wanafanya mambo ya muzuri ili tu kusifiwa na wengine, Yehova hatawapatia zawabu ao kuwabariki. Sababu gani? Kwa sababu, kama vile Yesu alisema, wakati wengine wanawasifu, hiyo ndiyo zawabu yao. (Soma Matayo 6:1-5.) Lakini, Yehova “anaona akiwa mahali pa siri” watu wenye hawasifiwe juu ya mema yenye wanatendea wengine. Anaona mambo yenye wanafanya, na anawapatia zawabu, ao kuwabariki. Na wakati fulani Yehova anabariki watu wake katika njia zenye hawakuwazia. Tuzungumuzie basi mifano fulani.

KIJANA MWANAMUKE MUNYENYEKEVU ANAKUBALIWA NA YEHOVA KATIKA NJIA YENYE HAKUWAZIA

11. Namna gani Yehova alionyesha kama anamukubali Maria?

11 Yehova alichagua kijana mwanamuke munyenyekevu mwenye kuitwa Maria ili akuwe mama ya Mwana wake, Yesu. Maria aliishi katika muji mudogo wenye uliitwa Nazareti; muji huo ulikuwa mbali na Yerusalemu na hekalu lake la muzuri. (Soma Luka 1:26-33.) Sababu gani Yehova alimuchagua Maria? Malaika Gabrieli alimuambia hivi: “Umekubaliwa na Mungu.” Kisha pale, mambo yenye Maria alimuambia Elizabeti, mutu wa jamaa yake, yanaonyesha kama alikuwa rafiki wa sana wa Yehova. (Lu. 1:46-55) Yehova alikuwa amemuchunguza Maria, na alimupatia baraka hiyo yenye hakuwazia, kwa sababu alikuwa muaminifu kwake.

12, 13. Namna gani Yesu alipewa heshima (a) wakati alizaliwa? (b) wakati Maria alimupeleka kwenye hekalu siku 40 kisha kuzaliwa kwake?

12 Wakati Yesu alizaliwa, ni nani wenye Yehova aliambia juu ya kuzaliwa kwake? Hakuambia hata mumoja kati ya maofisa ao watawala wenye mamlaka zaidi katika Yerusalemu na Betlehemu. Lakini, alituma malaika kwa wachungaji wanyenyekevu wenye walikuwa wanachunga kondoo katika mashamba inje ya muji wa Betlehemu. (Lu. 2:8-14) Kisha, wachungaji hao walienda kuona mutoto huyo mwenye alizaliwa. (Lu. 2:15-17) Maria na Yosefu walipaswa kushangaa kabisa wakati waliona kama Yesu alipewa heshima katika njia hiyo. Namna Yehova anafanya mambo iko tofauti na namna Ibilisi anafanya mambo. Wakati Shetani alituma watu wenye elimu ya nyota ili waende kumuona Yesu na wazazi wake, kila mutu katika Yerusalemu alijua kama Yesu alikuwa amezaliwa, na jambo hilo lilileta shida sana. (Mt. 2:3) Watoto wengi wenye hawana makosa waliuawa kwa sababu ya jambo hilo.​—Mt. 2:16.

13 Sheria yenye Yehova alipatia Waisraeli ilisema kama mwanamuke alipaswa kumutolea Yehova zabihu siku 40 kisha kuzaa mutoto mwanaume. Kwa hiyo, Maria alisafiri kilometre kenda hivi pamoja na Yosefu na Yesu kutoka Betlehemu ili kuenda Yerusalemu kwenye hekalu. (Lu. 2:22-24) Wakati walikuwa katika njia, pengine Maria alijiuliza ikiwa kuhani atafanya jambo fulani la pekee ili kumuonyesha Yesu heshima. Yesu alipewa heshima, lakini katika njia yenye pengine Maria hakuwazia. Yehova alimuchagua Simeoni, mutu “mwenye haki na mwenye kumuogopa Mungu,” na nabii mwanamuke Ana, mujane mwenye alikuwa na miaka 84, ili watangaze kama Yesu angekuwa Masiya mwenye aliahidiwa, ao Kristo.​—Lu. 2:25-38.

14. Namna gani Yehova alimubariki Maria?

14 Je, Yehova aliendelea kuonyesha kama anamukubali Maria kwa sababu alimukomalisha Yesu na kumuhangaikia kwa uaminifu? Ndiyo. Mungu alihakikisha kwamba mambo fulani yenye Maria alisema na kufanya yanaandikwa katika Biblia. Inaonekana kuwa Maria hakuweza kusafiri pamoja na Yesu kwa miaka tatu na nusu yenye Yesu alihubiri. Pengine kwa sababu alikuwa mujane, alipaswa kubakia Nazareti. Kwa hiyo, hakuona mambo mengi ya muzuri yenye wengine walijionea. Lakini wakati Yesu alikufa, Maria alikuwa pale. (Yoh. 19:26) Kisha, alikuwa Yerusalemu pamoja na wanafunzi wa Yesu mbele wapokee roho takatifu kwenye Pentekoste. (Mdo. 1:13, 14) Inawezekana kabisa alitiwa mafuta pamoja na wanafunzi wengine. Kama ni vile, alipata pendeleo la kuwa pamoja na Yesu mbinguni milele. Kwa kweli, hiyo ni baraka ya muzuri kwa sababu ya utumishi wake muaminifu!

YEHOVA ALIONYESHA KAMA ANAMUKUBALI MWANA WAKE

15. Namna gani Yehova alionyesha kama anamukubali Yesu wakati alikuwa katika dunia?

15 Yesu hakutafuta kupata heshima kutoka kwa viongozi wa dini ao wa politike. Lakini mara tatu, Yehova alisema moja kwa moja kutoka mbinguni ili kumujulisha Mwana wake kama alimupenda. Kwa kweli, hilo lilimutia Yesu moyo sana! Kisha tu Yesu kubatizwa katika Muto Yordani, Yehova alisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” (Mt. 3:17) Inaonekana kuwa ni Yohana Mubatizaji tu ndiye mutu mwingine mwenye alisikia maneno hayo. Kisha, mwaka moja hivi mbele ya kifo cha Yesu, mitume tatu kati ya mitume wake walisikia wakati Yehova alisema maneno haya juu ya Yesu: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali. Mumusikilize.” (Mt. 17:5) Mwishowe, siku kidogo tu mbele ya kifo cha Yesu, Yehova alisema tena na Mwana wake kutoka mbinguni.​—Yoh. 12:28.

Namna Yehova alionyesha kama anamukubali Mwana wake, inakufundisha nini? (Picha hizi zinapatana na fungu la 15-17)

16, 17. Namna gani Yehova alimutukuza Yesu katika njia yenye Yesu hakuwazia?

16 Yesu alijua kama watu watasema kwamba amemutukana Mungu na alijua pia kama angekufa kifo cha haya. Hata hivyo, alisali mapenzi ya Mungu yafanyike, hapana mapenzi yake mwenyewe. (Mt. 26:39, 42) “Alivumilia muti wa mateso, akazarau haya,” kwa sababu alitafuta kukubaliwa na Baba yake, kuliko kukubaliwa na ulimwengu. (Ebr. 12:2) Namna gani Yehova alionyesha kama anamukubali Yesu?

17 Wakati Yesu alikuwa katika dunia, alisali apate utukufu wenye alikuwa nao mbele, wakati alikuwa mbinguni pamoja na Baba yake. (Yoh. 17:5) Biblia haiseme kama Yesu alitumainia kupata utukufu zaidi ya ule wenye alikuwa nao. Hakutazamia kupata baraka ya pekee kwa sababu alifanya mapenzi ya Yehova katika dunia. Lakini, Yehova alifanya nini? Alimutukuza Yesu katika njia yenye Yesu hakuwazia. Wakati Yehova alimufufua Yesu, alimupatia “cheo cha juu zaidi” mbinguni. Pia, alimupatia Yesu uzima wa roho wenye hauwezi kufa; hakuna mutu mwingine mwenye alikuwa amepewa uzima huo! * (Ona maelezo ya chini.) (Flp. 2:9; 1 Ti. 6:16) Kwa kweli, Yehova alimubariki Yesu katika njia ya ajabu sana kwa ajili ya utumishi wake wa uaminifu!

18. Ni nini itatusaidia tutafute kukubaliwa na Yehova kuliko kukubaliwa na ulimwengu huu?

18 Ni nini itatusaidia tutafute kukubaliwa na Yehova kuliko kukubaliwa na ulimwengu huu? Tunapaswa kukumbuka kama sikuzote Yehova anaonyesha kama anakubali watumishi wake waaminifu, na kama mara nyingi anawabariki katika njia zenye hawakuwazia. Ni vigumu kuwazia baraka zote zenye Yehova atatupatia wakati wenye kuja! Lakini leo, wakati tunavumilia magumu katika ulimwengu huu muovu, tunapaswa kukumbuka kama ulimwengu huu utapita. Kwa hiyo, wale wote wenye kukubaliwa na ulimwengu huu watapita pia. (1 Yo. 2:17) Lakini, Yehova Baba yetu mwenye upendo hatasahau hata kidogo kazi yetu na upendo wenye tunaonyesha kwa ajili ya jina lake, kwa sababu “hana ukosefu wa haki.” (Ebr. 6:10) Bila shaka, ataonyesha kama anatukubali, pengine katika njia zenye hatujawaziaka hata kidogo!

^ fu. 17 Inawezekana Yesu hakuwazia baraka hiyo, kwa sababu uzima wenye hauwezi kufa hautajwe katika Maandiko ya Kiebrania.