Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Ikiwa watu wawili wa jinsia tofauti ambao hawajaoana watalala katika chumba kilekile usiku bila sababu zinazoeleweka, je, hilo lingeonwa kuwa dhambi inayostahili kuchukuliwa hatua ya kihukumu?

 

Baraza la wazee huchanganua kwa makini kila kisa ili kuamua ikiwa halmashauri ya hukumu inahitaji kuundwa. Kwa mfano: Je, Wakristo hao ni wachumba? Je, waliwahi kushauriwa kuhusu jinsi wanavyojiendesha wakiwa pamoja? Kwa nini walilala ndani ya chumba kilekile usiku? Je, walipanga mapema kufanya hivyo? Je, walikuwa na njia nyingine yoyote ya kushughulikia hali hiyo, au, sababu zozote zinazoeleweka, labda tukio lisilotazamiwa au hali fulani nzito ya dharura ambayo iliwalazimisha walale kwenye chumba kilekile usiku huo? (Mhu. 9:11) Walilala wapi? Kwa kuwa kila kisa ni tofauti, huenda kukawa na mambo mengine yanayohusika ambayo wazee watachunguza ili kufikia uamuzi.

Baada ya kupata habari kamili, baraza la wazee litaamua ikiwa jambo ambalo Wakristo hao wawili walifanya linapaswa kuchukuliwa hatua ya kihukumu.